Chuo cha SAUT kinara ufaulu Shule ya Sheria

Chuo cha SAUT kinara ufaulu Shule ya Sheria

Chuo cha Mtakatifu Augustino cha Mwanza Campus Ya Malimbe Imeendelea Kushika Kasi katika Nafasi za Ufaulu Shule ya Sheria Kwa wahitimu Wanamaliza

Hayo Yanajiri Baada Ya idadi Kubwa Ya Wanafunzi Wanao fanya Vizuri Kutokea Chuo Cha SAUT

Mwaka jana wanafunzi 633 walifanya mtihani wa kuhitimu stashahada ya juu ya sheria kwa vitendo (PGD in Legal Practice). Kati yao ni wanafunzi 26 tu waliofaulu kwenye mkao wa kwanza (first sitting). Kati ya hao 26 wanafunzi 11 (sawa na 42%) ni wahitimu wa chuo kikuu cha St.Augustine, Mwanza (SAUT). 15 waliosalia walitoka vyuo vingine.

Mwaka huu (waliohitimu mwezi January) ni wanafunzi 821. Waliofaulu (first sitting) ni 23 tu. Kati ya hao 23, wanafunzi 10 sawa na 46% wametoka SAUT. 14 waliosalia wametoka vyuo vingine kama UDSM, Mzumbe, Tumaini, Open University, Makumira, SMMCO, St.John, MOCU etc.

Kwa miaka miwili mfululizo karibu nusu ya wanafunzi wanaofaulu Law School ni wahitimu wa SAUT.


SOURCES Via Malisa Gj
Hongera SAUT
 
Ll.b3 wa mwaka huu SAUT wapo Karib 1000plus unadhani mazingira ya kujifunza yatakuwa rahisi kulinganisha na chuo kama UDSM wanachukua watu 100 ni wote ni Division one?
Mazingira ya kufundisha au kujifunza hayawi mepesi au magumu kwa sababu ya idadi ya wanafunzi, bali kwa uwiano kati ya walimu na wanafunzi na pia miundombinu.

Ufaulu wa mwanafunzi pia hausaidii kitu kama shule anakosoma hakuna walimu, au wapo wachache na miundombinu hafifu.

Nimalize kwa kusema Law School inaharibu sana future za vijana. Mwanafunzi unafanya mtihani, ila kujua idadi ya mliofanya exams inakuwa siri, kujua idadi ya waliofaulu inakuwa siri na kujua umepata maksi ngapi (sio grade) napo inakuwa siri. Ahsante gazeti la Mwananchi walau matokeo siku hizi yanajulikana mapema.
 
Mazingira ya kufundisha au kujifunza hayawi mepesi au magumu kwa sababu ya idadi ya wanafunzi, bali kwa uwiano kati ya walimu na wanafunzi na pia miundombinu.

Ufaulu wa mwanafunzi pia hausaidii kitu kama shule anakosoma hakuna walimu, au wapo wachache na miundombinu hafifu.

Nimalize kwa kusema Law School inaharibu sana future za vijana. Mwanafunzi unafanya mtihani, ila kujua idadi ya mliofanya exams inakuwa siri, kujua idadi ya waliofaulu inakuwa siri na kujua umepata maksi ngapi (sio grade) napo inakuwa siri. Ahsante gazeti la Mwananchi walau matokeo siku hizi yanajulikana mapema.
Je report ya mbunge wa zamani wa Kyela imesaidia nini kuhusu ufaulu wa Law school?
 
SAUT ukiachana ujinga walionao kwenye suala zima la administration ya chuo huwa wanafundisha vizuri sana na mwanafunzi anatoka na ujuzi kuanzia vitendo na hata theory.
Kule malecturer wanapishana darasani kama wanafundisha seminari kwa kweli warumi kwenye swala la elimu wapo vizuri sana. Waliniudhi tu kutuwekea magrade makubwa ya ufaulu wakati vyuo vingine grade zao zilikuwa chini tulipambana kweli watubadilishie walikataa wakawashushia wale wa nyuma yetu. Nilikwenda pale sijui kiingereza hasa tenses aiseee madam Munga ashukuriwe sana.
 
