Comoro: Shein awekwa Baka Bencha

Comoro: Shein awekwa Baka Bencha

Sasa kama ka nchi kadogo wamemfanyia hivi je akienda kwenye nchi kubwa si watakuwa kwa wauza vitumbua @ joking not serious

Unataka kusema akitumwa kumwakilisha Joni mahali kama Geneva anaweza kuzuiwa getini na kuulizwa "we ndo nanii?" Hahaha, Joni aache kumtuma.
 
Dah, unfairly treated, hasa ukiangalia namna BG anavyo husle kumtuliza, nadhani hii ni dharau ya hali ya juu no matter what.....mtu ana BG unamuweka Last corner na nyuma yake kuna watu..vip usalama wake...?
Anyways......lazima kuna kitu anakumbuka....
Ishakuwa taabu maamlaka kamili ndiyo dili.
 
Kacomoro ni ka nchi kadogo sana hakawezi kuitunishia misuli Tanzania hata serikali yao ilipopinduliwa ni Tanzania ndio iliongoza majeshi ya kurudisha serikali halali iliyochaguliwa isistoshe wanaitegemea Tanzania kwa kiasi kikubwa kwa biashara ya chakula kwa wale mnaojifariji lazima mjue hivyo kama rais wetu atataka maelezo na kuvunja uhusiano nao wao ndio wataathirika zaidi lazima kutakuwa na sababu za kidplomasia za kufanya hivyo

Ilikua operation ya UN na AU . Na Tanzania walilipwa kupeleka majeshi ya amani kuweka mambo sawa.
 
Sidhani kama alikuwa na hamu tena ya kula urojo wa kingazija!

ADC ni kama anamnong'oneza "sheikh jahazi lishatia nanga mwambao tayari kwa safari kamavipi jifanye umepatwa kadhia ya kuhara tuishie zetu yakhee nishai hii atiii" (in pemba swagz)
 
Kukaa hio siti sijui vinaendana na ushindi wa mwaka jn,nasikia alishindaga kihalali sa sijui kweli..
 
Mleta maada ni mpumbavu na lofa. Kwani mlitaka akae wapi?? Mbona hata akina Kagame walikaa sehemu za nyuma kama hizo kipindi Dr Magufuli anaapishwa. Yaani watu wengine akili zenu zimekaa kuwaza mambo mabaya kwa wenzenu, na bado mtakoma, Dr Shein ndiye rais mpaka 5 years iishe, na Dr Magufuli ndiye rais wa JMT.
 
Back
Top Bottom