CRDB Bank ya hovyo kabisa

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Apr 12, 2018
2,499
4,211
Habari za asubuhi,

Moja kwa moja niende kwenye mada kuhoji uendeshaji wa hii bank maana huenda wahusika wameshaikatia tamaa maana malalamiko ya wateja yamekuwepo kwa muda mrefu lakini hakuna hatua zinazochukuliwa zaidi ya kuongeza huduma zisizo na msingi kila kukicha. baadhi ya kero zake ni kama zifuatazo.

1: Kuchukua muda mrefu kufungua account
Hivi kweli kwenye zama hizi za ushindani wa kibiashara na teknolojia kama Mpesa, TigoPesa, AirtelMoney e.t.c unawezaje kumwambia mteja nenda urudi baada ya siku saba?

2: SimBanking USSD menu
Hapa ndio balaa! yaani kwanza mpaka uweze kupata hii huduma utaambiwa nenda uje wiki ijayo! Kasheshe inaanzia pale unapotaka kupata huduma kwa njia ya simu kwa kubonyeza *150*03# unaambiwa muamala haujakamilika! Yaani Account ni yangu na pesa ni zangu lakini kupata taarifa zake mpaka niwe na salio kwenye simu! Upuuzi mkubwa! Sasa hiyo SimBanking ina maana gani? Mbaya zaidi miamala inayofanyika kwenye ATM hautumiwi taarifa zozote kwamba kuna kiasi fulani cha pesa kimetolewa! Je kama ni wizi unafanyika? Kwa kifupi SimBanking is a crap service.

3: Kupata kadi ya ATM
Hapa ni tatizo kubwa! Yaani utaambiwa nenda urudi wiki ijayo! Kweli kwenye karne hii ambapo ID zinakuwa printed papo hapo unamwambia mteja ondoka urudi siku fulani? Najua kuna issue za security lakini ndio mchukue wiki tatu kutengeneza kadi?

Kama ni security kwanini isitumike biometrics tu kama finger prints hata kwenye atm kurahisisha mambo na kuongeza usalama?

N:B CRDB msipojirekebisha mtapoteza wateja wengi sana
 
Mkuu kwanza pole maana wanakupotezea time yako. Labda nikuulize ni wapi huko unaambiwa kupata kadi ya Crdb baada ya wiki. Miaka kama miwili hivi nilifungua Account Crdb nilikamilisha kila kitu ndani ya kama saa 2 tu. Kuanzia kujaza fomu, kupiga picha, kupata bank card na hadi simbanking hapa Arusha.

Hiyo Branch ya Crdb wazembe sana huwezi subiri wiki moja kwa kitu simple kama hicho. Inabidi wabadilike.
 
Hilo la kufungua account na ATM Card mbona hata NMB ndio hivyo hivyo baada ya wiki, inategemea na account unayofungua Kuna unazopewa hapo hapo na nyingine zinachukua muda

NMB mobile nao Ni mpaka uwe na hela ya vocha kwenye simu na wanaikata
Na wanaikata kwelikweli! Yaani ukiweka 1000 ukiingia tu simbanking inaisha! Kuendelea inabidi uongeze salio! Kama ni makato ya kupata huduma kwanini wasikate moja kwa moja kwenye salio bank kama wafanyavyo mitandao ya simu?
 
Hilo la kufungua account na ATM Card mbona hata NMB ndio hivyo hivyo baada ya wiki, inategemea na account unayofungua Kuna unazopewa hapo hapo na nyingine zinachukua muda

NMB mobile nao Ni mpaka uwe na hela ya vocha kwenye simu na wanaikata
Ila kuna mitandao ya simu kama tigo unaweza kutumia ATM mobile bila ya kuwa na salio.
Vodacom ndio kinyaa! Hadi uwe na salio
 
Mkuu kwanza pole maana wanakupotezea time yako. Labda nikuulize ni wapi huko unaambiwa kupata kadi ya Crdb baada ya wiki. Miaka kama miwili hivi nilifungua Account Crdb nilikamilisha kila kitu ndani ya kama saa 2 tu. Kuanzia kujaza fomu, kupiga picha, kupata bank card na hadi simbanking hapa Arusha.

