Tatizo ni kwamba serikali yetu tukufu haitoi taarifa za mara kwa mara kuhusu hali ya janga hili. Kwa sababu hii, tusiwalaumu raia kubishana kwa kuwepo au kutokuwepo Corona. Hakuna mwenye uhakika. Wale wanaoamini kuwa ugonwa upo waendelee kuchukua tahadhari. Wale wasioamini waendelee kujirusha bila ya tahadhari wala PPE. Hatimaye na kwa mazingira haya, anaye faidika ni yule anayeamini gonjwa lipo kwa sababu kama lipo amejikinga, na kama halipo basi hapotezi kitu. Kwa hiyo anayepoteza (mjinga) ni yule anayeamini kuwa gonjwa halipo.