Clouds fm inaliangamiza taifa

Uingereza wamesema tz haitopata msaada wowo,kama haitakubali kuwatambua mashoga,wao lini wataanza promo,sijawaskia nayo ni mambo yao!!
 
Umeona eh! Redio gani watangazaji hawana profesional? Kipindi pekee kinachoelimisha clouds ni njia panda tu. Vingine nyanya
 
Hata kama kuna uhuru wa habari bado Clouds haifai tu,kwa mnaoifagilia endeleeni ila kiukweli pale hakuna kitu na nilishaach siku nyingi wala kwangu akuna ruhusa kusikiliza upuuzi wa redio kama hiyo,ni afdhali nisikilize WAPO FM
 
ile radio ina vilaza watupu,
tena hawaelewi hata wanachotamka, puuuuuuuuuu.
 
mm nashindwa kuelewa,kila cku clouds clouds clouds,km huipendi si usisikilize,tune wapo.radio 1,praise power etc.mnaipenda ndo mana mnawasikiliza,na wenyewe wanajuwa hivyo,asilimia 60 ya watu wanaoenda maofisini asbh ama jioni kurudi iwe kwenye daladala ama magari binafsi wanatune clouds,huo ndo ukweli.ndo mana hoja za power break fast na jahazi haziishi humu,
Kwi kwi kwi kwi VIVA CLOUDS
 
Unapokosa ajira sehemu isiwe sababu ya kuanza matusi kuna usemi
unasema "usitukane mamba wakati hujavuka mto" Nakumbuka Tambwe
Hiza alisema "mtu kujiunga na CCM ni sawa na kumuoa mama yako mzazi"

Hakuna Sababu ya kuwashambulia na kuwakandia kiasi hicho kama umeshindwa
bora usikilize redio uhuru, hii chuki si nzuri we unafikiri Watanzania wana muda wa
kusikiliza redio kwa sana kiasi hicho? Maisha yenyewe yako wapi?

Kama unataka sikiliza hutaki kaa kando au sikiliza TBC taifa!
 
Ukisikiliza Clouds Fm kwa muda mrefu lazima uwe punguani..kuna watangazaji pale uwa nashindwa kuelewa wanafanya nini;
Bonge wa PB
Gerald Hando
Barba Masoud
PJ
Kibonde nk

Mi nawazimia sana hao wote uliowataja. they always make ma day!!!! keep it up guys!!
 
Radio Clouds isipoangaliwa italiangamiza taifa. Radio hii inayojinasibu kuwa ni radio ya vijana haina jambo la maana zaidi ya kuwajrngea watanzania utamaduni wa kitumwa, utamaduni wa kuthamini utamaduni wa nje hasa wa Marekani na watu wa Marekani. Utamaduni ambao umepelekea vijana wengi wa ktanzania kuiita nchi yao jalalani.

Radio hii pia inajenga msingi wa kuwatenga vijana kimatabaka. Imejipa taswira ni radio ya vijana wa ushuani ambao wana nafasi nayeyote anayetaka kuonekana ameendelea ni sharti ajiunge nao. Radio hii inawafundisha vijana tabia ya kujipendekeza kwa wakubwa kwa hali yoyote ile hata kama hao wakubwa wanatenda mambo ya ovyo na bahati mbaya sana kuna baadhi ya wakubwa wenye nydhifa za kitaifa wanaliunga mkono hili kiasi cha kukubali hata kununuliwa keki zao za birthday na radio hii.

Radio hii haiwapi mwongozo vijana inaodai kuwalenga washiriki kikamilifu katika kuamua na kusimamia ustawi wa taifa lao badala yake wamejengwa kuwa wapokeaji na wanaosubiri kudra kutoka kwa wanaotoa neema.

Watangazaji wa radio hii wanajikweza na kujilazimisha kuwa macebreties wakiwa kwenye vipindi wazungumzie magari yao, wawataje watu maarufu ili kuonekana nao ni muhimu na pia wana uhusiano na watu mashuhuri ili kijipa uhalali wa wao kuendelea kuwahadaa na kuwatia kiini macho vijana na wananchi wa Tanzania.

Radio hii inafika mbali kiasi cha kuwafanya watangazaji wao kuwa watu maarufu na mashuhuri hata kama wakiwa watupu vichwani kiasi kwamba wanatumia umaafurufu huo kujipatia nafasi mbalimbali za uongozi katika vyama vya michezo na baadae kuchukua uongozi wa kisiasa.

Radio inawatenga vijana kutokana na wapi wametokea na nasaba zao ni zipi. Inajihusisha zaidi na matajiri na endapo kama watajuhusisha na mtoto wa uswazi basi jua kuwa huyo ana kipaji na wanataka kumtumia kwa manufaa yao.

Radio hii inapandikiza chuki ya makundi na matabaka ndani ya vijana. bahati mbay zaidi wanasiasa wariho wenye kutaka sifa wanajisogeza karibu na radio hii kwa uchu wao na tamaa zao za kisiasa.

Tanzania yetu sote. Wote tulikuwa katika hali ya usawa na kupendana kabla wenzetu wachache walipoanza kuiba na kufuja. Huko hakuwafanyi wawe na haki ya kidhihaki na kuwacheka wengine kwani hicho wanachoringia ni mali yetu sote. Wale vijana wanoipenda nchi wakaamua kwenda shule na kuijenga nchi kupitia njia stahiki, halali na zinazoeleweka wasidhihakiwe na kuonekana wajinga. So vijana wote wa kitanzania wenye kutaka kufanya mzee Juma mwapachu anachokiita Bongoism na si vijan wote baba wakwe ama mama wakwe zao wan music systema za kuwafanya wapige kwenye matamasha na si vijana wote wenye Ma God father wa kupewa kazi ambazo malipo yake ni makubwa kuliko uhalisia wa kazi yenyewe. Clouds wanapaswa walifahamu hili na pia wajue kuwa wanjukumu la kuwaelimisha vijana wa kitanzania kuhusu haki zao na kuwasaidia kuwatangaza pale wanapozidai na si kuwabeza kama vile walipowabeza vijana wa chuo kikuu walipodai kuongezewa posho zao.

Kama kuna jambo ambalo naliiona lapaswa kuangaliwa kwa macho mawili basi ni hili la kuwepo kwa radio zenye kuwafanya au kutaka kuwafunza watanzania hasa vijana utumwa wa fikra na Clouds Fm yapaswa kuangaliwa kwa macho mawili na kama zipo radio nyingine za namna hii basi kwa pamoja tuseme walichokipanda chatosha, sasa basi.

Mhhhhh nyie wafuasi wa chadema si muanzishe redio yenu! kwani lazima muasikilize clouds. Aaah mnanichosha na malalamiko ya clouds kila siku hapa Jf.
 
wivu wa kike wa kitotoooo donge la pipi ya kijiti!!!

N haibu kuwa na chombo cha habar ambacho cku nzma hakiongelei suala la kuijenga nch yetu maskn hv..km vyombo vya habar vngekua vnahmiza vjana wasome na kufanya kaz kwa bdii hawa vjana wangeelewa na kua hvyo..Lakn hch kredio knafundsha Ushalabalo ambao unafanya vtoto vnafel vnabak na vsifur vyao mitaan..Nngekua na uwezo nngejtoa mhanga hapo nkalipulie mbal..Mkia wao..wanaharbu taifa la nyerere
 
hiki kredio uchuara knachochangiana na nchi za nje kuharbu taifa il waje kututawala n cha nan?..knajaza mawimbi hewan tuu..Ndo maana alkua anakataza vyombo huru vya habar maana aljua athar zake..Nitumen nikajtoe mhanga pale 2katekeze kabsa maana 2kfuata sheria watatoa rushwa..Watanzania wenzangu hamjui athar za redio ITEREHEMWE ya Rwanda?..ZIFUNGIWE hz redio uchuara
 
Nyerere alkua ana akil sana..Nch za wenzet hakuna redio za uchuara wala magazet ya udaku wakja kwe2 huwa wanakosa magazet yanayohusu kujenga nch km ya kwao..Cku nkckia imefungiwa h redio na kupewa taasis yoyote ya mazngra au klmo il iitumie kuelmisha watanzania maana ndio k2 kinachotakiwa ntafurah sn...
 
hawa ni viraza tu twaache na siasa za kudandia na kubeza watu awana tofauti na magazeti ya shigongo
 
mm nashindwa kuelewa,kila cku clouds clouds clouds,km huipendi si usisikilize,tune wapo.radio 1,praise power etc.mnaipenda ndo mana mnawasikiliza,na wenyewe wanajuwa hivyo,asilimia 60 ya watu wanaoenda maofisini asbh ama jioni kurudi iwe kwenye daladala ama magari binafsi wanatune clouds,huo ndo ukweli.ndo mana hoja za power break fast na jahazi haziishi humu,
Kwi kwi kwi kwi VIVA CLOUDS

We nae c walewale.
 
Back
Top Bottom