CRDB Tawi la Chanika mmeniibia

CRDB Tawi la Chanika mmeniibia

Mnamo mwezi wa pili (tarehe siikumbuki) nilienda kutoa pesa Tawi la CRDB Chanika Mwisho kiasi cha milioni mbili. Basi baada ya kukaa foleni kwa muda mlefu nikafika dilishani, huku nje madalali wananisubiri nikalipie kiwanja kata ya Yondwe.

Kilichonikuta sitosahau. Kwanza yule dada anayenihudumia alikuw amenuna sana pale kidirishani; namkumbuka alikua mweusi, akanipatia 5000 tupu kiasi cha milioni mbili, mzigo huo. Nikamwambia anipe 10000 akakataa.

Basi nikaona uvivu kuhesabu, kumbe dada kanipiga 20000 kwenye ile pesa; kufika kule kwa mtendaji, 20000 haipo.

Hawa wahudumu wa benki sio waaminifu, mnisamehe jamani kwa uandishi wangu mbovu. Si mnajua shule zetu kayumba?

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu uwe unahesabu kwanza kabla hujaondoka counter, teller wenyewe huwa wanakosea ndio maana wanataka ujiridhishe, ukiwaamini na ukaondoka kumbe pesa imepelea hiyo inakuwa uzembe wako mwenyewe
 
Mkuu hivi kwa yale mazingira ya bank unaweza kukaa Counter ukahesabu hizo elfu tano tano mpaka zifike mfano milioni 4. Huku kuna kuna msululu wa watu umekaa nyuma wanakusubiri ?
atumie mashine vinginevyo ahesabu hata kama atatumia masaa mawili. unaharakia wapi kwani
 
Halafu Nmb kwanini hamtaki kufungua tawi Chanika ?mnatusumbua sana aisee huku kuna wakazi (sio yule wa hip hop)wengi sana ila huduma tunafata gomz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole siku ingine mwambie ahesabu kwenye mashine ile screen ya mashine ikiwa imegeukia usawa ambao unaona, hatakataa!

Ni kweli ni jukumu lako kuhesabu, ila itakua matumizi mabaya na kutokutumia tech wakati kuna mashine uanze kuhesabu vinoti kwa mkono hadi umalize.

Mimi natumia hiyo ya kumwambia heaabu hapo kwenye mashine na sijawahi kulizwa.

Anahesabu tena vizuri sana na skrini anakugeuzia, kupigwa ni pale mrembo anazitoa hizo noti kwenye mashine ili azipange akukabidhi.

Zimehesabiwa mbele yako hivyo hutakuwa na muda tena wala wasiwasi kuhakiki, naye anatumia vema mwanya huo kuchezesha noti mbili tatu ili maisha yasonge.

Mjini shule bwashee.
 
Mnamo mwezi wa pili (tarehe siikumbuki) nilienda kutoa pesa Tawi la CRDB Chanika Mwisho kiasi cha milioni mbili. Basi baada ya kukaa foleni kwa muda mlefu nikafika dilishani, huku nje madalali wananisubiri nikalipie kiwanja kata ya Yondwe.

Kilichonikuta sitosahau. Kwanza yule dada anayenihudumia alikuw amenuna sana pale kidirishani; namkumbuka alikua mweusi, akanipatia 5000 tupu kiasi cha milioni mbili, mzigo huo. Nikamwambia anipe 10000 akakataa.

Basi nikaona uvivu kuhesabu, kumbe dada kanipiga 20000 kwenye ile pesa; kufika kule kwa mtendaji, 20000 haipo.

Hawa wahudumu wa benki sio waaminifu, mnisamehe jamani kwa uandishi wangu mbovu. Si mnajua shule zetu kayumba?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao hizo ndio tabia zao mkuu, siku nyingine hesabu mpunga wako hapo , mm pia imeshanitokea walinipiga 10,000 CRDB tabata

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anahesabu tena vizuri sana na skrini anakugeuzia, kupigwa ni pale mrembo anazitoa hizo noti kwenye mashine ili azipange akukabidhi.

Zimehesabiwa mbele yako hivyo hutakuwa na muda tena wala wasiwasi kuhakiki, naye anatumia vema mwanya huo kuchezesha noti mbili tatu ili maisha yasonge.

Mjini shule bwashee.
Ni njaaa sana Hawa wadada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mada humu watu walizungumzia jinsi hao wahudum wanavyoiba. Wanazidondosha pale chini anapokua amekaa.
 
Mimi sio mvivu kabisa wa kuhesabu pesa hata unipe silver za mia tano tano kiasi cha milioni mbili nitahesabu vizuri tu sinaga ubishoo kabisa kwenye kuhesabu pesa


Sent using IPhone X
 
Kuna mpuuz mmoja alinipa mil4 alaf buku buku imagine...
 
Back
Top Bottom