Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,646
CHOMBEZO: TOROJO BAMIA( Winga teleza)
SEHEMU: 01
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500
TOROJO BAMIA( Winga teleza)
Ilikuwa mara ya pili akipita na ndoo kichwani akionesha akichukua maji nyumba ya mbali kidogo kutoka anapoishi. Vazi lake la dela alilolichomekea kwenye nguo ya ndani lilifanya umbile lake ya nyuma lililojaa sawa bin sawia kuonekana.
John Shuku kila alipopita alishindwa kufanya kazi ya kuteremsha bidhaa kwenye fuso na kumsindikiza kwa macho mpaka alipopotea na kutikisa kichwa kisha aliendelea na kazi.
Moyoni alijikuta akisononeka na kujisemea “Wakubwa wanafaidi.”
Wakiwa wanaendelea kuteremsha mizigo kwenye gari alipopata day worker ya kuteremsha mizigo kwenye gari na kulipwa ujira mdogo aliamini kabisa wanawake wazuri kama wale angewalia macho kwa vile hakuwa na hadhi ya kusimama naye hata fedha za kumhonga.
Wakiwa wanaendelea kushusha mzigo iliyokuwa mingi sana mara mvua ilianza kunyesha, ilibidi waache kazi ya kushusha mizigo na kusimama pembeni ya duka kusubiri ikatike ndipo waendelee. Lakini mwanamke aliyekuwa amemchanganya akili Shuku aliendelea kupita akichota maji na kunyeshewa na mvua na kuifanya nguo aliyopkuwa amevaa igande kwenye mwili na kuweza kuchora ramani ya nguo ya ndani na umbile tamu ya mrembo yule.
John Shuku alizidi kuteseka chini hali ilikuwa mbaya ilibidi kila wakati aweke mkono mfukoni ili watu wasijue jamaa kama ameshikika. Baada ya muda mvua ilikatika wakati yule dada alikuwa amekwisha maliza kuchota maji na wao waliingia mzigoni kumalizia kuteremsha mizigo iliyobakia ndani ya Fuso. Moyoni bado aliamini wenye fedha ndiyo pekee wenye kufaidi majumba na magari mazuri hata wanawake wazuri kama dada aliyepita akichota maji.
Kilichomchanganya kilikuwa vito vya thamani alivyokuwa amevaa na kusomba navyo maji bila kuhofia mvua. Kila sikio lilikuwa na tundu tatu na kila sikuo lilikuwa na hereni ya dhahabu pia mkononi alikuwa na bangiri na pete vyote vya dhahabu. Alijiuliza yeye akimsimamisha atamueleze kitu gani hata uwezo wa kumnunulia vocha ya elfu tano hakuwa nao.
Akiwa anaendelea kuteremsha mizigo lilikuja gari moja aina ya spoti yenye uwezo wa kubeba watu wawili tu. Baada ya gari lile kusimama aliteremka sharobaro mmoja aliyekuwa amenyoa kiduku na kuvaa pensi aliyoiteremsha na kuwa kata kei, chini alikuwa na raba ya bei mbaya.
Baada ya kushuka kwenye gari alikaa kwa mbele ya gari na kutoa simu ya bei mbaya kisha alipiga simu na kuzunguza kwa muda na kukata, kisha alisogea kwenye duka alilokuwa akiteresha mizigo John Shuku na kununua vocha za laini tatu za simu za shilingi elfu sitini.
Baada ya kununua alirudi kwenye gari lake, haikupita muda watu wote waligeuza shingo kuangalia upande ule. John Shuku naye aliangalia na kumuona yule msichana aliyemchanganya akili akiwa amepiga pamba za hatari kigauni kifupi cha kuishia chini kidogo ya makalio na kukifanya kuninginia kama kimetundikwa juu ya mti na kuyafanya makalio yapendeze kuyaona na kutamani ainame kuokota kitu ili uone vilivyopo chini ya kigauni kile.
Sehemu ya juu mgongo ulikuwa wazi karibia na kuuno, chini alivaa viatu virefu vya mikanda hakika alipendeza sana. Wote waliteseka kwa umbile la yule msichana lililokuwa wazi zaidi tofauti na wakati alipokuwa amevaa dela lililouficha mwili wake lakini aliyeteseka sana alikuwa Shuku kwa kuona umaskini sawa na ugonjwa wa ukoma kwani vitamu kama vile aliamini ataishia kula kwa macho au kumvutia hizia wakati akiitafuta pwani kwa mkono.
Baada ya kumfikia yule sharobaro alikumbatiana na kuanza kulana mate hadharani. Kitendo kile kilimchanganya sana Shuku anakujisahau kama alikuwa amebeba boksi la glasi na kujikuta likimdondoka boksi lililosababisha kuvunja baadhi ya glasi.
“Ooh! My Good,” Shuku alishtuka.
“Bwa mzee hizo glasi nakata kwenye hela yako.”
“Kata tu bwa nshee,” Shuku alilidhika kukatwa hela kutokana na hali iliyomtokea hakuelewa hata boksi lilivyomponyoka. Yule msichana alimtesa sana moyoni na kujikuta akishindwa kujielewa.
Rafiki yake yaliyekuwa karibu aliyekuwa akiona picha yote ya Shuku kuchanganywa na yule msichana alimuuliza:
“Shuku vipi?”
“Wee acha tu yule demu kanichanganya sana hata sijielewi na si kawaida yangu.”
“Tafuta ipo siku nawe utakula bata.”
“Wapi?”
“Usikate tamaa ukiwa bado unaishi, mbona mambo ya kawaida tu yale.”
“Aah wapi, tutaendelea kula kwa macho wenye fedha kila kituzuri watapata wao, majumba, magari na wanawake wazuri kama wale.”
“Maisha kibidubidu unaweza kulala maskini kesho unatumwagia maji unasahau kuna siku ulivunja glasi kwa ajili ya mrembo mmoja wakati huo wanakugombania kama mpira wa kona. Kaka fedha kama maua kila nyuki atatua.”
“Hizo ni ndoto za mchana.”
Shuku akiwa ameshindwa kabisa kuendelea na kazi macho yale yaliendelea kushuhudia mateso bila chuki jinsi yule mwanamke na sharobaro walivyojifanya wazungu kwa kuonesha mambo ya chumbani hadharani. Baada ya kuachiana msichana alikwenda upande wa uskani na mwanaume upande wa pili kisha yule mwanamke aliondoa gari kwa kasi.
ITEAENDELEA