denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,149
Hii pointi nzuri; wengi wanakuja na wazo la kususa lakini hawana plan B ya nini kifanyike badala yake, hayo kwangu ni mawazo ya kitoto, ukiwasusia CCM bado maisha yataendelea tu, hawajali, na kama wakisusa kweli, bora na uchaguzi mkuu ujao wasishiriki kabisa, kwasababu wakishiriki matokeo yake watawasababishia wafuasi wao madhara kama haya yaliyowapata kwenye uchaguzi huu.Baada ya kususia nini kifuate. Kama kuna guarantee ya haki kutendeka sawa. Nahofia kama ya 2015.
Katika mazingira hayo ndio nikasema bora waingie tu.
Unafiki was CCM unaendelea tu. Roho za wazanzibari zinazidi kupotea.
Tutulie kufanya tathmini. Jazba haina maana.
Mimi naamini katika kupunguza madhara na kuyafanya mapambano yadumu.
Sasa hivi kuna dhoruba LA kisiasa, linahitaji majemedari hodari kuusoma mchezo.
Narudia tena jazba haifai lazima uwe na focus. Kususia kutapoteza hata network ya ndani.
Walau kushiriki kutapunguza madhara ambayo naamini CCM wameshayapanga.
Hiyo GNU yenyewe inaenda kufutwa.
Itoshe tu. Maalim na ACT wawatafute wazee na kamati zao wajadili kwa kina na kupanga mikakati ya kuishi na adui na isiinekane usaliti.
Zanzibar iko pabaya sana. Nahodha hodari anahitajika sio jazba.
Bora waache kushiriki uchaguzi kabisa ili kulinda roho za wafuasi wao. Hili linatakiwa kufanyika hata huku Bara.