Cleopa Msuya awafuata Lowassa na Sumaye?

Cleopa Msuya awafuata Lowassa na Sumaye?

Nchi mpya ya Kilimanjaro/Ngorongoro????
Not yet uhuru jamani.
Haya ni mambo madogomadogo.
 
mda si mrefu tunaanzisha North empire, ngoja nijiandae kuhamie.yaani wana arusha pamoja na jitihada za magufuli kukonga nyonyo za watanzania bado wamethubuti kumchagua lema! yaani wanaamini CCM yale anayofanya magu ni manzingaombwe
Wala hilo litakuwa kifo kwa watu wa Kilimanjaro na Arusha.Sababu ukiwachukua watu wote wa mikoa hiyo walioko nchi nzima na nje uwarudishe wote kule hawatoshi.Ardhi hamna wataishia kufanyiana ujambazi na kuuana hovyo .Kusambaa mikoa mingine kumesaidia sana wao KUEPUKANA NA migogoro.Serikali iliendeshe kampeni nyingi na kuwahamisha kwa makundi kutoka mikoa hiyo na kuwapeleka mikoa mingine.

Wamasai na ng`ombe zao zote walizonazo mikoa mingine uwatimue warudi kwao itakuwa kiyama kwa Arusha haitawameza.Watu wa kilimanjaro nao ukisema uwatimue kote waliko mikoa mingine warudi kwao kwenye hiyo jamhuri yao hawatoshi.Ardhi haiwezi watosha na fursa haziwezi watosha NA KUWAMBIA serikali haijafanya chochote miaka 54 Anavyosema Lowasa na Sumaye wake ni uongo na utapeli kwa wakazi wa arusha na Kilimanjaro.Hao watu ni wabaya mno mbele ya Mungu na wanadamu.Wao wenyewe walibebwa na serikali iliyopo hata viatu walikuwa hawana wakasomeshwa na kujengwa na chama na serikali iliyopo.Leo wanakenua mebno eti serikali haijafanya kitu.

Aliwayewashauri kusema CCM haijawafanyia kitu wakati ilihangaika kuwabeba wafugaji na wachaga wasio na ardhi kuwapeleka maeneo ya mikoa ya Tanga,MOROGORO NK ni kukosa shukrani Na MUNGU atawalipa kwa huo ukosefu wao wa shukrani kwa serikali wao na Lowasa na Sumaye wao anayewachochea.

Ninawalaani kwa jina la Mungu WOTE wanaosema serikali na CCM haijafanya kitu miaka yote 54.wALAANIWE WALALAPO NA WAAMUKAPO MAANA HAWANA SHUKRANI KILA WANALOGUSA LISIFANIKIWE.
 
Wala hilo litakuwa kifo kwa watu wa Kilimanjaro na Arusha.Sababu ukiwachukua watu wote wa mikoa hiyo walioko nchi nzima na nje uwarudishe wote kule hawatoshi.Ardhi hamna wataishia kufanyiana ujambazi na kuuana hovyo .Kusambaa mikoa mingine kumesaidia sana wao KUEPUKANA NA migogoro.Serikali iliendeshe kampeni nyingi na kuwahamisha kwa makundi kutoka mikoa hiyo na kuwapeleka mikoa mingine.

Wamasai na ng`ombe zao zote walizonazo mikoa mingine uwatimue warudi kwao itakuwa kiyama kwa Arusha haitawameza.Watu wa kilimanjaro nao ukisema uwatimue kote waliko mikoa mingine warudi kwao kwenye hiyo jamhuri yao hawatoshi.Ardhi haiwezi watosha na fursa haziwezi watosha NA KUWAMBIA serikali haijafanya chochote miaka 54 na Sumaye wake.Hao watu ni wabaya mno mbele ya Mungu na wanadamu.

Aliwashauri kusema CCM haijawafanyia kitu wakati ilihangaika kuwabeba wafugaji na wachaga wasio na ardhi kuwapeleka maeneo ya mikoa ya Tanga,MOROGORO NK ni kukosa shukrani Na MUNGU atawalipa kwa huo ukosefu wao wa shukrani kwa serikali wao na Lowasa wao anayewachochea.


Acha kuongea mambo yasiyo na msingi. Hata ukisema uwarudishe wamasai na wachaga hutaacha kuwarudisha Wasukuma na ngombe zao ambao ndio moja ya makabila makubwa hapa nchini. Suala kubwa hapa ni mfumo wa uongozi ambao umeishiwa pumzi ukisapotiwa na katiba ambayo inalinda maslahi ya chama kimoja. Ndio maana leo hii Magufuli hana jipya zaidi ya kunakili sera na mikakati ya wapinzani. Hakuna aliyekaataa kwamba Ccm haijafanya kitu ila ukilinganisha ukilinganisha umri wa madaraka na maendeleo ya nchi havilingani kabisa. Hata Leo hii Magufuli kujitutumua hivi nikutokana na changamoto za wapinzani.
 
