Dola Iddy Wa Chelsea
JF-Expert Member
- Sep 26, 2014
- 2,114
- 1,485
- Thread starter
- #81
Heri yako kiongozi umetumia hisia halisi na busara kutoa hoja yenye msingi na nguvu,Usalama wa mtu unaanzia kwake lakini haimaanishi kua tusitoe msaada kwa mtu wa pembeni, wadau mnauliza kwanini mleta uzi hakuingilia, kuingilia kungemaanisha kubishana na watu saba (kama anavyodai ingawa sielewi walipandaje pikipiki) wenye nia ovu.
Ingawa sioni sababu ya kutokwenda kuripoti polisi tukio zima, na pia unataka kusema hiyo klabu haina mabaunsa? Kama hawapo hapo Wadutya ugomvi ukianza nani hua anatuliza?
Anayetuliza ugomvi aulizwe ilikuaje akashindwa kuzuia tukio au kufanya observe and report.
Pole sana mkuu, napata picha mtu unapotamani kutoa msaada lakini hauwezi kuutoa kutokana na mazingira jinsi unavyojisikia.
Angalau tutafute na tumiliki bunduki, tutasaidia wengi sana.
Kiongozi labda nianze kwa kukujulisha kuwa wadutya hapo zamani ilikuwa na mabaunsa kipindi hicho pesa ilikuwepo na watu walikuwepo hivyo ilisaidia kufanya uendeshaji wa club hii kuwa bora lakini tangu mh magu atinge madarakani kituo cha polisi kikapiga marufuku ukumbi wowote wa starehe kupiga muziki mpaka saa 11 alfajiri hapo ndo ugumu wa biashara ukaanza kuonekana hao mabaunsa wakaacha kazi na idadi ya wateja ikaporomoka sana na ukizingatia kupunguzwa kwa muda wa kufanya kazi ndo kukapoteza kabisa wateja na hivi juzi tu ijumaa usiku zilichapwa ngumi za hatari na atakaepigwa ndio anasalenda na ugomvi unaishia hapo ,
Mkuu hata kama yule dada alikuwa ni kahaba vipi ila kwa jinsi alivyobebwa inatia huruma sana aisee,
Laiti ningekuwa na chombo cha moto ningelimsaidia aisee.