Sooth
JF-Expert Member
- Apr 27, 2009
- 3,922
- 5,626
aha! si hasa za kwetu.........akija waziri mkuu au presidaa toka Tabora......tutakuwa na project hiyo huko.........then akija toka IR .....tunahamishia huko..................akitoka Kagera ....................tunahamishia huko. Ni mwendo wa viporo vya miradi mpaka cycle ije tena ya PM au Presidaa atoke sehemu hiyo, then project inafufuka.
Ni kweli kabisa, hatufanyi mambo strategically, bali kwa ajili ya kuwaridhisha wakubwa. Huo uwanja hauna manufaa sawa na kuimarisha reli ya kati. Reli ya kati inaweza ikaleta mabadiliko makubwa kiuchumi maana itahudumia kanda ya ziwa, kigoma, tabora na mizigo ya landlocked countries kama Rwanda na Burundi.
Ndio maana inatarajiwa kujengwa bandari bagamoyo, chuo kikuu cha kilimo katavi (wakati graduates wa SUA serikali haiwatumii) na sasa uwanja wa kimataifa wa mpanda. Akija mwingine, atajenga barabara za juu na chini Kigoma, sio kwasababu ameona ya mbele, bali kwakuwa anataka kupendezesha kwao. Lazima tupangilie vipaumbele maana hatuna resources zakutosha.
Uwanja wa Kimataifa wa Mbeya uko wapi? Kwani ungemaliziwa usingetosha kuhudumia nyanda za juu kusini-ikiwemo Mpanda? Au wa Mbeya ukimaliziwa utampa sifa Mwandosya?Hatuwezi kujenga uwanja leo ambao utashindwa kujiendesha kwa faida kwa miaka 20 ijayo, wakati kuna vipaumbele vinavyoweza kulipa na kubadilisha uchumi wa nchi leo. Yaani watu wameanza kupanda nyasi Mpanda wakati wizara ya miundombinu haikutenga fedha kwa ajili ya reli ya kati, mpaka wamerudishwa na kamati? No wonder we are so poor!