Wala hilo litakuwa kifo kwa watu wa Kilimanjaro na Arusha.Sababu ukiwachukua watu wote wa mikoa hiyo walioko nchi nzima na nje uwarudishe wote kule hawatoshi.Ardhi hamna wataishia kufanyiana ujambazi na kuuana hovyo .Kusambaa mikoa mingine kumesaidia sana wao KUEPUKANA NA migogoro.Serikali iliendeshe kampeni nyingi na kuwahamisha kwa makundi kutoka mikoa hiyo na kuwapeleka mikoa mingine.

Wamasai na ng`ombe zao zote walizonazo mikoa mingine uwatimue warudi kwao itakuwa kiyama kwa Arusha haitawameza.Watu wa kilimanjaro nao ukisema uwatimue kote waliko mikoa mingine warudi kwao kwenye hiyo jamhuri yao hawatoshi.Ardhi haiwezi watosha na fursa haziwezi watosha NA KUWAMBIA serikali haijafanya chochote miaka 54 na Sumaye wake.Hao watu ni wabaya mno mbele ya Mungu na wanadamu.

Aliwashauri kusema CCM haijawafanyia kitu wakati ilihangaika kuwabeba wafugaji na wachaga wasio na ardhi kuwapeleka maeneo ya mikoa ya Tanga,MOROGORO NK ni kukosa shukrani Na MUNGU atawalipa kwa huo ukosefu wao wa shukrani kwa serikali wao na Lowasa wao anayewachochea.
Kuna wasukuma Mbeya, kuna wajita Morogoro; halimradi watanzania wamakabila yote wametapakaa kila sehemu...iweje uwatarget hawa tu? Haya mambo ya kusema CCM hawajafanya lolote yanakuzwa na hata hivyo yaliyofanyika hayakufanyika kama fadhila ilikuwa ni wajibu. Ikiwa mzazi hujafanya kwa kadri ya matarajio ya watoto wako utaambiwa tu na huwezi kuzila na kuwafukuza ati wamekwambia hayo. Kila nchi tunayasikia haya na hata CCM wanayatumia hayo hayo kwa kauli wapinzani hawana chochote - wakati huo huo mnashangilia kwa kutekeleza waliyokuwa wakiyapigia kelele kwa muda mrefu!
 
DSC00063.jpg

Wezi wamekutana. Hawa jamaa wameitafuna hii nchi na bado wanaitafuna pesa ya walipa kodi - majangili wakubwa, Huyu aliponapona baada ya Sokoine kufariki. Chacha JPM lazima awasafishe viongozi waliokuwa wanafanya biashara wakati wako ofisini sio lazima waendelee kula pesa za walipa kodi. Ati mawaziri wakuu wastaafu wakati walikuwa wanajitajirisha isivyo halali. Go JPM go clean this mess.
 
North zone inainclude Tanga pia? nauliza tu maana Lushoto ndio makazi ya mstaafu Ben Mkapa! kadhalika Bumbuli yupo mstaafu mgosi Yusuph Makamba.
 
Acha kuongea mambo yasiyo na msingi. Hata ukisema uwarudishe wamasai na wachaga hutaacha kuwarudisha Wasukuma na ngombe zao ambao ndio moja ya makabila makubwa hapa nchini.

Wasukuma wana shukrani na CCM na serikali yake wanashukuru na ndio maana walipigia kura CCM wakitambua ilivyowasaidia kuwatoa kule walikobanana na kuwapeleka kwingine kwenye mikoa mingine kuwapa ardhi na makazi.Ninaongelea wale wa Arusha na Kilimanjaro ambao hawana shukrani.Mungu na awalaani walalapo na waamkapo wote wanaosema serikali na CCM hawajafanya kitu miaka 54.

Ni ajabu watu waliosaidiwa hivyo kuiponda serikali.Wakati wa mkoloni wachaga na wamasi hawakuwa mikoa yote kama ilivyo sasa.Serikali iliyopo imewaachilia ikawasaidia wakapata maendeleo makubwa mikoa mingine sio kwao wakachuma hicho walichopata mikoa mingine kinawapa jeuri na kuiponda CCM na SERIKALI.mTU KAMA Lowasa na Sumaye utajiri wao wameupatia mikoa mingine leo ndi vinara wa kuponda CCM na serikali Mungu na awalaani asiwaache wakae hata siku na saa bila laana wao na wote waipondao serikali na CCM kuwa haijafanya lolote.
 
