Monetary policy kwa lugha yetu inamaana ni sera ya fedha, kwa maana ya matendo ya banki kuu katika kuongeza au kupunguza ujazi wa fedha au money supply.
Kwahiyo hii sera ya fedha inaweza kuwa contractionary pale ambapo benki kuu ina nia ya dhati ya kupunguza ujazi wa fedha sokoni, ili kuleta uwiano katika uhitaji wa fedha na shughuli za uzalishaji.
Kwakuwa sote tunaju kwamba kma fedha zitakuwa nyingi zaidi ya shughuli za uchumi basi hii husababisha kuwepo kwa mfumuko wa bei au inflation.
Sasa kinyume cha contrationary monetary policy ndio tunaona expansionary monetary policy, ambapo hapa sasa banki kuu inakuwa na nia ya kuongeza fedha kwenye uchumi kwa makusudi kabisa.
Ilihali, fiscal policies hizi sera za mapato na matumizi kwa serikali kuu. Ambazo zinaweza pia kulenga matumizi ya serikali kwenye uchumi ikiwa ni pamoja na matumizi ya kimaendeleo au development expenditures, lakini pia sera za ukusanyaji wa kodi nchin.