weka mamaHahahah kuna story nyingine sijui kikuwekee link
Moyo Ulioonja Maumivu - JamiiForums usiku huu najua utahangaika nayoweka mama
👋👋👋 bye..ngoja nielekee hukoMoyo Ulioonja Maumivu - JamiiForums usiku najua utahangaika nayo
ayaHahahhaha elekea uko ukimaliza nikupe nyingine
Mambo sio mambo...*CHOZI LISILOFUTIKA-04*
Mtunzi:Juma Hiza
Walipoambiwa hivyo hawakutaka kuamini, walihisi labda walidanganywa. Walichokifanya wakachukua simu zao, wakaingia Facebook kisha wakaanza kulitafuta jina la Suzani Mushi.
Yakatokea majina ya Suzani kama kumi, wakaanza kupitia akaunti moja baada ya nyingine. Kila picha ya Suzani waliyekuwa wakimuangalia, hakuwa Suzani yule waliyemfahamu. Hilo likazidi kuwachanganya.
Hawakutaka Suzani aendelee kuishi maisha ya kizamani kwani kwa kipindi hicho dunia ilikuwa tayari imetawaliwa na utandawazi.
Licha ya kwamba msichana huyo alilelewa katika mazingira ya kidini na wazazi wake yaliyomfanya mpaka ashindwe kuwa bize na mtandao huo, hata pale alipoenda kufanya ibada kwenye kanisa la Seventh Day Adventist, mchungaji wa kanisa hilo alikuwa akisema kwamba shetani alikuwa akifanya kazi yake katika mtandao wa facebook kwa ajili ya kuwapotosha watu ili wasahau kufanya ibada.
Hilo hawakutaka kukubaliana nalo, walichoamua kukifanya wakaanza kumshawishi ajiunge na mtandao huo kwani kuna mengi mazuri yalikuwa yakimpita.
“Watu wamepata wapenzi, kazi, marafiki kwenye mtandao huu,” alisema Brenda rafiki yake Suzani.
“Kama mimi facebook imenikutanisha na marafiki wengi sana ambao sikuwahi kuwaza kama kuna siku ningewafahamu,” alisema Rukia huku akiendelea kuusifia mtandao huo.
Kwa jinsi Brenda na Rukia walivyokuwa wakiusifia mtandao huo wa Facebook, Suzani akajikuta akitamani na yeye kufungua akaunti katika mtandao huo. Hilo wala halikuwa tatizo hata kidogo, akafanikiwa kufungua akaunti.
Moyo wake ulikuwa ni wenye furaha baada ya kuwa na akaunti facebook. Akaanza kupost picha zake huku kila siku akizidi kupata idadi kubwa ya marafiki.
Wanaume wengi waliyokuwa watumiaji wazuri wa facebook walipoziona picha zake walizipenda na kumtamani hivyo wakaanza kumsumbua kwa kumtumia ujumbe inbox. Kila ujumbe aliyotumiwa ulikuwa ni wa mapenzi na kila mwanaume alitamani kuwa naye.
Picha zake zikazidi kuwachanganya wanaume wa facebook. Humo kulikuwa kuna wazungu, waarabu, wachina na wanaume kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambao walitokea kuvutiwa naye.
Hakukuwa kuna mwanaume aliyeziona picha za msichana huyo kisha asiache kuingia katika akaunti yake ili aendelee kuzitazama picha zake nyingine zaidi na zaidi.
Suzani alikuwa na mvuto na hii ndiyo sababu ambayo ilipelekea kila mwanaume aliyemuona akamtamani na kuanza kumsumbua.
“I need to talk with you,” (Ninahitaji kuzungumza na wewe) ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa mzungu mmoja facebook aliyekuwa akitumia jina la Kenedy.
“I love you Suzani,” (Nakupenda Suzani) alituma mzungu mwingine.
Kipindi hicho Suzani kila alipokuwa akiingia facebook, alikutana na meseji nyingi ambazo alitumiwa na wanaume tofautitofauti. Kila mwanaume alisema anampenda na hivyo kutaka kumuoa.
Hakukuwa kuna mwanaume aliyepata nafasi ya kuchati ama kuzungumza na msichana huyo kwani hata pale walipokuwa wakimtumia ujumbe, haukuweza kujibiwa, Suzani alikuwa akiusoma na kuachana nao.
Akazidi kuonekana kuwa msichana wa gharama, thamani yake ikazidi kupanda siku hadi siku.
Sio chuoni tu bali hata wanaume waliyokuwa wakimuona Facebook walizidi kuchanganyikiwa.
Siku ziliendelea kukatika, Suzani akaanza kuonekana akiutumia muda wake mwingi kuperuzi Facebook.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kila kitu. Akazidi kuwa mtumiaji mzuri wa facebook mpaka pale alipoanzisha urafiki na mwanaume mmoja kwenye mtandao huo aliyejulikana kwa jina la Enock Mabula.
Huyu Enock alimsumbua sana, kila siku kazi yake kubwa alikuwa akimtumia ujumbe Suzani lakini haukuwa ukijibiwa. Hilo lilimsononesha mno na kumfanya kuanza kukata tamaa.
Siku moja Suzani alipost picha yake facebook akiwa maeno ya chuo, akaandika kwamba hakuwa sawa siku hiyo hivyo alihitaji marafiki wa facebook ambao wangeweza kumfariji mpaka arudi katika hali yake ya kawaida.
Siku hiyo Enock alipoiona post ya msichana huyo kwa kuwa mara kwa mara alikuwa akiingia facebook na kumuangalia, haraka sana akakumbuka kulike na kucomment kwa kumpa pole na kumsifia lakini pia hakuishia hapo, akamtumia ujumbe.
Baada ya kupita dakika moja ujumbe huo ukajibiwa. Enock hakutaka kuamini kama msichana huyo aliweza kumjibu ujumbe wake kwani kabla ya hapo aliwahi kumtumia ujumbe zaidi ya mara tano tena katika siku tofauti tofauti lakini hakuwahi kujibiwa hata mara moja.
Siku hiyo ikawa ni siku yenye furaha kwa upande wake, akaurudia kuusoma ujumbe huo mara mbilimbili huku akiwa haamini kabisa. Hakutaka kupoteza muda na yeye akaujibu na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuchati kwao.
Walichati sana siku hiyo mpaka kufikia hatua wakabadilishana namba za simu. Enock alifurahi sana, hakutaka kuamini kama aliweza kuchati siku hiyo na msichana huyo mpaka kufikia hatua ya kupewa namba ya simu.
****
Revocatius mapenzi yaliendelea kumtesa moyoni mwake, kila alipomuona Suzani alizidi kuchanganyikiwa. Alimpenda sana lakini msichana huyo hakuonekana kujali kitu.
Alimpigia sana simu, alimtumia kila aina ya ujumbe msichana huyo lakini majibu aliyokuwa akijibiwa yalizidi kumuumiza. Hakujua kama kipindi hicho ambapo alikuwa akimfuatilia tayari alishakuwa na ukaribu na Enock mwanaume ambaye alimpatia Facebook.
Je, nini kitaendelea?
Tayari*CHOZI LISILOFUTIKA-05*
Mtunzi:Juma Hiza
Hakutaka kukata tamaa, aliendelea kumfuatilia huku hitaji lake kubwa likiwa ni kumueleza ukweli kuhusu hisia zake. Usumbufu uliendelea kuzidi zaidi na zaidi mpaka kikafikia kipindi kwa Suzani ikawa ni kero.
Hakutaka kuona akiendelea kusumbuliwa na mwanaume huyo hivyo alichoamua kukifanya ni kumwambia kwamba walitakiwa kwenda sehemu kwa ajili ya kuzungumza. Hilo halikuwa na tatizo hata kidogo, wakapanga mchana wa siku hiyo kwenda kwenye mgahawa wa Fresh coach.
Walipofika kwenye mgahawa huo wakaagiza chakula kisha wakaanza kuzungumza. Muda wote Revocatius alikuwa akitabasamu, aliamini ndoto yake ya kuwa na msichana huyo ilikuwa inakwenda kutimia.