Hiyo Branch ya Crdb wazembe sana huwezi subiri wiki moja kwa kitu simple kama hicho. Inabidi wabadilike.
Mkuu ni tawi la mjini kabisa CRDB vijana branch pale Lumumba!
 
Kikuweli Crdb sio ile ya miaka mitatu iliyopita, credibility yao inashuka kwa kasi wajiangalie

Nimekuwa mteja wao kwa miaka mingi ila naanza kupata wazo la kuwahama
Kwa hili tunafanana mawazo. Kila siku natafakari hilo halafu sauti inaniambia "ACHANA NAO". Siwaelewi CRDB siku Hizi. Kilichobaki kwa sasa ni siku ya KUKATA SHAURI tu.
 
Ila wabongo vichwa ugoro sana.

Malalamiko na kujilizaliza kama kunguru.

Hivi Nchi hii kuna Bank moja ?

Uteswe Na Monopoly CCM, Magufuli, TANESCO, ATCL, NSSF/PSSF, MWENDOKASI KIMARA halafu uteswe tena na pesa zako mwenyewe ?

Pumbavv Sana.

Mimi hata duka la mangi/muha/mpemba huwa silalamiki, nikifika dukani kama hueleweki naenda kwingine.

Mteja Siyo Mimi Peke Yangu, Na Huna Duka Peke Yako Hapa Mtaani.

Bank ndio kabisaa, nilianza na NMB wakaniletea uswahili nikahamia EQUITY, Naona wakileta upupu nahamia STANBIC.

Staki stress uchwara wakati nina mambo mengi productive ya kuumiza kichwa changu.

Na Ninyi ndio mnaosababisha hali hiyo ya wao kubweteka, kama wanawapa huduma mbovu na bado mpo tu mnalialia kama mazwazwa ndio ndio hawaoni sababu ya kuboresha.
 
Mkuu kwanza pole maana wanakupotezea time yako. Labda nikuulize ni wapi huko unaambiwa kupata kadi ya Crdb baada ya wiki. Miaka kama miwili hivi nilifungua Account Crdb nilikamilisha kila kitu ndani ya kama saa 2 tu. Kuanzia kujaza fomu, kupiga picha, kupata bank card na hadi simbanking hapa Arusha.

Hiyo Branch ya Crdb wazembe sana huwezi subiri wiki moja kwa kitu simple kama hicho. Inabidi wabadilike.
Azikiwe kwenye hupati card mda huo huo.. labda kama wameanza hivi karibuni
 
Na wanaikata kwelikweli! Yaani ukiweka 1000 ukiingia tu simbanking inaisha! Kuendelea inabidi uongeze salio! Kama ni makato ya kupata huduma kwanini wasikate moja kwa moja kwenye salio bank kama wafanyavyo mitandao ya simu?
Hawa wezi wanakata kote kote.. chunguza tu utaona.. kama unatumia USSD wanalamba salio na wanalamba kwa account .. na kama unaangalia kwa app wanalamba kwenye account kitu ambacho ABSA hawafanyi
 
Ila wabongo vichwa ugoro sana.

Malalamiko na kujilizaliza kama kunguru.

Hivi Nchi hii kuna Bank moja ?

Uteswe Na Monopoly CCM, Magufuli, TANESCO, ATCL, NSSF/PSSF, MWENDOKASI KIMARA halafu uteswe tena na pesa zako mwenyewe ?

Pumbavv Sana.

Mimi hata duka la mangi/muha/mpemba huwa silalamiki, nikifika dukani kama hueleweki naenda kwingine.

Mteja Siyo Mimi Peke Yangu, Na Huna Duka Peke Yako Hapa Mtaani.

Bank ndio kabisaa, nilianza na NMB wakaniletea uswahili nikahamia EQUITY, Naona wakileta upupu nahamia STANBIC.

Staki stress uchwara wakati nina mambo mengi productive ya kuumiza kichwa changu.

Na Ninyi ndio mnaosababisha hali hiyo ya wao kubweteka, kama wanawapa huduma mbovu na bado mpo tu mnalialia kama mazwazwa ndio ndio hawaoni sababu ya kuboresha.


🤣🤣🤣🙌🙌Jamaa umenyooka Kama rula..sipatii picha Kama una mke! Nimecheka sana
 
Back
Top Bottom