Chombezo: Paula Mfaransa mwenye visa

Eng Kimox Kimokole

JF-Expert Member
Jun 9, 2010
1,032
759
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU YA KWANZA

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Ni asubuhi njema sana yenye kajimvua ka kiaina kanakosababisha kuwepo na hali ya vuguvugu lenye kukera kiasi. Naamka kivivu kitandani kama nimelazimishwa. Nasikilizia viungo vya mwili vinavyokataa kunipa ushirikiano. Mwili kama nimepigwa na virungu usiku kucha.

Najivuta kukaa kitandani mikono nimeitambaliza kulia na kushoto kichwa nakitupa kifuani kuegemea na kidevu kukipa sapoti nikivuta kumbukumbu namna usiku wa jana tulivyoitumia na ‘mchizi’ wangu Baraka Lusewa pale SamakiSamaki Posta tukigonga vitu. Baraka akipiga KVANT kama kawaida yake na Sprite mimi nikisukuma vitu vya Whisky. Natokwa na tabasamu namna mara ya mwisho alivyokuwa anaamka huku miguu imepoteza uwezo wa kubeba mwili.

Nikamkamata mkono kumkalisha chini nikamwambia, “Kaka mambo si mambo, twende nikusindikize hapo hotelini ukapumzike maana kesho una issue zako mahakamani unakumbuka?” Hatunaga shida mimi na Baraka kwenye swala la maelewano. Akanyanyuka kachangamka sana. Tukaanza kukatoka huku tumeshikana mabega.

Akakipoka kichupa cha KVant kilichobaki mezani kama mwivi vile. Tukatoka nje na kumuelekeza akae kiti cha abiria nimpeleke Kilimanjaro Hyatt alikofikia.

Fikra zangu zikatibuliwa na maumivu fulani ya kimsumali shingoni, nikajikata kofi la hasira Phaaa!! Mbu gani wa asubuhi hawa aagh!!! Naamka kinyonye kuingia bafuni kujiswafi kisha natengeneza kifungua kinywa. Mayai mawili, chai ya maziwa na soseji tatu. Kidogo najihisi nguvu za mwili zikitamalaki ninapoitupia chai kwenye koo langu. Hu undo uzuri wa whisky ninazokunywa, sinaga mning’inio asubuhi wa kukera.

Najikuta navutiwa na kaudadisi ka kutaka kujua rafiki niliyekutana naye jana usiku pale Kilimanjaro Hotel Hyatt usiku wakati nikimuacha Baraka. Ooooh Paula. Najiegemeza kwenye kochi taratibu na kikombe changu cha chai, nashusha pumzi nikivuta kumbukumbu za mara ya kwanza tulipokutana na Paula binti wa Kifaransa nilipozulu Dortmund Ujerumani kwenye mishe za maisha.

Mimi na Paula kwa mara ya kwanza tulipanda wote treni kutoka Bochum Nord kwenda Dortmund. Mimi nikifika pale Dorstfeld na yeye akiwa Westfalenhalle. Tulikutana kwenye mishe mishe za kusaka noti maisha yaende tukajikuta marafiki. Unajua hawa wenzetu wenye ngozi nyeupe urafiki kwao ni jambo jema.

Kumbukumbu zinanijia namna ilivyokuwa rahisi kuwa na urafiki na Paula kutokana na ubaguzi mkubwa kutoka kwa Wajerumani. Ukienda hata dukani ukauliza kitu ili ununue kwa kiingereza muuzaji anakutumbulia macho tu mpaka utamke hiko unachokitaka kwa kijerumani ndo anakuuzia. Hali hii mara nyingi ilinikera. Lakini baada ya kuwa na kampani ya Paula angalau nikapata wa kuchonga chonga nae na kupiga hadithi mbili tatu.

Sasa hamadi!!! Jana usiku nagongana kibega na Paula Hyatt The Kilimanjaro Hotel baada ya kupita pale kwenye kipimo cha kukagua vitu vya chuma. Nilikuwa napaki vitu vyangu mfukoni huku nafunga mkanda wa kiuno vyema na wakati huo nimesogelea mlango wa kioo wa pili. Kama hujafika Hyatt baada ya checkup ya vitu vya chuma na kuji sanitizer kujiepusha na corona kuna milango ya vioo miwili inayofunguka yenyewe ukiikaribia.

Sasa Baraka akiwa nyuma yangu mimi mbele nafunga mkanda mlango wa kioo ulipofunguka nikapigana kikumbo kiasi na mtoto wa kizungu. Nikanyanyua sura kumpa samahani, mara paaaap!!! Hamad ni Paula!!!!

Aliponyanyua sura naye akawa kama ameganda hivi ananifananisha. Neno likanitoka kibwege bwege hivi “...Paula?”. Naye akaendelea kunitazama na mara akasema “Kimox, is that you again?”. My gosh!!! Paula alikuwa ametupia vazi la kiafrika hasa utadhani mtoto wa Kitanga flani hivi.

Ana dera kama la Kihindi na mtandio aliouzunguusha shingoni wa rangi ya hudhurungi, masikioni kaning’iniza hereni ndefu za duara zinazogusa mabegani zile kubwa. Nywele kazimwaga kwa nyuma. Chini ana viatu vya kimasai vilivyomkaa vizuri kama alitengenezewa maalumu kwa ajili yake. Na vile ana shepu ya kibantu, utadhani siyo Mzungu wa Ufaransa kama una macho juu juu waweza jikwaa akikupita na bahati mbaya ukageuka uone kama yaliyomo yamo.

Mkono wa kulia alishika simu kali Vivo X50 Pro na bega la kulia kaning’iniza kijimkoba kinachoendana na rangi ya dera na mtandio. Tukabaki tunatazamana kama majogoo yanayogombea mtetea. Akanisogelea nami nikamsogelea akanipa kumbatio mwanana sana. Rafiki yangu wa Dortmund Ujerumani leo nakumbana naye tena Tanzania....

Nikapiga tena funda la chai ya maziwa na kuisokomeza soseji yote iliyokuwa mkononi mwangu huku nikitabasamu. Nikamwemwesa midomo huku fikra zikipita kichwani mwangu, “...hivi huyu Paula, Bongo hii kafata nini?”. Nikajijibu mwenyewe tena macho nimeyakodoa kulitazama feni la pangaboi linalozunguuka kimya kimya kama vile ndiyo mara yangu ya kwanza kuliona “...ila haina mbaya, amenambia namba ya chumba alichopo na kesho atakuwa na mapumziko, basi nitakwenda kumuona Rafiki yangu huyu dah!!!”

Mara unaingia ujumbe kwenye simu yangu, namba ni ngeni ila ni ya tiGo 0679 547...., nakutana na ujumbe “Hello! Kimox!! Good morning. Its Paula...”. Nikakumbuka kumbe jana alichukua namba yangu. That’s great. Nikabofya kitufe cha reply nikamjibu...

Itaendelea
 
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU 2

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Namaliza kunywa chai na kuvaa haraka haraka niwahi mihangaikoni mwangu. Mjini kila kitu ni pesa lazima nizisake hasa. Navitafuta viatu vyangu vile vizuri vya kiofisi vya brown kwenye shelf ya viatu. Navuta pea moja kali hv natinga. Najivuta kwenye kioo kikubwa cha kabati la milango minne kujitazama kama niko smart. Nachukua uturi kwenye dressing table na kujinyunyiza. Najihisi niko sawa sasa kwa mtoko.

Navuta hatua kadhaa kuziruka ngazi mbili mlangoni na kuubamiza mlango nyuma yangu mdogo mdogo mpaka parking naanza kujishauri kati ya hizi gari mbili Mazda RX-8 na Subaru Legacy ipi nitoke nayo. Najitazama nilivyovaa chaguo linadondoka kwa Mazda, Kwanza ni nyepesi, sport car halafu ina mlio wa kibabe. Vaa yangu leo si ya kiofisi though am looking more handsome kwa shati jeupe la vidoadoa vyeusi niliyotinga, suruali ya modo nyeusi, mkanda mweusi na saa aina ya Lorex. Na kwa vile mikono mirefu ya shati nimeikunja kidogo mpaka katikati ya mkono (kiganja na kiwiko) it looks more attractive ku drive Mazda than Subaru Legacy.

Nasogea kibanda cha parking na kufungua kiboksi cha funguo na kuto key ya Mazda. Nikafungua mlango wa mbele na kutumbukiza funguo kwenye switch nikaitekenya jino moja tu ikapasuka kwa mlio mtamu. Wale wa sport car mnajua mzuka wake. Nikainama kidogo kukifikia kifungulio cha boneti nikavuta nikasikia mlio wa boneti ukiachia mbele. Nikarudishia mlango na kwenda kuifungua boneti kisha nikasogea pembeni kwenye kiti cha garden nikakaa kizembe nikiisikilizia engine ikinguruma silence. Nina kawaida kabla ya kuondoka na gari niiwashe kwanza kwa atleast 10 minute niisikilizie kama iko poa kwa safari na kuipasha moto mashine.

Nikachomoa simu baada ya kusikia mlio wa sms. Nafungua msm nakutana na ujumbe wa Rose wa Mbezi Beach akinitakia asubuhi njema. Rose nib inti wa Kikerewe, mtoto ana rangi flani ya kibantu black beauty. Miguu ya Kihaya isiyokera inayobeba makalio makubwa kiasi ambayo yanapokea nguo yoyote na kuitunisha kama yana hasira hivi. Pua ndefu ya kisomali na macho ya mbalamwezi yaliyobeba kope ndefu na nyusi nyembamba. Ana macho yenye mboni nyeusi malegevu flani hivi. Akiniangalia huwa ananimaliza kabisa huyu mtoto.

Rose ana makusudi sana. Nikiwa naye lazima anitupiage jicho la mahaba huku akimwemwesa midomo yenye lips za chini nene na lips ya juu nyembamba kiasi, mdomo uliobeba meno yaliyojipangilia vyema meupeeeee. Kuna wakati akifungua kinywa nabaki puzzled kama bwege nikitamani awe anazungumza tuuuuu kwa sauti ya nyembamba yenye kubembeleza, tabasamu la kuniambia “am dying for you honey”. Akiongea na vile kuna wakati akilegeza jicho la kimahaba kwangu anaramba na lips hivi kwa kupitisha kiulimi chake kwa pembeni deiiiiim shit. This girl knows better. Vidole vyake vyembamba na nywele ndefu yaani ananimaliza kabisa. Rose bhana!!!!! Kifua kilichobeba maziwa madogomadogo size ya kati kama embe bolibo, kiuno cha size 28 na hips pana dooooh!!! Ananivurugaga sana akili wallahi Kimox mimi. Mawazo ya haraka haraka yananipitia kuhusu Rose.

Nabofya kitufe cha reply na kumjibu kimahaba mtoto mzuri huyu. Naandika huku nikitabasamu maana uwepo wake maishani mwangu ni kama tunu. Rose hawezi kutoka nyumbani kwao bila kunijulia hali. Ukifika mchana hawezi kwenda kula bila kunitafuta kujua nitakula nini. Akitoka kazini lazima anitafute, akiwa njiani ataniambia, akifika home atasema, kiufupi kila kitu anachofanya mimi ni namba moja wake. Najihisi Mfalme tena ninayedekezwa hasa kwa huyu mtoto wa Kikerewe.

Naitazama saa yangu nakuta dakika 10 tayari na gari iko poa. Naingia kwenye gari baada ya kuifunga boneti, nafunga mkanda kisha naukamata usukani kwa mikono yote miwili kichwa nimekiegemesha kwenye siti kwa kukisukuma kwa nyuma kama naangalia juu kidogo. Nimefumba macho na kumshukuru Mungu kwa kunipa nguvu ya kutaka kutoka sasa. Ni kawaida yangu nikiamka nashukuru Mung una nikiwa kwenye gari nikamate usukani na kumshukuru Mung una kuomba ulinzi wake ninapoingia kwenye shughuli zangu. Nakanyaga pedali ya mafuta kidogo niusikilize mlio wa Mazda kwa mara nyingine kisha natabasamu. Nikatumbukiza gia ya kurudi nyuma na kukanyaga mafuta. Kitu kikaitika taratibu, nikanyonga usukani na kurudi kinyume nyume kidogo kupata namna ya kugeuka. Nikageuza gari na na kulisogelea geti mkono ukiwa kwenye remote na kuibofya kitufe cha OPEN na geti likaanza kufunguka taratibu sana nami naendelea kulisogelea lenyewe likifunguka. Mazda ikagusa eneo la geti na kuchungulia pua nje kisha taratibu nikakunja usukani na kuliongoza kuiacha nyumba yang una geti likijifunga lenyewe taratibu kabisa.

Kutoka Kigamboni ninakoishi nikaona ngoja nipitie njia ya Ferry iwe rahisi kumsabahi Baraka pale Kilimanjaro Hotel kisha niendelee na mishe nyingine. Nikafika kivukoni na kuitumbukiza gari ndani ya kivuko. Nikakereka kidogo maana Pantoni haliondoki tumekaa tu. Kumbe kuna meli inapita hivyo ni lazima tuisubiri mpaka ipite ndipo Kivuko cha MV Kazi kivuke. Inakera kisai ukichukulia meli bado iko mbali kabisa lakini kile kiboti cha kuongozea meli kimekaa mbele yetu kutuzuia tusiondoke. Hii sheria inakera sometimes. Baada ya meli kupita tukasogea kwa mwendo wa konokono mpaka upande wa pili. Nikaiongoza gari kutoka kwenye gati, nikazunguuka upande wa Ikulu nikatokea hapa Mahakama ya Kazi kisha taratibu nafika Hyatt Kilimanjaro hotel. Nafika getini haraka sana askali anakuja na kimashine cha kukagulia mabomu kisha ananiongoza sehemu ya parking.

Nikatoka kwa mwendo wa kihandsome boy, najua kunesa yaani, bado mbwembwe za ujana ninazo ingawa age inakimbia, 40+ years si mchezo lakini bado naonekana wamoooo. Naji sanitizer kisha napita kwenye ukaguzi wa vitu vya chum ana kuingia moja kwa moja ndani kwenye room ya Baraka. Namkuta alishaamka siku nyingi tu akiwa anafunga tai yake vyema. Koti la suti nyeusi lipo mkononi, shati nyeupe na suruali nyeusi. Wakili huyu yuko smart sana. Sijui huwa wanafundishwa uvaaji wa hizi suti ama ni nini. Nikawaza nitamuuliza wakati mwingine. Tukasalimiana huku akiwa busy na kioo kurekebisha tai. Nikamwambia Baraka kuwa nakuja ngoja nimsalimie Paula mara moja.

Nikapanda lift mpaka ghorofa ya juu yake, nikakisogelea chumba cha Paula na kugonga mlango taratibu. Ni kama alikuwa ananisubiri mimi. Sekunde tu mlango ukafunguliwa na nikapata kumbatio la haja kutoka kwa Paula. Akanivutia ndani kana kwamba sikutaka kuingia vile. Yeye mbele mimi nyuma yake kanishika mkono ananikokota. Akanisogeza mpaka kwenye kochi akasimama mbele yangu, akanitazama na kutabasamu. Akanishika mabega na kunisukuma kidogo kwa kunikalisha akiniambia. Hebu ka ana jisikie huru. Tukaulizana salamu na vistori vya hap ana pale. Akanyanyuka kuingia chumba cha pili, nikamtazama kwa kufaidi mirindimo ya makalio yake. Nikajikuta midomo kama imeachama hivi. Makario yananesa nesa kana kwamba kuna spring, miguu mizuri ya kizungu iliyovaa high hills nadhani ndo sababu ya mirindimo ile ya makalio. Ana mwendo wa kimiss yaani, hawa watoto wa kizungu sometime wana makusudi sana. Hivi hajui hap ani Bongo. Mimi ni mbongo tena mtoto wa Kiafrika hasa, chaji mara moja mnara full kama ni gari jino moja tu ingini inaitika. Sasa kama ananifanyia kusudi huyu ujue. Huu urafiki utanishinda sasa, maana nishaanza kuona mapicha picha na kama network not reachable at this moment.

Akarudi na kukaa kochi la mbele yangu, chuchu zimemsimama kama zinataka kutoboa blauzi aliyovaa, midomo yake imejaa tabasamu nadhani ni kwa sababu hatujaonana muda mrefu. Macho yake akawa anayaelekeza kwangu straight, yaani hapepesi pembeni hata chembe. Nikahisi ugiligili kama unaanza kuniletea shida, macho yangu yakawa hayana ujasiri sana wa kumtazama, nilikuwa naongea mara nyingi nikitazama pembeni au chini na mara chache nikiibia kulitazama umbo lake. Nikawa najiwazia, “…hivi huyu kwa nini sikumla kule Ujerumani lakini?”. Uchu tu umenijaaa sina lolote. Kuna wakati nakosa maneno kama napatwa kigugumizi hivi.

Nikanyanyua sura na kumtazama kwa macho makavu sasa. Nikamuuliza “enhe, nambie Paula. Unajua nimekumic aisee?”. Akanitazama bila kusema neno, akanyanyuka na kunifuata nilipokaa. Kochi lina kijitoto cha kuwekea vinywaji kwa pembeni. Akakaa hapo. Akanishika shingoni na kuniangalia usoni kisha akasema “…mmmh, Kimox nimekumic pia, ni muda mrefu unajua tangu tukiwa Ujerumani. Sijui kwa nini sikukutafuta tena wakati ulinipa contact zako. Nakumbuka mara moja tu tuliwasiliana kwa Signal messenger…” Nikamtazama na kuushika mkono wake nikawa kama naupapasa hivi nikamwambia “ni kweli, umenipotezea sana unajua…” Nikamtupia jicho la kama namwambia “Nakuhitaji Paula”, sijui kama alisoma ujumbe huo ama laa atajua mwenyewe mi ndo nishatoa ishara sasa…

Itaendelea
 
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU 3

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Paula akashusha mkono wake mpaka kwenye shingo yangu kwa vidole vyake vyenye kucha nyembamba akawa anaviterezesha juu na chini huku ananiangalia, kisha akasema “nashukuru nimekuona, na hata sikujua kwa nini sikukutafuta rafiki yangu… nimekuwa na tabia mbaya sana. Ule mguso wa vidole nyuma ya shingo ulikuwa kama kunipigisha shoti ya umeme na vijidudu kunitambaa kwenye mtima. Nikaona huyu ananitafuta la rohoni si bure. Mi siyo mtoto wa kizungu, hapa kama nimefungwa busta yaani, jino moja tu gari inawaka. Hii dharau sasa aisee.

Nikazunguusha mkono wangu nyuma ya kiuno chake huku najiweka vizuri. Nikanyanyua sura yangu kumtazama maana alikuwa kwa juu kwenye kile kisehemu cha kuwekea vinywaji kwenye kochi. Nikamwambia hakufanya poa kuja na kuendelea na mishe zake bila kunitafuta. Nikambinya kidogo kati ya mwanzo wa hips na kiuno, mbinyo wa taratibu sana kama natafuta kijipu hivi ama nalikagua parachichi lililoiva sana nisije nikalipasua kabisa. Mkono wa kulia nimemshika mkono wake nikivibinya vidole na mkono wa kushoto kiunoni kwake nikifanya ukorofi usioudhi taratibu sana. Nadhani msg ilikuwa ‘delivered’ maana alijibetua kwa mbele kidogo na kiuno kama anakipeleka nyuma kwa mkao ule wa kimiss (kifua juu na makalio kuyabinua nyuma kidogo). Ishara zikanijia hapa nimetikisa ikulu kwa mbaaaaali.

Nikahisi mizuka ya Kizaramo ishanivaa na vinyamkera vyake. Hii sasa ishakuwa vita. Nikanyanyuka huku bado nimeushika mkono wake, nikasimama, nikamshika mabega, nikaweka mguu mmoja juu ya kochi nilipokuwa nimekaa huku namwambia… “Paula, hutakiwi kufanya hivi. Sikugombana na wewe sasa iweje uje na usinicheki mama?”. Namtazama machoni moja kwa moja bila kupepesa jicho maana Wazaramo walishaniambia kichwani kuwa kuna heshima lazima ilindwe. Nikapeleka mkono wa kushoto kwenye nywele zake na kuzisukuma kwa nyuma hivi ili zisifunike jicho lake na mkono wa kulia umeendelea kushikilia mkono wake wa kushoto. Nikazisukuma tena nywele kwa nyuma na mkono huo nikauteremsha mpaka kwenye shingo na kukishika kidevu chake. Nikahisi vinyweleo vya kifuani kwangu vimenisimama. Ghafla simu yangu ikaita mfuko wa kulia. Nikaingiza mkono kuitoa na huku mfuko wa kushoto umetuna ikitengeneza alama kama ya ndizi mshale hivi. Nilipoitoa simu nikakuta ni Advocate Baraka ananipigia. Akili zikanirudi kuwa nahitajika kazini haraka sana. Nikiwa nimesimama nikamwambia Paula, “…upo kwa siku ngapi hapa Tanzania?” Akanijibu bado ana mwezi na siku sita kuna kazi ya kampuni imemleta. Nikamwambia tukutane jioni baada ya mishe zake. Anitaarifu wakati akimaliza kazi zake ili tuongee Mawili matatu ya tangu wakati ule wa Dortmung Ujerumani mpaka sasa. Nikamuachia mkono Paula na kumuaga nikiharakisha kutoka chumbani kumuwahi Baraka na kwenda kazini.

Nikakutana na Baraka floor ya chini kabisa tukatoka mpaka parking yeye akichukua gari yake nami nikichukua yangu. Akaniuliza mbona nimekawia kidogo kwa mtoto wa kizungu nilikuwa nachombeza nini? Nikamjibu hapana ni rafiki yang utu kama nilivyokwambia jana, ila kuna changamoto kidogo. Baraka akacheka sana na kunigongesha kiganja maana tunajuaga stori zetu za kibabe. Tukaachana yeye akielekea mahakamani nami nikielekea kazini kwangu. Saa saba kamili mchana Rose akanicheki kwa ajili ya kujua kama nishapata msosi. Nilipomwambia bado akanifurusha kwa simu yake nikale haraka sana. Huyu binti bhana sijui ana nini? Nadhani hawezi kulai yeye bila mimi kula kwanza. Nikajizoa zoa mpaka mgahawani kupata wali samaki. Baada ya kuletea msosi nikaupiga picha na kumtumia Rose kwa whatsapp ili nimringishie. Akanijibu kwa viemoji vya matamanio na kufurahi kwa kwenda kula.

Wakati napiga msosi akaja binti anaitwa Rahma mtoto wa Mombasa Ukonga. Huyu binti Rahma tumezoea kumuita “Nino” naye analifurahia sana jina hilo la nino kuliko la Rahma. Tunafanya naye kazi yeye akiwa kitengo cha Biashara na Matangazo. Kuna wakati namuitaga “Nino wa Kimox” basi anafuraaaahi. Alikuja kwenye meza yangu akiwa ameongozana na Rajabu ambaye pia ni mfanyakazi mwenzetu.

Wakavuta viti wakajumuika nami kwenye msosi baada ya order zao nao kuletwa. Baada ya msosi tukanyanyuka na kuanza kurudi kazini mdogo mdogo maana si mbali. Stori za hapa na pale. Nikamwambia Rahma aka Nino kuwa jioni nitaelekea maeneo ya kwao il ani Gongo la Mboto mwisho kuna mchizi naenda kumuona kuna deal Fulani ya kupanga kwa hiyo nitapita maeneo ya kwao. Nino akanitazama kwa furaha na tabasamu limemjaa. Akaniambia “Basi nakuomba unipe lift uniache pale Mombasa maana mi nakaa maeneo ya Bombambili.” Nikamjibu kwa hilo tu wala asikonde. Nitamuacha Mombasa mi nikamuone mshkaji. Hapo mawazo yangu yapo kwa paula tu. Zile ‘touches’ za asubuhi kila mara naziwaza yaani. Nikawa najisemea hivi huyu mzungu atapona kweli safari hii? Ngoja tuone.

Kazi zilikuwa nyingi kiasimpaka kwenye saa 11:47 hv jioni ndo nikawa namalizia ili nichomoke zangu. Nino alikuwa ameshamaliza kazi kitambo yupo viti vya mapokezi ananisubiri mimi nimpe lift. Nikamaliza kazi na kushuka ngazi kwa mwendo wa kuruka ili nisiendelee kumuweka mtoto wa watu. Nikamkuta mapokezi nikamfuata na kumshika mkono kwa unyenyekevu sana nikimuomba samahani kwa kumchelewesha. Akatabasamu na kuniambia “Usijali Kimox, nakuelewa mbona”, katoto kana sauti tamu sana haka jamani… Kana sura ya upole kama hakajawahi kutenda dhambi kabisa. Tukaenda kwenye parking ya magari nikabofya kitufe cha kuondoa lock za milango. Nikaenda moja kwa moja mlango wa abiria na kumfungulia Nino mlango kisha nikampa ishara ya aingie akae kama malkia vile. Akatabasamu kama kawaida yake na macho yake meupeeee akiyarembua. Alipokaa tu sikumpa nafasi, nikamuinamia na kuuchukua mkanda nikamfunga halafu nikafunga mlango taratibu ubavuni kwake. Nikaenda upande wa dereva nikaingia nikatekenya switch ya kuwasha gari. Mazda RX-8 ikaitika kwa furaha. Huwa nausikilizia sana muungurumo wa Mazda kwa kweli. Naenjoy namna inavyonikubalia nikikandamiza pedeli ya mafuta na clutch kubadili gia. Gari hii ni Manual kwa maana napenda kuendesha gari Manual sana kuliko Automatic.

Nikaiingiza gari barabarani na safari ya Gongo la Mboto ikaanza kutokea Posta. Nikakamata barabara ya Samora mpaka mzunguuko wa pale Railway nikanyoosha na kutokea makutano ya taa za Mnazi Mmoja unapoanzia Mtaa wa Lumumba nikiikamata GoldStar. Pale tukakutana na kifoleni cha njiapanda ya gerezani. Nikaona humu kwenye gari tutakuwa bored tu maana Nino hakuwa na stori nyingi. Ni mkimya mpaka aongeleshwe yeye muda mwingi. Nikabofya kitufe TV na ikajifungua. Mazda hii n imeifunga mziki mmoja matata sana, umechujwa ukachujika hasaaaa. Sasa mziki pekee haukututosha kwa kuwa bado uchovu wa vijifoleni unazingua bora niweke movie kupunguza makali ya foleni za Dar.

Nikachomeka flash yangu ya 512GB na kuchagua movie moja inayoenda kwa jina la UNFAITHFUL ya mwaka 2002. Movie hii imechezwa na Richard Gere akiwa kama Edward, Diana Lane akivaa uhusika wa Connie na Adrian Lyne akiwa kama Paul. Ni movie tamu sanaaaaa katika movie zangu za muda wote. Kama hujawahi kuiona itafute ni bonge la movie. Basi Nino akawa interested sana na movie hii maana nit amu mwanzo mwisho. Kila hatua inakusisimua kuendelea kuitazama. Connie kutokana na ubize wa mumewe akajikuta anadondoka kimapenzi kwa kijana wa Maktaba Paul na kuchanganyikiwa na penzi la ajabu la kijana huyu. Ni hatari na nusu kwa kweli. Movie hii inatazamwa na watu wenye miaka 18 kwenda juu tuu. Mpaka tunakaribia Mombasa ilishafika saa mbili na robo usiku. Nikamwambia Nino ni bora twende wote kwa jamaa kisha wakati narudi nitamfikisha mpaka kwao Mbombambili maana Gongo la Mboto si mbali nami sitakaa sana huko. Nino kwa kunogewa na movie na usumbufu alioniambia wa kusubiria vihiace mpaka vijae akaona ni wazo zuri.

Muda wote wa safari nilipata wasaa wa kulitathmini toto hili la Kikwele kutoka Chalinze Pwani. Kwanza ameenda hewani kidogo, ana shebu matata ya kibantu ambayo ameisitiri kwa gauni refu kama baibui hivi. Niligundua shepu hii alipokuwa anaingia kwenye gari. Mashaallah Mungu kamjaalia. Ana jicho jeupeee lililolegea na pua ya kisomali. Meno yake madogo madogo yamejipangilia vizuri na meupe sana. Ana shingo ndefu ya upanga na mwendo wa twiga anapotembea. Weusi wake wa kawaida usio na makeups wala vikorokoro. Yaani kuku wa kienyeji hasa lakini mtamu hatari. Alipokaa kwenye gari gauni lilikuwa limepanda kwa juu hivi na nikamuona mara kadhaa akilishusha pale linapopanda wakati akijiweka vizuri kwa utamu wa movie hii. Kifua chake kimebeba maziwa makubwa yenye afya yanayomfanya abalance mwili na kuonekana kama mtoto wa Kinyarwanda kabisa. Nina macho ya wizi miye hatari sana.

Kutoka Ukonga hakukuwa na foleni sana hivyo Mazda nikaitemesha mwendo dakika sifuri niko Gongo la Mboto. Nikaongea na jamaa kwa kifupi nikimuacha Nino kwenye gari akicheki movie na kurudi fasta nimuwahishe kwao mtoto wa watu. Tukarudi mpaka Mombasa tukakunja kulia kushika njia ya Bombambili. Nino akawa na kazi ya kuniambia njia mpaka maeneo ya kwao. Kwao nyumba ziko mbalimbali na wengi wanaonekana watu wa kishua hivi. Kila nyumba geti na hakuna movements utadhani mtaa umehamwa. Tulipokaribia na kwao akaniambia nipaki gari sehemu atashukia hapo kwa maana si vyema kuonekana nimemshusha kabisa getini kwao. Kwake si picha nzuri kabisa. Nikapaki gari pembeni na kuzima taa za mbele. Movie ilikuwa kwenye sehemu tamu zaidi ya maloveee yaani ile ndindindi. Nikaona si vyema kumkatisha movie na hivi inaelekea mwishoni ni bora amalizie then nitaondoka.

Movie ikanoga sana, kuna sehemu yenye vitu na box nikamuona Nino akijinyonga nyonga na miguu kama anavaa ndala na kuvua. Mikao ikawa inabadilika badilika kwenye siti. Taa ya hadhari ikagonga kichwani mwangu kwamba hapa maji yashamzidi unga mtu. Nikalaza kiti change kidogo na kujifanya kama nakaa vizuri hivi na mkono nikautupa kwenye gear lever. Halafu kwa makusudi nikaudondoshea kwenye paja lake nikaugandisha hapo. Nino hakutikisika, nikaupandisha juu kidogo taratibu kama natafuta kitu kilichopotea mpaka kati ya tumbo na paja. Nikabinya hapo kwa uchokozi wa makusudi kabisa. Nino akaguna “mmmh”. Nikageuza shingo kumtazama, naye akanitazama kisha akaangalia chini kwa aibu za kike. Nikawa nabinya binya paja lake kama natomasa papai kupima ubora. Nikamsogelea na kumnong’oneza kwa kumuita jina lake kabisa “Rahma”, akaitika kwa sauti ya kike nyembamba sana “bee”. Nikamuangalia kwa matamanio makubwa huku nikiramba lips, nikamvuta na kumpa kiss la kwenye lips zake. Akaguna tu “mmh” wakati huo mkono wangu wa kulia unatambaa kwenye paja lake taratibu sana kana kwamba sitaki kumuumiza. Nikaendelea kumbusu busu huku yeye akiwa ameyafumba macho na nadhani hakujua kwamba mkono wangu wa kulia ulishalivuta gauni na nilikuwa sasa napapasa ndani ya paja na si juu ya gauni tena. Nikazinyonya lips zake za chini kama namung’unya pipi na wakati huo mkono wa kulia ushafika katikati ya pacha mbili ukipembua mchele bila kusababisha mikwaruzo ya kucha za kuku. Nikafyatua kitufe cha kulazia kiti na akajikuta kalalia kiti kama yuko kitandani. Mazda pale kati kuna kisehemu kimejengwa ukilaza siti za mbele kinakuwa kama kitanda hivi. Haraka sana niliiruka gear lever na kuwa upande wake mkono wa kulia sasa ukiwa kwenye embe bolibo, mkono wa kushoto nimeupitisha chini ya kiuno chake, midomo wangu na ulimi ukifanya kazi ya kusababisha mtibuko wa akili kwenye shingo wakati kichwa amekitupia kwa nyuma kwa haraka nikashusha mkono wa kulia kulegeza nati kisha nikapanda kwa juu kama nyoka.

Kitendo bila kuchelewa nikaunyanyua mguu wake wa kushoto na kuukunja kwenye siti wakati nikimsogeza nyuma kidogo. Nadhani fahamu zilishapotea kwake hakujua chochote kinachoendelea. Dunia nzima ilikuwa kama imehamishwa kwa muda. Mkono wa kulia uliivuta “washeli” kwa pembeni na nati haikuelekezwa njia wapi inatakiwa kufunga. Ulisikika mlio kama wa nati yenye kutu ikifungwa kutoka kinywani kwa Nino “aaaywhu”. Nati za tairi zilifungwa na kufunguliwa mara tatu mfululizo kutokana na mikao ya bodi wakati mwingine kuhitaji kuwekwa vizuri. Nilipofunga nati za tairi ya nne nikajiachia taratibu sana kama nafanya tahadhari ili wazungu wasikimbilie nje wakati wazungu wako zao kwenye ndege kama wote. Nino aliganda akiwa anatetemeka kama kashikwa na ugonjwa wa degedege. Mkono mmoja kaushika kifuani mwingine kakilazia kiti kama yupo kwenye mto anatetemeka mkapa nikasema leo kuna mtu ana maruhani hapa. Nikanyanyua kiti chake kidogo, nikamsogelea na kumbusu kwenye lips akiwa ananitazama tu kama nimekuwa mzimu hivi. Yaani yupo kimya ananitazama tu, sijui vitu gani muda ule anawaza. Nikarudisha movie nyuma kidogo ili kumalizia maana ilibaki kidogo na nimrudishe kwenye mood. Ilipoisha akaniangalia tena na kuniambia kwa sauti ya upole mno na yenye kubembeleza, “Kimox, asante!!!!”. Nikamtazama, nikamshika kidevu na kumpa kiss la kinywa nami nikamwambia, “Asante Rahma, asante Nino wa kimox!!!”. Akaniomba aende sasa nyumbani. Makubwa haya aisee, sasa hata kwenda nyumbani nafanya kuombwa dah!!! Nikafungua walletNi na kutoa fedha kiasi kama wekundu watatu na kumuelekezea kwake. Akanitazama na kuniambia. “Asante Kimox, ulichonipa leo ni bora zaidi kuliko hiki unachonipa sasa. Nashukuru ila sitakipokea kwa sababu wewe ni zaidi ya hiki unachonipa”. Nikabaki namtumbulia macho tu, akaniomba tena kwenda. Nikamwambia, “sawa Nino, unaweza kwenda huku bado namtumbulia macho na fedha zangu mkononi. Akasogea akanibusu kwenye paji la uso kisha akafungua mlango wa gari akashuka akielekea kwao.

Nikabaki namtazama Nino akiingia kwenye geti lao kisha akasimama kidogo kuniangalia kana kwamba anajua kuwa namtazama. Akanipungia mkono akaingia ndani. Nikawasha gari na kupiga uturn kuelekea Mombasa kisha nishike Uwanja wa Ndege nipitie njia ya Kipawa, Buza Uhasibu mpaka Kigamboni kwangu. Njia nzima nawaza mtifuano wa muda mfupi uliopita. Hatari na nusu….

Itaendelea
 
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU 4

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Nikafika mataa ya Kipawa pale Uwanja wa Ndege Terminal Three nikakunja kulia, nikakandamiza kidogo pedeli ya mafuta Mazda ikaitika na kukubali amri yangu. Nilipofika maeneo ya Buza kwa Abiola simu yangu ikaanza kuita. Simu ilikuwa kwenye handle ya kushikilia simu kwenye dashboard. Nikabofya kitufe cha kupokelea na mziki uliokuwa ukilia ukakoma na simu ikaunga na Bluetooth ya kwenye gari na sauti laini sana ikasikika, “uko wapi Kimox mpenzi wangu?” Alikuwa ni Rose akitaka kujua nilipo kwa wakati huo maana ni kitambo kidogo tangu mara ya mwisho aliponicheki naye akiwa kwenye foleni ya Lugalo kuelekea Mbezi Beach maeneo ya Jogoo.

Nikamjibu, “Niko poa utamu wangu, mi ndo narudi niko maeneo ya Buza huku naitafuta Tandika.” Akaniambia nimcheki mara tu nikifika home, tukaagana. Fikra zangu bado zina mvurugano wa jambo letu na Nino. Naanza kuvuta kumbukumbu namna nilivyoivuta ‘washel’ pembeni kutokana na mazingira ya ufinyu wa eneo na jinsi bonde la ufa lilivyokuwa na unyevu oevu ambao ulinipandisha midadi ya kulegeza nati ili niifunge vizuri kwenye bolt. Nikavuta picha namna nilivyokuwa nalengesha nati kwenye bolt na kupokewa na kilainishi cha uvuguvugu mfano wa grisi nyepesi. Ule moto wa engine wakati nafunga bolt ulikuwa si wa nchi hii ahahahaaaaa.

Nikawa naikumbuka minyumbuliko ya Nino taratibu sana kama Kambale aliye kwenye tope baada ya kina cha maji kupungua na akihangaika kutafuta ahueni. Navuta picha namna alivyokuwa anang’ata lips na jicho limepotelea juu. Hizi mambo si za kawaida kutokea hasa namna Nino alivyokuwa anafuatisha mikito ya Piston. Nikakanyaga breki kidogo baada ya mawazo yangu kutibuliwa na mbwa aliyekuwa anakatisha barabara. Nikakamata usukani vizuri kwa mkono wa kuliahuku mkono wa kushoto ukiwa kwenye kirungu cha gia, nikakanyaga clutch miguu ikipishana wa kushoto ukienda chini na wa kulia ukiachia padeli ya mafuta, nikatupia gia na Mazda ikaitika baada ya kukanyaga tena padeli ya mafuta mara mbili, mkanyago wa kwanza nikibonyeza nusu pedali na wa pili nikiikandamiza. Woyooooo, Mazda ikatetema na kupokea amri.

Nikaikamata Tandika Sokoni na kuserereka kuitafuta Uhasibu kupitia Kwa Aziz Ally. Mwendo kibati kama nimeibiwa lakini kwa umakini sana kwa maana njia ya darajani (Daraja la Nyerere) inaita hasa. Barabara pana na inayoruhusu kufunguka. Kufumba na kufumbua nikawa getini kwangu. Nikabofya remote na geti likawa linafunguka taratibu. Nikaiongoza Mazda mpaka parking. Nikaweka funguo kwenye kisanduku cha kuhifadhia nikiiacha Mazda ikiwa kwenye Auto Turnoff. Gari zangu nimezitega ukiizima kwa kuchomoa funguo basi itabaki ikiunguruma silence kwa dakika mbili kisha itajizima yenyewe. Nikaingia sebuleni na kujitupa kwenye kochi. Hapa kwangu naishi na mdogo wangu Japhet. Nikamkuta anatazama mpira wa ligi za Ulaya. Misiyo mpenzi wa mipira aisee kwa hiyo hapo huwa tunatofautiana sana.

Nikakuta kashaandaa msosi maana tunaishi kisela sana. Baada ya salamu na vistori vya hapa na pale akaingia jikoni na kuniletea msosi. Nikawa nakula huku namsindikiza kuangalia mpira hata kama siyo sehemu ya hobby yangu. Nikachomoa simu kutoka mfukoni, nikazitafuta namba za Nino na kumpigia. Simu ikawa inaita tu bila kupokelewa. Nikaipotezea na kuzitafuta namba za Rose, nikampigia na kuongea naye sana tu maana mtoto ana swags flan za stori zisizoisha na kudeka. Wakati naongea na Rose nikasikia mlio wa simu nyingine ikitafuta njia. Nikaichungulia na kukuta ni Paula anapiga. Nikiongea na Rose siwezi kukata simu mpaka nimalizane naye maana huwa sipendi kumkwaza mtoto wa Kikerewe huyu. Tuliongea kiasi cha dakika 23 hv kisha tukaagana kwa bashasha na huba. Nikasubiri yeye akate simu.

Nikafungua sehemu ya missed calls nikabofya kitufe cha kupiga na punde simu ikaanza kuita upande wa pili na kupokelewa haraka sana. Akaniambia, “nilikuwa nakupigia, leo nilitingwa sana Kimox sikupata muda wa kuwa nawe kwa chakula cha jioni na kuongea…” Nikamwambia, “Usijali, hata mimi nilikuwa busy leo.”

Tukaongea mambo mawili matatu kisha tukaagana tukiweka ahadi ya kukutana kesho yake maana ni weekend. Paula ana umri wa miaka 26 ama 27 hivi kama sikosei, hawezi kuwa amezidi miaka hiyo wala kupungua. Ni binti mwenye utulivu wa sura, matendo na akili. Mkiongea jambo unajua kabisa hapa naongea na mtu anayejielewa hasa. Hanywi pombe wala kuvuta sigara. Si binti mwenye kupenda makundi makundi na hili nililigundua tulipokuwa Ujerumani. Ni mpole kwa kumtazama sijajua hayo mengine. Mara zote tulipokuwa Ujerumani sikuwahi kumsikia akiongea na simu ya kimapenzi au kuongelea mambo ya mahusiano. Kuna wakati nilitaka kujua upande wake wa mahusiani lakini hakuwahi kunipa nafasi ya kuuliza jambo hilo. Kwa hiyo upande wake wa kimahusiano ya kimapenzi siujui kabisa.

Nikamaliza kula na kunyanyuka na sahani yangu mpaka jikoni. Nikaiosha kwenye sehemu ya kuoshea vyombo nikaiweka kwenye kijitray cha vyombo na kuelekea chumbani. Nikavua shati na suruali nikaingia bafuni. Nina kawaida ya kula kwanza na ninaoga nikiingia kulala. Nikajifuta maji na kujibwaga kwenye tanda la futi nane kwa sita. Nikaweka mto mweupe wa sufi vizuri kichwani mwangu kama egemeo nikiwa nimelala chali na kuanza kujiuliza maswali kadhaa wa kadhaa. Kwa nini Nino alikataa zile elfu thelathini zangu? Ameniona kama namnunua ama nini?

Halafu hakuwahi hata siku moja kuonesha kwangu dalili za kunipenda sasa kwa nini akatae hela? Lakini labda kwao mambo safi hivyo hana shida ndogondogo za vihela…Hapana, angekuwa na hela asingekuwa siku nyingine anakula mihogo ya kukaanga ofisini ama mpaka wakati mwingine namlazimisha twende tukale. Mara nyingi nikipita sehemu yao pale chini muda wa kula ninapokurupushwaga na Rose nitamuita, “Nino wa Kimox twende tukale…” Naweza kumtania kwa kumfuata na kusimama mbele yake kisha naweka mkono wa kushoto kifuani na mkono wa kulia namuelekezea huku nimeinama kidogo kama naomba kitu ili ashike mkono wangu tuelekee mgahawani kula. Nilikuwa naifanyaga hii kama sehemu ya ucheshi wangu na mahusiano mazuri kwa wafanyakazi wenzangu. Sikuwa na wazo ama hisia za kimapenzi zaidi ya ucheshi tu.

Nikaendelea kuwaza vitu vingi vya nino ofisini. Nikaanza kuhisi macho mazito na sikumbuki ni muda gani usingizi ulinibeba ila nilikurupushwa na mlio wa alarm ya saa ya mezani ya chumbani ikiwa ni saa 12:00 asubuhi. Nikajigeuza na kukuta shuka jeupe nimelifinyanga finyanga kana kwamba nilikuwa nagalagala kitandani peke yangu. Nikaamka kuingia bafuni kusafisha kinywa kisha nikaenda sebuleni na kukuta dogo Japhet wakati mwingine tumezoea kumuita Kalunga bado hajaamka chumbani kwake. Nikajitengenezea kifungua kinywa kama kawaida yangu nikakaa mbele ya TV kuangalia habari za asubuhi.

Kama kawaida Rose akawa hewani na bashasha zake za kike za asubuhi. Akaniambia naye ameshaamka na anafanya usafi wa nyumba. Kisha akasema leo atakuja kwangu akimaliza usafi hivyo chakula cha mchana ataandaa yeye. Nikasema leo nitakula mahanjumati ya mtoto wa Kikerewe. Japhet naye akaja kujiunga nami sebuleni kuangalia habari. Nikamwambia leo Rose atakuja kutuandalia msosi hivyo ni mwendo wa kurelax tu leo. Akatabasamu maana anamjua shimeji yake huyu akilikalia jiko basi sisi kazi yetu ni kujiandaa kusosomola.

Tukatoka nje na Japhet mpaka kwenye garden na kujipumzisha kwenye viti vya kunesa tukipiga stori mbili tatu na hii ni kutokana na kuchoshwa na kushindana kucheza game kwenye PS4 pale sebuleni. Tukaona tukajipumzishe nje kupata hewa ya Mungu kwa utukufu wake. Kidogo tukasikia kengele getini ikiunguruma. Japhet akasimama na kuelekea getini kutazama ni nani. Tayari mawazo yangu yalishajua ni Rose tu na si mwingine maana alipokuwa anatoka alishanitaarifu. Uzuri wa Rose ni mwanamke anayekupa taarifa ya kila anachofanya na ni kitu ambacho kinanifanya nimpende kwa kweli.

Japhet akafungua geti na nikaiona miondoko ya kunesa nesa ya Rose akiwa nyuma ya Japhet. Rose alitinga pama kubwa iliyofanya sura yake kukwepa mwanga wa jua. Alivaa blauzi nyeupe ya mikono mirefu na suruali ya khaki iliyobana na kuifanya miguu yake iwe ya kuvutia kwa namna anavyotembea, vifungo vya juu amevifungua na kufanya mstari wa maziwa kuonekana. Begani kaning’iniza mkoba mdogo mweusi wenye Kamba ndefu hivi. Akawa anatembea huku mkono mmoja ameshika kibegi na mkono mwingine akiweka kofia yap ama vizuri na mwendo wa kimiss wenyewe mnaita catwalks. Mashaallah huyu mtoto anajijua ni mzuri na anajua kunata na mwendo.

Nikabaki namtazama namna anavyonijongelea pale nilipo nikiwa nimekaa kwenye kiti kwa kujilaza kimwinyi, kiwiko cha mkono wangu kiko kwenye egemeo la kiti na vidole vyangu vinachezea ndevu zangu nilizonyoa muundo wa O. Sikutaka kunyanyuka ili niendelee kumfaidi kadri anavyonisogelea na kupata fahari ya macho. Viatu vyake vyenye visigino virefu viliongeza ulimbwende wake. Tabasamu limemjaa muda wote akanifikia na kuninyooshea mikono yake niinuke anipe kumbatio. Nikaipokea mikono yake na kunyanyuka kisha nikampa hug ya kufa mtu. Nikahisi chuchu zake zikinipa shida kwenye kifua changu kipana na vile amenikumbatia kwa nguvu basi amejaa kifuani kwangu. Akanipa mabusu kama mwehu kisha akatumbukiza ulimi wake mwembamba sana kinyani mwangu na kuuchomoa. Kwa kutumia kidole gumba chake akawa ananifuta lipshine kwenye midomo yangu huku akitabasamu.

Japhet aka Kalunga alikuwa amekaa kwenye kiti akinesa nesa huku anatabasamu tu akiyatazama mahaba ya kaka na shimeji yake wanavyopokeana kwa huba. Uturi aliopaka Rose ulihanikiza pua zangu na kutamani aendelee kuwepo pale, bila shaka hata Japhet pia alivutiwa na harufu nzuri ile ya uturi. Rose ni binti anayependa sana kazi za nyumbani. Hivyo akanipiga kibao cha mahaba kidogo sana shavuni kisha moja kwa moja akajiongoza ndani akaanze mishe zake mi nikiendelea kupiga stori na dogo pale garden.

Itaendelea
 
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU YA KWANZA

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Ni asubuhi njema sana yenye kajimvua ka kiaina kanakosababisha kuwepo na hali ya vuguvugu lenye kukera kiasi. Naamka kivivu kitandani kama nimelazimishwa. Nasikilizia viungo vya mwili vinavyokataa kunipa ushirikiano. Mwili kama nimepigwa na virungu usiku kucha.

Najivuta kukaa kitandani mikono nimeitambaliza kulia na kushoto kichwa nakitupa kifuani kuegemea na kidevu kukipa sapoti nikivuta kumbukumbu namna usiku wa jana tulivyoitumia na ‘mchizi’ wangu Baraka Lusewa pale SamakiSamaki Posta tukigonga vitu. Baraka akipiga KVANT kama kawaida yake na Sprite mimi nikisukuma vitu vya Whisky. Natokwa na tabasamu namna mara ya mwisho alivyokuwa anaamka huku miguu imepoteza uwezo wa kubeba mwili.

Nikamkamata mkono kumkalisha chini nikamwambia, “Kaka mambo si mambo, twende nikusindikize hapo hotelini ukapumzike maana kesho una issue zako mahakamani unakumbuka?” Hatunaga shida mimi na Baraka kwenye swala la maelewano. Akanyanyuka kachangamka sana. Tukaanza kukatoka huku tumeshikana mabega. Akakipoka kichupa cha KVant kilichobaki mezani kama mwivi vile. Tukatoka nje na kumuelekeza akae kiti cha abiria nimpeleke Kilimanjaro Hyatt alikofikia.

Fikra zangu zikatibuliwa na maumivu fulani ya kimsumali shingoni, nikajikata kofi la hasira Phaaa!! Mbu gani wa asubuhi hawa aagh!!! Naamka kinyonye kuingia bafuni kujiswafi kisha natengeneza kifungua kinywa. Mayai mawili, chai ya maziwa na soseji tatu. Kidogo najihisi nguvu za mwili zikitamalaki ninapoitupia chai kwenye koo langu. Hu undo uzuri wa whisky ninazokunywa, sinaga mning’inio asubuhi wa kukera.

Najikuta navutiwa na kaudadisi ka kutaka kujua rafiki niliyekutana naye jana usiku pale Kilimanjaro Hotel Hyatt usiku wakati nikimuacha Baraka. Ooooh Paula. Najiegemeza kwenye kochi taratibu na kikombe changu cha chai, nashusha pumzi nikivuta kumbukumbu za mara ya kwanza tulipokutana na Paula binti wa Kifaransa nilipozulu Dortmund Ujerumani kwenye mishe za maisha.

