CRDB Tawi la Chanika mmeniibia

CRDB Tawi la Chanika mmeniibia

Hizo pesa uliibiwa njiani acha kulaumu tellers maana kutoka hapo benki mpaka huko kwenye kuandikishana ni hatua pia watu siku hizi ni wezi sana wanaweza kukuibia bila hata kuwa na physical contact binafsi ilishawahi nitokea nilienda tawi moja la backlays pale karikoo nikatoa laki 5 kwenye mashine na nikahesabu kabsa bt nafika home mbagala nikakuta laki 4 tu so mshukuru sir god kwa kuwa hawajachomoa pakubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo michezo IPO hata kwa baadhi mawakala kutoa na kuweka pesa ukienda kwa ajili ya kuweka usipohesabu mbele yake imekula kwako yamenikuta kariakoo meeneo big born kona ya kuingilia magari ya abiria ya muhimbili kwa wakala mwenye 11121 Issa Mdolwa nilijua labda nimedondosha nauliza majirani waniambia ni michezo yake ila nimemwambia hiyo michezo itakutokea puani utakuja kuingia sehemu siyo
 
Anahesabu tena vizuri sana na skrini anakugeuzia, kupigwa ni pale mrembo anazitoa hizo noti kwenye mashine ili azipange akukabidhi.

Zimehesabiwa mbele yako hivyo hutakuwa na muda tena wala wasiwasi kuhakiki, naye anatumia vema mwanya huo kuchezesha noti mbili tatu ili maisha yasonge.

Mjini shule bwashee.
Huwa wanao mchezo flani hv... anahesabu mbele yako kwa mashine then wakati anazifunga kwa rubber band hudondosha chini noti kadhaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnamo mwezi wa pili (tarehe siikumbuki) nilienda kutoa pesa Tawi la CRDB Chanika Mwisho kiasi cha milioni mbili. Basi baada ya kukaa foleni kwa muda mlefu nikafika dirishani, huku nje madalali wananisubiri nikalipie kiwanja kata ya Yondwe.

Kilichonikuta sitosahau. Kwanza yule dada anayenihudumia alikuwa amenuna sana pale kidirishani; namkumbuka alikua mweusi, akanipatia 5,000 tupu kiasi cha milioni mbili, mzigo huo. Nikamwambia anipe 10,000 akakataa.

Basi nikaona uvivu kuhesabu, kumbe dada kanipiga 20,000 kwenye ile pesa; kufika kule kwa mtendaji, 20,000 haipo.

Hawa wahudumu wa benki sio waaminifu,

Sent using Jamii Forums mobile app
Recklessness, a likukong'oli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hivi kwa yale mazingira ya bank unaweza kukaa Counter ukahesabu hizo elfu tano tano mpaka zifike mfano milioni 4. Huku kuna kuna msululu wa watu umekaa nyuma wanakusubiri ?
Kama unatoa hela mara kwa mara mzigo mwingi, ni kucheza na mashine tu na mara nyingi teller anakuangalia na kukuelekezea mashine pale anapotoa kibunda cha fedha na kuhesabu kwenye mashine hivyo kwa kutumia mashine unaangalia wakati anahakiki zile yale mabunda ya fedha kabla ya kukupatia
 
Mkuu pole sana kalikuwa ka hela ka kiwanja nini, manaake nimeona umetaja mjumbe hapo...

Kwa Bati Nzuri nipigie 0658339930
 
Huwa wanao mchezo flani hv... anahesabu mbele yako kwa mashine then wakati anazifunga kwa rubber band hudondosha chini noti kadhaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana sio rahisi, counter za wahumu wa bank ziko wazi sana chochote atakachofanya kinaonekana, Ninadhani watakuwa wamehesabu vibaya wakati wa kukabidhiana, noti za elf5 hugandamana hasa zinapokuwa chakavu ni rahisi kukosea kuhesabu, hata baadhi ya mashine za kuhesabia hukosea sembuse mikono!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama unatoa hela mara kwa mara mzigo mwingi, ni kucheza na mashine tu na mara nyingi teller anakuangalia na kukuelekezea mashine pale anapotoa kibunda cha fedha na kuhesabu kwenye mashine hivyo kwa kutumia mashine unaangalia wakati anahakiki zile yale mabunda ya fedha kabla ya kukupatia
Hapana hua vibuli sana hawa wafanyakazi utakuta wamenuna tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapana sio rahisi, counter za wahumu wa bank ziko wazi sana chochote atakachofanya kinaonekana, Ninadhani watakuwa wamehesabu vibaya wakati wa kukabidhiana, noti za elf5 hugandamana hasa zinapokuwa chakavu ni rahisi kukosea kuhesabu, hata baadhi ya mashine za kuhesabia hukosea sembuse mikono!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kibunda kimoja ndo kilipungua 20000

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaambuwa "Count your money before leaving the counter"..Sababu wanajua kuna human errors huwa zinatokea,.wewe unachukua hela unakimbia,unakuja kumlaumu dada wa watu huku JF,ambae unaweza kuta hata hajui kama alikupa hela nusu...
 
Unaambuwa "Count your money before leaving the counter"..Sababu wanajua kuna human errors huwa zinatokea,.wewe unachukua hela unakimbia,unakuja kumlaumu dada wa watu huku JF,ambae unaweza kuta hata hajui kama alikupa hela nusu...
Nimetoa dukuduku lg sijalalamika tambua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom