Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Jana jioni majira ya saa 2 usiku nilikuwa maeneo ya Ilala kumtembelea rafiki yangu mmoja aishie Mtaa wa Utete. Nikakuta hakuna umeme maeneo hayo – biula shaka kutokana na mgao.
Nilipita mtaa wa Pangani na nilishtuka sana nilipoikuta ile police station ya mtaa huo iko kwenye giza totororooo.
Hakuna hata mshumaa ulikuwa unawaka kutoka ndani. Hiyo ni station kubwa – siyo police post. Yaani hakuna hata jenereta?
Jamani hii si hatari hasa katika kipindi hiki cha wasiwasi hapa nchini? Wavamizi wangeweza kuvamia amory na kuondoka na silaha, askari wangewazuia vipi?
Aidha mtu aliyeumizwa vibaya atapataje fomu ya P3 kwenye giza. Ripoti zitaandikwaje kwenye RB gizani?
Jamani tunacheza na haya mambo. Komanda Kova – unalielewa hili? Au unakazania tu kutimiza amri za mahakama za kuwakamata viongozi wa upinzani?
Hebu fikiria scenario hii: Mtu anakwenda kuripoti majambazi yameonekana mahala fulani yanapanga njama zao. Akifika hapo wakati huo haoni kitu, ni giza tupu! Atajua ofisi gani ya kuingia? Au klwanza polisi wakaanunue mshumaa duka la jhirani? Halafu bila shaka gari iliyopo hapo itakuwa haina petroli!
Hii nchi imefikia hali mbaya sana – Kova na Chagonja wanachojua ni kupambana na upinzani kwa kutoa kauli za hovyo lakini masuala haya ya msingi ya kuboresha vituo vya polisi hawana kabisa habari nayo.
Ni aibu tupu kwa jeshi letu na kwa wakuu wanaloliongoza. Nyumba ya tatu kutoka kituo hicho cha polisi cha Pangani kulikuwapo jenereta inafanya kazi.
Yaani tuseme siku hizi wananchi wana hela kuliko serikali? Ndiyo matunda ya ufisadi?
Nilipita mtaa wa Pangani na nilishtuka sana nilipoikuta ile police station ya mtaa huo iko kwenye giza totororooo.
Hakuna hata mshumaa ulikuwa unawaka kutoka ndani. Hiyo ni station kubwa – siyo police post. Yaani hakuna hata jenereta?
Jamani hii si hatari hasa katika kipindi hiki cha wasiwasi hapa nchini? Wavamizi wangeweza kuvamia amory na kuondoka na silaha, askari wangewazuia vipi?
Aidha mtu aliyeumizwa vibaya atapataje fomu ya P3 kwenye giza. Ripoti zitaandikwaje kwenye RB gizani?
Jamani tunacheza na haya mambo. Komanda Kova – unalielewa hili? Au unakazania tu kutimiza amri za mahakama za kuwakamata viongozi wa upinzani?
Hebu fikiria scenario hii: Mtu anakwenda kuripoti majambazi yameonekana mahala fulani yanapanga njama zao. Akifika hapo wakati huo haoni kitu, ni giza tupu! Atajua ofisi gani ya kuingia? Au klwanza polisi wakaanunue mshumaa duka la jhirani? Halafu bila shaka gari iliyopo hapo itakuwa haina petroli!
Hii nchi imefikia hali mbaya sana – Kova na Chagonja wanachojua ni kupambana na upinzani kwa kutoa kauli za hovyo lakini masuala haya ya msingi ya kuboresha vituo vya polisi hawana kabisa habari nayo.
Ni aibu tupu kwa jeshi letu na kwa wakuu wanaloliongoza. Nyumba ya tatu kutoka kituo hicho cha polisi cha Pangani kulikuwapo jenereta inafanya kazi.
Yaani tuseme siku hizi wananchi wana hela kuliko serikali? Ndiyo matunda ya ufisadi?