Kule malecturer wanapishana darasani kama wanafundisha seminari kwa kweli warumi kwenye swala la elimu wapo vizuri sana. Waliniudhi tu kutuwekea magrade makubwa ya ufaulu wakati vyuo vingine grade zao zilikuwa chini tulipambana kweli watubadilishie walikataa wakawashushia wale wa nyuma yetu. Nilikwenda pale sijui kiingereza hasa tenses aiseee madam Munga ashukuriwe sana.
Bora usifie Wewe Mkuu Mimi GENTAMYCINE nikisema hapa sijaona Chuo Kikuu Bora, Cha Geniuses tupu na kinachotoa Elimu tukuka kama SAUT Mwanza huwa sieleweki na Wapumbavu wengi wakiongozwa nae Tate Mkuu
 
Ungeweka idadi ya wanafunzi wanajiunga law school kutokea SAUT

Mfano UDSM wanafunzi waliojiunga law school wapo 100, alafu 10 wakafaulu
SAUT wanafunzi waliojiunga law school wapo 500, aalfu 30 wakafaulu. Hapo utassma wanafunzi wa SAUT wanafaulu sana law school?
 
Ungeweka idadi ya wanafunzi wanajiunga law school kutokea SAUT

Mfano UDSM wanafunzi waliojiunga law school wapo 100, alafu 10 wakafaulu
SAUT wanafunzi waliojiunga law school wapo 500, aalfu 30 wakafaulu. Hapo utassma wanafunzi wa SAUT wanafaulu sana law school?
Kinachokutesa na Roho Mbaya yako ni kwanini SAUT Mwanza Unayoidharau imefaulisha vyema kuliko UDSM yako Unayoipenda na Kuiamini.

Hovyoooooooo......!!!!!!
 
Mleta mada (mwandishi) hayuko makini katika uchambuzi wake.
Alipaswa kutuambia hiyo idadi ya wahitimu waliofaulu Law school kutoja SAUT ni kati ya wahitimu wangapi kutoka SAUT ambao walijiunga Law school.
(Note: SAUT ndio chuo kinachodahili wanafunzi wengi zaidi wa shahada ya sheria, na ndio kinachotoa wahitimu wengi zaidi wa sheria, ndio kinachoongoza kuandikisha wanafunzi wengi zaidi kuanza mafunzo pale Law school, itakuwa maajabu kama wengi watakaofaulu Law school hawatatokea SAUT)

Kwa mfano, embu tuwaze tu, labda
Wahitimu wa SAUT waliojiunga Law school walikuwa 500, kati yao waliofaulu ni 10 (hiyo ni sawa na 2%)

Wahitimu wa vyuo vingine (UDSM, Mzumbe, Tumaini nk) waliojiunga Law school walikuwa 321, kati yao waliofaulu ni 14 (sawa na 4.4%).

Ni vipi utaiona SAUT ni bora zaidi ya wengine?
Hapa haijalishi unaleta wangapi, kikubwa ni kuwa wakifika Law school ngoma inaanza upya! UD si inajinasibu inachukua div I kutoka best sec school kama ilboru, Kibaha, mzumbe, Tabora boys nk.. mbona hawafurukuti sasa? Makanjanja tu hamna kitu!
 
Bora usifie Wewe Mkuu Mimi GENTAMYCINE nikisema hapa sijaona Chuo Kikuu Bora, Cha Geniuses tupu na kinachotoa Elimu tukuka kama SAUT Mwanza huwa sieleweki na Wapumbavu wengi wakiongozwa nae Tate Mkuu
Ni ukweli uliowazi kuwa taasisi za catholic huwa hazina mzaha mzaha tujiulize tu kwa nini mwanafunzi hasa miaka ile ya nyuma unakuta kafail primary kwenda shule bora za serikali kama Ilboru, Tabora boys nk. Lakini mwanafunzi huyohuyo anaopt kwenda Maua semiry, Imboru au Kipalapala halafu mwisho wa siku mwanafunzi huyu anaibuka na ufaulu mzuri zaidi ya wale waliokwenda huko kwa vipanga. Nilichogundua mapadre wanaelimu zuri sana akikufundisha usipoelewa basi wewe ni tatizo.
 
