CRDB wakataa fedha za mteja!

lakini zile form za kuwekea fedha nazo nadhani zitakuwa na tatizo kwana nadhani hakuna sehemu wameonyesha 10,20,50,100...!!sasa mteja atajaza vipi akiwa na sarafu!!!
 
Bank yoyote tanzania hairuhusiwi kukataa pesa zozote hata sarafu ya sh. 10 lazima wapokee na bank yoyote ikikataa kupokea hela labda iwe imeharibika inatakiwa kufutiwa leseni mhusika apeleke lalamiko hilo kama lipo kwa waziri wa fedha, na pesa ikiwa mbovu ipelekwe bot.
 
lakini zile form za kuwekea fedha nazo nadhani zitakuwa na tatizo kwana nadhani hakuna sehemu wameonyesha 10,20,50,100...!!sasa mteja atajaza vipi akiwa na sarafu!!!

ipo kila form za benki maana ni sheria hupewi leseni bila hiyo.
 
Swala la kujiuliza ni je?, teller amepata elimu yoyote ya banking au kazi yake ameambiwa ni kupokea noti tu?'
Hapa hata huyo mteja anauelewa mdogo wa fedha na huduma kwa wateja, alipaswa kumuona meneja kabla ya kuondoka.
Ndugu zangu, katika hali isiyo ya kawaida, leo nimeshuhudia tukio la kusikitisha. Nilikuwa katika Benki ya CRDB, Tawi la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam; nimeshuhudia mhudumu wa dirisha namba 2 akikataa kupokea fedha za mteja mmoja kijana. Kisa ni kwamnba kijana huyo alikuwa na fedha nyingi za Sh 50, 100 na 200 ambazo kwa kawaida ni sarafu. Mhudumu amekataa kuzipokea kwa maelezo kwamba hawapokei "masimbi". Akamtaka kijana huyo azipeleke kwa makondakta wa daladala, azibadili ili wampe noti, au masimbi hayo ayapeleke BoT. Kukawa na vuta nikuvute, mwisho yule kijana akaondoka bila kuweza fedha kwenye akaunti.

Hoja: Hii ni sahihi kwa benki kukataa kupokea sarafu? Je, sarafu hazitambuliwi kama fedha halali hapa nchini? Naomba wadau tulijadili suala hili.

Nawasilisha.
 
Watanzania ushirikiano ni zero kabisa wewe umeshindwa nini kumshauri pamoja na wenzio angalau amuone hata meneja muhusika kuliko kumuacha akaondoka bila kupata huduma?

yani hapa ndio napata shida sana kuelewa sisi huwa tuna matatizo gani unakuta mtu anashuhudia tatizo fulani anakaa kimya tu na kuanza kulalamika ama kukaa kimya bila kutoa msaada wowote kwa mwenye tatizo. baadae tunajitia kuelezea jinsi tulivyoumizwa na tukio.
 
kaona uvivu kuzihesabu...si unajua noti zinahesabiwa na mashine sasa coins inabidi ahesabu yeye akaona uvivu..bt hilo ni kosa bt that explains alot about crdb hii benki mi siipendagi na sijawahi kuipenda toka siku ya kwanza...customer service yao ni ZERO
 
mivyuo ya kata imeanza kutrapika product zake.......

lakin customer care kwa tanzania ni tatizo, tusipobadilika kwa ubinafsishaji huu wa kila kitu wazungu na wahindi watakuwa wanakuja na wafanyakazi wao toka huko kwao, alafu mwisho wa siku tuseme kazi hakuna!! hata tukipata kazi ndo upumbavu huo tunafanya, mara tukatae sarafu, mara waibe tomato sosi, mara karoti, mara waibie wateja mahotelini basi kero tupu,....kwa mtaji huu kuendelea nchi hii ni badae sana, hadi hapo tutakapoamua kubadilika.
 
Nadhani hapo ishu kubwa si ya CRDB, itakuwa ni huyo Teller kuona uvivu kuzihesabu hizo coins. Kama swala lingeenda kwenye ngazi za juu lazima wangezipokea tu. Kijana alitakiwa kusaidiwa mawazo ya kuwaona wakubwa wa Teller husika.
 
hapana ipo sehemu ya coin....sema tu haisemi 50,100,200 etc
bali unatakiwa uandike una coin za sh ngapi?
ok!!!kwa hiyo huyu jamaa akalalamike wapi!!nakumbuka issue kama hii iliwahi kutokea siku za nyuma na ilibidi mhusika azipeleke zile 'simbi' benki kuu!
 
......inaonekana CRDB wameshiba pesa...na pia wanaamini kwamba wao wanao wateja wengi kwa na wanawatosha....... huyo jamaa alitakiwa aonane na meneja au mhasibu...
 
Back
Top Bottom