Congo nchi inayotamaniwa na mataifa makubwa duniani

Congo nchi inayotamaniwa na mataifa makubwa duniani

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
23,676
Reaction score
57,094
Congo ndo kila kitu. Nchi yenye utajiri mkubwa wa rasilimali pengine ndo inaoongoza Dunia nzima.congo ndo njiapanda ya utajiri. Congo ndo chanzo cha Africa kugawanywa ndo chanzo cha mkutano wa Berlin..

Tazama congo ilikuwa under Belgium na hapo hapo makao makuu ya umoja wa ulaya yapo Belgium..madini ya congo ndo yalitumika kwenye vita kuu ya dunia.Congo ndo kila kitu na hata gorilla mnyama mwenye uwezo karibia ya binadamu anapatikana congo.

Utazaliwa utakufa mgogoro wa Congo utauacha maana ni mgogoro wa kidunia ule.

Poleni sana wa congo man
 
Ni ngumu sana kulinda madini ndani ya ardhi ya nchi kubwa yenye wajinga na maskini wengi kama DRC. Congo inapaswa kugawanywa kutoa nchi kama nne hivi kwa uchache ili kukomesha uwizi wa madini na kupeleka maendeleo na serikali karibu na wananchi. Lakini kwa jinsi ilivyosasa wananchi wataendelea kuwa maskini wa kutupwa huku kila Pepari duniani akijichukulia madini ya Congo.
 
Congo ndo kila kitu. Nchi yenye utajiri mkubwa wa rasilimali pengine ndo inaoongoza Dunia nzima.congo ndo njiapanda ya utajiri. Congo ndo chanzo cha Africa kugawanywa ndo chanzo cha mkutano wa Berlin..

Tazama congo ilikuwa under Belgium na hapo hapo makao makuu ya umoja wa ulaya yapo Belgium..madini ya congo ndo yalitumika kwenye vita kuu ya dunia.Congo ndo kila kitu na hata gorilla mnyama mwenye uwezo karibia ya binadamu anapatikana congo.

Utazaliwa utakufa mgogoro wa Congo utauacha maana ni mgogoro wa kidunia ule.

Poleni sana wa congo man
Uliyoandika yote hapa ni UONGO.
 
kwanini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ni ngumu kutawalika licha ya kuwa na utajiri mkubwa wa rasilimali? Kuna sababu kadhaa zinazochangia, na nyingi zimekuwa zikijirudia tangu enzi za ukoloni hadi sasa:




1. Rasilimali Zilizowekwa na Laana (Resource Curse)


  • DRC ina dhahabu, almasi, cobalt, coltan (muhimu sana kwa simu na magari ya umeme), shaba n.k.
  • Badala ya kuleta maendeleo, rasilimali hizi zimevutia vita, ufisadi, na uingiliaji wa mataifa ya nje.
  • Makampuni ya kimataifa na mataifa makubwa yanachochea migogoro ili kuendelea kupata rasilimali kwa bei ya chini.



2. Historia ya Ukoloni wa Kikatili


  • Utawala wa King Leopold II wa Ubelgiji (mwisho wa 1800s hadi 1960) ulikuwa wa kinyama sana — watu walikatwa mikono, waliuawa kwa maelfu.
  • Ukoloni haukuweka taasisi madhubuti za utawala, elimu, au uchumi. Ilipojipatia uhuru, nchi haikuwa tayari kujiongoza vizuri.



3. Migogoro ya Ndani na Makundi ya Waasi


  • Kuna makundi mengi ya waasi (kama M23, FDLR, n.k.) hasa mashariki mwa Congo.
  • Baadhi ya makundi haya yanapata misaada kutoka nchi jirani au mataifa yenye maslahi ya kiuchumi.
  • Serikali haina udhibiti kamili wa maeneo yote ya nchi.



4. Udhaifu wa Serikali na Ufisadi


  • Taasisi nyingi ni dhaifu au zimejaa ufisadi.
  • Viongozi mara nyingi hutanguliza maslahi binafsi au ya kikabila kuliko taifa.
  • Jeshi na polisi hawana uwezo wa kutosha kuleta amani ya kudumu.



5. Uingiliaji wa Mataifa ya Nje


  • Mataifa jirani kama Rwanda, Uganda, na hata baadhi ya mataifa ya Magharibi yameshutumiwa kuingilia DRC moja kwa moja au kwa njia za kisiasa/kiuchumi.
  • Mashirika ya kimataifa na makampuni ya madini yanatajwa kushirikiana na waasi au vikundi vya kihalifu kuchukua madini.



Kwa kifupi: utajiri mkubwa wa madini + historia ya giza + uingiliaji wa nje + uongozi dhaifu = nchi ngumu kutawalika.
 
Unajua maana ya kutamaniwa.
Unakitamani kitu kama hujakipata.
 
Kuna nchi zenye rasilimali nyingi zaidi duniani kuishinda Congo mfano Russia, Australia, Canada, Marekani, Brazil
Rudi tena alichoandika mkuu,then chakata!amesema ni nchi inayotamaniwa na mataifa makubwa kutokana na uwepo wa rasilimali zake(refer cobalt, lithium na titanium,mto Congo,misitu nk) na hajasema NI NCHI YENYE RASILIMALI NYINGI ZAIDI DUNIANI
 
Back
Top Bottom