Comrade Julius Mtatiro


Kwani akiwa CUF haitoshi kuwa presidential material?

Hivi cdm bado hamjarizika na akina marando, Lwakatare, Mnyika, Mpendazote na shibuda?? zoa zoa bado mnataka kumzoa na Mtatiro..

Hivi cdm mnajenga upinzani au mko kwenye mkakakti wa kuboa upinzani..

Kuna tatizo kubwa la uelewa kwa funs wa cdm??
 
Ndugu Julius Mtatiro,

Ningependa kupata maelezo zaidi ya kujitosheleza Kuhusu Imani yako kwa chama cha CUF Kuwa ni chama makini na hakifanyi maamuzi kutokana na special interest group ndani ya CUF, Kwani mimi na watanzania wengi tuna amini kuwa CUF bado ni chama chenye weakness nyingi sana na hivyo kupoteza mvuto wa kisiasa na malengo ya kuwa chama cha ukombozi wa kifikra na kiuchumi.

Nitazitaja baadhi ya kasoro kuu za CUF zinachokifanya kufutika taratibu kwenye siasa za Tanzania bara na hata huko visiwani.

1. Ni dhahiri kabisa kuwa kuna watu au group la viongozi wa CUF wenye nguvu kubwa ya kushinikiza baadhi ya maamuzi hususani viongozi wa CUF kutoka ZNZ, ndo maana Prof. Safari alikata tamaa na kukili kuwa kuna agenda ndani ya CUF ya ZNZ kwanza bara baadae. hilo hata wewe mwenyewe binafsi unalifahamu.

2. CUF wamepoteza uhalali wa kupigania demokrasia na haki za wananchi wa ZNZ baada ya kiongozi mmoja wa juu kuafikiana na CCM kuingizwa kwenye SUK na kuacha harakati za kweli za kutetea ushindi wa kura walizozipata baada ya uchaguzi wa 2010, kwani viongozi wengi wa ngazi za juu wakiwemo Ismail Jussa kukiri wazi kuwa CUF walishinda uchaguzi wa 2010 lakini hawakutangazwa washindi, na hata ukiangalia matokeo ya uchaguzi wa ZNZ, Inakuwaje mgombea wa Muungano Prof Lipumba kumshinda JK kwa kura nyingi ZNZ, Je Lipumba ni maarufu zaidi ya Maalimu Seif ZNZ? Je kama CUF wasingeahidiwa kupewa ceremonial post ndani ya serikari ya mapinduzi ZNZ wangekubali kuachia ushindi wao kirahisi hivyo? Je kitendo cha CUF kutopigania haki ya wananchi wake ni usaliti kwa wazanzibari na watanzania waliokwisha kuikataa ccm na kutoa uhai wao ili watoto wao wasiendelee kunyanyasika ndani ya nchi yao huru.

3. Je kuna sababu zipi za msingi CUF wasizotaka kukiri hadharani juu ya kuporomoka kwao kisiasa hasa Tanzania bara zaidi ya hiyo ya propaganda, Je CUF haitambui kuwa propaganda ni sehemu ya SIASA? Na kama ndivyo kwa nini propaganda za CUF haziungwi mkono na watanzani wengi?

4. Je utakubaliana nami kuwa baada ya CUF kulegeza harakati zake za ukombozi na kukubaliana na matakwa ya ccm, imekuwa ikibebwa na CCM angalau kiwe chama kikuu cha upinzani Tanzania? na hilo ndo linaondoa imani yetu na nia ya dhati ya CUF ya kupambana na utawala dhalimu wa CCM, na Je lengo la CUF ni kuendelea kuwa chama kikuu cha upinzani na kuwasaidia CCM waendelee kupalanganya taifa letu au kuunganisha nguvu na wapambanaji na wapenda mageuzi wote kuindoa ccm? hili limejidhihirisha kutokana na jitihada kubwa za wabunge wa CUF na statements nyingi za viongozi wakuu wa CUF kuhujumu wapambanaji wenzao bungeni na nje ya bunge.

