Wizi wa Mtandao (ATM) unaotokea katika banki ya NMB tawi la Benki House Dar es Salaam

displayname

JF-Expert Member
Feb 15, 2013
1,950
1,039
Habari wanajamvi,

Nimeona niwashirikishe wadau naona tangu pesa iwe adimu awamu hii ya tano kama wengi wanavyo amini hivyo, (mimi si mwamini wa hayo) kumekuwepo kwa matukio ya wizo wa fedha hasa katika Benki ya NMB.

Pana jamaa zangu kadha wamepigwa pesa mwezi huu wa tano wote toka akaunti za NMB na wote ni watumishi wa Serikali na matukio yote yamepigwa katika Benki House Dar es Salaam, kupitia ATM mashine tena nyakati za usiku.

Niliopata taarifa zao waliibiwa;-
Mtu wa 1. 700,000
Mtu wa 2. 300,000
Mtu wa 3. 300,000
Mtu wa 4. 200,000
Mtu wa 5. 500,000
Hao ni baadhi ya jamaa zangu tu wakaribu niliopata sikia wakilalamika>

Mazigira ya kuibiwa yalikuwa hivi
Pesa zote zimetokea nyakati za usiku wakiwa majubmani mwao, ila wakapokea ujumbe mfupi (sms) kwamba kadi namba yako inasihia na.....imetoa pesa kiasi cha shilingi tajwa hapo...kwa kila mmoja wajua ule ujumbe unavyomalizikia kwamba kama hutambua muhamala huu piga simu namba....jamaa huyo Namba 2. 3000,000 pasipo kupoteza muda akapiga simu akawataarifu banki, nao wakamjibu aende kesho katika tawi lililo karibu nae.

Palipo kucha akafanya hivyo banki wakaiblock akaunti yake na wakaprint taarifa fupi ya akaunti ya jamaa, kweli ikaonekana kadi yake imetoa kiasi hicho cha pesa katika moja ya ATM iliyopo Banki House jijini Dar es Salaam.

Maswali ya kujiuliza hapo sasa?
· Kwa nini wote ni watumishi?
· Usalama wa fedha zetu NMB sasa ni wamashaka? tangu wazindua huduma za VISA/MASTERCARD? Japo wakati fulani pesa nyingi za akaunti za NMB ziliibiwa sana na watumisha wa VODACOM kwa huduma ya NMB MOBILE hadi kufikia wateja wa NMB kukataa huduma ya NMB mobile na kisha baaadae VODACOM wakapiga biti kali na kuwachukulia hatua watumishi waliobainika kuhusika na wizi huo.
· Kwa nini Benki House tu imehusika na matukio yote? tena usiku tu?

Baada ya kutoa taarifa benki, wao hadi leo akaunti hizo zimefungwa na kushusu kurudishwa fedha zao wanasema hadi watakapo anza kulipa kwa batch.

Bado na jiuliza je wizi huu unafanyikaje pasipo kufanywa na watumishi wenyewe wa benki ya NMB? Hivyo benki wanawajibu wakujichungiza, sina hakika kama nihujuma ila mashaka yangu ni wale waliozoeapiga pesa kidezo dezo sasa wameamua kujihusisha na uhalifu huo ili tu kuendele piga raound za Heineken kwenye viti virefuu.

Tahadhali!
Wenye akaunti benki zao NMB ni vyema mkafanya uhakiki wa salio lako mara kwa mara, ili kujua kama na wewe hao wasio waaminifu wamekutembele au lah! Au ukahamisha fedha zako katika benki yenye usalama wa hali ya juu.

Kama kuna wengine walioukmbwa na janga hili tushirikiane uzoefu na kupeana taarifa tuweze jua ukubwa watatizo hili!

UPDATES.....
Nimetoka bank NMB kwenda tazama salio langu nimekutana na mtu amepigwa milioni 7 ni pesa alizokopa benki, inaonekana benki walisha zitoa kwenda kwa akaunti husika ila hao wapiga dili wakazichota juu kwa juu kabla ya mwenye mkopo kuuchukua!!

Analia kama mtoto mdogo aisee....wezi muwe na huruma basi kiducho.



Ipo hivi, mtandao wa aina hii ya wizi makao makuu yake yapo Nairobi Kenya chini ya Raia wa Africa Magharibi na raioa wa Kenya! Na Kwa hapa Tanzania, wahusika wakuu walikuwa wanaishi maeneo ya kinondoni nadhani kwa sasa watakuwa kila mahali! Pia raia kutoka Uturuki, ugiriki na Italy na China ni wataalamu mno wa aina hii ya wizi!

Jinsi Wanavyoiba!

1. Wezi hawa hushirikiana na maafisa wa benki husika wa vitengo vya IT, ili wawape information za mteja, ambazo ndio hujazwa kwnye kadi ya ATM. Wafanya kazi wa benk hutoa infromation za wateja katika kwnye karatasi, au kuzipiga picha kwa simu zao na kuzirusha kwa wezi, ambzo hao wezi kwa kutumia kompyuta zao na vifaa maalumu hudurufu kadi nyingine ya ATM kama ya ile ya mteja aliopewa na bank!

kwahiyo mteja X mwnye ATM kadi aliopewa na bank ambaye bahati mbaya taarifa zake zimeenda kwa wezi, basi atambue wezi wana kadi pacha ya ATM kama yake! Namba ya siri ya ATM kadi hao wezi wanajuaje, mara nyingi huwa wanajaribu kuweka mwaka wa kuzaliwa wa muhusika, maana watnzania wengi tunapenda kutumia mwaka wa kuzaliwa kwnye pin zenye digit nne! Pia, kuna baadhi ya benk, kbala ya kupewa ATM kadi yako, wanakuambia ubonyeze kifaa maalumu ili utengeneze pin, sasa kifaa hicho hulazimishwa na watu wa IT wa bank husika kutoa taarifa ya pin yako kwenda kwa wezi!

Hizi ATM kadi zimegawanyika sehemu mbili (kwa ufahamu wangu hadi kipindi hicho), yaani track 1 na track 2, wezi hupendelea sana mteja mwenye kadi ya track 2, ama ni kwavile track 2 inakuwa na hela nyingio au mteja anakuwa natabia ya kutoa hela na kuweka mara kwa mara, sifahamu...naamini humu kuna wataalamu wa bank na IT watatupa ufafanuzi wa Track 1 na Track 2!

2. Namna nyingine wanazoiba taarifa ya ATM ya ili wakatengeneze kadi pacha kama yako, wanakuwa na kifaa maalumu kidgo hivi kama vidole vyako viwili ukivichanganya, kwa ukubwa wake, wanachokifanya ni kuwapa wauzaji wanaouza bidhaa au huduma ambayo malipo yake yanaweza kulipwa kwa kadi ya ATM. Yule muhudumu akifanikiwa kuipitisha kadi yako kwenye kile kifaa, zoezi linakuwa limekamilika!

#Wezi na wizi huu, hauwezi kuwa na mizizi kama hamna watu wa bank husika kutoa taarifa za mteja/wateja kwa wezi ili wakadurufu kadi nyingine, hasa taarifa za track1 na track 2, zile za "<<<<<<<<<<<0081818,"

#njia ya pili, sidhani kama inatumika sana sana!

#watanzania kutokuwa na elimu ya namna ya kutumia ATM amshine, mfano mtuu anakaa mbali na mashine na anatumia kidole kama kudonoa hivi, yaani mtu wa nyuma yako au pembeni anaweza akaona umebonyeza namba zipi!
-unapo tumia ATM, isogelee vyakutosha katika kuhakikisha hata wa nyuma yako haoni unachoandika! LAkini la muhimu zaidi ni kuweka mikono yako yote miwili juu ya ile mashine ili vidole vya mikono yote ndio zibonyeze hizo namba zako za siri!

#epuka kwenda kwanye ATM usiku sana, na kuwa makini na kifaa chchte kipya ambacho hukijui, maana vinakuwa na kazi moja tu ya kurekodi namba yako ya siri!

Mwisho, wezi walikuwa wakilalamika kuwa system za CRDB pekee ndiyo zilikuwa zinawasumbua, maana kwamba ukiingiza kadi doto, inamezwa na hairudi tena!
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Ili kupunguza wizi wa aina hii na ule wakutumia silaha, ambapo wateja wanauwawa!

Bank zote ziweke MARUFUKU zifuatazo;-
1. Wafanya kazi woote wa benki, wapigwe marufuku kuingia kazini na simu. Yaani, kuwe na private rooms (ya wanawake na wanaume) ambapo kila mfanyakazi anapoingia kazini anaenda kuweka simu na vitu vyake kwenye safe yake maalumu ndani ya chumba hicho! Simu zao zirudishwe pale tu anapomaliza kazi, sio anapotoka nje ya jengo la bank hata kama anaenda branch nyingine! Wateja watoe taarifa police au mahali maalumu, wanapomwona mfanyakazi wa bank ndani ya bank ameshika mobile phone!
-itazuia wafanyakazi kutoa taarifa kwa majambazi, pia kutopiga picha taarifa za mteja na kuwarushia wezi!

2.System zote za bank, ziwekwe software maalum itakayozuia mfanyakazi kuchomeka flash au memory card nk!

3. sijui mtazuiaje mfanyakazi asitoke na karatasi yeyote nje ya bank!
 
kunasiku nilikuwa na draw tsh 200000,ikatoka 260,000 then sms ikasema ndugu mteja account yako imetoa tsh 200,000 ,nikahesabu mara mbili mbili naona bado 260000. kuangalia risiti inasoma 200,000
nikaona ngoja nisepe nazo weekend ilikuwa poa sana hiyo.........
 
kunasiku nilikuwa na draw tsh 200000,ikatoka 260,000 then sms ikasema ndugu mteja account yako imetoa tsh 200,000 ,nikahesabu mara mbili mbili naona bado 260000. kuangalia risiti inasoma 200,000
nikaona ngoja nisepe nazo weekend ilikuwa poa sana hiyo.........
Duh hata mashibe hukosea... na wala hawajawahi kukusumbua hao jamaa?!
Una zari kweli aisee!
 
Cash Machine za bongo zote mbovu tu siku zingine naendaga kutoa hela nakuta wakati pale inafunguka ili itoe hela kuna hela zingine nyingi kwa ndani kama mtu una tamaaa unaweza kuzivuta na zile zingine....kwa kutumia kijiti tu....
Bro kamare si itakunyaka ukiichokonoa na ukajikuta matatani labda kama zile CCTV wameziweka kama bosheni tu
 
kunasiku nilikuwa na draw tsh 200000,ikatoka 260,000 then sms ikasema ndugu mteja account yako imetoa tsh 200,000 ,nikahesabu mara mbili mbili naona bado 260000. kuangalia risiti inasoma 200,000
nikaona ngoja nisepe nazo weekend ilikuwa poa sana hiyo.........
Hivi wabongo tuna shida gani? Kwanini mtu anapoelezea habari ya maana lazima atokee limbukeni mmoja aweke hadithi yake ya kujidai ili aonekane zinga la janja kumbe ni limbukeni? Sasa ulichoandika kina uhusiano gani na thread?
 
Hivi wabongo tuna shida gani? Kwanini mtu anapoelezea habari ya maana lazima atokee limbukeni mmoja aweke hadithi yake ya kujidai ili aonekane zinga la janja kumbe ni limbukeni? Sasa ulichoandika kina uhusiano gani na thread?
kwani kuna tatizo dada? tuna share uzoefu
ila sawa nimekuelewa muungwana.
 
Hivi wabongo tuna shida gani? Kwanini mtu anapoelezea habari ya maana lazima atokee limbukeni mmoja aweke hadithi yake ya kujidai ili aonekane zinga la janja kumbe ni limbukeni? Sasa ulichoandika kina uhusiano gani na thread?
Mkuu mimi naona usiangalie tu kilichoandikwa pale mwishoni mwa post ya mchangiaji.

Kwa kuzingatia kwamba mada inahusu upotevu wa fedha za wateja kupitia ATM mchangiaji huyo nae katuletea uzoefu wake kuhusu ATM zinavoweza ku misbehave na kufanya makosa kwenye kutoa fedha kwa mteja. Tena hapo ni bahati kwamba fedha zilikuwa zimezidishwa kwa mteja.

Kwa maana hiyo kuna uwezekano pia mashine hiyo hiyo ikafanya makosa na kumpunja mteja kwa kumpa kiasi pungufu ya alichodhamiria kutoa au kiasi sawa alichodhamiria kutoa lakini wakati huo huo risiti ikisoma kuwa fedha iliyotoka ni kubwa zaidi ya ile aliyopokea kwenye mashine. Na hii inaweza kuwaumiza zaidi wale wateja ambao mara nyingi uamini ATM na kuondoka bila kuhesabu fedha zao walizotoa.

Hivyo binafsi naona nimefaidika na post ya mchangiaji uliyemkosoa.
 
kunasiku nilikuwa na draw tsh 200000,ikatoka 260,000 then sms ikasema ndugu mteja account yako imetoa tsh 200,000 ,nikahesabu mara mbili mbili naona bado 260000. kuangalia risiti inasoma 200,000
nikaona ngoja nisepe nazo weekend ilikuwa poa sana hiyo.........
hahaha
 
kwani kuna tatizo dada? tuna share uzoefu
ila sawa nimekuelewa muungwana.
Na ulimbukeni mwingine wa kibongo bongo nao umekuandama... Kufikiri kumjibu mtu kwa kumwita ''dada'' ni ujanja! Tokeni kwenye ushamba uliwafunika ndugu zangu, dunia kubwa hii.
 
Mkuu mimi naona usiangalie tu kilichoandikwa pale mwishoni mwa post ya mchangiaji.

Kwa kuzingatia kwamba mada inahusu upotevu wa fedha za wateja kupitia ATM mchangiaji huyo nae katuletea uzoefu wake kuhusu ATM zinavoweza ku misbehave na kufanya makosa kwenye kutoa fedha kwa mteja. Tena hapo ni bahati kwamba fedha zilikuwa zimezidishwa kwa mteja.

Kwa maana hiyo kuna uwezekano pia mashine hiyo hiyo ikafanya makosa na kumpunja mteja kwa kumpa kiasi pungufu ya alichodhamiria kutoa au kiasi sawa alichodhamiria kutoa lakini wakati huo huo risiti ikisoma kuwa fedha iliyotoka ni kubwa zaidi ya ile aliyopokea kwenye mashine. Na hii inaweza kuwaumiza zaidi wale wateja ambao mara nyingi uamini ATM na kuondoka bila kuhesabu fedha zao walizotoa.

Hivyo binafsi naona nimefaidika na post ya mchangiaji uliyemkosoa.
Umefaidika vipi?
 
Back
Top Bottom