CHOMBEZO: Torojo bamia(Winga teleza)

CHOMBEZO: Torojo bamia(Winga teleza)

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,646
Image may contain: 1 person, standing, shoes and text

CHOMBEZO: TOROJO BAMIA( Winga teleza)
SEHEMU: 01
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

TOROJO BAMIA( Winga teleza)

Ilikuwa mara ya pili akipita na ndoo kichwani akionesha akichukua maji nyumba ya mbali kidogo kutoka anapoishi. Vazi lake la dela alilolichomekea kwenye nguo ya ndani lilifanya umbile lake ya nyuma lililojaa sawa bin sawia kuonekana.
John Shuku kila alipopita alishindwa kufanya kazi ya kuteremsha bidhaa kwenye fuso na kumsindikiza kwa macho mpaka alipopotea na kutikisa kichwa kisha aliendelea na kazi.
Moyoni alijikuta akisononeka na kujisemea “Wakubwa wanafaidi.”
Wakiwa wanaendelea kuteremsha mizigo kwenye gari alipopata day worker ya kuteremsha mizigo kwenye gari na kulipwa ujira mdogo aliamini kabisa wanawake wazuri kama wale angewalia macho kwa vile hakuwa na hadhi ya kusimama naye hata fedha za kumhonga.
Wakiwa wanaendelea kushusha mzigo iliyokuwa mingi sana mara mvua ilianza kunyesha, ilibidi waache kazi ya kushusha mizigo na kusimama pembeni ya duka kusubiri ikatike ndipo waendelee. Lakini mwanamke aliyekuwa amemchanganya akili Shuku aliendelea kupita akichota maji na kunyeshewa na mvua na kuifanya nguo aliyopkuwa amevaa igande kwenye mwili na kuweza kuchora ramani ya nguo ya ndani na umbile tamu ya mrembo yule.
John Shuku alizidi kuteseka chini hali ilikuwa mbaya ilibidi kila wakati aweke mkono mfukoni ili watu wasijue jamaa kama ameshikika. Baada ya muda mvua ilikatika wakati yule dada alikuwa amekwisha maliza kuchota maji na wao waliingia mzigoni kumalizia kuteremsha mizigo iliyobakia ndani ya Fuso. Moyoni bado aliamini wenye fedha ndiyo pekee wenye kufaidi majumba na magari mazuri hata wanawake wazuri kama dada aliyepita akichota maji.
Kilichomchanganya kilikuwa vito vya thamani alivyokuwa amevaa na kusomba navyo maji bila kuhofia mvua. Kila sikio lilikuwa na tundu tatu na kila sikuo lilikuwa na hereni ya dhahabu pia mkononi alikuwa na bangiri na pete vyote vya dhahabu. Alijiuliza yeye akimsimamisha atamueleze kitu gani hata uwezo wa kumnunulia vocha ya elfu tano hakuwa nao.
Akiwa anaendelea kuteremsha mizigo lilikuja gari moja aina ya spoti yenye uwezo wa kubeba watu wawili tu. Baada ya gari lile kusimama aliteremka sharobaro mmoja aliyekuwa amenyoa kiduku na kuvaa pensi aliyoiteremsha na kuwa kata kei, chini alikuwa na raba ya bei mbaya.
Baada ya kushuka kwenye gari alikaa kwa mbele ya gari na kutoa simu ya bei mbaya kisha alipiga simu na kuzunguza kwa muda na kukata, kisha alisogea kwenye duka alilokuwa akiteresha mizigo John Shuku na kununua vocha za laini tatu za simu za shilingi elfu sitini.
Baada ya kununua alirudi kwenye gari lake, haikupita muda watu wote waligeuza shingo kuangalia upande ule. John Shuku naye aliangalia na kumuona yule msichana aliyemchanganya akili akiwa amepiga pamba za hatari kigauni kifupi cha kuishia chini kidogo ya makalio na kukifanya kuninginia kama kimetundikwa juu ya mti na kuyafanya makalio yapendeze kuyaona na kutamani ainame kuokota kitu ili uone vilivyopo chini ya kigauni kile.
Sehemu ya juu mgongo ulikuwa wazi karibia na kuuno, chini alivaa viatu virefu vya mikanda hakika alipendeza sana. Wote waliteseka kwa umbile la yule msichana lililokuwa wazi zaidi tofauti na wakati alipokuwa amevaa dela lililouficha mwili wake lakini aliyeteseka sana alikuwa Shuku kwa kuona umaskini sawa na ugonjwa wa ukoma kwani vitamu kama vile aliamini ataishia kula kwa macho au kumvutia hizia wakati akiitafuta pwani kwa mkono.
Baada ya kumfikia yule sharobaro alikumbatiana na kuanza kulana mate hadharani. Kitendo kile kilimchanganya sana Shuku anakujisahau kama alikuwa amebeba boksi la glasi na kujikuta likimdondoka boksi lililosababisha kuvunja baadhi ya glasi.
“Ooh! My Good,” Shuku alishtuka.
“Bwa mzee hizo glasi nakata kwenye hela yako.”
“Kata tu bwa nshee,” Shuku alilidhika kukatwa hela kutokana na hali iliyomtokea hakuelewa hata boksi lilivyomponyoka. Yule msichana alimtesa sana moyoni na kujikuta akishindwa kujielewa.
Rafiki yake yaliyekuwa karibu aliyekuwa akiona picha yote ya Shuku kuchanganywa na yule msichana alimuuliza:
“Shuku vipi?”
“Wee acha tu yule demu kanichanganya sana hata sijielewi na si kawaida yangu.”
“Tafuta ipo siku nawe utakula bata.”
“Wapi?”
“Usikate tamaa ukiwa bado unaishi, mbona mambo ya kawaida tu yale.”
“Aah wapi, tutaendelea kula kwa macho wenye fedha kila kituzuri watapata wao, majumba, magari na wanawake wazuri kama wale.”
“Maisha kibidubidu unaweza kulala maskini kesho unatumwagia maji unasahau kuna siku ulivunja glasi kwa ajili ya mrembo mmoja wakati huo wanakugombania kama mpira wa kona. Kaka fedha kama maua kila nyuki atatua.”
“Hizo ni ndoto za mchana.”
Shuku akiwa ameshindwa kabisa kuendelea na kazi macho yale yaliendelea kushuhudia mateso bila chuki jinsi yule mwanamke na sharobaro walivyojifanya wazungu kwa kuonesha mambo ya chumbani hadharani. Baada ya kuachiana msichana alikwenda upande wa uskani na mwanaume upande wa pili kisha yule mwanamke aliondoa gari kwa kasi.

ITEAENDELEA
 
CHOMBEZO: TOROJO BAMIA( Winga teleza)
SEHEMU: 02
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500
ILIPOISHIA:
Shuku akiwa ameshindwa kabisa kuendelea na kazi macho yale yaliendelea kushuhudia mateso bila chuki jinsi yule mwanamke na sharobaro walivyojifanya wazungu kwa kuonesha mambo ya chumbani hadharani. Baada ya kuachiana msichana alikwenda upande wa uskani na mwanaume upande wa pili kisha yule mwanamke aliondoa gari kwa kasi.
SASA ENDELEA...

Baada ya gari kuondoka eneo lile walimalizia mzigo ulikuwa umebakia kidogo kwenye gari na kulipwa fedha yao waliyokatwa fedha kwa ajili ya glasi alizovunja Shuku. Kwa vile ilikuwa bado asubuhi washikaji zake walimweleza watafute sehemu nyingine wakapige mzigo.
Lakini Shuku aliyekuwa amechanganywa sana na yule msichana aliona siku ile kwake mbaya aliamjua mfadhaiko aliopata asubuhi ile heri aende nyumbani kulala ili siku ile ipite salama. Kama kawaida alipanga akifika nyumbani lazima amvutie hisia na kuitafuta pwani ya utamu kwa mkono.
Akiwa anarudi nyumbani toka Temeke kwenda gheto kwake Buguruni kwa Mnyamani. Alitembea huku akiwaonea wivu vijana wote wenye kutembelea mikoko ya nguvu pembeni yao wakiwa na warembo wa nguvu. Alipofika mataa ya Tazara akiwa anataka kuvuka barabara aliliona gari moja lilikuwa si la kawaida lilipofika pale ilijifungua na kuwafanya vijana waliokuwa karibu kushangilia.
Kitendo kile kiliongeza maumivu kwa Shuku na kutamani gari lile angekuwa akilitumia yeye basi angerudi kwa yule mwanamke aliyemfanya ashindwe kujielewa. Gari lile la rangi nyekundu baada ya kufanya manjonjo lilisimama kusubiri mataa.
Shuku alipokuwa akilishangaa huku akilisogelea alishtuka kumuona mtu aliyekuwa akiendesha lile gari na kujikuta akipayuka kwa sauti.
“Ha! Mjuni.”
Yule aliyekuwa ndani ya gari aliyelipuka na mikufu na mipete ya kizungu la unga alishtuka kidogo na kujiuliza nani anayemfahamu jina la utoto ambalo toka akinyake mapene kwa kuuza unga alijiita Tajiri mtoto au MJ.
“Wee nani?” alimuuliza huku kamkazia macho.
“Mjuni ni mimi Shuku.”
“Shukuuu..John?”
“Eeh Mjuni.”
“I cant beliave my eyes, ni wewe Shuku?” Zungu hakuamini kukutana na rafiki yake walipotezana muda mrefu sana.
“Ni mimi Mjuni.”
“Ingia kwenye gari tutakwenda kuzungumza mbele ya safari.”
Shuku aliingia kwenye gari wakati huo mataa yalikuwa yanaruhusu Mjuni aliondoa gari kufuata barabara ya Mandela kuelekea Ubungo.
Gari lilitembea kwa mwendo mrefu bila mtu kuzungumza, muda wote Shuku alikuwa akimshangaa Mjuni jinsi alivyoyakatia denge maisha. Alikuwa amelipuka pamba za uhakika pia kumiliki gari la bei mbaya. Alikumbuka mara ya mwisho kuachana na Mjuni ilikuwa nyumbani kwao Mbeya baada ya Mjuni kuzamia magari yanayokwenda South kutafuta maisha.
Shuku yeye baada ya kuondoka rafiki yake alikaa mwaka mmoja na kuhamia Dar kwa mjomba wake na kutafutiwa kazi katika kiwanda cha Simba Plastic akiwa kama wafanyakazi wa kutwa.
Alifanya kazi kwa zaidi ya miaka miwili, kwa vile fedha aliyopata ilimtosha aliamua kuhama kwa mjomba wake na kuhamia Buguruni kwa Mnyamani aliyaanza maisha ya kujitegemea ambako alipanga chumba chake cha uani.
Kutokana na kupungua kwa kazi za uzalishaji kiwandani kwao baadhi ya wafanyakazi wa kutwa walisimamishwa kwa muda usiojulika mpaka uzalishaji utakapokuwa mzuri.
Mmoja wapo alikuwa Shuku ambaye aliamua kutafuta katika makampuni mengine lakini hali ilikuwa ileile. Yeye na washikaji zake waliosimamishwa pamoja waliamua kujichanganya kufanya kazi yoyote kupunguza ukali wa maisha.
Kila siku walikuwa wakijichanganya kila kona kila kazi iliyotokea mbele yao hawakuchagua mpaka siku alipotokewa na kimuhemuhe kile cha kuchanganyikiwa kumuona msichana mrembo ambaye aliamini hawezi kumpata zaidi ya kumla kwa macho na kumpa kasi ya kumfikisha pwani kwa mkono.
Mpaka gari linaingia ndani ya jumba la kifahari Shuku bado alikuwa katika ndoto za kumkumbuka Mjuni aliyeondoka kwenda South akiwa mwembamba lakini baada ya kurudi kaonekana mtu mwenye mwili wa fedha.
“Shukuuuu, karibu mtu wangu,” Mjuni amkaribisha rafiki yake huku akishuka kwenye gari.
“Ooh! Tumefika?” alikuwa kama mtu aliyetoka usingizini.
“Tumefika, karibu sana ndugu yangu.”
“Asante Mjuni.”
“Nitafurahi ukiniita MJ.”
“Poa MJ.”
“Basi karibu sana,” MJ alisema huku akibonyeza rimoti na mlango ulifunguka kitu kilichomuacha hoi Shuku na kuona mambo mageni kwake. Waliingia wote ndani ya jumba la Mjuni lilikuwa na kila kitu cha thamani kuonesha jamaa alikuwa amejipanga kimaisha na maisha alikuwa ameyapatia.
“Karibu sana rafiki yangu.”
“Asante sana.”
“Nimefurahi sana kukuona, nilikwenda home baada ya kurudi Bongo kutoka duniani nikaambiwa amezamia jijini. Nilishangaa kusikia umezamia Bongo badala ya nje ya nchi.”
“Ndugu yangu elimu yangu unaijua nitaweza kwenda sehemu gani, najua lugha ya asili na kiswahili tu.”
“Maisha ukifikiria hivyo utakufa bila kelele kama wafuasi wa kibwetele, mimi darasa la ngapi darasani wewe ulikuwa unaniburuza.”
“Mmh! Za siku?”
“Kama unavyoziona sasa hivi nafahamika kama umeme wa mgao hakuna mtu jijini asiyemjua MJ tajiri mtoto.”
“Mmh! Kweli unatisha siku hizi unavaa hereni wewe si ulikuwa ukisema wanaofanya hivyo mashoga?” Shuku alimuuliza rafiki yake.
“Ndugu yangu kama hujatembea utaona ajabu nimekutana na mambo ya ajabu na kuona kumbe kawaida. Kama mchungaji anaingia kanisani katoga sikio mimi nani mbele ya Mungu?”
“Lakini mila na destuli zetu hazikubaliani na utamaduni huo.”
“Kweli Shuku upo nyuma, pamoja na kuwahi jiji bado mgeni wa mambo, mbona huwashangai Wakulya wanaume wanatoga sikio na kuvaa hereni pia Wamasai wanawake wananyoa wanaume wanasuka.”
“Haya kaka umeshinda, Za siku?”
“Kama unavyoziona, vipi wewe maana nakuona umezeeka bado kijana mdogo?”
“Maisha ndugu yangu,” Shuku alimueleza maisha yake yalivyo, baada ya kumsikiliza alimuuliza.
“Ulipokuwa unakaa kuna kitu gani chako cha muhimu sana kwako?”
“Una maanisha?”
“Namaanisha kuwa hapa umefika sitaki uondoke, nataka kukurudisha katika ujana nakuona umezeeka kama unavuta sigara kali.”
“Kuna documenti zangu redio tivi kochi kitandani na vitu vichache nilipokuwa nimepanga.”
“Vitu vyote achana navyo utahamia hapa.”
“Nitashukuru lakini pale nadaiwa fedha ya mwaka mzima.”
“Shilingi ngapi?”
“Laki tatu na sitini.” Shuku aliongeza fedha nyingi makusudi wakati chumba alikuwa akilipa elfu kumi yeye aliongeza elfu ishirini kila mwezi. Nia yake kulipia miaka mitatu kwa vile asingemuamini mtu moja kwa moja.
“Okay, basi nitakupa ukalipe, unajua kudrive gari?”
“Ndiyo lakini sina leseni.”
“Nitakukatia.”
MJ alinyanyua simu na kumpigia mkuu wa polisi barabarani kumuomba leseni yenye jina la John Shuku.
“Sasa pumzika baadaye utakwenda kulipia chumba na kuchukua documenti zako kisha vitu vyote vya ndani vitoe sadaka kwa majirani zako.”
“Hakuna tatizo.”

Itaendelea kesho
 
CHOMBEZO: TOROJO BAMIA( Winga teleza)
SEHEMU: 03
MTUNZI: DR AMBE
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
MJ alinyanyua simu na kumpigia mkuu wa polisi barabarani kumuomba leseni yenye jina la John Shuku.
“Sasa pumzika baadaye utakwenda kulipia chumba na kuchukua documenti zako kisha vitu vyote vya ndani vitoe sadaka kwa majirani zako.”
“Hakuna tatizo.”
SASA ENDELEA...

“Basi utakwenda kupiga picha ya haraka kisha utazipeleka kesho utaipata.”
“Nitashukuru.”
“Sasa tukaoge ili uuage umaskini.”
Shuku alipelekwa kuoga, baada ya kuoga alipelekwa kwenye chumba kilichokuwa na kila kitu ndani.
“Hiki ndicho chumba chako.”
“Asante sana ndugu yangu.”
“Hizo nguo nina imani zitakutosha aliyekuwepo huku unalingana naye mwili.”
“Asante.”
“Mimi nipo sebuleni kuna demu wangu anakuja muda si mrefu.”
“Poa.”
Shuku alibadili nguo kwa kuvaa bukta kubwa na singland kama mcheza basket ball, alitoka sebuleni na kumkuta rafiki yake akiangali mkanda wa blue printi.
“Mbona unaangali mkanda huu muda huu?” Shuku aliuliza.
“Kwani muda wake saa ngapi?”
“Usiku.”
“Acha ushamba mkanda huu unaungalia muda wowote, na mimi navutia kasi kuna mtoto si wa kawaida ataingia muda si mrefu.”
Shuku hakujibu naye alikaa kwenye sofa lingine na kujilaza kula kupupwe cha kiyoyozi naye alikula kideo.
“Shuku una demu?” MJ alimuuliza rafiki yake bila kumtazama.
“Sina.”
“Huna! Una matatizo gani?”
“Sina tatizo basi nimeamua.”
“Hapana Shuku lazima utakuwa na tatizo, kwa nini usiwe na mpenzi wakati dunia ya leo imejaa wanawake wazuri wanaotafuta wanaume hata kwa kuwahonga.”
“Hao wazuri wanagharama, wa kuhonga sijapata.”
“Kwa hiyo hata wa siku mojamoja huna?”
“Nikiwa nimezichanga nakwenda Kimboka au Sewa najipigia juu kwa juu tunaachana, wale hawana gharama sijui wameishiwa lotion au kwenda salon mkilipana na kumalizana hamjui tena hawana gharama ya guest kwenye kichochoro anapandisha nguo wewe unamwaga mzigo mnaachana.”
“Mmh! Sikuwezi.”
“Kawaida, nami ningekuwa nazo ningetafuta mrembo mmoja wa kula naye bata kama wewe.”
“Usiwe na wasiwasi changu chako nitahakikisha raha ulizozikosa unazipata hapa.”
“Nitashukuru, vipi wewe hujaoa?”
“Nioe watoto wote wazuri na watamu nimuachie nani?”
“Kwa hiyo huna mke?”
“Sina.”
’Ila?”
“Nina watoto wazuri.”
Mara kengere ililia MJ alichukua limoti na kufungua mlango, baada ya kufunguka aliingia msichana mmoja mbichi aliyekuwa na mgongo wa kufa mtu. Alikwenda kumkalia MJ alipokaa na kuanza kumla denda mbele ya Shuku aliyechanganyikiwa baada ya kuinama sketi kuteremka chini na kufanya kiuno chake chenye cheni ya dhahabu. Kilichommaliza kilikuwa bikini iliyomezwa na mgogo wa kufa mtu.
Shuku akiwahi kupeleka mkono kambi ya jeshi mkumsihi mwanajeshi wake awe mpole kwani ile haikuwa vita yake.
“Mmmh! Nimekumisi ile mbaya sweet,” mtoto wa kike alimung’unya maneno.
“Karibu baby.”
“Ha! Baby unaangalia hii?” Yule msichana alishtuka na kugeuka baada ya kusikia sauti za uchokozi toka kwenye kideo.
“Si nilikuwa nakuvutia kasi.”
“Basi na mimi nalianzia hapahapa nataka nile koni kama wa kwenye kioo,” msichana alisema huku akiteremsha bukta ya shuku na kuishika maiki mbele ya Shuku na kutaka kuanza kuimba. MJ alimshuka na kuirushisha maiki ndani.
“Baby utaniudhi,” mtoto wa kike alilalamika.
