Engineermsuya
Member
- May 23, 2011
- 32
- 7
Hii ni kampuni ya ujenzi ya waChina hapa Tanzania
hii kampuni inaongoza kwa kutuhumiwa kuwatajirisha maofisa wa serikali ambao wanahusika kwa namna moja au nyingine kutoa tenda za ujenzi.
CRB nao inaonekana hawana uwezo wa kuwafanya kitu lakini kwa sababu kampuni za wazalendo hazipendwi na maofisa waserikali kwani hazitoi rushwa, sasa hivi wazalendo wengi wameamua eidha kuuza au kuhamia nchi za jirani huku Tanzania inaachiwa CRJE
Kama hamumini tazameni nani anapitisha tenda za hiii kampuni na hali zao za kimaisha zikoje. Pia kwa kuwa waChina bei zao ni za chini mno lakini ukweli ni kuwa wanaweka materials ambazo ni hafifu sana kwenye majengo lakini of course kwa sababu washawanuanua ma inspectors hakuna anayeweza kutia neno.
sisi kama wama taaluma hiii tumefika hatua ya kukata tamaa na juzi nilikutana na wanafunzi toka ardhi ambao ilibidi niwape hali halisi ilivyo huku nje ya shule.
Kama serikali ispoliangalia hili kwa undani basi muda si mrefu mtaona industry nzima inaanguka Tanzania wakati Rwanda na Kenya serikali zao zina linda local companies.