Chuo Kikuu Dar es Salaam kinatia aibu

Chuo Kikuu Dar es Salaam kinatia aibu

Gpa ya 5 ya udom,saut,mzumbe na uchafu mwingine wa aina hyo ni sawa na Gpa ya 2.0 ya udsm.asa ni jishangae wewe unaesema cjui mshkaji wako aliachwa,hayo mengne ni changamoto za maisha tu.

Hivi udsm wanatumia syllabus gani tofauti na udom, mzumbe etc.. Hata wewe ni jipu, public institutions course content zinafanana. Intelligence haijalishi chuo.
 
Mkuu nadhani hakuna ulazima wa serikali kuingilia majukumu ya kununua vitabu vya maktaba wakati chuo kinaingiza mabilioni ya fedha kila mwaka,
Chuo kinaweza tumia hizi pesa Ku upgrade miundombinu yake,
Ukiangalia kwenye ranks udsm inalinganishwa na vyuo bora kabisa Africa kama university of cape town na u university of KwaZulu Natal ambavyo vina miundombinu ya kisasa mno, kiukweli udsm inatuaibisha,
Walimu wa udsm ukiwaskia wanajisifu madarasani utadhani ni kina newton wakati miongoni mwao ndio wanagawa marks kwa penzi na wengine wanashika wanafunzi coz of chuki binafsi,

Udsm inahitaji flexibility,
Udsm inahitaji Ku upgrade miundombinu yake,
Udsm inahitaji kutoa elimu bora, fair education..
Nafikiri kuna haja ya kuwalipa vizuri pia walimu wake ili wafocus kudeliver material kwa wanafunzi badala ya kuwa busy na miradi yao kama chuo cha ardhi..

Waige mfano wa college ya Informatics ya udom.
Mkuu nadhani hakuna ulazima wa serikali kuingilia majukumu ya kununua vitabu vya maktaba wakati chuo kinaingiza mabilioni ya fedha kila mwaka,
Chuo kinaweza tumia hizi pesa Ku upgrade miundombinu yake,
Ukiangalia kwenye ranks udsm inalinganishwa na vyuo bora kabisa Africa kama university of cape town na u university of KwaZulu Natal ambavyo vina miundombinu ya kisasa mno, kiukweli udsm inatuaibisha,
Walimu wa udsm ukiwaskia wanajisifu madarasani utadhani ni kina newton wakati miongoni mwao ndio wanagawa marks kwa penzi na wengine wanashika wanafunzi coz of chuki binafsi,

Udsm inahitaji flexibility,
Udsm inahitaji Ku upgrade miundombinu yake,
Udsm inahitaji kutoa elimu bora, fair education..
Nafikiri kuna haja ya kuwalipa vizuri pia walimu wake ili wafocus kudeliver material kwa wanafunzi badala ya kuwa busy na miradi yao kama chuo cha ardhi..

Waige mfano wa college ya Informatics ya udom.

Nakubalina na wewe kuwa UDSM ina tatizo kubwa la kutosimamia maprofesa wake. Kuna maprofesa hawawajali kabisa wanafunzi wao. Hawaingii darasani kufundisha, ambayo ni kazi waliyoomba na kuajiriwa. Tatizo siyo mishahara tu bali nadhani ni tabia iliyoendekezwa. Ni kama wizi an rushwa, wenye mishahara mikubwa ndiyo wanaofanya zaidi.

Masuala la ngono, wanafunzi kuonewa nk yanasikika kwenye vyuo vingi duniani. Hata hivyo nijuavyo mimi ni vigumu sana mwanafunzi wa kike kufaulu Chuo Kikuu kwa kutumia ngono tu, la sivyo atatoka amechakaa kwelikweli maana atakutana na walimu wengi sana.

Sijui waige kitu gani kutoka kwenye hiyo College of Informatics UDom. Hujafafanua kile ambacho hiyo College imefanya ambacho ni cha kuiga.

Ukweli ni kuwa elimu ya chuo kikuu ni aghali sana popote duniani hasa pale hiyo elimu inapotakiwa kukidhi viwango fulani.

Kwa Tanzania bado ni jukumu la serikali kugharimia elimu ya Chuo Kikuu. Vyuo kama Cape Town, Pretoria, n.k. vinapewa pesa nyingi sana na serikali yao na bado wanafunzi wanalipa ada kubwa sana ukilinganisha na wanafunzi wa Tanzania.