Je, CUF wameamua ku surrender kwa CCM na kutoa ujumbe kwetu watanzania wapenda mabadiliko kuwa there is no other way kwa vyama vya upinzani kushinda uchaguzi na kuindoa CCM ila kwa fadhila za ccm tu? Chama kilichokata tamaa na kuacha misingi yake ya kupigania haki na kuamua kukubali kubebwa kinapoteza legitemacy ya agenda ya mabadiliko. We dont need all of the same, we want firm party which will stick to what they believe is right at any cost, sio chama kinachoyumbishwa na kufikia uamuzi wa to cut some deals!

5.Je utakubaliana nami kuwa SUK it was a big mistake politically kwa chama as whole? huwezi kumiliki BUCHA LA NGURUWE halafu ukaendelea kudai eti wewe ni muislamu swafi, hali kadhalika huwezi kumkana na kumpinga shetani kwa maneno wakati unafungamana nae kwa matendo yako. Watanzania ni waelevu sana na tunaona mwenendo wa CUF on closed door meetings and publically, na ni halali kupata laana na ghadhabu ya usaliti kutoka kwa watanzania.

6. Ni imani yangu kubwa sana kuwa CUF have a lot in common with CHADEMA, and NCCR-MAGEUZI rather than CCM, Kama kuna tofauti zinaweza kurekebishwa na kuhakikisha CCM inang'oka mapema iwezekanavyo, Je inakuwaje rahisi kwa CUF kuunganisha nguvu na CCM kuliko vyama vingine vya upinzani? au kwa sababu CCM has a lot to offer rather than CHADEMA au NCCR?

Mtatiro, it is not too late kwa CUF to correct their mistake, simameni imara muwambie wakina Maalimu Seif, Jussa na Hamad Rashidi, Tanzania kwanza ndo muhimu kuliko u sisi, otherwise very soon wataanza kuwa simanga kuwa nyinyi CUF bara hamna tija mnakula jasho la RUZUKU inayotokana na wabunge wao na kura zao za ZNZ,

Nitashukuru sana kama utafanikiwa kunipatia maelezo ya hayo yangu hapo juu.
 
kwa hali ya siasa ilivyo Julius unatuchanganya,haueleweki
 
Una digri ya uwalimu wa kiswahili, ulitaka ulipwa sh. Ngap? Hyo mbona ajira yako inakufa? Diploma ya walim mastaz open, unajigamba nini? Njaa ndio imekupeleka kilaza wewe, nakubuka ulivyokuwa mnoko ifakara. Tunaokujua tunakutazama unahaha na njaa zako. Tumia akili usitumie masaburi.
 

Mkuu sisi ni binadamu kila tunachokifanya huwa tunaamua kwa utashi wetu na kwa sababu ya wakati uliopo na ujao

Tumetofautiana sana maamuzi yetu na maamuzi yeyote mazuri huja kwa extent ya ujuaji wa jambo hilo

Ila ni makosa sana kusema kuwa ukimwambia mtu fulani kuwa kuna jambo baya litatokea, basi ni lazima litokee au likitokea ni kwa sababu wewe umesema! naona ni mawazo uliyo nayo wewe , pasco na director.

Maamuzi ya sasa ya JM ndiyo yanayomfanya awe yeye vile alivyo....mmeona anavyojibu maswali


mkuu wewe umemaliza kabisa kwa kusema aende CDM, kisa CDM ni wapiganaji wazuri?? Kafulila ni mpiganaji m'baya? je si alikuwa humohumo CDM, what made him to leave the party?? wakati unazungumzia CDM as a party, CDM hakijajengwa na kujiunda kama chama, hakuna tofauti ya CDM, CUF,TLP,NCCR, .....vyote vina watu na ukitaka kuamini vizuri angalia CCM, vyama vingine vina-uccm ila kwa low extent!!


Ukija kwenye uhuru wa uchaguzi umepractise udikteta.....umemuogopesha, na umenuia mabaya yatokee CUF kwa sababu si umesema??

Ila tungekuwa na lengo moja na nguvu moja, tungechukuana vijana na kushikana mikono , haijalishi huyu wa chama gani, tumewatenga wengine kwa jina la chama fulani, tumejitenga na kuwaona wengine wasio upande wetu si wenzetu! hata pale tunapoona kabisa wanapigania maslahi ya nchi..ila kwa sababu si wanachadema basi kwishney! Chadema ni kila kitu !!


Tanzania tunaweza sisi wote pasi vyama vyetu tukafikia ukombozi wa kweli bila kujali matabaka na kuwa fulani yuko wapi

NCCR wakitoa tamko la kuipinga CCM jambo fulani...halipokelewi na wana CDM baadhi, ila statement ile ile akiitoa mwana chadema basi itapokelewa kwa mikono yote, bila kujali waliotoa statement wote lengo lao ni moja na wanaitakia mema TANZANIA

Julius baki CUF kwa sababu una sababu za kufanya hivyo, wengine humu hawana hata kadi ya chadema ila wanawaambia wenzao hivi na vile!

Ikifikia kwenda chadema uende tu, lakini naamini hautakwenda kwa sababu kuna watu kwenye thread hii wanasema unapoteza muda.

Let him be.....

Julius waambie kuwa

''And I am not afraid to try it on my own
I don't care if I'm right or wrong
I'll live my life the way I feel no matter what I'll keep it real
You know
Time for me to do it on my own''
-WH

Akifikia muda wa kwenda chama kingine kama CCM... he will have learned from the best!!!!!!!!!!!
 
Mkuu Waberoya,

Ume mtetea sana Mtatiro as if your his lawyer mzee, and the way you presented your defense as if your in his mind,

Mzee politician wote ni wanafki, hiyo ndo politics ilivyo, wanasiasa wangapi wana flip flop mitazamo yao? si kuna waliopa kutokwenda CCM na kusema wakifanya hivyo itabidi walale na mama zao! Si wapo CCM hivi sasa Je wamelala na mama Zao?

Inawezekana huyo Director alieanzisha thread hii ndo JM mwenyewe anapima upepo na kuandaa mazingira ili aone atatoka vipi?

Hivyo mzee usijipachike kuwa advocate wa JM kwa sababu wanasiasa wengi husema hili huku mawazo yao tofauti na wanachonena.


 
Mtatiro ni uamuzi mgumu, ingawa najua ndani ya nafsi yako unakubaliana na wale wanaosema CUF sio kikombe chako cha chai. Tatizo naloliona ni ''Nitoke vipi ?''
 
Cdm ni debe lilo jaa lakini linatundu linalovuja bila ya kujitambua nawala hawatambui kama tundu hilo lipo . Wanadhani ukiwa cdm ndio mpambanaji. Wanadhani kuchukua ubunge ni lazima uwe Cdm. Hizi ni akili za kushikizwa. Tunawaona kina kafulila, mkosamali, machali, ni wapambanaji kweli lakini hawapo cdm, wapambanaji silazima wawe vyama vya upinzani hata ccm wapo pia cuf wapo akina baruani, ***** ,sakaya, habib mnyaa. So hata mtatiro wakati wake bado.
 
Pasco kwa maoni yako unafikiri angeenda chama gani?
Waberoya, kama ulinisoma posti yangu No. humu nimempa ushauri wangu.

Naamini wote tumeyasoma majibu ya Mtatiro mwenyewe kuwa ameingia kwenye siasa kwa malengo, na kabla ya kujiunga hapo alipo, amefanya upembuzi yakinifu kuwa hapo ndipo na malengo yake yatatimia.

Nadhani pia umeniona nikimuwish all the best hapo alipo, aende chama gani tena wakati hapo kafika?.

Kwa vile time ndio the best judge, lets wait for the time to tell ili tuone what will become of him.

Pasco.
 

Sijajipachika uadvocate, otherwise we are all advocates sometime and accuser other times! ninachoangalia ni uhuru wa mawazo na uhuru wa mtu kuchagua ndipo niliposimamia..ni sawa na mtu akubane kwa nini ulichagua kujiita executive humu ndani!!.Nimesimamia logic hiyo. kumwambia mwenzako ondoka hapa nenda pale is as if telling someone who is a kid ,does not reason or think!

Kweli wanasiasa wote ni wanafiki, however ndio tunawapigia kura na kushinda humu kuwajadili wao! I think we all tunaweza kuwa wanafiki mida mingine
 
Ungesema tu wewe ni shabiki wa chadema basi tungejua
Ni maoni pia umejitahidi..
Lakini CUF ndio chama makini cha upinzania tanzania
Chadema bila kanisa hakuna kitu

CUF ni chama cha misikiti na mashekhe! Na sasa ni CCM B kwa Hilo wako makini
 
Waberoya, nimeipenda sana "the independence" on you na sense yako ya nationalism kuwa Tanzania ni yetu sote no matter tuko vyama tofauti.
Nadhani ulisoma Eng. unaweza kuwa ni moto wa aina yake kwenye field yako, ila ninavyokusoma humu, ulipaswa upige LL.B na ungekuwa ni balaa zaidi!.

Naamini Mtatiro kajieleza vizuri na watetezi wake mnaomsuport amewasoma, na naamini japo sio lazima atufuate, ila sauti zetu kuwa he is in a wrong side of the right road amezisikia, anachofanya sasa, ni either a proof us wrong kwa sisi kudhani kuwa yuko kwenye wrong side, atakapofikia destination ya safari yake salama, ama kwa vile Mtatiro ni mpambanaji wa kweli, anaweza pia kuprove kuwa hata ukipitia wrong side of the road unaweza kufika destination yako sawasawa na wale ombao wako kwenye the right track, tumpe nafasi na time will tell.

Asante mwanzisha uzi, asante wachangiaji makini, asante zaidi kwa Mtatiro, japo nami nilikuwa UDSM, time za kina Zitto, na kina Mtatiro, wengine wetu tulikuwa too busy na mambo yetu, siasa za chuo zikatupita kando, lakini kupitia uzi huu, ndio tumemfahamu Mtatiro better na kweli ni jembe haswa!. Sasa hivi ni msimu wa kutayarisha mashamba, tusubiri mavuno baada ya 2015 ndipo tuje tena tutoe sifa za majembe ya kweli kwa kipimo cha mavuno, bila kutoa visingizio vya matatizo ya hali ya hewa.

All the best.

Pasco.
 
EXECUTIVE,
Hata mimi nimenote kama Wabe angekuwa Lawyer, angemake advocate mzuri sana!
 
Waberoya, if its not too late, please be one, the real one!
 
EXECUTIVE,
Kwa vile siasa ni malengo, kwa vile CUF nguvu yake kubwa ni Zanzibar na Pemba, na hali ya kusiasa katika visiwa hivyo ilikuwa mbaya sio tuu ilitishia amani, bali imeshaletwa umagwaji damu na mpaka kutoa wakimbizi. Kwa CUF kukubali SUK ni good compromise kwa ustawi wa Zanzibar, hivyo kwa CUF Zanzibar haya ni mafanikio kuondoa siasa za uhasama na umwagaji damu, japo at the cost of kupigiwa vigora na kutekeleza sera za CCM.

Kwa vile Zanzibar, asilimia 98% ya Wazanzibari ni Waislamu, chama chochote cha siasa ili kupata ustawi Zanzibar, lazima kiwakumbatie hao 98%. Sasa kwa sababu CUF bara inakabiliwa na jinamizi la udini, CUF lazima ipate prone ya kuicheza mbele kenye gama yake ya chess, ili kuliondoa jinamizi hilo, ndivyo walivyomtumia Rwakatare, na sasa ndivyo watakavyomtumia Mtatiro bila yeye kujijua, watampa kila anachokitaka, kila cheo na vilemba vya ukoka, lakini wakati utakapofika, ndipo atakapoijua what CUF really is and what does it stand for!. Only time will tell!.
 

kweli mkuu field yenyewe hailipi sana, wachina wameivamia.....
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…