“Kwanini umependa tuje sehemu hii na isiwe sehemu nyingine?” aliuliza Revocatius huku akitabasamu.
“Ni kwasababu ninamazungumzo muhimu na wewe,” alijibu Suzani huku mikononi akiwa ameshikilia uma na kisu tayari kwa kula chips kuku kwenye sahani aliyoagiza.
Revocatius alimtazama Suzani kwa macho ya huba, uzuri wa msichana huyo ulizidi kumchanganya vilivyo.
Mpaka kufikia hapo hakutaka kuamini kama kweli alikuwa amekaa meza moja na msichana huyo tena walitakiwa wakizungumza kwa wakati huo.
Hilo hatuka kuamini, alihisi labda alikuwa katika ndoto lakini haikuwa hivyo. Aliendelea kumtazama Suzani huku moyo wake ukijawa na furaha isiyokuwa na kifani.
Siku hiyo Suzani alihitaji kuzungumza na Revocatius jambo moja muhimu. Lilikuwa ni kuhusu usumbufu wake, hakutaka kusumbuliwa na ndiyo sababu iliyompelekea akamuita sehemu hiyo ili amueleze na huo ndiyo uwe mwisho wa usumbufu kwani hakuhitaji kuwa naye.
Kwa upande wa Revocatius aliwaza tofauti na mawazo ya Suzani, alichoamini siku hiyo ndiyo siku ambayo alitakiwa kumueleza ukweli kwamba alimpenda na alimuhitaji katika maisha yake.
Kabla hajamueleza hilo, alihitaji kufahamu kitu kimoja ambacho kwa muda mrefu kilimchanganya na kumuumiza moyoni mwake tangu alipomfahamu.
“Kitu gani?” aliuliza Suzani huku akionekana kushangaa.
“Unanichukia?” aliuliza Revocatius.
“Siwezi kumchukia binadamu mwenzangu na kwanini nikuchukie kwani umenikosea kitu gani?” alijibu Suzani kisha akauliza swali.
“Nimehisi unanichukia ndiyo sababu nimekuuliza,” alijibu Revocatius.
“Hapana,” alisema Suzani.
Revocatius alipoambiwa hivyo akavuta pumzi na kutulia kwa kidogo, akaonekana akitafakari jambo fulani. Akaichukua glass ya juisi na kuanza kuinywa taratibu, alipotosheka akairudisha mezani halafu akainyoosha mikono yake yote miwili.
Muda huo alihitaji kushika mikono ya Suzani. Suzani akafanya kama alivyoombwa, viganja vyao vikakutana na kushikana huku sahani za vyakula na vinywaji vikiwa katikakati yao.
“Suzani,” alimuita huku akimtazama kwa macho ya huba.
“Abee,” aliitika.
“U msichana mrembo mno, una kila sifa ya kuwa msichana aliyekamilika. Hivi ni kitu gani ambacho umekikosa katika mwili wako? Jibu ni hapana. Embu angalia uzuri wako, mvuto wako, Mungu amekujaaliwa shepu ya kuvutia, angalia rangi ya ngozi yako nyororo, sauti yako yenye mvuto wa kimapenzi.
Kabla yako niliwahi kusikia watu wakisema kwamba wasichana wa kabila hasa lenu wachaga huwa hamnaga mvuto isipokuwa mmejikita zaidi kwenye utafutaji.
Tangu nikuone kwa mara ya kwanza umefanya nisiyaamini maneno hayo,” alisema Revocatius huku vigana vyake vikiwa bado vimeshikana na vya Suzani.
Alipoambiwa maneno hayo Suzani akavuta pumzi ndefu na kuziachia. Akatabasamu.
“Tazama hata tabasamu lako, linamvuto wa aina yake,” alisema Revocatius maneno yaliyomfanya Suzani kuanza kucheka.
“Asante kwa sifa zako,” alisema Suzani.
“Siyo sifa zangu hizi ni zako wewe.”
“Kwahiyo unataka kuniambia nini?”
“Ninakupenda Suzani, ninahitaji kuwa na wewe.”
“Hapana haiwezekani.”
“Kwanini?”
“Haiwezekani tu.”
“Unamaanisha nini?”
“Yaani sipo tayari kuwa na mwanaume kwasasa,” alijibu Suzani.
Revocatius hakutaka kuamini kama kweli alimkosa msichana huyo tena katika mazingira hayo ambapo palikuwa na uwezekano mkubwa wa kumpata lakini ilishindikana.
Suzani alimaanisha kile alichokuwa akikizungumza, hakutaka kuishia kumwambia kwamba hakuhitaji mwanaume tu bali aliendelea kumwambia kwamba alitakiwa kusoma na kuyaacha mapenzi kwani hayakuwa sababu iliyompeleka chuo kusoma.
Hakutaka kupoteza muda wake, alipomaliza kuyazungumza hayo aliinuka na kuanza kuondoka eneo hilo huku akimuacha Revocatius akiwa bado amekaa.
Siku hiyo kwa upande wa Revocatius ilikuwa ni siku ya maumivu, hakuamini kama msichana huyo alimuacha katika mazingira yale huku akiwa amemuambia maneno makali kiasi kile.
Mawazo yalimzonga kichwani kiasi kwamba mpaka akashindwa kuendelea kula, alichokifanya akalipa bili ya chakula na kisha haraka sana akaanza kumkimbilia Suzani. Alipofika nje ya mgahawa huo hakumuona, akazidi kuchanganyikiwa.
****
Urafiki kati ya Suzani na Enock uliendelea, kutoka Facebook ambapo waliishia kuchati na sasa walifikia kubadilishana namba za simu, wakawa wanapigiana simu na hata wakati mwingine kupigiana kwa njia ya video call, WhatsApp.
Suzani alijisikia furaha sana kuwa na urafiki na mwanaume huyo ambaye alikuwa akiishi Mwanza.
Alionekana kuwa mcheshi, aliyefahamu mambo mengi sana kuhusu dunia lakini pia alikuwa na hofu ya Mungu.
Sifa za mwanaume huyo zilimchanganya sana Suzani, kila siku hakuacha kuwasiliana naye huku muda mwingi alipokuwa peke yake kichwa chake kilikuwa kikimuwaza mno.
Baada ya kupita wiki mbili Enock uvumilivu ulimshinda, akaamua kumueleza ukweli Suzani kwamba alimpenda. Tofauti na ilivyokuwa kwa wanaume wengine, Suzani akakubali kuwa na mwanaume huyo ambaye alimuona kuwa ni mtu sahihi. Alichokiamini ni kwamba Mungu alimleta katika maisha yake kupitia mtandao huo wa kijamii wa Facebook.
Siku zikaendelea kukatika huku wawili hao wakiwa tayari ni wapenzi.
Wakaonekana kuhitaji kuonana, kwa upande wa Suzani ilikuwa ni vigumu kufunga safari mpaka Mwanza kumfuata mwanaume huyo hivyo alichoamua kukifanya ni kumwambia Enock kwamba alitakiwa kumfuata Kilimanjaro, Moshi mjini.
Hilo halikuwa tatizo hata kidogo. Enock alikubali na baada ya kupita siku tano akafunga safari mpaka Moshi mjini. Alipofika akachukua chumba katika hoteli ya nyota tatu ya Osy Grand iliyokuwepo mtaa wa riadha.
Alikumbuka kumwambia Suzani kwamba alifika Moshi mjini na kwa wakati huo alikuwa hotelini. Suzani hakutaka kuamini kama mwanaume huyo ambaye alikutana naye Facebook mpaka kufikia hatua wakaanzisha mahusiano ya kimapenzi alikuwa amemfuata Moshi kama alivyomwambia. Hilo lilimfurahisha mno, muda wote alikuwa haamini.
Kwa kuwa kilikuwa ni kipindi cha kukaribia kufanya mitihani ya Mid semister ya chuo na aliomba ruhusa nyumbani kwamba angekaa hostel kwa muda wa mwezi mzima kwa ajili ya kujiandaa na mitihani hiyo hivyo hakukuwa na tatizo la yeye kwenda kukutana na mwanaume huyo kwenye hoteli hiyo ya Osy Grand.
Kutoka chuo cha ushirika mpaka kufika mtaa wa riadha ambapo ilikuwa hoteli hiyo hakukuwa kuna umbali mrefu sana kwa usafiri wa kawaida kama hiace, lakini kutokana na hamu kubwa aliyokuwa nayo Suzani ya kumuona mwanaume huyo, aliamua kuchukua bajaji ambayo ilimfikisha haraka mpaka ilipokuwa hoteli hiyo.
Alipofika hotelini hapo alimpigia simu Enock na kumwambia kwamba alikuwa nje ya hoteli hiyo. Baada ya dakika chache Enock alitoka nje na macho yake kukutana na macho ya Suzani. Kwa furaha Suzani akamkimbilia Enock kisha wakakumbatiana.
*Je, nini kitaendelea?*
*Huu ndiyo mwanzo wa kisa cha Suzani kupata ujauzito mpaka kutelekezwa na kufukuzwa nyumbani kwao.*
*Endeleakuifuatilia simulizi hii yenye kuumiza na kutia moyo wa waliyokata tamaa.*
kweli mapenzi hayana mwenyewe....!!!*CHOZI LISILOFUTIKA-05*
Mtunzi:Juma Hiza
Hakutaka kukata tamaa, aliendelea kumfuatilia huku hitaji lake kubwa likiwa ni kumueleza ukweli kuhusu hisia zake. Usumbufu uliendelea kuzidi zaidi na zaidi mpaka kikafikia kipindi kwa Suzani ikawa ni kero.
Hakutaka kuona akiendelea kusumbuliwa na mwanaume huyo hivyo alichoamua kukifanya ni kumwambia kwamba walitakiwa kwenda sehemu kwa ajili ya kuzungumza. Hilo halikuwa na tatizo hata kidogo, wakapanga mchana wa siku hiyo kwenda kwenye mgahawa wa Fresh coach.
Walipofika kwenye mgahawa huo wakaagiza chakula kisha wakaanza kuzungumza. Muda wote Revocatius alikuwa akitabasamu, aliamini ndoto yake ya kuwa na msichana huyo ilikuwa inakwenda kutimia.
“Kwanini umependa tuje sehemu hii na isiwe sehemu nyingine?” aliuliza Revocatius huku akitabasamu.
“Ni kwasababu ninamazungumzo muhimu na wewe,” alijibu Suzani huku mikononi akiwa ameshikilia uma na kisu tayari kwa kula chips kuku kwenye sahani aliyoagiza.
Revocatius alimtazama Suzani kwa macho ya huba, uzuri wa msichana huyo ulizidi kumchanganya vilivyo.
Mpaka kufikia hapo hakutaka kuamini kama kweli alikuwa amekaa meza moja na msichana huyo tena walitakiwa wakizungumza kwa wakati huo.
Hilo hatuka kuamini, alihisi labda alikuwa katika ndoto lakini haikuwa hivyo. Aliendelea kumtazama Suzani huku moyo wake ukijawa na furaha isiyokuwa na kifani.
Siku hiyo Suzani alihitaji kuzungumza na Revocatius jambo moja muhimu. Lilikuwa ni kuhusu usumbufu wake, hakutaka kusumbuliwa na ndiyo sababu iliyompelekea akamuita sehemu hiyo ili amueleze na huo ndiyo uwe mwisho wa usumbufu kwani hakuhitaji kuwa naye.
Kwa upande wa Revocatius aliwaza tofauti na mawazo ya Suzani, alichoamini siku hiyo ndiyo siku ambayo alitakiwa kumueleza ukweli kwamba alimpenda na alimuhitaji katika maisha yake.
Kabla hajamueleza hilo, alihitaji kufahamu kitu kimoja ambacho kwa muda mrefu kilimchanganya na kumuumiza moyoni mwake tangu alipomfahamu.
“Kitu gani?” aliuliza Suzani huku akionekana kushangaa.
“Unanichukia?” aliuliza Revocatius.
“Siwezi kumchukia binadamu mwenzangu na kwanini nikuchukie kwani umenikosea kitu gani?” alijibu Suzani kisha akauliza swali.
“Nimehisi unanichukia ndiyo sababu nimekuuliza,” alijibu Revocatius.
“Hapana,” alisema Suzani.
Revocatius alipoambiwa hivyo akavuta pumzi na kutulia kwa kidogo, akaonekana akitafakari jambo fulani. Akaichukua glass ya juisi na kuanza kuinywa taratibu, alipotosheka akairudisha mezani halafu akainyoosha mikono yake yote miwili.
Muda huo alihitaji kushika mikono ya Suzani. Suzani akafanya kama alivyoombwa, viganja vyao vikakutana na kushikana huku sahani za vyakula na vinywaji vikiwa katikakati yao.
“Suzani,” alimuita huku akimtazama kwa macho ya huba.
“Abee,” aliitika.
“U msichana mrembo mno, una kila sifa ya kuwa msichana aliyekamilika. Hivi ni kitu gani ambacho umekikosa katika mwili wako? Jibu ni hapana. Embu angalia uzuri wako, mvuto wako, Mungu amekujaaliwa shepu ya kuvutia, angalia rangi ya ngozi yako nyororo, sauti yako yenye mvuto wa kimapenzi.
Kabla yako niliwahi kusikia watu wakisema kwamba wasichana wa kabila hasa lenu wachaga huwa hamnaga mvuto isipokuwa mmejikita zaidi kwenye utafutaji.
Tangu nikuone kwa mara ya kwanza umefanya nisiyaamini maneno hayo,” alisema Revocatius huku vigana vyake vikiwa bado vimeshikana na vya Suzani.
Alipoambiwa maneno hayo Suzani akavuta pumzi ndefu na kuziachia. Akatabasamu.
“Tazama hata tabasamu lako, linamvuto wa aina yake,” alisema Revocatius maneno yaliyomfanya Suzani kuanza kucheka.
“Asante kwa sifa zako,” alisema Suzani.
“Siyo sifa zangu hizi ni zako wewe.”
“Kwahiyo unataka kuniambia nini?”
“Ninakupenda Suzani, ninahitaji kuwa na wewe.”
“Hapana haiwezekani.”
“Kwanini?”
“Haiwezekani tu.”
“Unamaanisha nini?”
“Yaani sipo tayari kuwa na mwanaume kwasasa,” alijibu Suzani.
Revocatius hakutaka kuamini kama kweli alimkosa msichana huyo tena katika mazingira hayo ambapo palikuwa na uwezekano mkubwa wa kumpata lakini ilishindikana.
Suzani alimaanisha kile alichokuwa akikizungumza, hakutaka kuishia kumwambia kwamba hakuhitaji mwanaume tu bali aliendelea kumwambia kwamba alitakiwa kusoma na kuyaacha mapenzi kwani hayakuwa sababu iliyompeleka chuo kusoma.
Hakutaka kupoteza muda wake, alipomaliza kuyazungumza hayo aliinuka na kuanza kuondoka eneo hilo huku akimuacha Revocatius akiwa bado amekaa.
Siku hiyo kwa upande wa Revocatius ilikuwa ni siku ya maumivu, hakuamini kama msichana huyo alimuacha katika mazingira yale huku akiwa amemuambia maneno makali kiasi kile.
Mawazo yalimzonga kichwani kiasi kwamba mpaka akashindwa kuendelea kula, alichokifanya akalipa bili ya chakula na kisha haraka sana akaanza kumkimbilia Suzani. Alipofika nje ya mgahawa huo hakumuona, akazidi kuchanganyikiwa.
****
Urafiki kati ya Suzani na Enock uliendelea, kutoka Facebook ambapo waliishia kuchati na sasa walifikia kubadilishana namba za simu, wakawa wanapigiana simu na hata wakati mwingine kupigiana kwa njia ya video call, WhatsApp.
Suzani alijisikia furaha sana kuwa na urafiki na mwanaume huyo ambaye alikuwa akiishi Mwanza.
Alionekana kuwa mcheshi, aliyefahamu mambo mengi sana kuhusu dunia lakini pia alikuwa na hofu ya Mungu.
Sifa za mwanaume huyo zilimchanganya sana Suzani, kila siku hakuacha kuwasiliana naye huku muda mwingi alipokuwa peke yake kichwa chake kilikuwa kikimuwaza mno.
Baada ya kupita wiki mbili Enock uvumilivu ulimshinda, akaamua kumueleza ukweli Suzani kwamba alimpenda. Tofauti na ilivyokuwa kwa wanaume wengine, Suzani akakubali kuwa na mwanaume huyo ambaye alimuona kuwa ni mtu sahihi. Alichokiamini ni kwamba Mungu alimleta katika maisha yake kupitia mtandao huo wa kijamii wa Facebook.
Siku zikaendelea kukatika huku wawili hao wakiwa tayari ni wapenzi.
Wakaonekana kuhitaji kuonana, kwa upande wa Suzani ilikuwa ni vigumu kufunga safari mpaka Mwanza kumfuata mwanaume huyo hivyo alichoamua kukifanya ni kumwambia Enock kwamba alitakiwa kumfuata Kilimanjaro, Moshi mjini.
Hilo halikuwa tatizo hata kidogo. Enock alikubali na baada ya kupita siku tano akafunga safari mpaka Moshi mjini. Alipofika akachukua chumba katika hoteli ya nyota tatu ya Osy Grand iliyokuwepo mtaa wa riadha.
Alikumbuka kumwambia Suzani kwamba alifika Moshi mjini na kwa wakati huo alikuwa hotelini. Suzani hakutaka kuamini kama mwanaume huyo ambaye alikutana naye Facebook mpaka kufikia hatua wakaanzisha mahusiano ya kimapenzi alikuwa amemfuata Moshi kama alivyomwambia. Hilo lilimfurahisha mno, muda wote alikuwa haamini.
Kwa kuwa kilikuwa ni kipindi cha kukaribia kufanya mitihani ya Mid semister ya chuo na aliomba ruhusa nyumbani kwamba angekaa hostel kwa muda wa mwezi mzima kwa ajili ya kujiandaa na mitihani hiyo hivyo hakukuwa na tatizo la yeye kwenda kukutana na mwanaume huyo kwenye hoteli hiyo ya Osy Grand.
Kutoka chuo cha ushirika mpaka kufika mtaa wa riadha ambapo ilikuwa hoteli hiyo hakukuwa kuna umbali mrefu sana kwa usafiri wa kawaida kama hiace, lakini kutokana na hamu kubwa aliyokuwa nayo Suzani ya kumuona mwanaume huyo, aliamua kuchukua bajaji ambayo ilimfikisha haraka mpaka ilipokuwa hoteli hiyo.
Alipofika hotelini hapo alimpigia simu Enock na kumwambia kwamba alikuwa nje ya hoteli hiyo. Baada ya dakika chache Enock alitoka nje na macho yake kukutana na macho ya Suzani. Kwa furaha Suzani akamkimbilia Enock kisha wakakumbatiana.
*Je, nini kitaendelea?*
*Huu ndiyo mwanzo wa kisa cha Suzani kupata ujauzito mpaka kutelekezwa na kufukuzwa nyumbani kwao.*
*Endeleakuifuatilia simulizi hii yenye kuumiza na kutia moyo wa waliyokata tamaa.*
Jamaniii poyeee usilie utampata wa kukufutakweli mapenzi hayana mwenyewe....!!!
#Acha nilie tu, i think ni zamu yangu ya kulia.....
Sent using Jamii Forums mobile app
Asantweeeh mamy....ila nadhani ni vizuri nikasimama hapa hapa "uzuni point". Maana moyo unaogopa kotekote mbele na nyuma...niende wapi sasa?!!!Jamaniii poyeee usilie utampata wa kukufuta