Siyo rahisi hata kidogo kwa vyuo vya Tanzania kama UDSM kujitegemea. Ikumbukwe kuwa miuondo mbinu iliyopo kama vitabu vya maktaba, barabara, na majengo vina gharama kubwa.

Pamoja na haya yote nadhani bado kuna sababu ya Viongozi wa UDSM kuonyesha ubunifu wao katika kutatua matatizo ya chuo chao. Kwa nini mpaka leo wakuu wa vitivo/Shule wapewe usafiri wa VX na dereva? Kweli chuuo kinashindwa kujenga vyoo na kuvisimamia? Watasingizia ukosefu wa maji. Kweli chuo kinashindwa kuchimba kisima kirefu na kupata maji angalau yatumike chooni tu?
 
Mimi pale hall 1 ilikuwa siendi kwenye vile vyoo, ni shida yaani unaachia mzigo then unaruka juu kdg ili maji yasikurukie. Halafu nilikuwa nakariri ili nisifeli
ulikuwa huendi kwenye hivyo vyoo sasa umejuaje kuwa ukiachia mzigo unaruka juu kidogo...sasa la kukariri si ndo ulikuwa uwezo wako!!!
 
UDSM ni jipu na lisipo angaliwa litapasuka lenyewe . Sijui kama kuna utawala wenye dhamira ya kweli ya kuiletea Tanzania maendeleo au kuna wapiga pesa wanao furahia kutumia VX , V8 na kuchupokea mshahara kila mwezi. Hadhi ya chuo haifanani na mazingira halisi yaliyopo, sijui watu wanasomaje hapo udsm.

Mfano
Ivi udsm pamoja na kuwa chuo cha kwanza kufundisha computer science hapa nchini, kwanini imeshindwa kuwa na website inayo lingana na hadhi yake. Website haina content, ipo offline most of the time, content zake nyingi ni static, poor design etc

Nikiangalia vyuo vya level yako kama Nairobi, Makerere etc vina website nzuri zimeshiba information. Labda wahusika kama wapo hapa watwambie shida ipo wapi?

Mfano kwa muda wa wiki 3 sasa website haipo hewani, ivi wahusika wanalionaje hilo kwa nyakati za leo ambazo information ndio mtaji wa biashara huwezi kaa gizani na ukajisikia vizuri, Mnajua mmepoteza fedha kiasi gani kwa kukaa offline?

Inavyo onekana udsm ni chuo ambacho kipo static sana. hakibadiliki, hakitaki mambo mapya, sijui ni uzee wa staff au ukiritimba usio na maana. oneni wenzenu wa nairobi na makerere mambo yao yapo so dynamic hata machango wao ktk jamii unaonekana mfano mzuri ni basi linalo tumia jua lililo zinduliwa juzi.

UDSM ukiacha kuandaa wana siasa (jipu) ambao ndio wamelipoteza taifa hili na bara la africa, hakuna kitu cha maana kilicho fanyika ktk maeneo mengine. Miaka yote wasomi wamekaa hapo udsm nadhani kazi kubwa ni kupokea mishahara, matokeo ya research yapo wapi?

Chuo kimepoteza mvuto kabisa, zamani kilikua chuo pendwa africa, watu walijisikia uoendeleo kusoma udsm, leo wanaunzi wangapi toka nje wanasoma hapo udsm na hao waliopo wanajisikiaje?

Ukiangalia vyuo vya jirani zetu tuu hapo karibu wapo vizuri na wamejipanga, kozi zao wanaenda na wakati na kozi zinazo endana na soko la ajira. udsm kozi zilezile miaka nenda rudi, hii ni shida. Madudu ya chuo hiki ni mengi huwezi kuyamakiza kwa siku moja.

Binafsi wahusika wachukue hatua, udsm ni chuo chenye hadhi na kinachukua sura ya taifa letu.

Ipo siku nafasi hii itachukuliwa na chuo kingine kwa uzembe kama huu

tabutupu.

