Chuki na husda dhidi ya wanaDiaspora

Utazuia vipi? maana kinachotakiwa ni kuukana tu uraia wa nje, jambo ambalo mgeni anaweza kufanya lakini siku akirudi kwao anaomba tu passport.
Kumbuka wakati wa Nyerere wahindi walokimbilia UK na Canada walikuwa na uraia pacha na wakafanyiwa mipango ya usafiri na tukalaaniwa sisi, japo hao hao waliukana wa nje walipopata uraia wa Tanzania. wao watatushinda tu kwa kila hila, hizi chuki ni kwa wazawa tu hazitazami nje ya sanduku.

Hivyo hivyo leo Mkenya akija kwetu anaweza kuukana Uraia wa Kenya, mkampa passport kesho akapanda ndege kurudi kenya na kuchukua tena ganda la Kenya. Huyu mtu utamzuia vipi wakati passport yake inaonysha wiki moja tu kapata uraia wa Tanzania! na utajuaje?
 
wengine hawakuondoka kwa kupenda, ndo shida ilipo.
 
Nimeoma point yako mkuu. Ni Watanzania ndio wanapata hasara wasipo ruhusu dual citizenship. Kwa hiyo ni naona kama tz wanakataa mzawa kuwa na urai pacha basi wazuie mgeni yeyote ambae kwao kuna uraia pacha asipate uraia tz which is not possible.

Hii sheria ya kinyanyembe ni ya kijuha kupitiliza, huwezi sema unalinda masilahi ya nchi kwa kumuadhibu nduguyo mtanzania eti ukiogopa usalama wa nchi, wakati huo huo unawapa dual uraia wananchi wa nchi zingine. Katika sheria za kijuha hii imepitiliza viwango vyote vya ujuha.

Kwa sababu hii sheria haimuzuii mkenya kuwa na citizenship (passport) ya Tanzania na pia kuwa na citizenship (passport) ya Kenya. Ila inamzuia mtanzania tu mzawa kumiliki passport ya Tanzania na Kenya. Sheria hii mangumashi sana sipati picha wanaojinadi nayo wanalinda masilahi yepi? Upuuzi kweli unapoona sheria ya namna hii eti wanaipigia vipeuo inabidi kuanza kuhoji uwezo wa uelewa na sio anachopinga.
 
Una akili za kitoto.
Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?
Bado nasisitiza kama wana nis ya kuwekeza hspa bongo hakuna kupingamizi, tatizo ni la mtu na akili yake!
 
Una akili za kitoto.
Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?
Bado nasisitiza kama wana nis ya kuwekeza hspa bongo hakuna kupingamizi, tatizo ni la mtu na akili yake!

Unawekeza kwenye masharti ahueni. Kwanini mtu aje kuwekeza bongo ambapo atakuwa na masharti magumu kuliko hata ya mzungu anayewekeza bongo? kwa nini asiwekeze hukohuko aliko?

Maana wazungu wakija kuwekeza bongo wanapewa holiday tax hata miaka 10, ikiisha miaka 10anabadirisha jina la kampuni anapewa tena mingine 10.
Akija mbongo hata hiyo holiday hapewi na on top, ndo anakuwa foreigner wa ukweli kweli, unapigwa tax from day one harafu sio ya uzawa. Kwi kwi kwi kwi kwanini aje kuwekeza??

Akija Mzungu tena bila pesa sababu ya ngozi yake anapewa hadi na mtaji kutoka bank za kibongo. Juzi juzi hapa mlikuwa mmeshapitisha kuwapa Wakenya Kenya airways fedha za bure kupitia Precious Air, naona mlisituka dakika ya mwisho. Najua mjanja hapo atakuwa Bernard Membe ndo aliwasitua dakika ya mwisho.
 



wao wanataka watoto wao tu ndio wawe na uraia wa nchi mbili si wewe wala mimi.
 
Kama ni hivyo basi watakuwa wamekosea sana kwa sababu uraia pacha utakuja kuwasaidia sana Wazanzibari huko mbeleni (baada ya uzinduzi wa Tanganyika) hasa hasa katika suala la umiliki wa ardhi.

Acha speculation tena kwenye suala la ardhi bora tushare na wabara walioko majuu lakini tukijitenga nanyi lazima sheria yetu kwa masuala ya ardhi iwape fursa “wazawa” na sio aina nyingine yeyote ya raia labda awe mwekezaji.
 

Mkuu ni vizuri kujitafutia kwanza usahihi wa kitu halafu ndio uongee, kupotosha si jambo jema.
 
Inaelekea wewe ni mgeni katika nchi yako.
Nenda TIC(Tanzania Investment Centre) na uone waTanzania wenzako wanavyofaidika na hizo Tax Exemptions katika miradi yao.

Tatizo kubwa la Watanzania, kama MkamaP ni ujinga wa kutothubutu na kubaki kulalama tu!!
 
Last edited by a moderator:

Naomba ujishirikishe zaidi, ninaposema waTanzania ktk context hii naongelea wale waTanzania waliohujumiwa uzawa wao na sheria ya kinyanyembe ndo wanasota. Na ndio maana wanapigania haki yao ya msingi ili wakienda TIC wawe kama waTanzania wengine wanavyofaidika. Kituo kikubwa.

Sihitaji league ya Simba na Yanga ktk hili. Kituo. Na hivyo nashauri tuwe tuna digest context kabla yakuanzisha league isiyo natija.
 
Huwezi kujilipua na bado ukafaidi matunda yake!
In life you cannot eat your cake, and yet have it.
 
Mkuu ni vizuri kujitafutia kwanza usahihi wa kitu halafu ndio uongee, kupotosha si jambo jema.

Pamoja natoka nje ya maada kidogo, lakini nashauri muwe mnaji update hado hado.


[h=1]Fastjet resists Precision's $32m bailout[/h]




Fastjet has termed the move as unfair, saying if the bailout is granted, it would adversely affect competition in the aviation industry in Tanzania.PHOTO|FILE
By Samuel Kamndaya,The Citizen Business Editor

Posted Thursday, December 19 2013 at 00:00

IN SUMMARY
But it is not clear why Fastjet sees the move as unfair while when the low-cost airline announced its lowest fare of $20 per one-way ticket, neither Precision Air nor Air Tanzania complained about the move.


Dar es Salaam.The battle to control Tanzania's skies has taken a new twist after Fastjet, a low-cost airline which entered the market with a bang, strongly opposed Precision Air's(PW) decision to seek a bailout amounting to $32 million (Sh51.2 billion) from the government.

Fastjet has termed the move as unfair, saying if the bailout is granted, it would adversely affect competition in the aviation industry in Tanzania.

But it is not clear why Fastjet sees the move as unfair while when the low-cost airline announced its lowest fare of $20 per one-way ticket, neither Precision Air nor Air Tanzania complained about the move.

In what points to a looming business war between the two airlines, Fastjet chief commercial officer Richard Bodin says that bailing out PW using taxpayers' money would create an unfair playing field among operators who are competing in the market. He says if Precision Air is bailed out, similar assistance should be extended to both Air Tanzania and Fastjet if the government wants to a create competitive and fair aviation industry.


http://www.thecitizen.co.tz/News/Fastjet-resists-Precision-s--32m-bailout/-/1840392/2117626/-/12by9ykz/-/index.html
 
Absolutely!
Hell is ones choice, think before you leap into the abyss!

Thank you, think tank. But however, Would you please depict the pros and cons for having dual citizenship. Again, please do it by the help of vivid example and use cases. Otherwise , I would much appreciate if you could mind your std.
 
Ati nini???-dual citzenship??-hakika mteteaji ajiandae vya kutosha,maana ,,,,,,duh.
 
Ati nini???-dual citzenship??-hakika mteteaji ajiandae vya kutosha,maana ,,,,,,duh.


Mteteaji ana kazi rahisi sana. Atawauliza, kwanini wanakataa dual citizenship(dual passport), najua watajibu wanalinda masilahi ya Taifa. Naye atawaambia ngoja niwapeni mfano.

Kwa sheria hii iliyopo inamruhusu Mkenya kupewa citizenship(passport) ya Tanzania kwa kuikana citizenship(passport) ya Kenya. Na hivyo basi,
Mkenya anakuja Tanzania anaoa/kuolewa anaomba citizenship(passport) ya Tanzania anapewa na anaikana yake ya kenya. Kisha huyu mkenya anarudi kwao kwa kutumia passport ya Tanzania akifika kwao anaomba passport nyingine ya Kenya, na kwa vile Kenya wanaruhusu kumiliki passport mbili, ile ya Tanzania wanamuachia na anakuwa na passport mbili (dual citizenship). Kisha anarudi Tanzania, na kwa vile nia ya mkenya ilikuwa kumiliki ardhi ya Tanzania basi ananunua maheka na maheka ya ardhi ya Tanzania na anayamiliki. Hapo masilahi ya Taifa watakuwa wameyalinda vipi?

Na unaendelea kuwahoji, kwa vile sheria hii inamzuia Mtanzania kumiliki passport mbili na wakati huo huo inaruhusu Mkenya na mnyarwanda kumiliki kwa pamoja passport ya Tanzania na Kenya ama Rwanda, je hayo ndio masilahi ya Taifa mnayolinda ktk hii sheria ya kinyanyembe? Ama masilahi ya Taifa ni pale tu inapomzuia mtanzania mzawa kumiliki passport nyingine?

Hii sheria inamwamini sana Mkenya, Mnyarwanda, mzungu, mchina na nk na kumpa passport na kwamba hawa jamaa hata wakimiliki passport mbili (dual citizenship) yani passport ya Tanzania na nchi yake hawahatarishi masilahi ya Taifa la Tanzania, ila tu masilahi ya Tanzania yatahatarishwa na mTanzania kumiliki passport ya Tanzania na ya nchi nyingine?

Hii ni sheria ya kinyanyembe ni ya kijuha kupita viwango vyote vya kijuha.
 

Naona hujanielewa au labda ni mi sijakuelewa. Me sitaki kuongelea swala la nationality, my concern hapa ni citizenship. Na niseme tu naona unajikanganya, Unaposema mtu akitaka uraia wa Tanzania, na kama yeye ni mkenya itabidi aukane uraia wa Kenya. Ndio hasa ambacho si tunakitaka. We know these guys, bado hatujafikia hatua ya kuwa comfortable nao.

Na unaposema sheria ya inayopinga dual citizenship haimzuii mkenya kuwa na uraia wa Tanzania, me sielewi. Una maana kwamba mtu anaweza akaja Tanzania na kupata uraia bila kuukana uraia wa nchi yake. Kama ndio maana yako, basi nadhani unapaswa ku-revisit the facts.
 

Article 16 of the Kenyan Constitution states, “A citizen by birth does not lose citizenship by acquiring the citizenship of another country”.

Habari ndo hiyo. Na huo ni mfano tu. Kwa maelezo zaidi hebu nenda hapa:
https://www.jamiiforums.com/katiba-...-uraia-pacha-na-wenzetu-afrika-mashariki.html
 
Una akili za kitoto.
Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?
Bado nasisitiza kama wana nis ya kuwekeza hspa bongo hakuna kupingamizi, tatizo ni la mtu na akili yake!

Really? Mbona majibu yanatolewa kila siku lakini hamtaki kufungua masikio? Nikupe mfano mmoja tu. Kuna dada Mtanzania ambaye anafanya kazi NASA. Huwezi kupata kazi sehemu kama NASA kama hauna uraia wa Marekani. Huyu dada, ndugu zake WOTE wako Tanzania, lakini ilibidi apate kazi anayopenda na inayoendana na kisomo chake. Sasa, kama mtu huyu ambaye ana PhD ya aerospace engineering, Bongo arudi afanye kazi wapi? Je, na watoto wake ambao ni Watanzania-Wamarekani, nao ni "wasaliti" kama ambavyo mnajaribu kuwasulubu "waliojilipua"?

Sidhani kama Watanzania ni wajanja sana kuliko Wanyarwanda, Wakenya, Waganda, Waghana, na mataifa mengine sana ya Afrika ambao wanaruhusu uraia pacha. Kama kuna practical experience ya madhara ya uraia pacha, ningependa kusikia mfano. Vinginevyo hoja zinazotoka upande wa kupinga uraia pacha kama mada hii inayosema, zinaonekana kujaa uoga, chuki tu na husda, badala ya nondo za nguvu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…