Hamna namna unaweza kulinganisha SAUT na UDSM kwenye kada ya sheria mkuu. Nimewahi kutana na wanafunzi wengi wa SAUT mwaka wa 4 hata plaint hajui kuandika, Ukimpa ajibu WSD ndo utacheka, ukitaka vituko mpe kazi aandae Charge, hata ku identify offence hajui.

Sijawahi kukutana na Hali kama hiyo Kwa wanafunzi wa UDSM na Mzumbe.

Hizo story za chuo flani kutoa watu wengi Huwa ni stori za vijiweni na wakufunzi Km mtaalamu Shonga au Don chuwa wakiziskia Huwa wanacheka sana Kwa dharau maana uhalisia ni tofauti.

Sijasoma UDSM lakini Kwa sheria UDSM na MZUMBE bado ni best Kwa nchi yetu Angalia hata wanafunzi wanaochukua, ni wachache na wanaufaulu mzuri hivyo rahisi kufundishika tofauti na SAUT ambao ni zoa zoa mpaka D 2 anaenda kusoma Ll.b

Ll.b3 wa mwaka huu SAUT wapo Karib 1000plus unadhani mazingira ya kujifunza yatakuwa rahisi kulinganisha na chuo kama UDSM wanachukua watu 100 ni wote ni Division one?
Ni kweli UDSM wanachukua cream ila kwenye practice huko mahakamani ni weupe.

Mzumbe wanasoma sana ila hawatishi sana.

Kwenye sheria Tumaini wanafanya vizuri sana.

Kwa ujumla wake bado watu wengi hawaijui sheria vizuri.
 
Hamna namna unaweza kulinganisha SAUT na UDSM kwenye kada ya sheria mkuu. Nimewahi kutana na wanafunzi wengi wa SAUT mwaka wa 4 hata plaint hajui kuandika, Ukimpa ajibu WSD ndo utacheka, ukitaka vituko mpe kazi aandae Charge, hata ku identify offence hajui.

Sijawahi kukutana na Hali kama hiyo Kwa wanafunzi wa UDSM na Mzumbe.

Hizo story za chuo flani kutoa watu wengi Huwa ni stori za vijiweni na wakufunzi Km mtaalamu Shonga au Don chuwa wakiziskia Huwa wanacheka sana Kwa dharau maana uhalisia ni tofauti.

Sijasoma UDSM lakini Kwa sheria UDSM na MZUMBE bado ni best Kwa nchi yetu Angalia hata wanafunzi wanaochukua, ni wachache na wanaufaulu mzuri hivyo rahisi kufundishika tofauti na SAUT ambao ni zoa zoa mpaka D 2 anaenda kusoma Ll.b

Ll.b3 wa mwaka huu SAUT wapo Karib 1000plus unadhani mazingira ya kujifunza yatakuwa rahisi kulinganisha na chuo kama UDSM wanachukua watu 100 ni wote ni Division one?
Unawwza ukawaita zoazoa lakini kuna kitu unapaswa kukielewa hapo. Kama walichukua wanafunzi wenye ufaulu mdogo na kwenda kuwabadilisha hadi wakafanya vizuri, basi chuo hicho kipo vizuri kuliko kile kinachochukua vipanga tu.
Kingine, pamoja na kuchukua wanafunzi wengi kama unavyodai, lakini idadi ya wanaomaliza huwa ni wale walioamua kuwa serious tu.
Wewe pia katika mifano yako unarejea kufanya kilekile kinachofanana na unachokipinga, ni wanafunzi wangapi wa SAUT uliokutana nao ambao walishindwa kuandika plaint au ku identify offense? Unadhani wa Mzumbe au UDSM wote wana uwezo huo? Maana sisi wateja pia tuna ushuhuda wetu vila wahitimu wa UDSM wametugharimu katika madai yetu kwa vitu ambavyo hata sisi ma lay-people tuliona mapema kuwa mbona kama haipo sawa ila tukasema kwa kuwa Daktari ndiye kasema basi acha tumeze tu, matokeo yake yakatukuta.
 
Back
Top Bottom