Mkuu bila shaka una hoja nzuri sana na kusema kweli ilikuwa akilini mwangu muda wote. Ila sintofikia kusema shame on them kwa sababu ndicho walichokitaka wao na wakatazama maswala mazima kisiasa na sio raia wananchi wa Tanzania...ccm wao hawataki katiba mpya lakini wanatuhadaa ya kuwa hapo ndipo roho yao inapodundia........................
chadema wanaikosoa ccm (rightly so) kuwa mchakato uliopitishwa kuwa sheria ni marekebisho ya 15 ya katiba iliyopo....................kwa maana ya viraka..............lakini la ajabu ufumbuzi wa chadema ni demokrasia ya vyama vya siasa na wala siyo demokrasia ya watanzania wote wenye vyama na tusiyo na vyama..................................mfano tu kwenye swala la tume chadema wanataka wao nao warudie kosa la jk la kuteua wajumbe wawili.........................kama jk hawezi kuteua wajumbe wa tume basi na chadema nao hawana uwezo wa kuteua hata mjumbe mmoja..........................well, chadema ought to face it that two wrongs can never be righted by anyway.........including colluding with ccm in a conspiratorial arrangements.........
kero ya chadema ni kuwa ccm mbona wanataka kula pekee yao na wao ndiyo chama kikuu cha upinzani hapa nchini?
nonsense..........tume ya kukusanya maoni ni haramu kwa sababu haikutoa fursa sawa kwa watanzania wote katika kushiriki katika kuiunda na wala siyo kwa sababu chadema hawakupewa nafasi nzuri wapange safu za ulaji ndani ya tume kama ccm inavyokusudia kuwazawadia akina profesa palamagamba na wengineo kwa kutetea dhuluma ya ccm ndani ya wanyonge wa kitanzania.....................kumbuk mgombea binafsi pamoja na mambo mengineyo.............
kwa hiyo ccm na chadema wote wapo nje ya mstari kwa kutetea masilahi yao na wala siyo masilahi ya taifa...........................shame on both of them..................
hapa ndipo wengi wa hawa viongozi wetu wanashindwa kutazama kwamba wao kabla ya kuwa viongozi ni raia na wananchi wa nchi hii hivyo walitazame swala hili kwa jicho la Utanzania na sio vyama. Na kama wataendelea kulitazama swala hili kwa rangi zao kamwe hawawezi kupata suluhu kwa sababu hii ni hatua ya pili mahala ambapo tume itakusanya hoja za makundi ya kijamii na asasi zetu ndipo vyama na makundi mengineyo yanapotakiwa kuwakilisha maoni yao..lakini sii mwanzo huu tuloanza nao hata kidogo, rais anasema yupo tayari kupokea mawazo ya watu wakati wowote kabla ya sheria hii irudi bungeni, sasa wapi wananchi wapeleke hoja zao, nani anashughulika na upokeaji wa mawazo haya haisemwi..Haya Je, kama tutasema hatutaki yeye achague tume, hivi kweli kwenda bungeni hiyo January, kipande hicho kitakuwepo?..
Tunataka Baraza la Mapinduzi liguswe kwa sababu sasa hivi Mapinduzi ya Zanzibar ni swala la Muungano na serikali ya jamhuri inatambua mapinduzi yale na itayalinda sii tenba jukumu la CCM..maana TANU ilipoungana na ASP walichukua jina la Chama Cha MAPINDUZI, hiyo mapinduzi wakijumuisha na hilo baraza la Mapinduzi ambalo leo ktk nchi ya demokrasia jukumu hilo sii la CCM tena bali la Jamhuri..
Lakini maadam sheria imeshapita, hoja hii kweli itaweza kupokelewa na kubadilishwa? maana twende mbele turudi nyuma.. Rais wetu hana title ya ceremonial bali anafungamana na chama, ndiye ni Mwenyekiti wa CCM, rais aloshika dola, Makamu wake ni mjumbe NEC - CCM na baraza la Mapinduzi, Rais wa Zanzibar vile vile mwanaCCM na Baraza la Mapinduzi sasa kweli ushauri huu utakuwa kwa malengo yapi ya Utaifa?...Na imefikia vipi hadi maswala yote yaliyosemekana yasiguswe ni ndiyo yapo ktk mwongozo wa CCM..Hivi kweli tunapounda katiba ya Taifa kuna sababu ya kurudia yale ya katiba ya chama na kuyaweka yawe mwongozo wa Kitaifa ili hali chama kina mrengo wake ktk utawala huu wa demokrasia?..
Hilo wote hawa hawalioni isipokuwa pengine wanachukulia Katiba Mpya ni swala dogo sana la marekebisho ya sheria lakini kila kitu kipo poa kwa sababu wao wanaitazama rangi ya Kijani kama ilivyo bendera yao na sisi tunasema ili upate rangi ya Kijani tunahitaji mchanganyiko wa rangi mbili Blue na Njano.. Wanaposikia Blue na Njano roho zinawatoka kwa sababu wanahofia ile kijani ya mundu na nini vile haitakuwepo tena..