Chunga sana ulimi wako mwanandoa

Hahah nilikumbuka hilo jina + kiswahili chako fulani hivi nikajua huyu ni USA baby tu. Pole kwa ban

Hahaaa eti nina Kiswahili changu fulani hivi.....kwani Kiswahili changu kikoje, kiko tofauti? Ni cha 'Kizungu'?😉
 
Hahaaa eti nina Kiswahili changu fulani hivi.....kwani Kiswahili changu kikoje, kiko tofauti? Ni cha 'Kizungu'?😉
Sijui ndo kiswahili cha ndani ndani teh , "ghaidhi, mintarafu, mlinganyo", sio maneno ambayo wengi wetu tunayatumia
 
Kweli kabisa mkuu..hiyo nilishuhudia mwenyewe wala si kuhadithiwa,jamaa alimwambia mkewe nakupata talaka moja ukajirekebishe kwenu..mke akamwambia nipe tatu zote,jamaa akampa kweli ,baada ya siku mbili mke akarudi analia na msamaha juu kuwa zilikuwa hasira,jamaa akamwambia sheria akaolewe na mtu mwingine akishaachika ndiyo jamaa amrudie,ndoa ikaisha kama utani tu..
 
Maneno hayo machafu ,alafu akipika unakula,anaweka maji ya kuoga unaoga ,ana lala kitandani unampandia,anazaa watoto unaita jina lako aisee ndio mana mwanamke akiamua kufanya roho mbaya inakua roho mbaya kweli
Kama kuna jambo wanaume wanakosea ni kudhani wanawake ni wajinga....
 
Kama wewe nimekuweka tu kiporo na yale maneno yako
 
Kama kuna jambo wanaume wanakosea ni kudhani wanawake ni wajinga....

Lakini mbona hata wanawake nao huwa wanakosea sana kudhani kwamba wana uwezo mkubwa wa kuwasoma wanaume ilhali nyakati nyingine sivyo kabisa.

Mwanamke unaweza ukamlengesha kudhani kwamba anakujua vizuri kwa kumpa ishara flani flani ili afikirie hivyo, na yeye kwenye akili yake akadhani kwamba hisia zake huwa ni sahihi mara nyingi kama si zote, wakati ukweli wa mambo ni wewe mwanaume ndiye uliyempa kwa makusudi viashiria vyote vya yeye kudhani hivyo.

Sasa akishadhani na kupatia anajiona mjanja...mwerevu...na kadhalika. Hajui kwamba wewe ulimrahisishia tu kazi na kama ungetaka ungeweza kuifanya iwe ngumu vilevile.

Sijui hata kama umenielewa.....
 
Labda nitakuelewa kwanzia kesho msukuma wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…