Mkuu, yaani vyuo vyetu kiukweli vinapoteza hadhi siku baada ya siku, hebu njoo uone hapa UDOM, system yake yaani ni kama talaka vile: iki-shake huna chuo. Mbaya zaidi na utawala unajivunia zaidi eti kwanza kuwa na system ya kujitegemea ni maendeleo, wakati huo huo ni kama wiki mbili tu zilizopita rafiki yangu kipenzi ameshindwa kuendelea na masomo na badala yake karudi nyumabani kisa system ime-shake, doh!! Yaani vyuo vyetu ni shida kweli.
 
Nadhani mengi yalosemwa kuhusu mapungufu ya UDSM ni kweli. Tukabali tu kuwa UDSM ndio chuo kikongwe,kimezalisha wataalamu wengi na hata wahadhiri wa vyuo vingine wengi wametokea UDSM.

Tatizo la UDSM ni kukosa ubunifu kwenye nyanja nyingi. Mathalani swala la pesa halikupaswa kuwa kubwa hivyo. UDSM walipaswa kuandaa na kuweka mikakati bora ya namna ya kupata fedha kama mdau mmoja alivosema.hapo juu. Ila kwakuwa ubunifu hakuna wameshindwa hata kuita wahitimu wa chuo na kuchangisha fedha kwa ukarabati au ujenzi wa miundo mbiniu husika. Watafiti wao wameshindwa kuandaa miradi ya kutosha na kuitafutia fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo.

Pia UDSM haibadiliki kulingana na soko la ajira na hali halisi ya dunia inavokwenda. Dunia ya leo imebadilika lakini kozi nyingi za ud bado zipo vile vile. Uanzishwaji wa kozi mpya zenye tija pia imekuwa shida. Mathalani kozi za ujasiriamali zilipaswa kutolewa kwa kiwango bora na ingewekana zingefundishwa kwa wanafunzi wengi(degree programs) ili kuwaanda vijana vizuri. Ila tofauti ingekuwa tu namna.zinavokuwa tailored ili kuendana na kozi husika. Mathalani mtu anayesoma law,kwenye ujasiriamali anafundishwa namna ya kuwa na kampuni yake.ya uanashria, yule wa socialogy angepata pia mafunzo kulingana na fani yake( mfano namna ya kufungua huduma kwa watu wenye matatizo mbalimbali,namna ya kujipenyeza na kupata tenda kwenye sekta kama.vile magereza, polisi,jeshini,mashuleni na pengine kwenye mahusiano kati ya wakulima na wafugaji) na COeT anafundishwa namna ya kuanzisha kampuni yake ya ukandarasi(kuanzia na namna.ya kusajili,vigezo vyakutimiza ili isajiliwe,namna ya.kupata wateja,namna ya kupata tenda nk.). Vitu kama hivyo vingesaidia kuweka tofauti ya UDSM na vyuo vingine na kusaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana.

Sasa kwabahati mbaya hayo hayafanyiki kwa namna hiyo. Kijana.anamaliza leo CoeT bado anakosa ujuzi wa kuunda vitu na maaarifa ya kuanzisha na kuendeleza kampuni mwisho wa simu naye anapata changamoto.za.ajira wakati yeye ndiye.alopaswa kutusaidia kupunguza tatizo la ajira
 
Kwa chuo kikubwa kama UDSM n.k. kuendelea kuitegemea Serikali Kuu kufanya renovation kwenye vyoo ni utahira wa kiwango cha PhD.

Kama ningekuwa VC ningefanya yafuatayo badala ya kuendelea kusubir fedha za kukarabati vyoo zitoke hazina kuu.

1. Kutumia rasilimali zilizopo vizuri na kwa weledi. Kwa mapato yote ya ndani ningetenga asilimia kadhaa kukarabati miundo mbinu ya umuhimu kama vyoo, lecture halls, barabara na kuhakikisha mawasiliano ndani ya chuo yanakuwepo muda wote.

2. Alumni Mobilization
Chuo kama UD kina alumni all over the world. Na kuna ambao wapo tayari kukisupport chuo kisongembele. Ningehakikisha wote waliosoma UD wanakuwa na platform ya pamoja na kuanzisha mfuko maalumu wa maendeleo ya UD.

3. Matumizi yenye Nidhamu
Haingii akilini chuo kinakuwa na V8s ambazo ni gharama kuzinunua na kuziendesha halafu unakuta wanafunzi wanategemea kwenda msalani mcity. Ningebana matumizi na kufuta matumiz yasio ya lazima ili kinachobaki kikaboreshe UD kwa faida ya wengi.

4. Bulk Purchasing
Kwa mafuta ya magari, stationaries, na vitu muhimu vinavyotumika chuoni kila siku. Hii itasaidia kusave kwenye manunuzi.

Me naamini kabisa kwa hivi vyuo vyetu vikubwa vikiamua kujiendesha venyewe vinaweza kabisa. Vina Rasilimali (Watu & Asset) nyingi sana.

Uwezo Vinao, Sababu Vinayo, Nia_________
point sana
 
Udsm mambo mazuri uozo upo Institute of Adult education mtu anasaini boom anakaa wiki mwezi na pesa ilishaingia account ya chuo
 
Udsm mambo mazuri uozo upo Institute of Adult education mtu anasaini boom anakaa wiki mwezi na pesa ilishaingia account ya chuo
Mkuu hujaelewa bado, hapa tunazungumzia udsm,
Udsm ndio chuo kinachotuwakilisha internationally kwa sasa , achana na hizo institutes, vyuo vyetu vina changamoto sana, ila kwa sasa tunahitaji tuone hiki chuo kinapata applicants toka europe,
Chuo hakiwezi kuwa kwenye top 10 za Africa halafu kionekane hivi?
Chuo hakina hata maabara ya kisasa moja kwa ulimwengu huu wa Leo? Na dvc yupo tu amejaza tumbo lake? Na mkuu wa nchi amekaa kimya tu??

Hebu angalia vyuo vya uingereza vinavyojitahidi..??
Watu wanaangalia Excellency excelling kwanza hizi pesa zitawafuata tu nyuma yao...
Chuo gani bora chenye wasomi professors kila kona halafu ubunifu SIFURI?
Please udsm do something..
 
Nakubalina na wewe kuwa UDSM ina tatizo kubwa la kutosimamia maprofesa wake. Kuna maprofesa hawawajali kabisa wanafunzi wao. Hawaingii darasani kufundisha, ambayo ni kazi waliyoomba na kuajiriwa. Tatizo siyo mishahara tu bali nadhani ni tabia iliyoendekezwa. Ni kama wizi an rushwa, wenye mishahara mikubwa ndiyo wanaofanya zaidi.

Masuala la ngono, wanafunzi kuonewa nk yanasikika kwenye vyuo vingi duniani. Hata hivyo nijuavyo mimi ni vigumu sana mwanafunzi wa kike kufaulu Chuo Kikuu kwa kutumia ngono tu, la sivyo atatoka amechakaa kwelikweli maana atakutana na walimu wengi sana.

Sijui waige kitu gani kutoka kwenye hiyo College of Informatics UDom. Hujafafanua kile ambacho hiyo College imefanya ambacho ni cha kuiga.

Ukweli ni kuwa elimu ya chuo kikuu ni aghali sana popote duniani hasa pale hiyo elimu inapotakiwa kukidhi viwango fulani.

Kwa Tanzania bado ni jukumu la serikali kugharimia elimu ya Chuo Kikuu. Vyuo kama Cape Town, Pretoria, n.k. vinapewa pesa nyingi sana na serikali yao na bado wanafunzi wanalipa ada kubwa sana ukilinganisha na wanafunzi wa Tanzania.

Siyo rahisi hata kidogo kwa vyuo vya Tanzania kama UDSM kujitegemea. Ikumbukwe kuwa miuondo mbinu iliyopo kama vitabu vya maktaba, barabara, na majengo vina gharama kubwa.

Pamoja na haya yote nadhani bado kuna sababu ya Viongozi wa UDSM kuonyesha ubunifu wao katika kutatua matatizo ya chuo chao. Kwa nini mpaka leo wakuu wa vitivo/Shule wapewe usafiri wa VX na dereva? Kweli chuuo kinashindwa kujenga vyoo na kuvisimamia? Watasingizia ukosefu wa maji. Kweli chuo kinashindwa kuchimba kisima kirefu na kupata maji angalau yatumike chooni tu?
Mkuu nimekuelewa vizuri sana, umefafanua vizuri, natumaini hata wale professors wa udsm watajitoa viburi japo wafanyie kazi haya mawazo yako so long as naamini wanapitia humu,
Kidogo ile college of informatics imejipanga kwenye miundombinu na ufundishaji, ingawa management ya juu ndio yaleyale,

my take,
dear professors and all other experts of Tanzania, you are just humans, and not Gods,
Dont be selfish, tuonyesheni ubunifu wenu ili japo nasi tujivunie uwepo wenu.
Msiangalie tu miradi yenu ya kilimo na mingine mkasahau kuwa mna deni la kulipa,
Kumbukeni maisha yetu yana ukomo, acheni kitu huku nyuma,
Hizi elimu za dunia mmesomeshwa na mmeelewa basi zitumieni kuwanufaisha wanadamu kabla siku zenu hazijaisha,
Dear udsm professors, na wengine wote, please try.
 
  • Thanks
Reactions: KVM
Tuliosoma pale miaka kadhaa ya nyuma najihisi furaha na hata ukiulizwa uligraduate wapi yani haufikirii Mara mbili ni kutaja tu udsm! Lakn ukweli utakuweka huru, udsm inahitaji overhaul, maana.....hata product za siku hizi......unakutana mtu anakwambia ni product ya udsm, lakini very substandard! Pale kuna jibu tena la usoni.
 
kinachoshangaza pamoja na mambo mengine ni jinsi wahitimu wa udsm wa phd, masters, n.k. wasivyoweza kuongea au kuandika kiingereza kilichonyooka (...mfano, reajea ile horror show majuzi kule arusha).
 
we acha tu,kuna jamaa angu aliachwa hivihivi kwenye u tutorial asistance kisa katoka udom japo alifunika kwenye usaili kuliko udsm leavers wote
Ulijuaje kwamba alifunika? Unazijua interview za udsm?
 
Gpa ya 5 ya udom,saut,mzumbe na uchafu mwingine wa aina hyo ni sawa na Gpa ya 2.0 ya udsm.asa ni jishangae wewe unaesema cjui mshkaji wako aliachwa,hayo mengne ni changamoto za maisha tu.
Shikamoo Mzee Wa udsm. Kwenye swala LA GPA hapo ndipo heshima IPO.....

GPA ya SaUT ya 4.8 ni sawa na 1.8 ya udsm ha haaa,.
 
Unaongea pasipo kufikiri! UDSM bado tupo na excellence kama kawaida, nadhani cha msimgi ni maboresho zaidi

Huyo hawajui UDSM leavers!

Unaogopa nini andika tujue unamaana gani halafu nyie ndo wataalamu wa kubebana matokeo yakeHalafu we

wewe Faiza unaonekana unahasira sana na UDSM! sisi bado tupo na excellence is maintained.Sidhani kama ulisoma au unasoma UDSM!
Huyo faiza hana Haata elimu ya kidato cha sita zaidi ya kutetea ujinga Wa pale Lumumba... Hakuwa na vigezo vya kusoma udsm
 
Acha kuongea upupu wewe....nmesoma udom 1st degree nkasoma udsm post graduate...nlichojifunza udsm mnakalili sana...yan ww kalili tu haijarish umeelewa au lah...tena mitihan mnarudia ..kuanzia test had Ue ..yan kama ilivyo wanachange date tu
Ukweli udsm jina tu...but hakuna lolote
nmesoma hapo nmepata gpa/grades ambazo sijawah pata maishan...
Watu muwe na logic...afu uwez dharau chuo flan wakati huna hata experience umesoma chuo kimoja tu unaamin ndo iko iko bora..
Wanafunzi wa udsm sifa nying..
Sijui kwanini watu Wa udom manaonea wivu saana udsm? Na chuki......
Unamaanisha changamoto za udsm udom hazipo?
 
kinachoshangaza pamoja na mambo mengine ni jinsi wahitimu wa udsm wa phd, masters, n.k. wasivyoweza kuongea au kuandika kiingereza kilichonyooka (...mfano, reajea ile horror show majuzi kule arusha).
Lugha sio kipimo cha usomi....kuna maprofesa wengi hawana ile fluently English. Unadhan pale ni English medium school ?
Pima vitu vingine na sio lugha,
 
Msisahau kuwa UDSM Ndio imezalisha karibu 90 % ya mafisadi wetu wote nchini
 
Back
Top Bottom