Chozi Lisilofutika

Chozi Lisilofutika

Asante shunie. Nimekumbuka enzi za shule ya sec.mpaka namaliza siijui sausage .kuna mtu aliniambia ndege mzuri hunasa kwenye tundu bovu. Ile kukaa nyumbani kusubiri majibu nikaangukia kwa bad boy player hatari. Mengine bora nijinyamazie tu
 
Asante shunie. Nimekumbuka enzi za shule ya sec.mpaka namaliza siijui sausage .kuna mtu aliniambia ndege mzuri hunasa kwenye tundu bovu. Ile kukaa nyumbani kusubiri majibu nikaangukia kwa bad boy player hatari. Mengine bora nijinyamazie tu
Ebu malizia bwana
 
*CHOZI LISILOFUTIKA-03*
Mtunzi:Juma Hiza

Revocatius hakutaka kuamini kama ule ndiyo ulikuwa mwisho wa kuzungumza na Suzani.

Kwa dakika kadhaa alizozungumza naye tayari moyo wake uliingiwa na hisia za kimapenzi. Alihitaji kumuelezea ukweli wa hisia hizo lakini alipoyakumbuka yale majibu ya mkato alisita kufanya hivyo.

Kadri siku zilivyokuwa zikisonga mbele ndivyo ambavyo moyo wake ulizidi kujawa na mapenzi kwa msichana huyo. Hakutaka kuficha hisia zake, aliamua kuwaeleza marafiki zake Hiza na Fredy juu ya hisia hizo.

Walipoambiwa hayo Hiza na Fredy hawakuta kumficha kitu, walimueleza ukweli kwamba msichana huyo hakuwa rahisi kama alivyokuwa akidhania. Mpaka kufikia muda huo alisumbuliwa na wavulana wengi na wote hakuna aliyefanikiwa kumpata.

“Hilo sijali, nataka ajue ukweli kwamba nampenda tu,” alisema Revocatius huku uso wake ukionekana kumaanisha kile alichokuwa akikizungumza.

Haraka sana hakutaka kupoteza muda, akaanza kumfuatilia msichana huyo. Alichokuwa akihitaji kwa wakati huo ni kumueleza ukweli kuhusu hisia zake ambazo zilianza kumuumiza.

“Samahani tunaweza kuzungumza?” aliuliza Revocatius huku akimtazama Suzani, wakati huo alikuwa kantini akila pamoja na marafiki zake.

“Huoni nakula jamani,” alijibu Suzani kwa sauti ya kulalamika.
“Ukimaliza.”
“Hapana sina muda huo.”
“Kwanini?”

“Nipo bize labda siku nyingine.”
“Okay basi naomba unipe namba yako ya simu ili nikutafute.”
“Siwezi kuitoa,” alijibu Suzani na kufanya marafiki zake wamshangae.

Kila mtu alihisi labda alifanya utani na kwamba angempa namba ya simu mvulana huyo aliyesimama mbele yao lakini haikuwa hivyo, kile alichokijibu ndicho alichokimaanisha.
****

Revocatius alipokuwa nyumbani kwao, akili yake ilimfikiria msichana huyo kupita kawaida.

Hakujua ni njia ipi alitakiwa kuitumia kumpata msichana huyo. Kila njia aliyoitumia ilishindikana na kibaya zaidi ni kwamba hata nafasi ya kuzungumza naye aliikosa. Hilo likazidi kumuumiza mno.

Dadika kadhaa alizokaa chumbani kwake huku akiwaza na kuwazua ni nini alichotakiwa kukifanya kwa msichana huyo, akapata wazo. Lilikuwa ni wazo la kutafuta namba yake ya simu.

Alichokiamini ni kwamba kama angefanikiwa kuipata namba ya simu ya msichana huyo kazi iliyokuwa imebaki ni kitendo cha kumpigia simu na kumueleza ukweli wa hisia zake, hata kama angemtukana lakini angekuwwa tayari amezungumza naye na kumueleza ukweli.

Kwa wakati huo aliwaza ni nani ambaye angeweza kuwa na namba ya simu ya msichana huyo.

Haraka sana akampigia simu rafiki yake Hiza, akumuomba namba ya simu ya Suzani. Alichojibu Hiza ni kwamba hakuwa na namba zake za msichana huyo lakini pia alimwambia kuwa Fredy na yeye asingeweza kuwa nazo.

“Ila nimepata wazo,” alisema Hiza.
“Wazo gani?”
“Wale marafiki zake hawawezi kukosa. Ukiwatumia wale vizuri lazima utaipata,” alisema Hiza.

Alichokizungumza Hiza kilikuwa ni kweli kabisa. Kama Revocatius alihitaji na namba ya Suzani basi alitakiwa kuwatumia marafiki zake kwani wasingeweza kuikosa.

Siku iliyofuata haraka sana hakutaka kupoteza muda, alimtafuta mmoja kati ya marafiki zake Suzani aliyejulikana kwa jina la Rukia.

Akamueleza shida yake kubwa ilikuwa ni namba ya simu ya Suzani. Rukia alishtuka baada ya kusikia hivyo, hakuwa tayari kuitoa namba ya simu.

“Hapana sina nia mbaya, nimekosa muda wa kuzungumza naye na ndiyo maana nimekuomba unipe namba yake ili nimpigie,” alisema Revocatius.

“Akijua nimekupa mimi itakuwa tatizo kwa upande wangu lakini.”

“Nakuahidi sitamwambia, shida yangu nataka kuzungumza naye,” alisema Revocatius huku akionekana kuwa na uhitaji mkubwa na namba hiyo.

Baada ya mazungumzo hayo Rukia alikubali kuitoa namba ya simu ya Suzani. Revocatius hakutaka kuamini kama alifanikiwa kuipata namba ya simu ya msichana huyo.

Hakutaka kupoteza muda, akamtumia ujumbe mfupi wa salamu na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuchati kwao.
“Safi nani wewe?” alijibu Suzani.

“Kisoka.”
“Yupi?”
“Revocatius?”
“Ndiyo yupi?”
“Mara ya mwisho tulikutana pale kantini nikaomba kuzungumza na wewe lakini ikashindikana.”

“Ooh! Nimekufahamu, namba yangu umeipata wapi?”
“Kwani kuna ubaya mimi kuwa na namba yako jamani?”

“Ndiyo tena sana.”
“Kwanini sasa?”
“Basi tu.”
“Nikuulize?”
“Uliza.”
“Hivi kwanini unanichukia, hutaki kabisa kuzungumza na mimi?”

“Sipendi tu.”
“Uko wapi?” aliuliza Revocatius kwenye ujumbe lakini haukujibiwa. Alihisi labda ujumbe huo haukufika hivyo akarudia kuutuma tena lakini haukuweza kujibiwa. Ukimya huo ukazidi kumchanganya na kumuumiza.

****
Katika kipindi chote hicho ambapo masomo yaliendelea chuoni hapo, tabia ya Suzani ilionekana kuwa tofauti na tabia za wasichana wengine.

Hakuwa ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii kama ilivyokuwa kwa marafiki zake ambao walikuwa na akaunti Facebook pamoja na mitandao mingine ya kijamii.

Hilo liliwashangaza sana marafiki zake, walipomuuliza aliwajibu kwamba hakujisikia kujiunga na mitandao hiyo.

*Je, nini kiliendelea?*
*Tukutane Kesho.*
 
*CHOZI LISILOFUTIKA-04*
Mtunzi:Juma Hiza

Walipoambiwa hivyo hawakutaka kuamini, walihisi labda walidanganywa. Walichokifanya wakachukua simu zao, wakaingia Facebook kisha wakaanza kulitafuta jina la Suzani Mushi.

Yakatokea majina ya Suzani kama kumi, wakaanza kupitia akaunti moja baada ya nyingine. Kila picha ya Suzani waliyekuwa wakimuangalia, hakuwa Suzani yule waliyemfahamu. Hilo likazidi kuwachanganya.

Hawakutaka Suzani aendelee kuishi maisha ya kizamani kwani kwa kipindi hicho dunia ilikuwa tayari imetawaliwa na utandawazi.

Licha ya kwamba msichana huyo alilelewa katika mazingira ya kidini na wazazi wake yaliyomfanya mpaka ashindwe kuwa bize na mtandao huo, hata pale alipoenda kufanya ibada kwenye kanisa la Seventh Day Adventist, mchungaji wa kanisa hilo alikuwa akisema kwamba shetani alikuwa akifanya kazi yake katika mtandao wa facebook kwa ajili ya kuwapotosha watu ili wasahau kufanya ibada.

Hilo hawakutaka kukubaliana nalo, walichoamua kukifanya wakaanza kumshawishi ajiunge na mtandao huo kwani kuna mengi mazuri yalikuwa yakimpita.

“Watu wamepata wapenzi, kazi, marafiki kwenye mtandao huu,” alisema Brenda rafiki yake Suzani.

“Kama mimi facebook imenikutanisha na marafiki wengi sana ambao sikuwahi kuwaza kama kuna siku ningewafahamu,” alisema Rukia huku akiendelea kuusifia mtandao huo.

Kwa jinsi Brenda na Rukia walivyokuwa wakiusifia mtandao huo wa Facebook, Suzani akajikuta akitamani na yeye kufungua akaunti katika mtandao huo. Hilo wala halikuwa tatizo hata kidogo, akafanikiwa kufungua akaunti.

Moyo wake ulikuwa ni wenye furaha baada ya kuwa na akaunti facebook. Akaanza kupost picha zake huku kila siku akizidi kupata idadi kubwa ya marafiki.

Wanaume wengi waliyokuwa watumiaji wazuri wa facebook walipoziona picha zake walizipenda na kumtamani hivyo wakaanza kumsumbua kwa kumtumia ujumbe inbox. Kila ujumbe aliyotumiwa ulikuwa ni wa mapenzi na kila mwanaume alitamani kuwa naye.

Picha zake zikazidi kuwachanganya wanaume wa facebook. Humo kulikuwa kuna wazungu, waarabu, wachina na wanaume kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambao walitokea kuvutiwa naye.

Hakukuwa kuna mwanaume aliyeziona picha za msichana huyo kisha asiache kuingia katika akaunti yake ili aendelee kuzitazama picha zake nyingine zaidi na zaidi.

Suzani alikuwa na mvuto na hii ndiyo sababu ambayo ilipelekea kila mwanaume aliyemuona akamtamani na kuanza kumsumbua.

“I need to talk with you,” (Ninahitaji kuzungumza na wewe) ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa mzungu mmoja facebook aliyekuwa akitumia jina la Kenedy.
“I love you Suzani,” (Nakupenda Suzani) alituma mzungu mwingine.

Kipindi hicho Suzani kila alipokuwa akiingia facebook, alikutana na meseji nyingi ambazo alitumiwa na wanaume tofautitofauti. Kila mwanaume alisema anampenda na hivyo kutaka kumuoa.

Hakukuwa kuna mwanaume aliyepata nafasi ya kuchati ama kuzungumza na msichana huyo kwani hata pale walipokuwa wakimtumia ujumbe, haukuweza kujibiwa, Suzani alikuwa akiusoma na kuachana nao.

Akazidi kuonekana kuwa msichana wa gharama, thamani yake ikazidi kupanda siku hadi siku.

Sio chuoni tu bali hata wanaume waliyokuwa wakimuona Facebook walizidi kuchanganyikiwa.
Siku ziliendelea kukatika, Suzani akaanza kuonekana akiutumia muda wake mwingi kuperuzi Facebook.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kila kitu. Akazidi kuwa mtumiaji mzuri wa facebook mpaka pale alipoanzisha urafiki na mwanaume mmoja kwenye mtandao huo aliyejulikana kwa jina la Enock Mabula.

Huyu Enock alimsumbua sana, kila siku kazi yake kubwa alikuwa akimtumia ujumbe Suzani lakini haukuwa ukijibiwa. Hilo lilimsononesha mno na kumfanya kuanza kukata tamaa.

Siku moja Suzani alipost picha yake facebook akiwa maeno ya chuo, akaandika kwamba hakuwa sawa siku hiyo hivyo alihitaji marafiki wa facebook ambao wangeweza kumfariji mpaka arudi katika hali yake ya kawaida.

Siku hiyo Enock alipoiona post ya msichana huyo kwa kuwa mara kwa mara alikuwa akiingia facebook na kumuangalia, haraka sana akakumbuka kulike na kucomment kwa kumpa pole na kumsifia lakini pia hakuishia hapo, akamtumia ujumbe.

Baada ya kupita dakika moja ujumbe huo ukajibiwa. Enock hakutaka kuamini kama msichana huyo aliweza kumjibu ujumbe wake kwani kabla ya hapo aliwahi kumtumia ujumbe zaidi ya mara tano tena katika siku tofauti tofauti lakini hakuwahi kujibiwa hata mara moja.

Siku hiyo ikawa ni siku yenye furaha kwa upande wake, akaurudia kuusoma ujumbe huo mara mbilimbili huku akiwa haamini kabisa. Hakutaka kupoteza muda na yeye akaujibu na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuchati kwao.

Walichati sana siku hiyo mpaka kufikia hatua wakabadilishana namba za simu. Enock alifurahi sana, hakutaka kuamini kama aliweza kuchati siku hiyo na msichana huyo mpaka kufikia hatua ya kupewa namba ya simu.
****
Revocatius mapenzi yaliendelea kumtesa moyoni mwake, kila alipomuona Suzani alizidi kuchanganyikiwa. Alimpenda sana lakini msichana huyo hakuonekana kujali kitu.

Alimpigia sana simu, alimtumia kila aina ya ujumbe msichana huyo lakini majibu aliyokuwa akijibiwa yalizidi kumuumiza. Hakujua kama kipindi hicho ambapo alikuwa akimfuatilia tayari alishakuwa na ukaribu na Enock mwanaume ambaye alimpatia Facebook.

Je, nini kitaendelea?
 
Mtunzi Juma hiza 01

Suzani alikuwa amejifungia chumbani kwake, wakati huo alikuwa akilia kwa uchungu. Hakutaka kuamini kile kilichokuwa kimetokea katika maisha yake.Mkononi mwake alikuwaameishikilia picha ya mwanaume mmoja. Aliitazama picha hiyo kwa muda wa dakika kadhaa huku machozi yakiendelea kumbubujika mashavuni mwake.

Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali mno, kila alipokuwa akiendelea kuitazama picha ya mwanaume huyo ndivyo ambavyo maumivu yalizidi kuongezeka moyoni mwake.

Alijisikia vibaya sana, alijutia mambo mengi mno aliyoyafanya katika maisha yake na mwanaume huyo.Kuna muda aliona kama alionewa, hakustahili kabisa kupitia maumivu yale aliyokuwa nayo katika kipindi hicho.

Kitendo cha kuendelea kuitazama picha ya mwanaume huyo ambayo kiukweli iliendelea kumuumiza tu! aliona sio jambo zuri hivyo alichoamua kukifanya ni kuigeuza upande wa pili. Alifanya hivyo ili asiendelee kuumia.

Hilo bado halikuwa suluhisho la maumivu ambayo alikuwa nayo moyoni mwake. Kichwani mwake bado taswira na kumbukumbu za mwanaume huyo zilimjia.
Alikumbuka mambo mengi mno aliyoyafanya na mwanaume huyo aliyekutana naye katika mtandao wa Facebook na kuanzisha mahusiano naye ya kimapenzi.

Katika kipindi hicho hakuwa naye, alimtelekeza tena na mimba ya miezi miwili. Hilo lilizidi kumuumiza mno.
Hakukuwa kuna kipindi ambacho moyo wake uliwahi kupata maumivu kama katika kipindi hicho, yalikuwa ni maumivu makali sana yaliyochanganyika na kumbukumbu zilizomuumiza kupita kawaida.

Muda mfupi kabla ya kuingia ndani ya chumba chake na kuanza kulia, alitoka kuzungumza na baba yake ambaye alimuweka kikao na kuanza kumuhoji juu ya ujauzito huo.

Baba yake aliyejulikana kwa jina la Mzee Mushi hakuonekana kupendezewa na tukio hilo hata kidogo na ndiyo sababu iliyompelekea mpaka akamuita mwanaye na kuanza kumuuliza juu ya mtu anayehusika kumpa ujauzito huo.

“Nakuuliza huu ujauzito ni wa nani?” aliuliza Mzee Mushihuku akimtazama binti yake kwa macho ya ukali.Suzani hakujibu kitu, alianza kulia kilio cha kwikwi.
Kilio hicho cha Suzani wala hakikumuingia akilini Mzee huyo ambaye tayari hasira zilikuwa zimempanda. Alichokuwa akihitaji kukifahamu ni mtu aliyehusika kumpa ujauzito mwanaye.

“Mwanangu baba yako si anakuuliza lakini mbona humjibu?” aliuliza Mama yake Suzani baada ya kumuona mumewe amezidi kupandwa na hasira.

“Mama na Baba naomba mnisamehee,” alisema Suzani huku akiendelea kulia.
“Jibu lako na swali langu ni vitu viwili tofauti, nimekuuliza huo ujauzito ni wa nani?” aliuliza Mzee Mushi huku macho yakimtoka.

Suzani hakujua ni wapi ambapo alitakiwa kuanza kuzungumza, hakujua ni lugha ipi ambayo alitakiwa kuitumia kuwaeleza wazazi wake juu ya mwanaume huyoambaye alihusika kumpa ujauzito.
Aliendelea kubaki kimya kitendo ambacho kilizidi kumuudhi mno Baba yake, akainuka pale kwenye kochi alipokuwa amekaa, akamsogelea mwanaye.

“Nakupa siku tatu uwe umeshaniambia mwanaume huyo aliyekupa ujauzito ni nani la sivyo hii nyumba utaiona ni chungu. Haiwezekani maana hii ni dharau kabisa yaani upo chuo tena nakusomesha kwa pesa zangu mwenyewe halafu unaniletea mimba kweli?” alisema Mzee huyo huku akimnyooshea kidole cha shahada mwanaye.

Baada ya Mzee Mushi kuzungumza hayo Suzani akainuka na kukimbilia chumbani kwake ambapo akajifungia mlango.Moyo wake ulikuwa katika maumivu makali mno, akakumbuka kuichukua picha ya mwanaume huyo aliyempa ujauzito na kuanza kuiangalia. Kila alipokuwa akiendelea kuitazama picha hiyo ndivyo ambavyo maumivu yalizidi kuongezeka moyoni mwake.

Baada ya kupita siku tatu Mzee Mushi alimuita tena mwanaye na kumuuliza. Hakutaka utani hata kidogo. Siku hiyo ndiyo siku ambayo alihitaji kumfahamu mtu huyo aliyehusika kumpa ujauzito mwanaye. Kama kawaida yake, macho ya ukali yakamtoka, akamtazama mwanaye ambaye ndiyo alikuwa akijiweka sawa kuzungumza, hofu ilikuwa imemtawala.
“Sema.”

“Anaitwa Enock,” alijibu Suzani huku akionekana kuwa ni mwenye wasiwasi.
“Anaishi wapi?” aliuliza Mzee Mushi kwa sauti ya ukali.
“Mwanza,” alijibu Suzani.
“Unapafahamu mpaka kwake?”
“Hapana.”
“Kivipi?”

“TulikutanaFacebook tukaanzisha mahusiano, alipanga kuja kuniona hivyo akafunga safari kutoka Mwanza akanifuata huku Moshi,” alijibu Suzani huku akionekana kuwa wasiwasi.
Wote wawili wakachoka, hawakutaka kuamini kile walichokuwa wakikisikia.Aliposikia jina la Facebook Mzee Mushi akaonekana kushangaa zaidi kushinda mke wake.

“Eti! mlikutana Facebook?” aliuliza kana kwamba hakusikia vizuri hapo mwanzo.
“Ndiyo.”
“Halafu ikawaje?”

“Tukaanzisha mahusiano na mwisho wa siku mpaka tukapanga kukutana,” alijibu Suzani kisha hapohapo Mzee Mushi akainuka na kumpiga kofi zito ambalo likamuacha na alama ya vidole shavuni mwake.

Kile kilichokuwa kimetokea kwa binti yake huyo kilikuwa ni aibu kubwa kwa upande wakehasa ukizingatia katika mtaa huo aliyokuwa akiishi Moshi mjini, Majengo kwa Mtei yeye ndiye Mzee aliyekuwa akisifika kuwana binti mrembo ambaye alijitunza na kuwa na hofu ya Mungu.
Kutokana na uzuri aliyokuwa nao Suzani kila mwanaume aliyemuona alimtamani na kuanza kumfuatilia.

Mpaka kufikia kipindi hicho hakukuwa kuna mwanaume hata mmoja katika mtaa huowala chuoniambaye alifanikiwa kuiona hata nguo yake ya ndani.Hilo lilizidi kuwachanganya sana wanaume ambao walitamani kufanya naye mapenzi tu!.

Kwa kile kilichokuwa kimetokea kwa binti yake huyo Mzee Mushi kilimuumiza sana, kilimchanganya mno. Kuna muda alitamani mpaka kulia kwa kufikiria ni wapi ambapo angeificha sura yake kutokana na aibu kubwa aliyoipata katika maisha yake.

Moyo wake uliingiwa na chuki kubwa, kila alipokuwa akimwangalia mwananye alihisi kumchukia vibaya mno. Hakutaka kumuona mbele ya macho yake kwani aliamini kwa kuendelea kumuona kuna jambo baya ambalo angeweza kumfanyia na dunia ingemshangaa.

Mke wake aliyejulikana kwa jina laBi Anna huruma ikamuingia,hakupenda kuona binti yake akiendelea kulia na kusononeka kila siku, kama ni kosa tayari alikuwa ameshalifanya hivyo hakukuwa na jinsi tena zaidi ya kusaidiwa.

Alichokuwa akihitaji kwa wakati huo ni kuona mume wake akimsamehe Suzani na kumsaidia kutokana na hali ambayo alikuwa nayo. Alimpenda mno binti yake huyo ambaye ndiye mtoto wa pekee ambaye alijaaliwa kumpata katika kipindi chote cha ndoa yake.

Hilo lilikuwa ni jambo gumu mno, Mzee Mushi hakutaka kukubali kirahisi msamaha huo kwa binti yake.
“Mume wanu lakini..”

“Nimesema sitaki kumuona hapa nyumbani kwangu. Nitamuua,” alisema Mzee Mushi huku uso wake ukiwa tayari umebadilika.

Kwa jinsi ambavyo alikuwa akionekana Mzee huyo na maneno aliyokuwa akiyazungumza. Vilikuwa ni vitu viwili vilivyofanana.Yaani kile alichokuwa akikizungumza ndicho hicho hicho ambacho alikimaanisha.

Uamuzi ambao aliamua kuuchukua ni kumfukuza binti yake huyo. Hakutaka kumuona.

Japokuwa mkewe Bi Anna alimsisitiza na kumuomba zaidi na zaidi asichukua uamuzi huo wa kumfukuzwa binti yaohuyo ambaye kwao alikuwa kama mboni ya jicho lakini hakutaka kumsikiliza. Aliamua kumfukuza Suzani.
Suzani hakutaka kuamini kama kweli alifukuzwa nyumbani kwao tena na Baba yake mzazi.

Machozi yalikuwa yakimdondoka. Kuna muda alianza kujutiayale yote aliyoyafanya katika maisha yake. Kitendo cha kukutana na mwanaume Facebook mpaka akamuamini na kumkabidhi moyo wake ambao aliuumiza.

Muda huo tayari alikuwa amechelewa kwani hata kama angeendelea kujutia kosa alilokuwa amelifanya bado ukweli usingeweza kubadilika.

*Je, nini kitaendelea?*
*Tukutane Jumamosi mahali hapahapa.*
😢😢
 
*CHOZI LISILOFUTIKA-04*
Mtunzi:Juma Hiza

Walipoambiwa hivyo hawakutaka kuamini, walihisi labda walidanganywa. Walichokifanya wakachukua simu zao, wakaingia Facebook kisha wakaanza kulitafuta jina la Suzani Mushi.

Yakatokea majina ya Suzani kama kumi, wakaanza kupitia akaunti moja baada ya nyingine. Kila picha ya Suzani waliyekuwa wakimuangalia, hakuwa Suzani yule waliyemfahamu. Hilo likazidi kuwachanganya.

Hawakutaka Suzani aendelee kuishi maisha ya kizamani kwani kwa kipindi hicho dunia ilikuwa tayari imetawaliwa na utandawazi.

Licha ya kwamba msichana huyo alilelewa katika mazingira ya kidini na wazazi wake yaliyomfanya mpaka ashindwe kuwa bize na mtandao huo, hata pale alipoenda kufanya ibada kwenye kanisa la Seventh Day Adventist, mchungaji wa kanisa hilo alikuwa akisema kwamba shetani alikuwa akifanya kazi yake katika mtandao wa facebook kwa ajili ya kuwapotosha watu ili wasahau kufanya ibada.

Hilo hawakutaka kukubaliana nalo, walichoamua kukifanya wakaanza kumshawishi ajiunge na mtandao huo kwani kuna mengi mazuri yalikuwa yakimpita.

“Watu wamepata wapenzi, kazi, marafiki kwenye mtandao huu,” alisema Brenda rafiki yake Suzani.

“Kama mimi facebook imenikutanisha na marafiki wengi sana ambao sikuwahi kuwaza kama kuna siku ningewafahamu,” alisema Rukia huku akiendelea kuusifia mtandao huo.

Kwa jinsi Brenda na Rukia walivyokuwa wakiusifia mtandao huo wa Facebook, Suzani akajikuta akitamani na yeye kufungua akaunti katika mtandao huo. Hilo wala halikuwa tatizo hata kidogo, akafanikiwa kufungua akaunti.

Moyo wake ulikuwa ni wenye furaha baada ya kuwa na akaunti facebook. Akaanza kupost picha zake huku kila siku akizidi kupata idadi kubwa ya marafiki.

Wanaume wengi waliyokuwa watumiaji wazuri wa facebook walipoziona picha zake walizipenda na kumtamani hivyo wakaanza kumsumbua kwa kumtumia ujumbe inbox. Kila ujumbe aliyotumiwa ulikuwa ni wa mapenzi na kila mwanaume alitamani kuwa naye.

Picha zake zikazidi kuwachanganya wanaume wa facebook. Humo kulikuwa kuna wazungu, waarabu, wachina na wanaume kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambao walitokea kuvutiwa naye.

Hakukuwa kuna mwanaume aliyeziona picha za msichana huyo kisha asiache kuingia katika akaunti yake ili aendelee kuzitazama picha zake nyingine zaidi na zaidi.

Suzani alikuwa na mvuto na hii ndiyo sababu ambayo ilipelekea kila mwanaume aliyemuona akamtamani na kuanza kumsumbua.

“I need to talk with you,” (Ninahitaji kuzungumza na wewe) ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa mzungu mmoja facebook aliyekuwa akitumia jina la Kenedy.
“I love you Suzani,” (Nakupenda Suzani) alituma mzungu mwingine.

Kipindi hicho Suzani kila alipokuwa akiingia facebook, alikutana na meseji nyingi ambazo alitumiwa na wanaume tofautitofauti. Kila mwanaume alisema anampenda na hivyo kutaka kumuoa.

Hakukuwa kuna mwanaume aliyepata nafasi ya kuchati ama kuzungumza na msichana huyo kwani hata pale walipokuwa wakimtumia ujumbe, haukuweza kujibiwa, Suzani alikuwa akiusoma na kuachana nao.

Akazidi kuonekana kuwa msichana wa gharama, thamani yake ikazidi kupanda siku hadi siku.

Sio chuoni tu bali hata wanaume waliyokuwa wakimuona Facebook walizidi kuchanganyikiwa.
Siku ziliendelea kukatika, Suzani akaanza kuonekana akiutumia muda wake mwingi kuperuzi Facebook.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kila kitu. Akazidi kuwa mtumiaji mzuri wa facebook mpaka pale alipoanzisha urafiki na mwanaume mmoja kwenye mtandao huo aliyejulikana kwa jina la Enock Mabula.

Huyu Enock alimsumbua sana, kila siku kazi yake kubwa alikuwa akimtumia ujumbe Suzani lakini haukuwa ukijibiwa. Hilo lilimsononesha mno na kumfanya kuanza kukata tamaa.

Siku moja Suzani alipost picha yake facebook akiwa maeno ya chuo, akaandika kwamba hakuwa sawa siku hiyo hivyo alihitaji marafiki wa facebook ambao wangeweza kumfariji mpaka arudi katika hali yake ya kawaida.

Siku hiyo Enock alipoiona post ya msichana huyo kwa kuwa mara kwa mara alikuwa akiingia facebook na kumuangalia, haraka sana akakumbuka kulike na kucomment kwa kumpa pole na kumsifia lakini pia hakuishia hapo, akamtumia ujumbe.

Baada ya kupita dakika moja ujumbe huo ukajibiwa. Enock hakutaka kuamini kama msichana huyo aliweza kumjibu ujumbe wake kwani kabla ya hapo aliwahi kumtumia ujumbe zaidi ya mara tano tena katika siku tofauti tofauti lakini hakuwahi kujibiwa hata mara moja.

Siku hiyo ikawa ni siku yenye furaha kwa upande wake, akaurudia kuusoma ujumbe huo mara mbilimbili huku akiwa haamini kabisa. Hakutaka kupoteza muda na yeye akaujibu na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kuchati kwao.

Walichati sana siku hiyo mpaka kufikia hatua wakabadilishana namba za simu. Enock alifurahi sana, hakutaka kuamini kama aliweza kuchati siku hiyo na msichana huyo mpaka kufikia hatua ya kupewa namba ya simu.
****
Revocatius mapenzi yaliendelea kumtesa moyoni mwake, kila alipomuona Suzani alizidi kuchanganyikiwa. Alimpenda sana lakini msichana huyo hakuonekana kujali kitu.

Alimpigia sana simu, alimtumia kila aina ya ujumbe msichana huyo lakini majibu aliyokuwa akijibiwa yalizidi kumuumiza. Hakujua kama kipindi hicho ambapo alikuwa akimfuatilia tayari alishakuwa na ukaribu na Enock mwanaume ambaye alimpatia Facebook.

Je, nini kitaendelea?
narudi,naweka alama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom