Clinical officer vs general agriculture

Clinical officer vs general agriculture

Fredrick Mmari

Senior Member
Joined
Jul 8, 2013
Posts
144
Reaction score
37
Habari wana Jf

Katika swala la fursa za kutoka kimaisha na kujiajiri

Diploma gani nzuri kati ya hizi?

Naomba sababu katika kutetea hoja yako

1.Clinical Officer

2.General Agriculture
 
Kama unataka kutumikishwa na serikali Clinical officer ni nzuri zaidi, ila kama unataka kazi za kujiajiri na mwepesi wa kuchangamkia fursa nenda agriculture kama jina lenyewe Agriculture general ,unakuwa upo wide na fursa ni nyingi tofauti na afya ambayo utategemea kwenda kushinda hospitali tu, na usisahau kuwa Uuguzi ni WITO pia.,Ni ushauri tu.
 
Mpaka sasa kwa hapa Tanzania, Diploma pekee yenye Maana, Fursa na Uhakika mkubwa Ajira ni CLINICAL OFFICER.

Kama Degree ya Agriculture General haina faida yoyote kwa sasa, Diploma yake itakuwa na nini cha maana?
 
Kama unataka kutumikishwa na serikali Clinical officer ni nzuri zaidi, ila kama unataka kazi za kujiajiri na mwepesi wa kuchangamkia fursa nenda agriculture kama jina lenyewe Agriculture general ,unakuwa upo wide na fursa ni nyingi tofauti na afya ambayo utategemea kwenda kushinda hospitali tu, na usisahau kuwa Uuguzi ni WITO pia.,Ni ushauri tu.
Unazungumza jambo usilolijua kabisa, suala la kujiajiri hapa Tanzania ni mtiti mzito sana, Ni kujidanganya kabisa kudhania kuwa Ukisoma basi utaweza kujiajiri kwa hapa Tanzania. Wasomi wengi ni waoga wa kujiajiri na pia hawawezi kujiajiri kabisa.

Ni vipi unaweza ukajiajiri kwa Diploma ya Agriculture General halafu ushindwe kujiajiri kwa Clinical Officer?

Haihitaji kuwa msomi wa mambo ya Agriculture ili kuweza kujiajiri kwenye Kilimo. Mtu yoyote yule hapa Tanzania anaweza kujiajiri kwenye Kilimo. Kilimo kwa tanzania ni kazi inayofanywa na mjinga(Ambaye hakukwenda shule), aliyekosa kazi nyingine ya kufanya.

Ni siku hizi tu, tena kwa wajasiriamali wachache ambao wamekwenda kuwekeza mitaji yao kwenye Kilimo. Na karibu watu wote hao, hawakusomea kabisa Agriculture.
 
Clinical officer ni best compaired Dip ib Agric General ukiwa mwajiri wa serikali Maana Mshahara anaolipwa CO ni sawa na mshahara wa graduates wa Elimu au Agriculture.
Pia kama una mtaji unanaweza ukafungu duka la madawa ama zahanati
Tukija kwa Dip Agr nayo ni nzuri kama utaamua kujiajiri kwanza hubanwi na mtu hata jama ukiwa mwajiri una mda wa kufanya mambo yako ila zote zina hitaji initial capital nzuri ili mambo yaende vizuri
 
Clinical officer ni best compaired Dip ib Agric General ukiwa mwajiri wa serikali Maana Mshahara anaolipwa CO ni sawa na mshahara wa graduates wa Elimu au Agriculture.
Pia kama una mtaji unanaweza ukafungu duka la madawa ama zahanati
Tukija kwa Dip Agr nayo ni nzuri kama utaamua kujiajiri kwanza hubanwi na mtu hata jama ukiwa mwajiri una mda wa kufanya mambo yako ila zote zina hitaji initial capital nzuri ili mambo yaende vizuri
Ahsante kwa ufafanuzi.

Nilichoelewa,
CO umesema ni best ila nikionacho ni kubanwa sana ila agriculture unaweza Fanya mambo yako vizuri na ukatoka bila kubanwa kama utajiajiri
 
Unazungumza jambo usilolijua kabisa, suala la kujiajiri hapa Tanzania ni mtiti mzito sana, Ni kujidanganya kabisa kudhania kuwa Ukisoma basi utaweza kujiajiri kwa hapa Tanzania. Wasomi wengi ni waoga wa kujiajiri na pia hawawezi kujiajiri kabisa.

Ni vipi unaweza ukajiajiri kwa Diploma ya Agriculture General halafu ushindwe kujiajiri kwa Clinical Officer?

Haihitaji kuwa msomi wa mambo ya Agriculture ili kuweza kujiajiri kwenye Kilimo. Mtu yoyote yule hapa Tanzania anaweza kujiajiri kwenye Kilimo. Kilimo kwa tanzania ni kazi inayofanywa na mjinga(Ambaye hakukwenda shule), aliyekosa kazi nyingine ya kufanya.

Ni siku hizi tu, tena kwa wajasiriamali wachache ambao wamekwenda kuwekeza mitaji yao kwenye Kilimo. Na karibu watu wote hao, hawakusomea kabisa Agriculture.
Ila hapa tunaangalia kilimo cha kisasa ambacho atataka aendeshe mwenye Taaluma hiyo na sio kile cha mazoea ambacho wa Tz wengi ndio wamejikita humo
 
Mpaka sasa kwa hapa Tanzania, Diploma pekee yenye Maana, Fursa na Uhakika mkubwa Ajira ni CLINICAL OFFICER.

Kama Degree ya Agriculture General haina faida yoyote kwa sasa, Diploma yake itakuwa na nini cha maana?
Hapo unazungumzia kuwa na uhakika wa kuajiriwa na serikali au hata kujiajiri?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom