Je,Mwakyembe alifichua Genge la Mauaji kwa nini Polisi wamegwaya??????

KING COBRA

JF-Expert Member
Nov 10, 2011
2,782
864
KIONGOZI wa chama kikuu cha upinzani nchini, Dk. Willibrod Slaa ametajwa kwenye orodha ya watu wanaotishiwa kuuawa.

Mwingine aliye kwenye orodha hiyo ni aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata wa Richmond, Dk. Harrison Mwakyembe, MwanaHALISI linaweza kuripoti.

Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IJP), Said Mwema amethibitisha kuwa ana taarifa kuhusiana na tishio hilo na kwamba ofisi yake inazifanyia kazi.

"Ni kweli, jeshi la polisi linazo taarifa hizo za kuwapo kwa tishio la mauaji. Lakini nafikiri hilo ni jambo la kiupelelezi zaidi," alisema IJP Mwema katika mahojiano yake na gazeti hili juzi Jumatatu.

Hata hivyo, Mwema alikataa kulizungumzia suala hilo kwa undani, badala yake alielekeza gazeti hili kumtafuta Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishina wa Polisi, Robert Manumba.

Naye Manumba alipoulizwa alikiri kuwapo kwa tishio hilo lakini aliishia kusema, "Bado tunafanya uchunguzi."

Alipoulizwa hatua walizofikia katika uchunguzi huo, Manumba alisema, "Unapofanya uchunguzi kuna mambo mengi ya kuzingatia. Kuna kukusanya ushahidi. Kwa jumla, bado tunafanya uchunguzi," alisisitiza na kusema muda ukifika taarifa kamili itatolewa.

Kufichuka kwa tishio la mauaji ya watu hao mashuhuri, kumeibuka kufuatia barua ya kurasa saba iliyoandikwa na Dk. Mwakyembe ambaye sasa ni naibu waziri wa ujenzi kwa IJP Mwema.

Katika barua hiyo ya 9 Februari 2011, iliyobebwa na kichwa kisemacho, "Taarifa ya njama za kuondoa maisha yangu na ombi kwa jeshi la polisi kulinda haki yangu ya kikatiba ya kuishi," Dk. Mwakyembe anataja watu wengine mashuhuri wanaotishiwa kuuawa.

Hao ni mfanyabiashara mashuhuri nchini, Reginald Mengi, waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe na mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Melecela.

Dk. Mwakyembe anasema katika barua yake, "Pamoja na kwamba taarifa hii ni mpya yenye matukio ya takribani mwezi mmoja tu, naamini kwa dhati kuwa msingi wake – kwa maana ya wahusika na maudhui – hautofautiani na ule wa matukio mengine ya awali ambayo baadhi yake yalisharipotiwa polisi na vyombo vingine vya usalama kwa lengo la kuchunguzwa."

Anasema pamoja na hayo, bado ana imani kubwa na jeshi la polisi kuwa litaifanyia kazi taarifa hiyo bila kujali nguvu ya ukwasi na ya kisiasa ya watuhumiwa.

Msingi mkuu wa yeye kuamua kuvitaarifu vyombo vya dola, anasema Dk. Mwakyembe, ni taarifa alizozipata kutoka Songea, 22 Januari 2011 zinazolihusu kundi la watu saba lililoingia mjini humo usiku wa 21 Januari 2011 wakitumia gari linalodaiwa kuwa la wizara yake.

Gari hilo aina ya Land Cruiser lilikuwa na namba za usajili STK 6868, lakini baadaye namba ilibadilishwa na kusomeka STK 6869.

Gari hilo liliwateremsha "abiria" hao saba sehemu iitwayo Madaba na kisha kuchukuliwa na gari jingine Land Cruiser hardtop, Na. T 768 BDU hadi baa ya Top Inn mjini Songea.

Anawataja baadhi ya abiria waliokuwamo katika gari hilo kuwa ni raia wawili wa Somalia, Hafidh na Faraj, "kijana mmoja wa Kichagga" kwa jina Mustafa a.k.a "Master" Mkusa ambaye imeelezwa kuwa ni ofisa wa idara ya usalama wa taifa na mwingine aliyejulikana kwa jina moja la Ramika kutoka Tanga, ambaye inadaiwa ndiye "mtaalamu" wa kukaba watu.

Dk. Mwakyembe anaeleza katika barua yake kwa IJP, kwamba aliyepokea genge hilo la wahalifu mjini Songea, ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Vijijini, Rajabu Mtiula akiongozana na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Manya.

"Usiku wa Jumamosi 22 Januari 2011, kundi hilo lilielekea Mbunde, wilayani Namtumbo kwa gari aina ya Defender STK 2654, likiendeshwa na Zuberi Komba kwa lengo la kukutana na ‘mganga' Majungu (kabila Mdendeule) ambaye anaishi ndani ya mbuga ya wanyama (Selous Game Reserve with impunity,)" anaeleza Dk. Mwakyembe katika barua yake.

Anasema, "Defender hiyo iligeuza kurejea Songea siku mbili baadaye na kuwaacha wageni hao kwa mganga ambako walikaa siku saba wakitengenezwa. Walirejea Songea 29 Januari 2011 na kesho yake, 30 Januari 2011 wakaanza safari kurejea Dar es Salaam."

Anasema kutoka Songea hadi Mafinga, watuhumiwa wa njama za kuua walitumia gari Na. T 768 BDU ambalo walilitumia awali kutoka Madaba hadi Songea. Anasema walifika Mafinga saa mbili usiku na kukuta magari mawibili yakiwasubiri. Moja, Hilux Mayai ya kampuni ya Vodacom na Defender iliyowaongoza hadi Morogoro.

Akiandika kwa kujiamini, Dk. Mwakyembe anasema, "…walipofika Morogoro walipokelewa na askari mmoja anayemtaja kwa jina la Sabasita. Hapo kundi likagawanyika: Watu wanne wakiwemo wale wasomali wawili wakaingia kwenye Nissan Patrol T 845 ADH mali ya kampuni ya Caspian, na wengine wakabaki Morogoro."

Kampuni ya Caspian ni mali ya Rostam Aziz, mfanyabiashara, mbunge wa Igunga (CCM) na wakala anayejitaja kuwakilisha kampuni ya kufua umeme ya Dowans ya Costa Rica. Gazeti lilipomtafuta, hakuweza kupatikana.

Anamwambia Mwema kuwa, Mganga Majungu mwenyewe, ambaye wapelelezi wake wanaweza kuongea naye kama walivyofanya waliompa taarifa hizi, aliwapa masharti ya kutotumia silaha za moto ila njia nyingine kumuua kwanza Mwakyembe, baadaye Dk. Slaa na wengine.

Anasema mganga huyo "ametengeneza dawa ya kuwapumbaza waliohukumiwa kifo na kuwa mfano wa mbwa mbele ya chatu" ili kukimbia hasira za wananchi pale mpango wa mauaji utakapotekelezwa.

Dk. Mwakyembe anamueleza IJP Mwema, kwamba awali mkakati wa kumuua Dk. Slaa ulipangwa kutekelezwa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, lakini ulisitishwa kwa hofu ya kuingiza nchi katika machafuko.

"…utabiri wa Sheikh Yahya Hussein mwaka jana kuwa mmoja wa presidential candidates (wagombea urais) atakufa, ulimlenga Dk. Slaa ambaye alidaiwa kubebwa na makinisa. Utabiri huo haukutimia kwa kuogopa kuiingiza nchi kwenye machafuko makubwa ya kisiasa/kidini ambayo yangewaweka pabaya hata wafadhili wa mpango wenyewe," anasema.

Wiki mbili zilizopita, Sheikh Yahaya alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kutatokea vifo vya watu kadhaa mashuhuri wakiwamo wanasiasa na mwandishi mmoja wa habari mashuhuri nchini. Wakati Shekh Yahaya anatoa utabiri wake, Mwakyembe alikuwa katika wiki ya tatu tangu awasilishe malalamiko yake polisi.

MwanaHALISI lilipowasiliana na Sheikh Yahya ili kufahamu iwapo utabiri wake unatokana na kutumiwa na watu maalum waliomlipa fedha ili kufanikisha mkakati huo wa mauaji, mnajimu huyo alisema, "Watu wasubiri matokeo."

Alisema anachokifanya yeye ni unajimu na tayari amefanya hivyo katika matukio kadhaa makubwa ikiwa ni pamoja na kuwako kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.

"Nilitabiri Raila Odinga kuunda serikali moja na Mwai Kibaki Kenya. Yametimia. Nilitabiri CCM itapata msukosuko baada ya uchaguzi mkuu, imekuwa hivyo. Sasa hapo unahoji nini?

"…Sijataja jina la mtu, hivyo watu wasijihisi kwa utabiri wangu, ila wao wasubiri matokeo. Halafu ninyi MwanaHALISI mnafanya kazi nzuri. Ipo siku nitawaita hapa kuzungumza nanyi. Ila nayi msihofu, msubiri matokeo."

Naye Dk. Slaa alipoulizwa kuhusu mpango huo, kwanza alicheka, kisha akauliza: "Nani kakuambia?" Alipoelezwa kuwa ni taarifa zilizothibitishwa na jeshi la polisi, Dk. Slaa alisema, "Basi nadhani wao ndiyo wanajua wanaohusika katika suala hilo."

Katika barua yake kwa IJP, Dk. Mwakyembe anasema kijana mmoja anayefahamika kwa jina la Hassani alitumwa kutoka Dar es Saalam kwenda Dodoma, 5 Februari mwaka huu kwa "maandalizi" ya kikosi cha mauaji. Amesema tayari kikosi hicho kimefanya utambuzi wa nyumba yake aliyopangiwa kuishi na serikali.

Anasema, "Tarehe 6 Februari 2011, mnamo saa nne usiku, kikosi hicho cha mauaji kikiwa na watu watano kiliondoka Dar es Salaam kwenda Dodoma kwa gari aina ya Land Cruiser nyeupe ya mkonga (T 360 AKU). Waliokuwa kwenye kikosi hicho ni wasomali wale wawili, mgeni mmoja wa kiume kutoka Uganda, Mustafa a.k.a ‘Master' na kijana mmoja ambaye tarehe 19 Januari 2011 aliwabeba wasomali hao kutoka Morogoro kwa gari aina ya VX Lands Cruiser T 656 APF. Kijana huyo ana shepu ya Kitusi na anaongea Kifaransa."

Jijini Dar es Salaam, Dk. Mwakyembe anasema, "Wahitimu hao wa Profesa Majungu walifikia Kiwalani karibu na Kiwanda cha Mohammed Enterprises. Jirani na kiwanda hicho kuna jengo la ghorofa, chini ni msikiti wa Waarabu unaoitwa MALKAZ na juu ni sehemu ya kuishi."

Anaeleza kuwa tarehe 5 Februari, wageni wawili zaidi waliwasili kwa ndege kutoka Uganda. Mwanaume mmoja (aliyechanganya rangi) na mwanamke mmoja (mweusi vilivyo). Anaripoti kuwa walipokelewa kwa magari mawili: moja la polisi, PT 0288 – polisi ujenzi na la pili lenye namba za kibalozi T 69 CD 82 aina ya RAV 4. Anasema, jioni wakawa na mazungumzo ya kina na raia wawili wa Somalia ambao inadaiwa ni kutoka kundi la Al-Shabaab.

Dk. Mwakyembe anasema katika maelezo yake kwamba amepata picha ya kwa nini wapiganaji wa kikundi hicho wameingizwa nchini.
Anasema, "Nimeweza kukusanya taarifa zinazodai kuwa awali walifikiriwa kuletwa wapiganaji kutoka Rwanda, lakini wazo hili lilikataliwa na wafadhili wa mpango huu ambao walitaka wanaharakati wa aina hiyo watoke Somalia. Ndipo kikundi hicho kikashawishiwa. Mimi na wenzangu hao watano tumejengewe hoja kuwa maadaui wa Uislamu tunaotumiwa na makanisa, hivyo hatuna budi kukatishwa maisha yetu."

Katika barua yake kwa IJP, Dk. Mwakyembe anasema kila siku hupata taarifa za ziada kutoka kwa raia wema kuhusu suala hili; anazitoa taarifa hizo kwa jeshi la polisi ili ziwasaidie katika upelelezi.

Kwanza, taarifa zinaonyesha raia hao wa kisomali waliingia nchini kutokea Kenya na walikwenda Dodoma kupitia njia ya barabara kwa kutumia gari aina ya RAV 4 (new model- T 816 AQS) tarehe 08 Januari 2011.

Pili, Dk. Mwakyembe anasema walipofika Morogoro walipokewa na askari Sabasita wa jeshi la polisi mkoani humo, ambapo walikaa katika hoteli mbili tofauti – Hillux Hotel na Top Life. Anamtaja aliyewafanyia booking wageni hao ni mmiliki wa Morogoro Hotel aliyemtaja kwa jina moja la Kari.

Tatu, Dk. Mwakyembe anasema magari waliyotumia wakiwa Morogoro, ni RAV 4 T 816 AQS, VX Land Cruiser STK 1287, Mercedez Benz (Station Wagon) T 874 BDT, Toyota Mark II GX100 nyeupe T 218 BKR na wakiwa Dar es Salaam wametumia magari VX Land Cruiser T 656 APF na Nissan patrol T 845 ADH.

Wakiwa Dar es Salaam, Dk. Mwakyembe anataja watu waliokuwa na mawasiliano na waliotumwa kuchukua roho yake kuwa ni "Masuhe wa Central Police Station (polisi kati), Fred Lowassa ambaye inadaiwa aliwapelekea mbuzi watatu huko Kiwalani tarehe 04 Februari 2011 na hata kuwatafutia gari VX Land Cruiser T 656 APF.

Anasema walipokuwa Dar es Salaam, tarehe 13 na 14, Januari wabaya wake walifikia nyumba Na. 551, Mtaa wa Chakechake, Upanga.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini, Rajab Mtiula, hakupatikana juzi kuzungumzia kuhusishwa kwake katika mikakati hiyo.

Gazeti lilipowasiliana na Fred Lowassa kueleza juu ya kuhusishwa katika maandalizi ya kifo cha Dk. Mwakyembe na wenzake alijibu, "Kaka katika mazingira ya kawaida tu, hilo jambo ni very serious (hilo jambo zito). Kuua ni tuhuma nzito.

Alisema, "Siku hizi kuna teknolojia ambako ukifanywa uchunguzi, itaonekana tu. Mimi nimekutana na mambo magumu sana maishani, lakini siwezi kufikia hatua ya kuua au kuhusika kuua."

Fred ambaye ni mtoto wa waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa alisema, "Yakinipata magumu, mwokozi wangu ni Mungu. Naomba Mungu, halafu huwa nasamehe. Siku zote huwa sipendi kuingia kwenye malumbano," alieleza.

Lakini Dk. Mwakyembe katika barua yake kwa IJP Mwema anasema, "Pamoja na kwamba sina imani na ushirikina au nguvu za giza, kutajwa kwa jina langu na fursa ya pekee niliyokuwa nayo ya kujua kilichokuwa kinafanyika, kukanipa ari, nguvu na shauku ya aina yake kutaka kulielewa zaidi suala hili ili ikibidi, niwataarifu wenzangu nao waelewe."

Taarifa zinasema kila aliyetajwa kuuawa amejulisha taarifa hizo na Dk. Mwakyembe kama ambavyo ameeleza katika maelezo yake polisi.


Gazeti toleo lenye makala hii
 
Mwakyembe mwizi tu ameweka watu wake bandarin na kila mwezi anapelekewa 40percent hana jpya huyu alkuwa anaganga njaa kujfanya kamanda wa ufsadi
 
Huyo ndio mwakyembe, kama ulikuwa na biashara za ubabaishaji kule bandarini, basi sitashangaa hivyo ulivyo comment!
 
Mwakyembe mwizi tu ameweka watu wake bandarin na kila mwezi anapelekewa 40percent hana jpya huyu alkuwa anaganga njaa kujfanya kamanda wa ufsadi

Acha umburula, changia hoja kwa kinachojadiliwa, sio kuingiza vitu ambavyo ni vya kufikirika.
Hiyo 40% inahusiana nini na yeye kutaka kuuwawa?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
KIONGOZI wa chama kikuu cha upinzani nchini, Dk. Willibrod Slaa ametajwa kwenye orodha ya watu wanaotishiwa kuuawa.

Mwingine aliye kwenye orodha hiyo ni aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba tata wa Richmond, Dk. Harrison Mwakyembe, MwanaHALISI linaweza kuripoti.

Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IJP), Said Mwema amethibitisha kuwa ana taarifa kuhusiana na tishio hilo na kwamba ofisi yake inazifanyia kazi.

"Ni kweli, jeshi la polisi linazo taarifa hizo za kuwapo kwa tishio la mauaji. Lakini nafikiri hilo ni jambo la kiupelelezi zaidi," alisema IJP Mwema katika mahojiano yake na gazeti hili juzi Jumatatu.

Hata hivyo, Mwema alikataa kulizungumzia suala hilo kwa undani, badala yake alielekeza gazeti hili kumtafuta Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishina wa Polisi, Robert Manumba.

Naye Manumba alipoulizwa alikiri kuwapo kwa tishio hilo lakini aliishia kusema, "Bado tunafanya uchunguzi."

Alipoulizwa hatua walizofikia katika uchunguzi huo, Manumba alisema, "Unapofanya uchunguzi kuna mambo mengi ya kuzingatia. Kuna kukusanya ushahidi. Kwa jumla, bado tunafanya uchunguzi," alisisitiza na kusema muda ukifika taarifa kamili itatolewa.

Kufichuka kwa tishio la mauaji ya watu hao mashuhuri, kumeibuka kufuatia barua ya kurasa saba iliyoandikwa na Dk. Mwakyembe ambaye sasa ni naibu waziri wa ujenzi kwa IJP Mwema.

Katika barua hiyo ya 9 Februari 2011, iliyobebwa na kichwa kisemacho, "Taarifa ya njama za kuondoa maisha yangu na ombi kwa jeshi la polisi kulinda haki yangu ya kikatiba ya kuishi," Dk. Mwakyembe anataja watu wengine mashuhuri wanaotishiwa kuuawa.

Hao ni mfanyabiashara mashuhuri nchini, Reginald Mengi, waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe na mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Melecela.

Dk. Mwakyembe anasema katika barua yake, "Pamoja na kwamba taarifa hii ni mpya yenye matukio ya takribani mwezi mmoja tu, naamini kwa dhati kuwa msingi wake – kwa maana ya wahusika na maudhui – hautofautiani na ule wa matukio mengine ya awali ambayo baadhi yake yalisharipotiwa polisi na vyombo vingine vya usalama kwa lengo la kuchunguzwa."

Anasema pamoja na hayo, bado ana imani kubwa na jeshi la polisi kuwa litaifanyia kazi taarifa hiyo bila kujali nguvu ya ukwasi na ya kisiasa ya watuhumiwa.

Msingi mkuu wa yeye kuamua kuvitaarifu vyombo vya dola, anasema Dk. Mwakyembe, ni taarifa alizozipata kutoka Songea, 22 Januari 2011 zinazolihusu kundi la watu saba lililoingia mjini humo usiku wa 21 Januari 2011 wakitumia gari linalodaiwa kuwa la wizara yake.

Gari hilo aina ya Land Cruiser lilikuwa na namba za usajili STK 6868, lakini baadaye namba ilibadilishwa na kusomeka STK 6869.

Gari hilo liliwateremsha "abiria" hao saba sehemu iitwayo Madaba na kisha kuchukuliwa na gari jingine Land Cruiser hardtop, Na. T 768 BDU hadi baa ya Top Inn mjini Songea.

Anawataja baadhi ya abiria waliokuwamo katika gari hilo kuwa ni raia wawili wa Somalia, Hafidh na Faraj, "kijana mmoja wa Kichagga" kwa jina Mustafa a.k.a "Master" Mkusa ambaye imeelezwa kuwa ni ofisa wa idara ya usalama wa taifa na mwingine aliyejulikana kwa jina moja la Ramika kutoka Tanga, ambaye inadaiwa ndiye "mtaalamu" wa kukaba watu.

Dk. Mwakyembe anaeleza katika barua yake kwa IJP, kwamba aliyepokea genge hilo la wahalifu mjini Songea, ni mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea Vijijini, Rajabu Mtiula akiongozana na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Manya.

"Usiku wa Jumamosi 22 Januari 2011, kundi hilo lilielekea Mbunde, wilayani Namtumbo kwa gari aina ya Defender STK 2654, likiendeshwa na Zuberi Komba kwa lengo la kukutana na ‘mganga' Majungu (kabila Mdendeule) ambaye anaishi ndani ya mbuga ya wanyama (Selous Game Reserve with impunity,)" anaeleza Dk. Mwakyembe katika barua yake.

Anasema, "Defender hiyo iligeuza kurejea Songea siku mbili baadaye na kuwaacha wageni hao kwa mganga ambako walikaa siku saba wakitengenezwa. Walirejea Songea 29 Januari 2011 na kesho yake, 30 Januari 2011 wakaanza safari kurejea Dar es Salaam."

Anasema kutoka Songea hadi Mafinga, watuhumiwa wa njama za kuua walitumia gari Na. T 768 BDU ambalo walilitumia awali kutoka Madaba hadi Songea. Anasema walifika Mafinga saa mbili usiku na kukuta magari mawibili yakiwasubiri. Moja, Hilux Mayai ya kampuni ya Vodacom na Defender iliyowaongoza hadi Morogoro.

Akiandika kwa kujiamini, Dk. Mwakyembe anasema, "…walipofika Morogoro walipokelewa na askari mmoja anayemtaja kwa jina la Sabasita. Hapo kundi likagawanyika: Watu wanne wakiwemo wale wasomali wawili wakaingia kwenye Nissan Patrol T 845 ADH mali ya kampuni ya Caspian, na wengine wakabaki Morogoro."

Kampuni ya Caspian ni mali ya Rostam Aziz, mfanyabiashara, mbunge wa Igunga (CCM) na wakala anayejitaja kuwakilisha kampuni ya kufua umeme ya Dowans ya Costa Rica. Gazeti lilipomtafuta, hakuweza kupatikana.

Anamwambia Mwema kuwa, Mganga Majungu mwenyewe, ambaye wapelelezi wake wanaweza kuongea naye kama walivyofanya waliompa taarifa hizi, aliwapa masharti ya kutotumia silaha za moto ila njia nyingine kumuua kwanza Mwakyembe, baadaye Dk. Slaa na wengine.

Anasema mganga huyo "ametengeneza dawa ya kuwapumbaza waliohukumiwa kifo na kuwa mfano wa mbwa mbele ya chatu" ili kukimbia hasira za wananchi pale mpango wa mauaji utakapotekelezwa.

Dk. Mwakyembe anamueleza IJP Mwema, kwamba awali mkakati wa kumuua Dk. Slaa ulipangwa kutekelezwa katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, lakini ulisitishwa kwa hofu ya kuingiza nchi katika machafuko.

"…utabiri wa Sheikh Yahya Hussein mwaka jana kuwa mmoja wa presidential candidates (wagombea urais) atakufa, ulimlenga Dk. Slaa ambaye alidaiwa kubebwa na makinisa. Utabiri huo haukutimia kwa kuogopa kuiingiza nchi kwenye machafuko makubwa ya kisiasa/kidini ambayo yangewaweka pabaya hata wafadhili wa mpango wenyewe," anasema.

Wiki mbili zilizopita, Sheikh Yahaya alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kutatokea vifo vya watu kadhaa mashuhuri wakiwamo wanasiasa na mwandishi mmoja wa habari mashuhuri nchini. Wakati Shekh Yahaya anatoa utabiri wake, Mwakyembe alikuwa katika wiki ya tatu tangu awasilishe malalamiko yake polisi.

MwanaHALISI lilipowasiliana na Sheikh Yahya ili kufahamu iwapo utabiri wake unatokana na kutumiwa na watu maalum waliomlipa fedha ili kufanikisha mkakati huo wa mauaji, mnajimu huyo alisema, "Watu wasubiri matokeo."

Alisema anachokifanya yeye ni unajimu na tayari amefanya hivyo katika matukio kadhaa makubwa ikiwa ni pamoja na kuwako kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.

"Nilitabiri Raila Odinga kuunda serikali moja na Mwai Kibaki Kenya. Yametimia. Nilitabiri CCM itapata msukosuko baada ya uchaguzi mkuu, imekuwa hivyo. Sasa hapo unahoji nini?

"…Sijataja jina la mtu, hivyo watu wasijihisi kwa utabiri wangu, ila wao wasubiri matokeo. Halafu ninyi MwanaHALISI mnafanya kazi nzuri. Ipo siku nitawaita hapa kuzungumza nanyi. Ila nayi msihofu, msubiri matokeo."

Naye Dk. Slaa alipoulizwa kuhusu mpango huo, kwanza alicheka, kisha akauliza: "Nani kakuambia?" Alipoelezwa kuwa ni taarifa zilizothibitishwa na jeshi la polisi, Dk. Slaa alisema, "Basi nadhani wao ndiyo wanajua wanaohusika katika suala hilo."

Katika barua yake kwa IJP, Dk. Mwakyembe anasema kijana mmoja anayefahamika kwa jina la Hassani alitumwa kutoka Dar es Saalam kwenda Dodoma, 5 Februari mwaka huu kwa "maandalizi" ya kikosi cha mauaji. Amesema tayari kikosi hicho kimefanya utambuzi wa nyumba yake aliyopangiwa kuishi na serikali.

Anasema, "Tarehe 6 Februari 2011, mnamo saa nne usiku, kikosi hicho cha mauaji kikiwa na watu watano kiliondoka Dar es Salaam kwenda Dodoma kwa gari aina ya Land Cruiser nyeupe ya mkonga (T 360 AKU). Waliokuwa kwenye kikosi hicho ni wasomali wale wawili, mgeni mmoja wa kiume kutoka Uganda, Mustafa a.k.a ‘Master' na kijana mmoja ambaye tarehe 19 Januari 2011 aliwabeba wasomali hao kutoka Morogoro kwa gari aina ya VX Lands Cruiser T 656 APF. Kijana huyo ana shepu ya Kitusi na anaongea Kifaransa."

Jijini Dar es Salaam, Dk. Mwakyembe anasema, "Wahitimu hao wa Profesa Majungu walifikia Kiwalani karibu na Kiwanda cha Mohammed Enterprises. Jirani na kiwanda hicho kuna jengo la ghorofa, chini ni msikiti wa Waarabu unaoitwa MALKAZ na juu ni sehemu ya kuishi."

Anaeleza kuwa tarehe 5 Februari, wageni wawili zaidi waliwasili kwa ndege kutoka Uganda. Mwanaume mmoja (aliyechanganya rangi) na mwanamke mmoja (mweusi vilivyo). Anaripoti kuwa walipokelewa kwa magari mawili: moja la polisi, PT 0288 – polisi ujenzi na la pili lenye namba za kibalozi T 69 CD 82 aina ya RAV 4. Anasema, jioni wakawa na mazungumzo ya kina na raia wawili wa Somalia ambao inadaiwa ni kutoka kundi la Al-Shabaab.

Dk. Mwakyembe anasema katika maelezo yake kwamba amepata picha ya kwa nini wapiganaji wa kikundi hicho wameingizwa nchini.
Anasema, "Nimeweza kukusanya taarifa zinazodai kuwa awali walifikiriwa kuletwa wapiganaji kutoka Rwanda, lakini wazo hili lilikataliwa na wafadhili wa mpango huu ambao walitaka wanaharakati wa aina hiyo watoke Somalia. Ndipo kikundi hicho kikashawishiwa. Mimi na wenzangu hao watano tumejengewe hoja kuwa maadaui wa Uislamu tunaotumiwa na makanisa, hivyo hatuna budi kukatishwa maisha yetu."

Katika barua yake kwa IJP, Dk. Mwakyembe anasema kila siku hupata taarifa za ziada kutoka kwa raia wema kuhusu suala hili; anazitoa taarifa hizo kwa jeshi la polisi ili ziwasaidie katika upelelezi.

Kwanza, taarifa zinaonyesha raia hao wa kisomali waliingia nchini kutokea Kenya na walikwenda Dodoma kupitia njia ya barabara kwa kutumia gari aina ya RAV 4 (new model- T 816 AQS) tarehe 08 Januari 2011.

Pili, Dk. Mwakyembe anasema walipofika Morogoro walipokewa na askari Sabasita wa jeshi la polisi mkoani humo, ambapo walikaa katika hoteli mbili tofauti – Hillux Hotel na Top Life. Anamtaja aliyewafanyia booking wageni hao ni mmiliki wa Morogoro Hotel aliyemtaja kwa jina moja la Kari.

Tatu, Dk. Mwakyembe anasema magari waliyotumia wakiwa Morogoro, ni RAV 4 T 816 AQS, VX Land Cruiser STK 1287, Mercedez Benz (Station Wagon) T 874 BDT, Toyota Mark II GX100 nyeupe T 218 BKR na wakiwa Dar es Salaam wametumia magari VX Land Cruiser T 656 APF na Nissan patrol T 845 ADH.

Wakiwa Dar es Salaam, Dk. Mwakyembe anataja watu waliokuwa na mawasiliano na waliotumwa kuchukua roho yake kuwa ni "Masuhe wa Central Police Station (polisi kati), Fred Lowassa ambaye inadaiwa aliwapelekea mbuzi watatu huko Kiwalani tarehe 04 Februari 2011 na hata kuwatafutia gari VX Land Cruiser T 656 APF.

Anasema walipokuwa Dar es Salaam, tarehe 13 na 14, Januari wabaya wake walifikia nyumba Na. 551, Mtaa wa Chakechake, Upanga.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini, Rajab Mtiula, hakupatikana juzi kuzungumzia kuhusishwa kwake katika mikakati hiyo.

Gazeti lilipowasiliana na Fred Lowassa kueleza juu ya kuhusishwa katika maandalizi ya kifo cha Dk. Mwakyembe na wenzake alijibu, "Kaka katika mazingira ya kawaida tu, hilo jambo ni very serious (hilo jambo zito). Kuua ni tuhuma nzito.

Alisema, "Siku hizi kuna teknolojia ambako ukifanywa uchunguzi, itaonekana tu. Mimi nimekutana na mambo magumu sana maishani, lakini siwezi kufikia hatua ya kuua au kuhusika kuua."

Fred ambaye ni mtoto wa waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa alisema, "Yakinipata magumu, mwokozi wangu ni Mungu. Naomba Mungu, halafu huwa nasamehe. Siku zote huwa sipendi kuingia kwenye malumbano," alieleza.

Lakini Dk. Mwakyembe katika barua yake kwa IJP Mwema anasema, "Pamoja na kwamba sina imani na ushirikina au nguvu za giza, kutajwa kwa jina langu na fursa ya pekee niliyokuwa nayo ya kujua kilichokuwa kinafanyika, kukanipa ari, nguvu na shauku ya aina yake kutaka kulielewa zaidi suala hili ili ikibidi, niwataarifu wenzangu nao waelewe."

Taarifa zinasema kila aliyetajwa kuuawa amejulisha taarifa hizo na Dk. Mwakyembe kama ambavyo ameeleza katika maelezo yake polisi.


Gazeti toleo lenye makala hii
Jambo la kutisha na Kushangaza Mwakyembe aliandika barua hiyo kwa siri na kupeleka kwa IGP mwema lakina usiku huo uo taarifa zikamufikia Rostam na gazeti lake la Mtanzania lika andika habari hoyo na kumukebehi Mwakyembe!!
Njama za kumuteka Kibanda, Ulimboka zina sura halisi ambayo Mwakyembe alifichua!!
Sasa kama jamii inaweza kung'amua ni kwa nini VODACOM,CASPIAN,KAGODA wameiweka dola mfukon???
Hili ndilo kundi la kuogopwa hapa!!!
 
Naona Mwakyembe anataka kuwahaadaa watanzania hii stor ni ya 2011 naona anataka kufufuka kisiasa huyu ni mganga njaa alikuwa anatafta ulaji baada ya kupewa uwaziri kakaa kimya...majembe ya CCM Kwa sasa ni DEO FULKUNJOMBE NA KAG LUGOLA plus CHADEMA kna mwakyembe na kna sita walkuwa wanatafta madaraka ...
 
Naona Mwakyembe anataka kuwahaadaa watanzania hii stor ni ya 2011 naona anataka kufufuka kisiasa huyu ni mganga njaa alikuwa anatafta ulaji baada ya kupewa uwaziri kakaa kimya...majembe ya CCM Kwa sasa ni DEO FULKUNJOMBE NA KAG LUGOLA plus CHADEMA kna mwakyembe na kna sita walkuwa wanatafta madaraka ...
Ngugu yangu yawezekana una ukweli lakini unachuki binafsi na Mwakyembe !!!
Lakini pia huoni kama Rostam na Lowassa wamepora nchi!!!
 
Back
Top Bottom