Sasa North Zone tumekamilika.. Kitakachofuata ni kupigania nchi yetu. Potelea mbali

Uchochezi huanza kama utani hivi hivi......... then balaah 👆👆👆👆👆🙏🙏
 
Wasukuma wana shukrani na CCM na serikali yake wanashukuru na ndio maana walipigia kura CCM wakitambua ilivyowasaidia kuwatoa kule walikobanana na kuwapeleka kwingine kwenye mikoa mingine kuwapa ardhi na makazi.Ninaongelea wale wa Arusha na Kilimanjaro ambao hawana shukrani.Mungu na awalaani walalapo na waamkapo wote wanaosema serikali na CCM hawajafanya kitu miaka 54.

Ni ajabu watu waliosaidiwa hivyo kuiponda serikali.Wakati wa mkoloni wachaga na wamasi hawakuwa mikoa yote kama ilivyo sasa.Serikali iliyopo imewaachilia ikawasaidia wakapata maendeleo makubwa mikoa mingine sio kwao wakachuma hicho walichopata mikoa mingine kinawapa jeuri na kuiponda CCM na SERIKALI.mTU KAMA Lowasa na Sumaye utajiri wao wameupatia mikoa mingine leo ndi vinara wa kuponda CCM na serikali Mungu na awalaani asiwaache wakae hata siku na saa bila laana wao na wote waipondao serikali na CCM kuwa haijafanya lolote.

wewe lazima utakua mwanke, nimekosea??
 
CCM ni Mbaya sana na wengi tunaichukia; lakini Chadema haijakaribia kuwa Mbadala. Chadema ya leo na CCM tofauti yao nini? Tuwe wakweli. CCM is messy Chadema is even so!

Tutafute uongozi wa nchi kwa kuzingatia misingi halali si kutumia ukabila na kuji-group kimkakati. Failure will be your ultimate destination. Kukosa Uongozi ndani ya CCM kwa Lowasa ndo kumezusha all this mess. Lowasa hakuwahi kuyasema haya, kabla ya kunyimwa uteuzi ndani ya CCM!

Kuna watu wakikosa madaraka wanaona afadhali nchi isambaratike ili tukose wote; among them is Lowasa. Alipokosa madaraka ndani ya CCM he wished CCM death! Kakosa madaraka ya Tanzania, he must be wishing death to Tanzania. Tumwangalie kwa macho mawili mawili!!
 
mkuu ni gazeti la nipashe

[h=2]Msuya awafuata Lowassa, Sumaye[/h]


Na Waandishi wetu



20th December 2015






MsuyaC.jpg

Cleopa Msuya


Cleopa Msuya jana alikuwa Waziri Mkuu wa tatu wa zamani kukosoa mwenendo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) chini ya uenyekiti wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, akungana na Edward Lowassa na Fredrick Sumaye.

Lowassa na Sumaye mbali na kukosoa mwenendo ulio kinyume na misingi iliyoasisiwa na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Nyerere walipigia debe upinzani wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Akizungumza jana, Msuya alisema rushwa, uchakachuaji na matendo ya ovyo ya baadhi ya viongozi wake ndiyo yamesababisha kipoteze umaarufu kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita.

Ingawa mgombea wa CCM, Rais John Magufuli ndiye aliyeshinda katika uchaguzi huo kwa kupata zaidi ya asilimia 58 ya kura, Watanzania kwa kiasi kikubwa walivutiwa na rekodi yake ya utendaji kazi uliotukuka akiwa Waziri wa Ujenzi chini ya Kikwete.

Msuya amekitaka chama chake hicho kujitathimini na kisha kuchukua hatua dhidi ya viongozi na makada watakaotajwa kukihujumu katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu.

Akizungumza wakati akifungua Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM mkoani Kilimanjaro ambayo iliketi kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya Uchaguzi Mkuu uliopita, Msuya alisema:

?Msiwatazame vibaya wanachama wenu kama wasaliti maana wao wamekosa imani na matendo yenu, wanaonyesha kukichoka chama kwa sababu ya rushwa, uchakachuaji na ukiukwaji wa haki za zao za msingi.

?Viongozi lazima tukubali, tuache unafiki na undumilakuwili ili jamii hii hii iweze kutuamini na kutupa tena dhamana ya kuyakomboa majimbo yetu yaliyochukuliwa na wapinzani lakini pia tutwae majimbo mengine zaidi.?

Alisema viongozi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro lazima wajitathimini upya kutokana na kushindwa vibaya katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu na kuongeza kuwa iko haja kwa watakaobainika kukihujumu chama wachukuliwe hatua kali.

Msuya, 83, aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu kwa vipindi viwili Novemba 7, 1980 na Februari 24, 1983. Sumaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 mfululizo akiteuliwa Novemba 28, 1995 na Desemban 30, 2005 wakati Lowassa alidumu kwa muda mfupi kati ya Desemba 30, 2005 na Februari 7, 2008.

Katika Uchaguzi Mkuu uliopita, CCM iliyapoteza majimbo matatu ya Siha, Same Mashariki na Moshi Vijijini ambayo ilikuwa ikiyashikilia.
Pia ilipoteza nafasi ya kuziongoza Halmashauri tano za Wilaya za Rombo, Moshi Mjini, Hai, Siha, Moshi Vijijini na Vunjo.

Akionyesha kutokubalina na utetezi unaotolewa mitaani na baadhi ya makada na viongozi wa CCM, Msuya alisema ?Mkoa wa Kilimanjaro utabakia kuwa kambi ya upinzani kutokana na baadhi ya viongozi na wanachama kufanya mambo yasiyofaa katika jamii.

"Mambo hayo ni pamoja na kuwa undumilakuwili na kuendekeza vitendo vya rushwa.?

Aidha, Waziri Mkuu huyo wa zamani alisisitiza msimamo wake, akidai kuwa kama viongozi hao hawatakuwa makini na kukubali wana makosa na kutokiri kwa wanachama; ama kukubaliana kuanza safari mpya ya ukombozi, basi hakuna sababu ya kuendelea kukaa hapa Kilimanjaro.

Awali, akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri Mkuu huyo wa zamani kuzungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya mkoa huo, Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Deogratius Rutagumirwa alishangaa kushindwa vibaya huko.

?Binafsi siamini ni kwa nini tumeshindwa, tulijipanga vizuri, tena kwa nguvu zote na tuliona dalili zote za ushindi... mpaka sasa hatujui nini kilichotokea kwa CCM kupoteza majimo hayo kwa wakati moja,? alisema Rutagumirwa.

Katibu huyo alisema kikao hicho cha tathimini, kinaweza kuwapa picha halisi ya nini kilichotokea, shida ilikuwa wapi na watajipangeje ili kuivunja ngome ya upinzani iliyosimikwa katika mkoa wa Kilimanjaro.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM mkoani humo, Iddi Juma alisema licha ya kuwepo kwa matatizo mbali mbali yaliyowakumba na kusababisha kupoteza majimbo hayo, pia aliwataka viongozi wake kuanzia ngazi ya matawi kuanza kujadili matatizo kwa uwazi ukweli na busara.

Imendikwa Na Mary Mosha na Rajabu Mmbughu



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
Wasukuma wana shukrani na CCM na serikali yake wanashukuru na ndio maana walipigia kura CCM wakitambua ilivyowasaidia kuwatoa kule walikobanana na kuwapeleka kwingine kwenye mikoa mingine kuwapa ardhi na makazi.Ninaongelea wale wa Arusha na Kilimanjaro ambao hawana shukrani.Mungu na awalaani walalapo na waamkapo wote wanaosema serikali na CCM hawajafanya kitu miaka 54.

Ni ajabu watu waliosaidiwa hivyo kuiponda serikali.Wakati wa mkoloni wachaga na wamasi hawakuwa mikoa yote kama ilivyo sasa.Serikali iliyopo imewaachilia ikawasaidia wakapata maendeleo makubwa mikoa mingine sio kwao wakachuma hicho walichopata mikoa mingine kinawapa jeuri na kuiponda CCM na SERIKALI.mTU KAMA Lowasa na Sumaye utajiri wao wameupatia mikoa mingine leo ndi vinara wa kuponda CCM na serikali Mungu na awalaani asiwaache wakae hata siku na saa bila laana wao na wote waipondao serikali na CCM kuwa haijafanya lolote.

Ndio maana mimi nimezungumzia suala la mfumo tawala. Kama ni utajiri kwa njia ambayo sio halali. Ukisema hivyo utakuwa unakosea kwani Mzee wa vijisenti na mama wa pesa za mboga je hawa ni wakaskazini. Sumaye na Lowassa waliyatambua haya kwa kuwahurumia watanzania na kuhimiza mchakato wa katiba mpya ambayo itawakomboa watanzania. Wanaodai wanalipa fadhila huku wamebaki kwenye mfumo ni sawa na kujichungulia mwenyewe alafu unacheka. Hata magufuli magufuli atahangaika sana bila kubadilisha mfumo ni sawa na kazi bure..
 
..Mzee Msuya anadai matendo ya rushwa, uchakachuaji, na ukiukwaji wa haki za msingi za wanachama, ndizo sababu zilizopelekea CCM kupokonywa majimbo mengi na wapinzani ktk mkoa wa Kilimanjaro.

..sasa mimi najiuliza, je mambo hayo yapo Kilimanjaro tu? Mbona maeneo mengine ya nchi hii, mfano mikoa ya kusini, kuna mateso na maisha magumu kuliko Kilimanjaro, lakini wananchi ktk maeneo hayo wameendelea kuipa ushindi CCM?

cc KipimaPembe, Getstart, @YEHODIA
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom