Habarini wapendwa!
Naleta kwenu kisa cha rafiki yangu mpendwa kwa mategemeo ya kupata msaada toka kwenu.
Tatizo linalomsumbua rafiki yangu huyu ni matiti yaliyotuna kifuani pake ilihali yeye ni mwanamume.
Katika watu kumi atakaokutana nao katika matembezi, tisa humcheka na kumfanyia dhihaka. Jambo hili linamnyima sana amani. Kusema kweli amekuwa kama mfungwa ndani ya gereza lake mwenyewe. Amekosa uhuru!
Kotokana na kukosa amani kila wakati, huyu bwana amejikuta akipoteza ndoto zake kila uchao.
Tatizo hili halikumuanza utotoni limempata akiwa na umri wa miaka takribani 14 hivi. Chanzo chake anasema, anahisi ni yai la kuku wa kisasa alilokula likiwa bichi akiwa na lengo la kulainisha koo kwani kuna mtu alimsimulia kuwa mayai mabichi ni kilainisho kizuri sana cha koo. Wakati huo alikuwa akipenda sana kuimba na koo lilikuwa likimsumbua. Pasipo kujiuliza vizuri mpendwa huyu alikwenda dukani na kujipatia yai la kuku wa kisasa na kulitumia kulingana na maelezo aliyopewa.
Baada ya miezi kadhaa alianza kuona mabadiliko katika mwili wake ambayo hakuyapenda mojawapo likiwa la kuchomoza kwa matiti kifuani pake. Pamoja na hilo, yalikuwepo pia mabadiliko mengine kama 'abdominal discomfort', kutoa harufu mbaya sehemu ya haja kubwa (uchafu unatoka), matatizo katika koo nk.
Japokuwa hasemi na anaonekana mwenye furaha machoni, moyoni anaumia sana! namwona ni mtu mwenye uchungu mkuu.
Madaktari wameshindwa kumsaidia jambo ambalo linazidi kumkatisha tamaa.
Ni mtu mwenye akili sana lakini ameonekana kufanya vibaya katika masomo yake ya A level na chuo kikuu.
Amekuwa hafikilii tena kuhusu maisha yake anachowaza ni jinsi gani ataondokana na tatizo hili. Naogopa endapo hali hii itaendelea atapoteza kabisa muelekeo wa maisha yake na nikiwa kama rafiki yake sipendi hilo litokee.
Hili ni tatizo gani jamani? Linatibika? Ni kweli hayo ni matokeo ya lile yai alilokula? Afanye nini sasa? Tafadhali sana naomba tumsaidie huyu mtu.
Naleta kwenu kisa cha rafiki yangu mpendwa kwa mategemeo ya kupata msaada toka kwenu.
Tatizo linalomsumbua rafiki yangu huyu ni matiti yaliyotuna kifuani pake ilihali yeye ni mwanamume.
Katika watu kumi atakaokutana nao katika matembezi, tisa humcheka na kumfanyia dhihaka. Jambo hili linamnyima sana amani. Kusema kweli amekuwa kama mfungwa ndani ya gereza lake mwenyewe. Amekosa uhuru!
Kotokana na kukosa amani kila wakati, huyu bwana amejikuta akipoteza ndoto zake kila uchao.
Tatizo hili halikumuanza utotoni limempata akiwa na umri wa miaka takribani 14 hivi. Chanzo chake anasema, anahisi ni yai la kuku wa kisasa alilokula likiwa bichi akiwa na lengo la kulainisha koo kwani kuna mtu alimsimulia kuwa mayai mabichi ni kilainisho kizuri sana cha koo. Wakati huo alikuwa akipenda sana kuimba na koo lilikuwa likimsumbua. Pasipo kujiuliza vizuri mpendwa huyu alikwenda dukani na kujipatia yai la kuku wa kisasa na kulitumia kulingana na maelezo aliyopewa.
Baada ya miezi kadhaa alianza kuona mabadiliko katika mwili wake ambayo hakuyapenda mojawapo likiwa la kuchomoza kwa matiti kifuani pake. Pamoja na hilo, yalikuwepo pia mabadiliko mengine kama 'abdominal discomfort', kutoa harufu mbaya sehemu ya haja kubwa (uchafu unatoka), matatizo katika koo nk.
Japokuwa hasemi na anaonekana mwenye furaha machoni, moyoni anaumia sana! namwona ni mtu mwenye uchungu mkuu.
Madaktari wameshindwa kumsaidia jambo ambalo linazidi kumkatisha tamaa.
Ni mtu mwenye akili sana lakini ameonekana kufanya vibaya katika masomo yake ya A level na chuo kikuu.
Amekuwa hafikilii tena kuhusu maisha yake anachowaza ni jinsi gani ataondokana na tatizo hili. Naogopa endapo hali hii itaendelea atapoteza kabisa muelekeo wa maisha yake na nikiwa kama rafiki yake sipendi hilo litokee.
Hili ni tatizo gani jamani? Linatibika? Ni kweli hayo ni matokeo ya lile yai alilokula? Afanye nini sasa? Tafadhali sana naomba tumsaidie huyu mtu.