Chonde chonde chama changu CHADEMA

Chonde chonde chama changu CHADEMA

mtz one

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2012
Posts
4,275
Reaction score
1,222
Wandugu nawaomba viongozi na wanachama wote wa CHADEMA kuachana na suala la maandamano ya DSM nawashauri watii mamlaka zilizopo hata biblia inatuagiza.

Tutaumiza wanachama wetu bure chonde chonde jamani AMANI NI KITU CHA THAMANI KUBWA HAIPATIKANI KWA BEI RAHISI
 
kwani maandamano ya CDM yamezuiliwa? binafsi sioni tatizo kama maandamano ni ya amani! kama hoja za wabunge wa upinzani zinapigwa teke huko Bungeni sasa wasemee wapi kama sio kwa wananchi?!
 
Amani ni tunda la haki.Akina Mandela na Steve biko wangeendelea kuitii malaka ya Makaburu hadi leo hii sijui wangekua wapi..

Dunia Ingeendelea kutii Mamlaka ya Adolf Hitler na Hegemony ya chama chake cha NAZI sijui leo Dunia ingekuaje!

Hata mitume na Manabii wa dini zote walilazimika kupambana na mamlaka zilizokuwepo ili kuleta haki na ukombozi kwa watu.Itumie mishafu vizuri
 
Wandugu nawaomba viongozi na wanachama wote wa chadema kuachana na suala la maandamano ya DSM nawashauri watii mamlaka zilizopo hata biblia inatuagiza tutaumiza wanachama wetu bure chonde chonde jamani AMANI NI KITU CHA THAMANI KUBWA HAIPATIKANI KWA BEI RAHISI

Umetumwa vipi, mbona hueleweki au ndo kufikiria kwa kutumia makalio? Tofautisha kati ya maandamano na matembezi ya mshikamano.
 
Amani ni tunda la haki.Akina Mandela na Steve biko wangeendelea kuitii malaka ya Makaburu hadi leo hii sijui wangekua wapi..

Dunia Ingeendelea kutii Mamlaka ya Adolf Hitler na Hegemony ya chama chake cha NAZI sijui leo Dunia ingekuaje!

Hata mitume na Manabii wa dini zote walilazimika kupambana na mamlaka zilizokuwepo ili kuleta haki na ukombozi kwa watu.Itumie mishafu vizuri
kaka ben huwezi fananisha ujerumani na tanzania kumbuka kule kulikuwa na utawala dhalimu,,,, mandela alipambana na wakoloni sasa sisi tuko huru tunajitawala wenyewe unajua kuruhusu maandamano hovyo inaweza kutokea ya misri nchi yetu ni changa sana kubeba madhila hayo ni bora tuone mbali bora ungefanyika mkutano bila maandamano
 
Wandugu nawaomba viongozi na wanachama wote wa chadema kuachana na suala la maandamano ya DSM nawashauri watii mamlaka zilizopo hata biblia inatuagiza tutaumiza wanachama wetu bure chonde chonde jamani AMANI NI KITU CHA THAMANI KUBWA HAIPATIKANI KWA BEI RAHISI

Ha we vipi kama we hautaki kuandamana siubaki nyumbani kwako na familia yako..Katiba ya nchi inaruhusu maandamano na chadema inafuata Katiba
 
Umetumwa vipi, mbona hueleweki au ndo kufikiria kwa kutumia makalio? Tofautisha kati ya maandamano na matembezi ya mshikamano.
tumeambiwa ni maandamano ya kuwapokea wabunge wetu toka dodoma
 
Ha we vipi kama we hautaki kuandamana siubaki nyumbani kwako na familia yako..Katiba ya nchi inaruhusu maandamano na chadema inafuata Katiba
ndugu yangu naangalia interest za utaifa si familia
 
Lakini nami kwa ili pia kwa upande wangu namuunga mkono mleta mada, ccm washaijua nguvu ya chadema ivo hawana amani nahisi watapanga kutumia policcm kuwaadhibu watu pia wafuasi wa chadema kwa lengo la kujustify kuwa chadema ndo wamekuwa chanzo cha lolote, ivo nashauri uongoz wa chadema wafuate taratibu zote za kupata kibali pia ulinzi na apo sote tutafurika mkutanoni kuwalaki viongozi bila shaka pia wasiwasi wa ktokea maafa
 
LAKINI NAMI KWA ILI PIA KWA UPANDE WANGU NAMUUNGA MKONO MLETA MADA, CCM WASHAIJUA NGUVU YA CHADEMA IVO HAWANA AMANI NAHISI WATAPANGA KUTUMIA POLICCM KUWAADHIBU WATU PIA WAFUASI WA CHADEMA KWA LENGO LA KUJUSTIFY KUWA CHADEMA NDO WAMEKUWA CHANZO CHA LOLOTE, IVO NASHAURI UONGOZ WA CHADEMA WAFUATE TARATIBU ZOTE ZA KUPATA KIBALI PIA ULINZI NA APO SOTE TUTAFURIKA MKUTANONI KUWALAKI VIONGOZI BILA SHAKA PIA WASIWASI WA KTOKEA MAAFa
 
Lakini nami kwa ili pia kwa upande wangu namuunga mkono mleta mada, ccm washaijua nguvu ya chadema ivo hawana amani nahisi watapanga kutumia policcm kuwaadhibu watu pia wafuasi wa chadema kwa lengo la kujustify kuwa chadema ndo wamekuwa chanzo cha lolote, ivo nashauri uongoz wa chadema wafuate taratibu zote za kupata kibali pia ulinzi na apo sote tutafurika mkutanoni kuwalaki viongozi bila shaka pia wasiwasi wa ktokea maafa
mi ningeshauri wafanye tu mkutano wa hadhara na waseme kile wanachotaka kusema kwa sababu lengo ni kufikisha ujumbe haina mana kuwa na maandamaano yatakayoumiza watu
 
maandamano yatasababisha foleni kuwa mbaya zaidi.
Kwanza ni kihoja mbunge wa Singida kupokelewa Dar es Salaam, hawa wabunge wanatakiwa warudi majimboni kwao kuwapa wananchi mrejesho. Huko ndio wapokewe...
 
maandamano yatasababisha foleni kuwa mbaya zaidi.
Kwanza ni kihoja mbunge wa Singida kupokelewa Dar es Salaam, hawa wabunge wanatakiwa warudi majimboni kwao kuwapa wananchi mrejesho. Huko ndio wapokewe...
hiyo point mkuu
 
kaka ben huwezi fananisha ujerumani na tanzania kumbuka kule kulikuwa na utawala dhalimu,,,, mandela alipambana na wakoloni sasa sisi tuko huru tunajitawala wenyewe unajua kuruhusu maandamano hovyo inaweza kutokea ya misri nchi yetu ni changa sana kubeba madhila hayo ni bora tuone mbali bora ungefanyika mkutano bila maandamano

Tunapambana na mkoloni mweusi.Hatutaki kutawaliwa,tunataka kuongozwa.....!


Ungetumia nguvu hizi unazotumia hapa kumtaka au kumshinikiza Spika kutenda haki na utawala dhalimu wa CCM kusikiliza matakwa ya umma ili yasitokee hayo ya Misri kama ndiyo yanyaokutisha
 
Back
Top Bottom