Clouds FM, hiki mnachofanya ni kampeni kwa CCM

Clouds FM, hiki mnachofanya ni kampeni kwa CCM

Halafu wacha kupotosha usijifanye hamnazo, kinacholalamikiwa hapo ni upendeleo wa wazi wazi kwa CCM ambao unafanywa na hao Chouds, haiwezekani wanaruhusu mgombea wa CCM anadi sera halafu wa UKAWA atoe tu salamu! Msitufanye sisi hatuna akili tunajua kutofautisha embe na nanasi!

hivi ile ya magufuli ni sera?mi sijaona sera yoyote hv ile kauli inaweza ikaleta mabadiliko yoyote ktk nchi?maana mi nnavojua sera yoyote itachochea mabadiliko ktka nchi....hv kusema vile tu wew unaweza ukawa tayar umevutiwa kumpgia magufuli kura?
 
Wakuu Radio CloudsFM ina promo ya tangazo lao la kipindi chao kipya kuhusu siasa kuelekea uchaguzi mkuu.

Kwenye tangazo lao la kipindi hicho kipya wameweka sauti ya Magufuli akiongea kwa zaidi ya sekunde kumi akisema "maendeleo ya kweli yatatoka kwenye kiongozi anayetoka CCM"

Alafu naweka sauti ya Lowassa anasema "Peopleees zungusha zungusha"

Moya kwa moja promo hii ni kampeni ya kwa CCM maana mgombea wake ana nadi sera za chama au kujipigia debe, kama wako huru na siyo kampeni kwa ccm , walipaswa kuweka sauti ya Magufuli akisema "CCM oyeee" ili kuendana na anachozungumza Lowassa kwani Lowassa anatoa salamu ya chama na Magufuli ana nadi sera za chama.

Hili ndilo bao la mkono alilosema Nape.


Acheni kulalamikia mambo ya kipuuzi.
 
Wadau, kuna tangazo moja linazungumzia watu na timu zao katika siasa, ambapo utakua unapokea updates juu ya wagombea wako wa urais kupitia simu yako ya Whatsapp.

Katika tangazo hilo, Magufuli anasikika akisema eti kiongozi makini anatoka ndani ya CCM, huku Lowassa anasema tu eti Peopleeez.!

Hivi hapa kuna nini? Kama siyo kumpigia kampeni fundi gereji? Au nyie wadau mnasemaje?
 
Hata mimi naona hawakuweka relation kama wangetaka wangeweka ya magufuri akisema ccm oyee
 
... Wadau, Kuna Tangazo Moja Linazungumzia Watu Na Timu Zao Katika Siasa, Ambapo Utakua Unapokea Updatez Juu Ya Wagombea Wako Wa Urais Kupitia Simu Yako Ya Watsup. Katika Tangazo Hilo Magufuli Anasikika Akisema Eti Kiongozi Makini Anatoka Ndani Ya Ccm, Huku Lowassa Anasema Tu Eti Peopleeez.! Hivi Hapa Kuna Nini? Kama Siyo Kumpigia Kampeni Fundi Gereji? Au Nyie Wadau Mnasemaje.?

Baada ya kujiridhisha kwamba wapo kwenye timu isiyotaka mabadiliko, nimeanza Kampeni ya
#KataAMawiNGu,

#KataAClouds ,
#KataawapingaMabadiliko
 
Hata mimi nilivyo sikiliza hilo tangazo kwa mara ya kwanza kabisa niliona kabisa kuwa tangazo lao limeegemea upande mmoja!
 
Kweli mkuu ni upumbavu wanaofanya clouds fm na hauta vumilika hata kidogo nawasihi waache kutumika haita wasaidia km redio yenu imejengwa kw misingi ya ccm bhasi kusaga na Ruge mtuambie lile tangazo nilakubaka democracy kabisa kama Chadema wanasema People's power!!!!!! Kwa nn CCM wasiseme Kidumu chama cha Mapinduzi!!!! Shame clouds nawambia mafuriko mwaka huuu hayaepukiki na tuta dial na nyie
 
Sina kumbukumbu mara ya mwisho lini nlisikiliza wafu fm
 
....sugu lazima awe kiongozi wa serikali kuwashugulikia wahuni wa habari wote ukawa itakapoandaa baraza la mawaziri...
 
Back
Top Bottom