Nimerudi tena na kupata moyo sana toka kwa wachangiaji kwamba kweli tunamtafuta mungu aliye hai. Kuna watu wameulize humu maswali ambayo hayajajibiwa kwa ufasaha. Kwa uzoefu wangu yawezekana wengine wana taarifa tofauti wazijaze hapa, source yangu ni experience yangu mwenyewe. Garama ya malazi kwa siku 5 mpaka 7 kule ndani scoan ikiwemo chakula milo mitatu, malazi ya ku share double deka vyumba visafi vyenye maji y akutosha, toilet papers na pengine sabuni, chakula kizuri tu na kingi, chai na mikate wakati wowote, na kule ndani kuna duka linalouza vinywaji, na vitafunio kama unataka, lakini kule eneo la congregation kuna restaurants za kumwaga. Hivi vyote havizidi us $ 600 - 800. Nauli kwa kupitia kwa madame Martha ni garama za kawaida za Ethiopia Airline. Visa ya Nigeria ni T.shs 100,000 garama official maana mimi ninatumia sana kwa kuwa nina consultancy ya muda mrefu Abuja naenda mara kwa mara na kurudi. Kwa hiyo unaweza ukalipa kati ya dola 1600 na 1800, Kwa hiyo kwa kuwa ananunua ticket kwa wingi anapata viti mbalimbali vyenye bei mbali mbali kwa hiyo anakupa rebate. Of course swala la agent anayemtumia ni kituko manake mnaweza kwenda huko kurudi mkaambiwa hamna confirmation na yeye bila haya wala aibu akajipakia yeye na yule mtoto wake wa kiume na wapambe wake wakaondoka na kuwaacha huko Lagos, Huyo ndio Madame Martha Kaaya.
Sasa kule ndani kuna alternative, kwenye wale wanaotaka private rooms kwa mwaka jana ilikua ni US$4000 kwa private room. Sasa hii sijui kama ni inclusive of nauli ya ndege kama unavyoona if it is so then it not bad baada mnakua kama vile mnalipa 200 -300 dollars per person from the average of the cost of those of us who stay in the dormitories.
Why do we need to go through the coordinator: inarahisisha sana huduma kwa wasafiri na hata kwa watoa huduma kule scoan, they pick you from the airport and therefore organise transportation for you, huhitaji kuzubaa zubaa na kutapeliwa na majambazi wa Nigeria, its safe and very descent. They organise escort ya polisi hivyo hamkumbwi na ile foleni ya kufa mtu ya jiji la lagos kwa kuwa mnakuta police wameweka blockages njia yenu na kusafirishwa kwa vin'gora. Given the challenge ya religious intolerance in Nigeria it is a very good option. Of course tatizo lake hakuna privacy kama wewe unaonea aibu hitaji lako. But this should not bother you kwa kuwa believe you me, kila aendaye huko anahitaji lake, yawezekana kabisa ukaona lako ni la aibu zaidi lakini kumbuka, mungu hakuonei aibu kwa kuwa all ungodly conducts ikiwemo aibu zetu ni kazi ya shetani. I have been to the scoan and have seen the living god in my life, Natamani ndugu zangu nyie, kaka na dada zangu, watanzania wenzangu wote mpate nafasi ya kwenda ili muwe huru. Pia kuna wanaowasiliana nae kwa facebook, kuna school mate wangu amepata baraka hiyo amewasiliana nae directly kwa facebook mara tatu na akamuonyesha siri ya haja ya moyo wake.
Sasa mungu atusamehe kwa kuwalalamikia wenzetu, Ni vizuri pia tujipime kwa mizani ya macho, na kuwaombe hawa wenzetu, kwa maana yawezekana Martha na kundi lake wanatuona sisi walalahoi, lakini bado tukawa rafiki za mungu, maana neno la mungu si kama uchawe ama charm, eti kwa sababu Blandina Nyoni yuko jikoni ndio shutuma zake juu ya ufisadi huku akiendelea kutumia gari la serikali na mafuta ya serikali hadi leo, havijalishi. Naamini hata Madame mwenyewe madhali anafanya haya yasiyoya kimungu, manake kiburi si cha bwana, basi na yeye amefunikwa na ukungu usio wa kitakatifu. Sisi pia mungu atusamehe maana tumehukumu, na wao pia mungu awasamehe ili wafanye yaliyo sawa. Lakini la kuandika kwa TB Joshua juu ya huu uhuni liko pale pape, maana imeandikwa ya kwamba tutahukumiwa sawasawa na matendo yetu. Mimi tayari tangu asubuhi nimeshatuma email 10 kwenda scoan. Simu ntaanza kupiga jumanne kwa sababu leo wako kwenye misa, tusiogope jamani.