Clouds FM, hiki mnachofanya ni kampeni kwa CCM

Clouds FM, hiki mnachofanya ni kampeni kwa CCM

na wasipo acha nguvu ya umma iwafuate apo ofisini kwao!!?
 
Ruge ameshakunja 1b kwaajili ya kazi hiyo yakumchafuwa mgombea wa ukawa kwahiyo hapo wako kazini
 
Ni kazi ya Ruge na January Makamba.... Uzuri wananchi tushaawapuuza clouds
 
mkiwamaliza kuwasema clouds, nendeni na ITV pia, wao habari zao khs ccm huwa ni zile mbaya mbaya tu
Kwani ccm wana habari mzuri kama chama wao ni ngumi tu hadi mawaziri wanapigana
 
wanamhujumu Lowassa hata kwenye cloud tv,cloud radio kwa nini hawatoe haki kwa wagombea...yaani Lowassa ana salimia,makufuli yeye anatangaza sera!magufuli nae aseme ccm oyeeee hapo ndio haki....jamani makamanda hujuma uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Mwaka huu na mgombea wenu huyo ambaye ana utiriri wa hoja dhidi yake kila mmoja mtamuona mbaya,maana kumzungumzia haikwepeki,mtalaumu vyombo vyote na bado kuanza case by case wakati wa kampeni
 
Ni sawa maana ccm wameteka vyombo vya taifa kuwa mali yao habarileo,tbc redio tanzania nk

kwahiyo itv inafanya vizuri
 
Kimantiki unaweza kuona kama ni tatizo ila kimkakati ni hatari lakini kwa kuwa anayetoka nje ya ccm ni lowassa na sio magufuli wajenga hoja wanaweza kulitumia hilo hilo tangazo kama promo ya lowassa dhidi ya magufuli kwani yeye bado yuko ndani ya ccm. Ni mitizamo tuu
 
Yah sijaoona sera ya lowasa mpaka wamuweke akinadi sera maana ye ni kusema tu anatamani wanachi wawe matajiri hahahahahaaa huyu kweli anafaa kua mfugaji tu hata kuingea hawezi FISADI TEMBOO
 
mkiwamaliza kuwasema clouds, nendeni na ITV pia, wao habari zao khs ccm huwa ni zile mbaya mbaya tu
Ni kwa sababu ccm hakuna zuri wanalofanya zaidi ya matatizo kila kukicha
 
Nyie jamaa mnalialia mpaka kero!Mbona wafuasi wa DP ya Mch.Mtikila hawalalamiki kutokusikia hata sauti ya mgombea wao kwenye hilo tangazo?Au wapinzani ni nyinyi tu?Anzisheni vituo vyenu eboo.
 
Naandika ujumbe huu nikiwa na akili timamu clouds fm sisi mashabiki wenu wengi ni vijana na tupo ukawa lkn kwa mnachokifanya sio kizuri mnapiga kampeni za wazi kabisa kwa ccm kwani kampeni zimeanza? tuna watahadharisha juu ya hilo sio vzr naomba muwaze kuhusu kesho kama ukawa ikashika nchi mtakuwa kwenye nafasi gani
MSIPENDELEE UPANDE MMOJA JAPO NDIO GARAMA YA KUNUNULIWA.
 
watanzania kama ndo akili zetu za kufikiri zimeishia hapa kweli hatustahili kulalamika kwanin hatuna maendeleo....!!
 
ninyi mna mwongelea bwana joseph kusaga na ruge?
Hawa ni walamba miguu wa ccm.niwa nafiki sana hawa watu. Kipindi lowassa yupo ccm hawa hawa walikua kila siku lowassa lowassa lakini leo lowassa kaamia chadema imekua nongwa kwao sasa wanajikomba kwa magufuli.

Mimi uwaga siwapendi watu wanafiki kama hawa hata watangazaji wao wamesha wa ambukiza hiki kitabia, wakina harson kamoga na samwel sasari kile kipindi chao cha 360% kimekua ni umbea umbea unafiki mtupu,

ngoja mzee wa maamuzi magumu aingie ikulu utawaona tena wanageuza mwelekeo na kutaka kumwandalia dhifa ili kujikomba komba,
Hawana tofauti na wewe ambae ni MLAMBA MIGUU ya MBOWE....................Na jiangalie sana utaolewa kam hawa.............................................
[h=3]UKOO WA CHADEMA BUNGENI WAANIKWA: GAZETI LA UHURU[/h]






BAADHI ya wabunge wameiumbua CHADEMA, wakieleza kuwa chama hicho ndicho kinaongozwa kwa utawala wa kifalme.


"Lissu kaja na dada yake. Ukienda kwa Mwenyekiti wa Chama ana ndugu watatu, Slaa kuna mke wake, nani ana utawala wa kifalme? Ndesamburo amekuja na mtoto wake na mkwe wake, Samahani Mh. Ndesamburo"

Akichangia juzi, muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011,
Assumpter Mshama (Nkenge –CCM), alisema utawala wa kifalme upo CHADEMA.

“Mfadhili wao amekuja na mtoto wake, kuna mdogo wake, ukienda kwa Lissu kaja na dada yake. Ukienda kwa mwenyekiti wa chama ana ndugu watatu, nani ameleta ufalme zaidi,” alihoji.

Aliongeza: “Slaa kuna mke wake, nani ana utawala wa kifalme, Ndesamburo amekuja na mtoto wake na mkwe wake, samahani mheshimiwa Ndesamburo.

“CCM ilitengeneza utaratibu wa kupata viongozi wa viti maalumu, wao si kifalme tu, tuseme ni kaskazini tu, nawashangaa watu wanaojiita CHADEMA, wenzako wako bungeni huulizi wamepatikanaje.”

Kwa upande wake, Livingstone Lusinde
(Mtera-CCM), akichangia jana, alisema CHADEMA ndiyo yenye tabia ya kupeana madaraka kwa kufuata unasaba.

Alisema viti maalumu vimetolewa kwa unasaba, na kama hilo lingefanywa na CCM ingekuwa wimbo kila siku.

“Ndiyo maana humu ndani wamo wakwe, dada, kaka, ingekuwa ni kwa CCM ingekuwa wimbo kila siku. Nashangaa wanaposema rais anaongoza kifalme,” alisema.

Lusinde alisema wanaotoa vitisho vya kuandamana na kwamba wapo tayari kufa kwa ajili ya katiba waachwe wafanye hivyo kwani wa kuzuia fujo wapo.

“Wanaotaka kufanya vurugu waachwe tu, wengine wanasema wapo tayari kufa kwa ajili ya katiba. Mimi sipo tayari nataka nione katiba mpya, ambayo Watanzania wamekuwa wakiitaka kwa muda mrefu,” alisema.

Lusinde aliohoji busara ya wazee wa CHADEMA ambao wameshindwa kutoa kauli baada ya vijana wao kuchafua hali ya hewa.

Mbunge huyo alisema CHADEMA inafanya hivyo kutokana na ahadi ya fedha waliyopewa na Ujerumani.

CHADEMA imesusa kujadili muswada huo unaohitimishwa leo, baada ya kujadiliwa kwa siku nne, kwa kile wanachodai umekosa uhalali kwa kukiuka Kanuni za Bunge.

Hata hivyo, CHADEMA imekuwa ikijibu hoja zinazojadiliwa na wabunge bungeni, kupitia mikutano na waandishi wa habari inayofanyika kila siku mchana, ambapo katika mkutano wa jana imeliomba bunge kutopitisha muswada huo.

Mikutano hiyo imekuwa ikiitishwa na viongozi wa CHADEMA, John Mnyika (Ubungo) na Tundu Lissu (Singida Mashariki), ambaye Jumatatu wiki hii aliwasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni, kuhusu muswada huo.

Katika maoni hayo, alipendekeza baadhi ya mambo kwenye muswada huo na pia aliwachefua wabunge kutokana na hoja zake kuhusu Muungano na pia kutamka kuwa Tanzania ina urais wa kifalme.

John Lwanji (Manyoni Magharibi-CCM), alisema wanachofanya CHADEMA ni sawa na kiini macho katika mazingaombwe, akitumia neno abrakadebra.

Benardetha Mushashu (Viti Maalumu-CCM), alihoji CHADEMA walitoka bungeni kwa kanuni gani na mbona hawachukuliwi hatua.

“Wanawalaghai wananchi, Lissu alichangia muswada. Wanaharakati wanatangaza kufanya maandamano yasiyo na kikomo kama kwamba hakuna serikali, wakijaribu wataona,” alisema.

Alisema kinachoendelea Arusha ni matokeo ya maandamano ya kila siku, ambayo hivi sasa yameanza kushamiri Mwanza, ambapo watu wanapigwa mabomu ya machozi.

“Libya walianza na maandamano, Gaddafi ameuawa, lakini hivi sasa wanauana,” alisema.

Wakati huo huo, Spika wa Bunge, Anne Makinda, amesema hamlazimishi mbunge kuingia kwenye kamati, bali anachofanya ni kufuata Kanuni za Bunge na Katiba.

Alisema hayo bungeni jana, kutokana na malalamiko yanayotolewa na CHADEMA na NCCR-Mageuzi kwamba, spika alilazimisha wabunge kuingia katika Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala, kujadili muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011.

Spika Anne alisema CHADEMA hawakutumia busara kutoka ndani ya ukumbi wa bunge, bali wangewasilisha hoja zao, na endapo wangeshindwa, basi wangeshindwa kishujaa.














 
Clouds Ni Maadui wa watu na umma wa watanzania.

Clouds wanaongoza kwa kukalia haki za wasanii, angalia bifu ya Sugu, Lady JD, mwisho wa siku wasanii walizidi kupaa juu.

Sasa hivi wamesimama na kupinga mabadiliko wakitumia redio hiyo. Hakika wamefanikiwa kuchora mstari wa kuonyesha wao ni wapinga mabadiliko na maadui wa mabadiliko.

Wana haki ya kufanya walivyofanya, lakini kwa wengi wamepoteza nafasi yao waliyokuwa wamebakiwa nayo mbele ya wananchi.

Walioifikisha clouds hapo ilipo ni wananchi wa kawaida , na ni wananchi hao hao waliowafikisha hapo walipo.

CCM haitawasaidia , nguvu ya chombo chochote ni umma, wamekwisha hao na hela mliyopata CCM ndio ya mwisho
 
Back
Top Bottom