Chuo Kikuu Dar es Salaam kinatia aibu

Chuo Kikuu Dar es Salaam kinatia aibu

baadhi ya vyuo vina mtazamo huo kuwa watu wanaowazalisha wao ni bora zaidi kuwaajiri kuliko vyuo vingine,kitu ambacho si kweli maana wanakosa exposure toka nje,hence to remain static!!
Ndio maana nikakuandikia labda Yesu ashuke, huyu aliyegomewa Havard hasira anakuja imalizia kwa vijana wengine kama hao toka kwenye hivyo vyuo tajwa.

mfano: SHule ya Sheria UDSM wanatoa LL.B na BALE huyu wa BALE hata apate GPA ya 5 kubakizwa ni ndoto kwake, wakati huo huo mtu wa LL.B anabakizwa kwa ajili ya wanafunzi wa BALE😀
hii ndio UDSM CHUO KIKUU CHA TAIFA
 
Ndio maana nikakuandikia labda Yesu ashuke, huyu aliyegomewa Havard hasira anakuja imalizia kwa vijana wengine kama hao toka kwenye hivyo vyuo tajwa.

mfano: SHule ya Sheria UDSM wanatoa LL.B na BALE huyu wa BALE hata apate GPA ya 5 kubakizwa ni ndoto kwake, wakati huo huo mtu wa LL.B anabakizwa kwa ajili ya wanafunzi wa BALE😀
hii ndio UDSM CHUO KIKUU CHA TAIFA
LLB coverage yake ni kubwa mno, unadhan mtu wa BALE anaweza kufundisha LLB??

By the way, BALE wanasoma 3yrs tu lakini LLB wanapiga 4yrs plus 1yr of law school,

BALE wanasoma law enforcement tu basi, kifupi Hawa ni law enforcers ambao actually ni mapolisi officers km OCCID, OCD etc.

Mtu wa BALE hawez kufundisha LLB kamwe!! Ila wa LLB anafundisha BALE, kwake ni kama module tu!
 
Umemaanisha kikwete ni bora zaidi ya nyerere?
Nadhani anamaanisha hivyo!!

Kikwete ameacha watu wanamiliki majumba, magari, mabiznes ya kila aina, mapesa kedekede, huduma za kijamii km usafiri,watu Wana magari kibao mpaka barabara hazitoshi mjini na kusababisha foleni, bidhaa km sukari, nguo nk zimejaa tele unanunua utakacho,

Ameacha watu mnajiachia kutoa maoni yenu mitandaoni km jamiiforums na kuiponda serikali, etc etc

Lakini mwl aliacha watu wakipanga foleni kwenye maduka ya ugawaji kutwa nzima ili wauziwe kilo moja ya sukari, wakina mama walikuwa wakivaa kaniki na matenge ya kaungua kwani nguo hazikuwepo, watu walitembea pekupeku na watoto makalio nje,

Aliacha watu wanakaa stand ya basi masaa Sita wakisubiri UDA ambalo lilikuwa moja tu kila ruti, Mtu unalisubiri UDA kariakoo litoke mbagala ndo lirudi kariakoo ili apande! [emoji1] [emoji85]

Aliacha watu wanaogopa hata kununua baskeli kwani mfumo wa ujamaa na ujima ulikataza private ownership of property,

Aliacha watu ni waoga wasioweza kuikosoa serikali na kutukana viongozi wa nchi km ilivyo sasa nk

Kutokana na tofauti hizi huenda mtoa Mada ana maanisha hivyo japo sina uhakika!!
 
Nafkiri watoa mada wengi labda hawajasoma pale udsm pako hivi watu wanakosa muda Wa kufanya rally za usafi desa gumu na kuhusu website's in active dah...matangazo huwa ktk notice board tuu watu wapo busy sana wakiingia web ya chuo ni aris tuu kuchek matokeo. Vyoo vibovu but watu wanawai lecture asubui afanyaje ? Na kuhusu walimu kuwa walewale kinachoangaliwa ni ubora sio wingi bila 3.8 huwezi kuwa academic staff na km umetoka St.s au cjui wapi lazima wakupime kwanza na wengi hudondoka ktk hizo measures
 
Kwa Tz udsm inaoongoza kitaaluma kama mngekuwa mnafuatilia publication zinazofanyika na staff wake profile za staff hiki nachokindika hapa kingeeleweka sana ingawa sibezi vyuo vingine lakini tujifunze Ku kukubaliana ktk ukweli ingawa as inst ina mapungyfu yake lakini ktk taaluma kwa kweli wanajitahidi sana
 
LLB coverage yake ni kubwa mno, unadhan mtu wa BALE anaweza kufundisha LLB??

By the way, BALE wanasoma 3yrs tu lakini LLB wanapiga 4yrs plus 1yr of law school,

BALE wanasoma law enforcement tu basi, kifupi Hawa ni law enforcers ambao actually ni mapolisi officers km OCCID, OCD etc.

Mtu wa BALE hawez kufundisha LLB kamwe!! Ila wa LLB anafundisha BALE, kwake ni kama module tu!
Kwanini huyu aliyehitimu BALE asibakishwe kufundisha wenzie?

Kuliko kuingia ghalama za kumfundisha mtu aliyemaliza LL.B masomo ya BALE?
 
Hicho chuo kila kitu ni kibovu na kimepitwa na wakati kwa sasa.

Panahitajika utawala wenye exposure ya hali ya juu kupaweka sawa.
Labda kwa sasa baada ya kumpata Mkuu wa chuo mpya mhe sana Jakaya Kikwete mabadiliko ya kina yatajitokeza kutokana na historia yake "iliyotukuka" ya utendaji kazi na usimamizi. AU SIO?
 
Kwanini huyu aliyehitimu BALE asibakishwe kufundisha wenzie?

Kuliko kuingia ghalama za kumfundisha mtu aliyemaliza LL.B masomo ya BALE?
BALE ni Bachelor of Arts in Law Enforcement, yenyewe inahusika na Law Enforcement tuuu,

Watu wote waliosoma LLB wanasoma law enforcement ndani ya kazi yao, hivyo mtu aliyehitimu LLB anaweza kufundisha BALE kwani kwake hiyo BALE ni km topic tu ambayo tayari ameshisoma,
 
Kwa Tz udsm inaoongoza kitaaluma kama mngekuwa mnafuatilia publication zinazofanyika na staff wake profile za staff hiki nachokindika hapa kingeeleweka sana ingawa sibezi vyuo vingine lakini tujifunze Ku kukubaliana ktk ukweli ingawa as inst ina mapungyfu yake lakini ktk taaluma kwa kweli wanajitahidi sana
unapima na vyuo vya ndani?
 
Hata mimi nilikuwa naendelea kushangaa, hadi nilipoina hii post yako ndo nikajua siko peke yangu

Website ni muhimu.

Lakini kuna vitu vingi vinavyokera UDSM na huenda vyuo vyote viko hivyo:
1. Chuo hakina Library ya maana
2. Walimu hawafundishi - wengi wao wapo kwenye miradi yao. Uhuru kwenye hili umezidi mno. Mara kadhaa kuna wanafunzi wamekuja kuniomba msaada wa dissertations zao. Ni aibu aibu aibu. Karibu wote wanalalamika kuwa Supervisors wao hawaonekani.
3. Chuo hakina Library ya maana. Vitabu ni editions za miaka nenda rudi na vimepauka kama nini. hili ni suala ambalo serikali inahusika moja kwa moja.
4. Kuchoka kwa majengo na barabara (driveways) - Hili ni suala la serikali. Serikali imeendelea kujenga vyuo vipya bila kuimarisha vilivyopo.
5. etc.
 
Hicho chuo kila kitu ni kibovu na kimepitwa na wakati kwa sasa.

Panahitajika utawala wenye exposure ya hali ya juu kupaweka sawa.

Haaaaaa hata wewe? Maana rafiki yako JK ndo kateuliwa kuwa Chancellor! Unless utwambie hata yeye hana "exposure ya hali ya juu"
 
Website ni muhimu.

Lakini kuna vitu vingi vinavyokera UDSM na huenda vyuo vyote viko hivyo:
1. Chuo hakina Library ya maana
2. Walimu hawafundishi - wengi wao wapo kwenye miradi yao. Uhuru kwenye hili umezidi mno. Mara kadhaa kuna wanafunzi wamekuja kuniomba msaada wa dissertations zao. Ni aibu aibu aibu. Karibu wote wanalalamika kuwa Supervisors wao hawaonekani.
3. Chuo hakina Library ya maana. Vitabu ni editions za miaka nenda rudi na vimepauka kama nini. hili ni suala ambalo serikali inahusika moja kwa moja.
4. Kuchoka kwa majengo na barabara (driveways) - Hili ni suala la serikali. Serikali imeendelea kujenga vyuo vipya bila kuimarisha vilivyopo.
5. etc.


hakuna library kubwa n yenye vitabu vingi zaid ya udsm
 
Haaaaaa hata wewe? Maana rafiki yako JK ndo kateuliwa kuwa Chancellor! Unless utwambie hata yeye hana "exposure ya hali ya juu"

Kwanza tueleze kuchaguliwa lini na kakikuta katika hali ipi na nani wa kabla yake?

Halafu soma hii :

A chancellor is a leader of a college or university, usually either the executive or ceremonial head of theuniversity or of a universitycampus. In most Commonwealth (or former Commonwealth) nations, thechancellor is usually a titular (ceremonial figurehead) non-resident head of theuniversity.
 
Facts:
  1. Uchakavu wa majengo: serikali kwa miaka 10-15 ilikitelekeza chuo hiki. Kuna uchakavu mkubwa wa majengo hasa hosteli za wanafunzi. Katika hosteli za main campus, hakuna vyoo vyenye hadhi ya kutumiwa na binadamu.
  2. Ushauri na Utafiti: Vyuo vinavyoongoza kwa tafiti bora Tanzania ni UDSM, MUHAS na SUA, hii ni kwa mujibu wa Elsevier ambapo wanaangalia mchango wa andiko na mara ngapi waandishi wengine wamelitumia andiko kwa rejea. Kampuni za ushauri kama UCC na BIDCO zanafanya (au zimewahi) vizuri katika tasnia zao. REDET pia wamewahi kufanya vizuri, kabla ya siasa kuingia.
  3. Ufundishaji: Unalegalega sana hasa uzamili na uzamivu ktk fani za sanaa, ualimu, sayansi na uhandisi. Wahadhiri wako bize na mambo yao binafsi na uongozi wa chuo hauwawajibishi wafanyakazi wake. Hili linaonekana kupitia wanafunzi wa uzamili na uzamivu kuchelewa sana kumaliza masomo.
  4. Udhibiti wa viwango: Ni moja ya vyuo vichache sana vinavyosimamia viwango kwa umakini mkubwa. Hakuna mwenye shahada moja anayeruhusiwa kufundisha UDSM. Hakimchukui yeyote kuwa mdhadhiri eti kwakuwa kasoma nje ya nchi. Kuna nchi na vyuo vinavyokubalika. Hii iko hivyo kwenye maandishi na ktk utendaji kazi wa kila siku. Vyuo vingine vinatenda kinyume na maandiko. Mitihani yao ina ubora wa kiasi fulani. Kuna vyuo wahadhiri wasiporudia maswali kwa asilimia zaidi ya hamsini, basi inakuwa kilio. Waangalizi wa nje wa tafiti za uzamili na uzamivu wanatoka nje ya nchi (Kenya, South Afrika) kwa kiasi kikubwa, hivyo kuna uhuru wa kitaaluma.
  5. UDSM inajitosheleza kwa wahadhiri, angalau kwa viwango vyetu hapa nchini. Hakuna chuo kikuu Tanzania ambacho hakijawahi kuwatumia au hakiwatumii wahadhiri wa UDSM kutokana na uhaba wa walimu, ukiacha SUA, MUHAS, na ARDHI ambavyo viliwahi kuwa sehemu ya UDSM.
  6. Hakuna chuo kikuu Tanzania chenye Library iliyojaa tafiti za kina ktk kila eneo la kiutafiti kama ile ya UDSM. Wanaofanya shahada za uzamili na uzamivu kutoka vyuo vingine wanaweza kuwa mashahid. Mfumo wa kisasa wa menejimenti ya maandiko. Kwa upande wa vitabu, vingi ni vya kizamani.
Matatizo ya Elimu Tanzania ni zaidi ya UDSM. Bajeti ya Kenya ya utafiti ni mara tano ya bajeti yetu tunayotenga kwa ajili ya utafiti. Hivyo tusitake maziwa mengi kutoka UDSM na vyuo vingine wakati havilishwi ipasavyo.
 
Back
Top Bottom