Clouds mnaudharaulisha Wimbo wa Taifa

Ili iwe nini!!?

Wimbo wa Taifa unachezwa katikati ya Shishi na Visingeli..

Ili iwe nini!??

Na kuna watu wanakula mshahara hapo TCRA...!??
KUNASHERIA INAYO KATAZA HAYO,AU UNAZUNGUMZA KWA UTASHI WAKO TUU?

KAMA IPO SHERIA TUWEKEE HAPATUIJUE KAMA NI UTASHI WAKO PIA TUFAHAMISHE
 
Hivi ninyi Cloudd huko vyuo mlienda somea ujinga...!!???

Wimbo wa TAIFA sio wimbo wa burudani.

Mnauplay hovyohovyo.. Wimbo huu tunapaswa kuuskia ktk special ocassion. Si hivi mnavyofanya..kuuweka wimbo wa taifa ktk playlist tena unakua ktk list ya kipumbavu.

HESHIMUNI WIMBO WA TAIFA.

We una yako. Na uhakika hujui hata kuimba. Pumba kama hizi hazitawasaidia. Sijui mnalipwa sh ngapi.
 
Ruge ndo aliasisi mpango wa kupiga wimbo wa Taifa saa Moja kamili. Hii kitu inanikera sana.
Clouds acheni kupiga wimbo huu, wimbo huu Si kila radio Au tv inaweza piga tu bila sababu za msingi Na pasipo kuwepo Na special event. Wimbo huu bwana ruge uheshimu, hujautendea haki; hata kama TBC Taifa Radio inaupiga ina haki ya kufanya hivyo kwasababu hiyo ni radio ya Taifa.
Sasa Ruge kama kweli wewe ni mzalendo na unaipenda nchi yako Na kuheshimu wimbo wa Taifa, Nakushauri acha kupiga wimbo wa Taifa mara moja ila napendekeza upige wimbo "Tanzania nakupenda kwa moyo wote, Kila nilalapo nakuota wewe"'Nakuhakikishia Clouds mtaongeza wasikilizaji na matangazo ya biashara kwani wimbo huu ndo wa kizalendo zaidi kuliko hata wimbo wa Taifa (ambao tuliuiga tu kwa wenzetu japo inabidi tu uheshimu kwasababu upo kisheria lakini hautii hamasa ya uzalendo kama huo nilioutaja)
Ahsante Mkuu....
 
Wewe hukwenda shule....

Au hata TV hutizami....

Mashuleni wimbo wa taifa huimbwa siku maalumu...tena bendera inapokua inapandishwa..

Unataka nini tena.
Kwasababu mashuleni wimbo huo huimbwa siku maalum, ndio unaleta hoja kuwa clouds wastopishwe kuupiga?

Nini tatizo na uvunjwaji washeria uliofanywa na Clouds juu ya wimbo huu??

Naona utashi umekutawala hata kwenye mambo usiyo yafaham
 
KUNASHERIA INAYO KATAZA HAYO,AU UNAZUNGUMZA KWA UTASHI WAKO TUU?

KAMA IPO SHERIA TUWEKEE HAPATUIJUE KAMA NI UTASHI WAKO PIA TUFAHAMISHE
Wewe mpuuzi sana...

Hivi hizi sheria ndo mnazijua leo....

Nakumbuka wimbo wa Taifa ni kati ya tunu katika nchi... Lazima uheshimiwe.
 
Ruge aliomba kufanya hivo akaruhusiwa
Sababu za kutaka wimbo wa taifa upigwe
1.kuimarisha uzalendo
2.watanzania tuujue
Na unapigwa weekdays saa moja Kamili
Binafsi sioni tatizo
Nani mtanzania asieujua wimbo wa taifa? Acheni upoyoyo, eti Ruge aliomba kwanani na maombi yake yalipitia mchakato gani? Mbaya zaidi ni radio binafsi inayosikika baadhi tu ya mikoa tena ile ambayo wanajua watafanya biashara. Acheni kufurahia hata mambo ya ovyo ili mradi anaefanya una uhusiano nae.
 
Mi naona kusikiliza wimbo wa taifa siyo mbaya ila tatizo muda unao pigwa bora upigwe saa 12kamili asubuhi
Kwanini? Hautakiwi kupigwa bila sababu ya kimantiki, kwani saa 12 asbh kuna nini? Tuache mazoea kwakuwa wenye nguvu mnavibasaba nao!!
 
Mimi sii kichaa kuanzisha uzi huu...

Leo kilichofanyika ni dharau kubwa kwa Wimbo wa TAIFA..
tatizo lako huwa una jazba mno kwani kuna mtu kakuambia we kichaa?
Ruge katoa sababu za wimbo kupigwa na kaomba kibali hajajiamulia.
Mi binafsi nshaanza kusahau mabeti ya wimbo na possible kuna watu hawaujui kabisa, hiyo mida ya sa moja tunapata fursa ya kuusikiliza kitu ambacho ni sawa kabisa.
Nawe useme sababu zako kwanini usipigwe acha bla bla
 
Nani mtanzania asieujua wimbo wa taifa? Acheni upoyoyo, eti Ruge aliomba kwanani na maombi yake yalipitia mchakato gani? Mbaya zaidi ni radio binafsi inayosikika baadhi tu ya mikoa tena ile ambayo wanajua watafanya biashara. Acheni kufurahia hata mambo ya ovyo ili mradi anaefanya una uhusiano nae.
Unajikuta unajua kumbe hata hujui aliomba wapi, paki pembeni, uhusiano gani sasa na we unavompinga ulikua na uhusiano nae?
 
Mimi sii kichaa kuanzisha uzi huu...

Leo kilichofanyika ni dharau kubwa kwa Wimbo wa TAIFA..
Tena kubwa, nilikaa na wanangu wote wali pay attention. Baba wimbo wa taifa unapigwa, nikawahi kukaa niusikilize, nikitafakali mambo mengi sana, nikiongea itakuwa uchulo au uchochezi. Shenzi type tena wapumbavu sana, inapigwa singeli. Ungeona sura za wanangu baada ya kupigwa songeli, ndio ungejua wameumia kiasi gani. Sasa watu, wanaofikilia kwa kutumia matumbo yao, washangilia eti ni uzalendo, pumbafu kabisa, tena mafi ya umbwa. Sisikilizi tena clouds radio.
 
tatizo lako huwa una jazba mno kwani kuna mtu kakuambia we kichaa?
Ruge katoa sababu za wimbo kupigwa na kaomba kibali hajajiamulia.
Mi binafsi nshaanza kusahau mabeti ya wimbo na possible kuna watu hawaujui kabisa, hiyo mida ya sa moja tunapata fursa ya kuusikiliza kitu ambacho ni sawa kabisa.
Nawe useme sababu zako kwanini usipigwe acha bla bla
Mjinga wewe umekuja na hoja dhaifu sana, eti wewe ulianza kusahau beat, una akili kweli? Beat wewe ulitaka ukaupige wapi, ndio maana unafurahia upuuzi huu wa mawingu radio.
 
Huo ni wimbo kama nyimbo nyingine tu
Hapana mkuu wimbo wa Taifa hauwezi kuwa sawa na seduce me, nataka kulewa, nampa papa, mwanaume mashine na nyingine kama hizo! Wimbo wa Taifa ni moja ya alama za Taifa letu pendwa! Kama sisi wenyewe hatuta uheshimu wimbo wetu wa Taifa na wengine pia hawata uheshimu! Tukichekea swala hili wataupiga mpaka kwenye vilabu vya pombe! Zamani wimbo huu ulipigwa kwenye matukio maalum ya kitaifa!
 
Unajikuta unajua kumbe hata hujui aliomba wapi, paki pembeni, uhusiano gani sasa na we unavompinga ulikua na uhusiano nae?
Mjinga si ulisema aliomba kwanani? Msishindane na akili kubwa, huku mkiwa na vikozi vya uhandishi wa Habari. Tuaongelea ethic's ya tunu za taifa mshamba wewe. Tunu za taifa ni pamoja na wimbo wa taifa, haiwezekani radio za mtaani ziwe zinaupiga kwa sababu zao binafsi tena za kujiongezea kipato, halafu wajinga kama wewe mnatetea. Pita mbali na huu uzi.
 
Back
Top Bottom