Dini za siku hizi balaaa, huwa nacheka sana matangazo ya dini siku hizi, utasikia Je umezidiwa na madeni? Njoo mlima wa moto/baraka ili ufunguliwe, anayekudai ikikuona tu hakudai tena, sasa hii ni dini au wizi? dawa ya deni ni kulipa tu sio kukwepa
Wewe Tabby haya maneno yanakuuma. una kiburi na umefilisika km unadhani unatoa huduma bora. na question kiwango chako cha kiroho. umeomba leo asubuhi?
Mimi pia sikupenda huduma zenu na aliyenituma nikamwambia aende mwenyewe ofisini kwenu. shame on you maana mnamuaibisha TB Joshua. badilikeni.
Moja ya watu ambao ni wagumu kuamini uwezo wa Mungu na kazi zake ni mafarisayo, japokuwa walikuwa na elimu za juu za sheria ya torati ya Musa na pamoja na kuwa na shuhuda zilizotikisa dunia mfano ushuhuda wa bahari ya shamu Mungu alipowavusha lakin bado waliendelea kuwa na mioyo migumu na ndio hao walipelekea Mungu akawazungusha jangwani wana wa Israel pia ni hao hao waliokuwa kkwazo na wapinzani kwa Bwana Yesu.
So hata ww mfarisayo siwezi kukushangaa lakini Biblia inasema ktk kitabu cha 2nyakati.." Mwaminini Mungu ndivyo mtakavyothibitika, Waaminin Manabii zake na ndivyo mtakavyofanikiwa"
päiva;6435571 said:Njia nyingine ya kwenda SCOAN ni kufuata maelekezo yaliyoko kwenye website yao wala huhitaji kupitia kwa mtu. Nimeshafanya hivyo mara tatu na kufanikiwa. Ubarikiwe sana.
Hivi mkuu zile anointing water and stickers zinapatikana wapi kwa hapa Tz and kama hazipatikani ni jinsi gan ya kuzipata.
Watumishi wa Mungu ni wanyenyekevu. Yesu alinyenyekea hata mauti. Kwa kifupi Tabby nikifanya summary ya maneno yako unasema...
Kelele za mlango hazimzuii mwenye nyumba kulala...au
Usipokuja wewe watakuja wengine...
Yani kwa heshima aliyokuwa nayo TB you dont deserve to be even the last person on the line serving on his behalf. Hapi ndiyo utaona tofauti ya kufanya huduma kama huduma au kazi kama kazi.
Pole sana.
Naamini sana Neno la Mungu ila siwaamini makanjanja wa kufanya ishara, tatizo kizazi cha sasa kinahangaika kutafuta Ishara badala ya kuamini neno.
Hivi ni Mungu gani huyo anayetenda Miujiza Nigeria tu? Mbona Nigeria yenyewe haipo Shwari?
Zinapatikana ofisi za scoan,posta mpya,jengo la benjamin william mkapa...na hyo coordinator anaelalamikiwa hapa ndo unamuona hapo
Mkuu huenda unaamini sana Neno la Mungu lakin somehow hulisomi thus why inakuwa vigumu kufumbua hata mafumbo mbalimbali ambayo majibu yake yanapatikana ktk neno, Ukisoma kitabu cha 2wafalme utaona ni jinsi gani nabii Elisha alivyokuwa akitenda miujiza kwa nguvu za Mungu hadi kupelekea mataifa mbalimbali kwenda samaria kumfuata, Pia hata mataifa yalitoka sehemu za mbali kufuata hekima ya Mfalme suleiman.
So sio ajabu watu kwenda Nigeria kwa Tb Joshua kwani ndio karama aliyopewa na Mungu na ujue kuwa karama kama hizi ni za wachache na huwa hazigawiwi na Mungu kama njugu bali ni kwa wateule wake wachache aliyowachagua yeye.
Yana mwisho haya, Kakobe alivuma weeee sasa kimya
umeongea ukweli wako na ndio mwisho wa akili zako kufikiria (etc).
No wonder you are a great thinker!
This explains why tourist hotels in tanzania are employing managers from kenya, while we have thousand of the so called "managers".
Wanaepuka kuchujua watu wenye mentality kama yako.
Shame on us tanzanians
Yana mwisho haya, Kakobe alivuma weeee sasa kimya
Hii ni Nyumba ndogo ya TB
Anointing water na sticker vinapayikana pale Benjamini Mkapa. Ila unahitaji kuwa na moyo waziada ili kuvipata. Huyu mtu anaye itwa Martha kweli anachokifanya pale sio kizuri kabisa. Anataka kuwa Mungu mtu hapa duniani, anataka kufanya iwe bila yeye huwezi fika SCOAN. Ana manyanyaso sana. Nilikwenda pale na hela mkononi akanizunguusha siku mbili na hakuniuzia maji. Kwanza anajibu mabaya sana na hata heshima hana. Mimi nadhani anahitaji kuombewa ili aweze kufanya hiyo kazi.