CRDB Bank ya hovyo kabisa

CRDB Bank ya hovyo kabisa

Hahaha wabongo bana nchi hii Kuna Best International Bank zenye huduma za kimataifa ila mtu unang'ang'ania na hizo bank za hovyo.

Unashangaa mtu anakwambia eti hizo bank Zina matawi mengi ya ATM wakati hajui kila bank Sasa hivi hata wakiwa na ATM moja nchi nzima unaweza kutoa hela koKote Tanzania ( Maendeleo ya sayansi na teknolojia)...


Kutafuta hela iwe shida na huduma iwe shida , hell No.
 
Ila wabongo vichwa ugoro sana.

Malalamiko na kujilizaliza kama kunguru.

Hivi Nchi hii kuna Bank moja ?

Uteswe Na Monopoly CCM, Magufuli, TANESCO, ATCL, NSSF/PSSF, MWENDOKASI KIMARA halafu uteswe tena na pesa zako mwenyewe ?

Pumbavv Sana.

Mimi hata duka la mangi/muha/mpemba huwa silalamiki, nikifika dukani kama hueleweki naenda kwingine.

Mteja Siyo Mimi Peke Yangu, Na Huna Duka Peke Yako Hapa Mtaani.

Bank ndio kabisaa, nilianza na NMB wakaniletea uswahili nikahamia EQUITY, Naona wakileta upupu nahamia STANBIC.

Staki stress uchwara wakati nina mambo mengi productive ya kuumiza kichwa changu.

Na Ninyi ndio mnaosababisha hali hiyo ya wao kubweteka, kama wanawapa huduma mbovu na bado mpo tu mnalialia kama mazwazwa ndio ndio hawaoni sababu ya kuboresha.


Nimecheka Sana
 
Habari za asubuhi,

Moja kwa moja niende kwenye mada kuhoji uendeshaji wa hii bank maana huenda wahusika wameshaikatia tamaa maana malalamiko ya wateja yamekuwepo kwa muda mrefu lakini hakuna hatua zinazochukuliwa zaidi ya kuongeza huduma zisizo na msingi kila kukicha. baadhi ya kero zake ni kama zifuatazo.

1: Kuchukua muda mrefu kufungua account
Hivi kweli kwenye zama hizi za ushindani wa kibiashara na teknolojia kama Mpesa, TigoPesa, AirtelMoney e.t.c unawezaje kumwambia mteja nenda urudi baada ya siku saba?

2: SimBanking USSD menu
Hapa ndio balaa! yaani kwanza mpaka uweze kupata hii huduma utaambiwa nenda uje wiki ijayo! Kasheshe inaanzia pale unapotaka kupata huduma kwa njia ya simu kwa kubonyeza *150*03# unaambiwa muamala haujakamilika! Yaani Account ni yangu na pesa ni zangu lakini kupata taarifa zake mpaka niwe na salio kwenye simu! Upuuzi mkubwa! Sasa hiyo SimBanking ina maana gani? Mbaya zaidi miamala inayofanyika kwenye ATM hautumiwi taarifa zozote kwamba kuna kiasi fulani cha pesa kimetolewa! Je kama ni wizi unafanyika? Kwa kifupi SimBanking is a crap service.

3: Kupata kadi ya ATM
Hapa ni tatizo kubwa! Yaani utaambiwa nenda urudi wiki ijayo! Kweli kwenye karne hii ambapo ID zinakuwa printed papo hapo unamwambia mteja ondoka urudi siku fulani? Najua kuna issue za security lakini ndio mchukue wiki tatu kutengeneza kadi?

Kama ni security kwanini isitumike biometrics tu kama finger prints hata kwenye atm kurahisisha mambo na kuongeza usalama?

N:B CRDB msipojirekebisha mtapoteza wateja wengi sana
Umejuwa leo? Rahisi ghali
 
🤣🤣🤣🙌🙌Jamaa umenyooka Kama rula..sipatii picha Kama una mke! Nimecheka sana

Watu wa aina hii wakiwa nyumbani unakuta kila siku wanavutwa tu masikio na hao wake zao!

Ila wakiwa humu jukwaani ni kutunanga tu Watanzania hatuna akili, sijui sisi Watanzania ni mazwazwa! as if yeye si Mtanzania au hakumbani na changamoto zozote kwenye maisha yake ya kila siku.
 