Yule msichana aliyekuwa bado kainama na sketi nawe kuweka mambo yote nje, mgongo uliokuwa kama deki iliyomeza kanda ulimfanya Shuku azidi kuteseka na kugugumia kwa maumivu na kujisemea mwenyewe “Wenye fedha wanafaidi.
“Noma baby humuoni ndugu yangu?” MJ alishikilia msimamo wake.
“Kwani hajui?”
“Hata kama anajua, lakini lazima tumuheshimu.”
“Mbona mlikuwa akiaangalia pamoja, heshima ipo wapi? Hebu nipe raha zangu.”
“Hapana twende chumbani.”
MJ alinyanyuka na kuelekea chumbani na yule mwanamke aliyevaa sketi fupi ya kitambaa laini iliyotelemka na kuonesha kifusi kilichomeza bikini. Walielekea chumbani wakiendelea kulishana mate, na kumwacha Shuku akiwasindikiza kwa macho. Hali yake ilikuwa mbaya sana na kuona kama mateso aliyoyakataa ameyafuata ndani.
Shuku alibakia akiwa na maumivu makali ya chini, baada ya mzizi kutaka kutoboa ardhi kwa hasira. Lakini hakuwa na jinsi alitulia macho yake yakiwa kwenye video kulikokuwa kunaendelea mkanda wa Blue print, aliona unamzingua aliamua kuizima na kujilaza kwenye kochi.
Baada ya muda yule binti chumbani macho yakiwa yamebadilika rangi na kuwa mekundu ilionesha alichezea makofi katika kichaka cha nyani. Alitoka akirekebisha sketi yake vizuri nyuma alifuata MJ akiwa kifua wazi huku amejifunga taulo kuonesha amegawa dozi. Bila kutegemea Shuku alimshangaa yule mchichana kuja alipokuwa amekaa na kumbusu mara tatu na kusema:
“Shemu kwa heri.”
“A..a..sa..,” hakumalizia alitulia baada ya joto la yule msichana mrembo kumfanya apasue dafu. Bila kutikiswa na upepo wala kuchumwa.
Hali ile yule msichana aliiona na kusema kwa upole:
”Oohh ! Shemu pole eeh,” alisema huku akimchezea ndevu chache chini ya kidevu na kumpiga busu lingine kisha alitoka kwa mwendo wa kuchepuka kuelekea mlangoni.
Baada ya kutoka nje MJ alimgeukia rafiki yake aliyekuwa amejishika ikulu kutokana na kuangukiwa na dafu na kumpasukia.
“Vipi?”
“Mmh! Wee mkali.”
“Umeona eeh.”
“Mmh! Mtoto mzuri kama huyu umemtoa wapi?”
“Ndiyo maana ndugu yangu sitaki kuona vitamu hivi ningevila saa ngapi?”
“Sasa MJ mwanamke mzuri kama huyu si ndiye ungemuoa.”
“Mbona huyu wa kawaida wapo kumi kama hawa.”
“Wote wapenzi wako?”
“Kipi cha ajabu, mwenye fedha chochote kizuri ni halali yake unafikiri kama nikimuoa vingine vitamu nilivile kwa macho?”
“Na ugonjwa.”
“Ugonjwa gani?”
“Ukimwi?”
“Ukiugua si umeugua, kwani wote wanaokufa wameugua ugonjwa huu?”
“Siyo, lakini unadhoofisha nguvu za mwili.”
“Magonjwa yapo mengi lakini hayazungumzwi, pia mwenye fedha huwa hauguwi.”
Wakiwa katika ya mazungumzo kengere ya mlangoni iliita, MJ alifungua mlango, mara aliingia msichana wa kiarabu aliyekuwa katika vazi la hijabu baada ya kuingia aliivua na kuitupia pembeni kisha alikwenda kumrukia MJ na kuanza kumla ndenda bila hata ya kuangalia pembeni kama kuna mtu.
Shuku alishangaa kumuona yule msichana baada ya kuvua hijabu hakuwa na kitu kingine zaidi ya bikini iliyomezwa na mgongo wa kufa mtu. Kila msichana aliyeingia kuwa na mgongo ilimshtua sana Shuku na kujiuliza kuna siri kwa rafiki yake kupenda wenye migongo mikubwa na kuwa na wasiwasi huenda ni wakala wa kampuni ya simu.

Itaendelea kesho,
 
Tuko pamoja mwanangu

*real is not real fake is not fake*
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom