Amalinze
JF-Expert Member
- May 6, 2012
- 6,780
- 5,318
Habari Wanabodi,
Nipo nasikiliza Clouds FM kipindi cha XXL Segment ya "Album Review". Leo wana Review Album (2003) ya Mwana FA ya "Toleo Lijalo" yenye nyimbo kama 'Wanapendana', 'Alikufa kwa Ngoma' etc. Kwenye wimbo wa 'Alikufa kwa ngoma' ameimba na Anaconda (Lady Jay Dee) cha kushangaza kwenye huo wimbo wakati wana review ikifika sehemu ya chorus ya Jide wana-mute inasikika beat tu. Kitendo cha Clouds FM kama taasisi kampuni nzima kuweka beef na msanii mmoja inajidhihirisha Clouds FM ni radio ya wahuni tu.
Clouds FM sio mara ya kwanza kufanya upumbavu huo, nakumbuka kipindi cha nyuma Inspector Haroun alienda nao tofauti, kipindi hiko wimbo wake wa "Buzi" ndio ulikuwa una-hit basi jamaa kila ikifika pale anapochana Inspector sauti wanaondoa inasikika beat tu.
Kwenye ngoma ya Ben Pol "Jikubali" kuna moja ya mstari unaimbwa "Nampenda Lady jay Dee,namzimia Zitto" ile sehemu ya neno Lady Jay Dee wanaisugua (Scratch) na ilo neno halisikiki kabisa.
Kwenye kuadhimisha miaka 15 ya Dully sykes, kwenye promo walikuwa wanapiga nyimbo za nyuma za Dully Sykes, kuna ngoma inaitwa Bijou inavyoanza ina neno "Okay mbili sifuri sifuri nne, P-funky kinywele kimoja" ilipoanza hapo kwenye P-funky wakaikata kabisa wakaipeleka mbele.
Kwa Mchezo huo wa kitoto unaofanywa na Clouds Media inaishushia hadhi sana hiyo kampuni. Kitendo cha kampuni hiyo kufanya mambo ya utoto ni wazi redio inaendeshwa na makanjanja na sio watu wenye weledi. Clouds FM ikubali pia matakwa ya wasanii, kama msanii akikataa kufanya deal kwa sababu anaona haimfaidishi yeye ni haki yake kukataa na si kigezo cha kutopiga nyimbo zake.
Kuna watu watasema kwamba redio zipo zaidi ya 60 na TV zaidi ya 20 kwanini wasanii wailalamikie Clouds tu? Hapa tunacholalamika ni kufinya (mute) sauti yeyote iliyopo kwenye nyimbo alizoshirikishwa msanii walioenda nae tofauti. Kama wanapiga wimbo wa Ben Pol waachie wimbo kama ulivyo na si ku-mute majina ya watu waliotajwa wenye beef nao.
CLOUDS MEDIA ACHENI UTOTO.
Nipo nasikiliza Clouds FM kipindi cha XXL Segment ya "Album Review". Leo wana Review Album (2003) ya Mwana FA ya "Toleo Lijalo" yenye nyimbo kama 'Wanapendana', 'Alikufa kwa Ngoma' etc. Kwenye wimbo wa 'Alikufa kwa ngoma' ameimba na Anaconda (Lady Jay Dee) cha kushangaza kwenye huo wimbo wakati wana review ikifika sehemu ya chorus ya Jide wana-mute inasikika beat tu. Kitendo cha Clouds FM kama taasisi kampuni nzima kuweka beef na msanii mmoja inajidhihirisha Clouds FM ni radio ya wahuni tu.
Clouds FM sio mara ya kwanza kufanya upumbavu huo, nakumbuka kipindi cha nyuma Inspector Haroun alienda nao tofauti, kipindi hiko wimbo wake wa "Buzi" ndio ulikuwa una-hit basi jamaa kila ikifika pale anapochana Inspector sauti wanaondoa inasikika beat tu.
Kwenye ngoma ya Ben Pol "Jikubali" kuna moja ya mstari unaimbwa "Nampenda Lady jay Dee,namzimia Zitto" ile sehemu ya neno Lady Jay Dee wanaisugua (Scratch) na ilo neno halisikiki kabisa.
Kwenye kuadhimisha miaka 15 ya Dully sykes, kwenye promo walikuwa wanapiga nyimbo za nyuma za Dully Sykes, kuna ngoma inaitwa Bijou inavyoanza ina neno "Okay mbili sifuri sifuri nne, P-funky kinywele kimoja" ilipoanza hapo kwenye P-funky wakaikata kabisa wakaipeleka mbele.
Kwa Mchezo huo wa kitoto unaofanywa na Clouds Media inaishushia hadhi sana hiyo kampuni. Kitendo cha kampuni hiyo kufanya mambo ya utoto ni wazi redio inaendeshwa na makanjanja na sio watu wenye weledi. Clouds FM ikubali pia matakwa ya wasanii, kama msanii akikataa kufanya deal kwa sababu anaona haimfaidishi yeye ni haki yake kukataa na si kigezo cha kutopiga nyimbo zake.
Kuna watu watasema kwamba redio zipo zaidi ya 60 na TV zaidi ya 20 kwanini wasanii wailalamikie Clouds tu? Hapa tunacholalamika ni kufinya (mute) sauti yeyote iliyopo kwenye nyimbo alizoshirikishwa msanii walioenda nae tofauti. Kama wanapiga wimbo wa Ben Pol waachie wimbo kama ulivyo na si ku-mute majina ya watu waliotajwa wenye beef nao.
CLOUDS MEDIA ACHENI UTOTO.