Na wanaikata kwelikweli! Yaani ukiweka 1000 ukiingia tu simbanking inaisha! Kuendelea inabidi uongeze salio! Kama ni makato ya kupata huduma kwanini wasikate moja kwa moja kwenye salio bank kama wafanyavyo mitandao ya simu?
Nmb? Mbona nimetoka kuuliza salio langu now ila sijakatwa na kwanza Sina salio kwenye simu?
 
Sema kuna vitu umechanganya Naona kama tunawasingizia sana.

1. Kuhusu kufungua akaunti, kwa benki ya CRDB ime improve kwa kiasi kikubwa

a) unafungua akaunti kwa mawakala sio lazima ufike bank.
b) unafungua akaunti kwa namba ya NIDA sio lazima uwe na kitambulisho wala picha .

2. Kuhusu swala la simbanking
Bila Shaka mtoa mada ni mtumiaji wa mtandao wa Vodacom Mimi nlikuwa natumia simbanking kwenye huo mtandao nkaambiwa kuna vocha natakiwa niwe nayo kila nkitumia simbanking nkahamisha huduma kwenda kwenye mtandao mwingine. So kwa hili CRDB hawahusiki ni nje ya uwezo wao.

3. Swala la Kadi kuchukua muda mrefu, hii inategemea ni kwenye upande gan, nachojua mm ni akaunti mpya zote huwa na kadi papo kwa papo labda tu uombe card special kama credit card, visagold etc.

Ikiwa ni swala la Kadi zilizo expire haribika au kupotea je utailaumu vp benk kwa kutokuwa na kadi yako ready wakat haijui kuwa utapoteza Kadi au kuibiwa au uta renew kadi kwa wakati.

Nlidhani tungelamikia mengine ila kwa haya yalioripotiwa yote Naona benki haina chakujibu hapo.

Nawaslisha.
 
Hilo la kufungua account na ATM Card mbona hata NMB ndio hivyo hivyo baada ya wiki, inategemea na account unayofungua Kuna unazopewa hapo hapo na nyingine zinachukua muda

NMB mobile nao Ni mpaka uwe na hela ya vocha kwenye simu na wanaikata
Nmb mkononi ndio sulihisho. Unatumia data kuangalia salio na kufanya transactions.

Ila nmb juzi ilikua kidogo wanicheleweshee safari. Nimekata tiketi ya ndege muda unaenda kuisha nilipie kwa bank hakuna mtandao. Kwenda kwenye atm hakuna mtandao, isingekua nina pesa bank nyingine ningeachwa na ndege halafu ningepoteza deal ya maana sana.

Hizi bank zetu sio za kuamini. Unapaswa kuchukua cash ukawa nayo nyumbani ama hata mpesa. Haziaminiki kwenye mtandao unaweza kupata shida na hela unazo.
 
Mkuu kwanza pole maana wanakupotezea time yako. Labda nikuulize ni wapi huko unaambiwa kupata kadi ya Crdb baada ya wiki. Miaka kama miwili hivi nilifungua Account Crdb nilikamilisha kila kitu ndani ya kama saa 2 tu. Kuanzia kujaza fomu, kupiga picha, kupata bank card na hadi simbanking hapa Arusha.

Hiyo Branch ya Crdb wazembe sana huwezi subiri wiki moja kwa kitu simple kama hicho. Inabidi wabadilike.
Mi mwaka huu nilifika branch flan saa nane paka saa kumi nilikuwa nishapata kadi pamoja na sim banking.


Tena sim banking niliunganishwa na mwanafunz wa field alikuwa pale.
 
Hilo la kufungua account na ATM Card mbona hata NMB ndio hivyo hivyo baada ya wiki, inategemea na account unayofungua Kuna unazopewa hapo hapo na nyingine zinachukua muda

NMB mobile nao Ni mpaka uwe na hela ya vocha kwenye simu na wanaikata

Two wrongs don't make a right.
 
Mkuu kwanza pole maana wanakupotezea time yako. Labda nikuulize ni wapi huko unaambiwa kupata kadi ya Crdb baada ya wiki. Miaka kama miwili hivi nilifungua Account Crdb nilikamilisha kila kitu ndani ya kama saa 2 tu. Kuanzia kujaza fomu, kupiga picha, kupata bank card na hadi simbanking hapa Arusha.

Hiyo Branch ya Crdb wazembe sana huwezi subiri wiki moja kwa kitu simple kama hicho. Inabidi wabadilike.
Acha upuuzi wewe, unasifia kila kitu wewe ni mwana CCM? Hao CRDB wana miezi kadhaa sasa wamekwama kutoa kadi kwa wateja. Usichangie vitu usivyovijua. Pumbavu.
 
Acha upuuzi wewe, unasifia kila kitu wewe ni mwana CCM? Hao CRDB wana miezi kadhaa sasa wamekwama kutoa kadi kwa wateja. Usichangie vitu usivyovijua. Pumbavu.
Sio kweli, sema Kadi yako ipo tawi gani na hujapata Kadi?! Mimi nliomba Kadi dar wiki moja hv nkaomba Kadi yangu itumwe mbeya na ikatumwa.
 
Habari za asubuhi,

Moja kwa moja niende kwenye mada kuhoji uendeshaji wa hii bank maana huenda wahusika wameshaikatia tamaa maana malalamiko ya wateja yamekuwepo kwa muda mrefu lakini hakuna hatua zinazochukuliwa zaidi ya kuongeza huduma zisizo na msingi kila kukicha. baadhi ya kero zake ni kama zifuatazo.

1: Kuchukua muda mrefu kufungua account
Hivi kweli kwenye zama hizi za ushindani wa kibiashara na teknolojia kama Mpesa, TigoPesa, AirtelMoney e.t.c unawezaje kumwambia mteja nenda urudi baada ya siku saba?

2: SimBanking USSD menu
Hapa ndio balaa! yaani kwanza mpaka uweze kupata hii huduma utaambiwa nenda uje wiki ijayo! Kasheshe inaanzia pale unapotaka kupata huduma kwa njia ya simu kwa kubonyeza *150*03# unaambiwa muamala haujakamilika! Yaani Account ni yangu na pesa ni zangu lakini kupata taarifa zake mpaka niwe na salio kwenye simu! Upuuzi mkubwa! Sasa hiyo SimBanking ina maana gani? Mbaya zaidi miamala inayofanyika kwenye ATM hautumiwi taarifa zozote kwamba kuna kiasi fulani cha pesa kimetolewa! Je kama ni wizi unafanyika? Kwa kifupi SimBanking is a crap service.

3: Kupata kadi ya ATM
Hapa ni tatizo kubwa! Yaani utaambiwa nenda urudi wiki ijayo! Kweli kwenye karne hii ambapo ID zinakuwa printed papo hapo unamwambia mteja ondoka urudi siku fulani? Najua kuna issue za security lakini ndio mchukue wiki tatu kutengeneza kadi?

Kama ni security kwanini isitumike biometrics tu kama finger prints hata kwenye atm kurahisisha mambo na kuongeza usalama?

N:B CRDB msipojirekebisha mtapoteza wateja wengi sana
Shida kubwa iko CRDB tawi la kibaha.Ikitokea kadi ikamezwa kwenya A TM Kama ni jumamosi utaipata Jumatano.Wahudumu hawako kikazi ,komputer anadonoa keybody,mara anatoka anaenda kutafuta kitabu mara meza hili mara meza ile.Yaan kero tupu.CRDB Kibaha ndo pa hovyo zaidi.
 
Sio kweli, sema Kadi yako ipo tawi gani na hujapata Kadi?! Mimi nliomba Kadi dar wiki moja hv nkaomba Kadi yangu itumwe mbeya na ikatumwa.
We Mpuuzi, wewe ni mteja pekee wa CRDB nchi nzima?
 
Watu wa aina hii wakiwa nyumbani unakuta kila siku wanavutwa tu masikio na hao wake zao!

Ila wakiwa humu jukwaani ni kutunanga tu Watanzania hatuna akili, sijui sisi Watanzania ni mazwazwa! as if yeye si Mtanzania au hakumbani na changamoto zozote kwenye maisha yake ya kila siku.
Watu wa aina hii wakiwa nyumbani unakuta kila siku wanavutwa tu masikio na hao wake zao!

Ila wakiwa humu jukwaani ni kutunanga tu Watanzania hatuna akili, sijui sisi Watanzania ni mazwazwa! as if yeye si Mtanzania au hakumbani na changamoto zozote kwenye maisha yake ya kila siku.
Mkuu Relax.

Mimi kuwa mtanzania hakunifanyi nisiseme ukweli.

Sijaoa, ishtoshe mimi siyo wa kufuatilia sana vitu vidogo vidogo na wala sipendi kumwonea wala kumdharau mtu.

Ila sipendi kabisa watu wanaposhindwa kuchukua maamuzi kwenye mambo yaliyo wazi kabisa.

Imagine,

Mkihama kama 200, watarekebisha wenyewe bila kuuliza
 
Back
Top Bottom