CRJE na ufisadi serikalini

CRJE na ufisadi serikalini

Hii kampuni ya WAPARE

Mnajua nani aliwapatia tenda pale RITA?
 
Mkandarasi wa uhakika local ni Estim Construction
 
1-26.jpg



Hii ni kampuni ya ujenzi ya waChina hapa Tanzania

hii kampuni inaongoza kwa kutuhumiwa kuwatajirisha maofisa wa serikali ambao wanahusika kwa namna moja au nyingine kutoa tenda za ujenzi.

CRB nao inaonekana hawana uwezo wa kuwafanya kitu lakini kwa sababu kampuni za wazalendo hazipendwi na maofisa waserikali kwani hazitoi rushwa, sasa hivi wazalendo wengi wameamua eidha kuuza au kuhamia nchi za jirani huku Tanzania inaachiwa CRJE

Kama hamumini tazameni nani anapitisha tenda za hiii kampuni na hali zao za kimaisha zikoje. Pia kwa kuwa waChina bei zao ni za chini mno lakini ukweli ni kuwa wanaweka materials ambazo ni hafifu sana kwenye majengo lakini of course kwa sababu washawanuanua ma inspectors hakuna anayeweza kutia neno.

sisi kama wama taaluma hiii tumefika hatua ya kukata tamaa na juzi nilikutana na wanafunzi toka ardhi ambao ilibidi niwape hali halisi ilivyo huku nje ya shule.

Kama serikali ispoliangalia hili kwa undani basi muda si mrefu mtaona industry nzima inaanguka Tanzania wakati Rwanda na Kenya serikali zao zina linda local companies.
Mtoa mada unaweza ukawa na ukweli au kukawa na hitilafu kidogo,kwanza tukumbuke waliokuwa wanaagiza tenda zifanyike chini ya viwango ni viongozi waliokuwa na dhamana ya kutoa hizo tenda ili kwanza wapate 10% na pia kupunguza gharama za mradi ziwe chini ili wagawane kiasi kitakachobakia ndio maana tumekuwa na miradi iliyojengwa chini ya viwango.
kuhusu kampuni za wazawa ndio hazifai kabisa maana zilikuwa zinapata tenda kwa kujuana,utendaji kazi hafifu,wizi wa vifaa,usimamizi mbovu ukilinganisha na wachina ambao wakiwa kwenye kazi huwezi kutofautisha injinia ni yupi na kibarua ni yupi wanapiga kazi kiukweli tofauti na sisi kampuni za wazawa msimamizi wa mradi yuko ofisini huku saiti watu wanaiba hadi malighafi.
kwenye hili namtafakari mgombea urais wa marekani DONALD TRUMP kama umepata kusoma aliyosema kutuhusu sisi waafrika utapata majibu,kwahiyo sijashangazwa kabisa na post kama hii,nilijua katika awamu hii ya magufuli contractors wengi wa ujanjaujanja kampuni zao zitakufa kutokana na kwamba hakuna atakayepata tenda kwa mazabe,rejea hotuba ya Raisi kule ARUSHA mapema mwaka huu alisema anafikiria kulitumia sana jeshi kuimarisha uchumi wa nchi,yani jeshi lipewe miradi mikubwa ya maendeleo kama ujenzi wa nyumba,madaraja barabara nk kwa kujua wanajeshi ni waaminifu na hawatahitaji 10% na wakisimamia kazi hatatokea kibarua wakuiba hata misumari,kwa mtaji huu kampuni za wazawa zenye kujiweza ndio zitabaki ,zile zilizokuwa zinategemea mazabe,blahblah kazi hawamalizi kwa wakati na kusababisha gharama za miradi kuwa kubwa kupita hata makadirio ya kwanza hawatakuwa na nafasi ni lazima watakuja kulialia humu.
 
Back
Top Bottom