Mimi na Paula kwa mara ya kwanza tulipanda wote treni kutoka Bochum Nord kwenda Dortmund. Mimi nikifika pale Dorstfeld na yeye akiwa Westfalenhalle. Tulikutana kwenye mishe mishe za kusaka noti maisha yaende tukajikuta marafiki. Unajua hawa wenzetu wenye ngozi nyeupe urafiki kwao ni jambo jema. Kumbukumbu zinanijia namna ilivyokuwa rahisi kuwa na urafiki na Paula kutokana na ubaguzi mkubwa kutoka kwa Wajerumani. Ukienda hata dukani ukauliza kitu ili ununue kwa kiingereza muuzaji anakutumbulia macho tu mpaka utamke hiko unachokitaka kwa kijerumani ndo anakuuzia. Hali hii mara nyingi ilinikera. Lakini baada ya kuwa na kampani ya Paula angalau nikapata wa kuchonga chonga nae na kupiga hadithi mbili tatu.

Sasa hamadi!!! Jana usiku nagongana kibega na Paula Hyatt The Kilimanjaro Hotel baada ya kupita pale kwenye kipimo cha kukagua vitu vya chuma. Nilikuwa napaki vitu vyangu mfukoni huku nafunga mkanda wa kiuno vyema na wakati huo nimesogelea mlango wa kioo wa pili. Kama hujafika Hyatt baada ya checkup ya vitu vya chuma na kuji sanitizer kujiepusha na corona kuna milango ya vioo miwili inayofunguka yenyewe ukiikaribia. Sasa Baraka akiwa nyuma yangu mimi mbele nafunga mkanda mlango wa kioo ulipofunguka nikapigana kikumbo kiasi na mtoto wa kizungu. Nikanyanyua sura kumpa samahani, mara paaaap!!! Hamad ni Paula!!!!

Aliponyanyua sura naye akawa kama ameganda hivi ananifananisha. Neno likanitoka kibwege bwege hivi “...Paula?”. Naye akaendelea kunitazama na mara akasema “Kimox, is that you again?”. My gosh!!! Paula alikuwa ametupia vazi la kiafrika hasa utadhani mtoto wa Kitanga flani hivi. Ana dera kama la Kihindi na mtandio aliouzunguusha shingoni wa rangi ya hudhurungi, masikioni kaning’iniza hereni ndefu za duara zinazogusa mabegani zile kubwa. Nywele kazimwaga kwa nyuma. Chini ana viatu vya kimasai vilivyomkaa vizuri kama alitengenezewa maalumu kwa ajili yake. Na vile ana shepu ya kibantu, utadhani siyo Mzungu wa Ufaransa kama una macho juu juu waweza jikwaa akikupita na bahati mbaya ukageuka uone kama yaliyomo yamo.

Mkono wa kulia alishika simu kali Vivo X50 Pro na bega la kulia kaning’iniza kijimkoba kinachoendana na rangi ya dera na mtandio. Tukabaki tunatazamana kama majogoo yanayogombea mtetea. Akanisogelea nami nikamsogelea akanipa kumbatio mwanana sana. Rafiki yangu wa Dortmund Ujerumani leo nakumbana naye tena Tanzania....

Nikapiga tena funda la chai ya maziwa na kuisokomeza soseji yote iliyokuwa mkononi mwangu huku nikitabasamu. Nikamwemwesa midomo huku fikra zikipita kichwani mwangu, “...hivi huyu Paula, Bongo hii kafata nini?”. Nikajijibu mwenyewe tena macho nimeyakodoa kulitazama feni la pangaboi linalozunguuka kimya kimya kama vile ndiyo mara yangu ya kwanza kuliona “...ila haina mbaya, amenambia namba ya chumba alichopo na kesho atakuwa na mapumziko, basi nitakwenda kumuona Rafiki yangu huyu dah!!!”

Mara unaingia ujumbe kwenye simu yangu, namba ni ngeni ila ni ya tiGo 0679 547...., nakutana na ujumbe “Hello! Kimox!! Good morning. Its Paula...”. Nikakumbuka kumbe jana alichukua namba yangu. That’s great. Nikabofya kitufe cha reply nikamjibu...

Itaendelea
CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tate Mkuu Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie moneytalk Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple Litro Plan Master Xav Emmanuel Mr Devil TOHATO Bujibuji Kibunango
 
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU 5

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Kijua kikaanza kupanda na kuwa kero hapa kwenye garden. Tukaamua kuingia ndani kujumuika na Rose pia kuchemi movie. Kwenye upande wa movies mimi na Japhet tunaiva sana. Tukachagua movie moja kali inaitwa Undesputed kinara akiwa ni Scott Adkins aka Boyka kama anavyojulikana kwenye movie.

Wakati tunacheki movie pua zetu zikawa zinapata shida kutokana na harufu ya msosi unaoandaliwa na Rose jikoni. Baadae Rose akaja kujitupa kwenye kochi ubavuni kwangu kujumuika kuangalia movie. Nikipendacho mimi naye hukipenda, akaupitisha mkono wake nyuma ya kiuno change kwa chini na kujiegemesha kichwa chake begani kwangu kwa deko huku akicheki movie.nami nikapitisha mkono wangu shingoni kwake na kumvutia kifuani kwangu ili alale vyema.

Baada ya muda akanyanyuka kwenda jikoni kuangalia chakula na kutuandalia. Alipomaliza akaja kutukaribisha kwa mlo wa mchana. Mimi na Japhet tuakaelekea sehemu ya chakula tukavuta viti na kukaa. Rose akaja kutunawisha kisha akakaa kwenye kiti jirani yangu. Chakula kitamu sana kwa kweli, wali samaki wa kupaka, mboga za majani na maharage ya nazi. Aliweka viungo flan na kunogesha chakula hiki kwa kweli. Mwanamke anajua kupika haswaaa. Nilikuwa nakula huku wakati mwingine natikisa kichwa kwa utamu wa msosi. Baada ya kula tukamshukuru kwa chakula kitamu, tukarejea sebuleni kuendelea na movie.

Rose akaja na juice kwenye tray, akatupatia kila mmoja na yeye akachukua yake kisha akakaa pembeni yangu ila safari hii upande wangu wa kushoto. Akadeka kama kawaida yake. Baada ya muda Japhet akaniaga kuwa anaenda Tabata mara moja, nikajisemea kimoyo moyo huyu hana lolote ananipisha tu kijanja. Mimi na Rose tukaendelea kutazama movie. Wakati huu alikuwa amavaa khanga kajifunga kifuani na nyingine kiunoni. Alikaa kinyumbani hasa.

Japhet alipoondoka akajilaza zaidi kifuani kwangu akijua sasa ana uhuru zaidi. Akanyanyua mguu wa kushoto na kuuweka juu ya kijisturi cha meza na mkono wake wa kushoto akautupa kifuani kwangu na huku wa kulia ukiwa eneo la pajani kwangu. Nilipitisha mkono wangu wa kushoto upande wake wa pili na kuzichezea nywele zake nyeusi taratibu sana.

Akashusha mkono wake wa kushoto kutoka kifuani kwangu mpaka kwenye paja langu la mguu wa kulia huku akijilaza vizuri. Akawa kama ananichua hivi kwa kunipapasa kutoka usawa wa goti kuja juu ya mfuko wa suruali. Akainua kichwa chake na kunitazama kisha akaniambia, “Kimox, nakupendaaaa.” Sauti iliyotoka kama mtu anayeonewa ama kudhulumiwa. Ule mpapaso wake ukaanza kuniletea shida kwa kuvuruga ubongo wangu taratibu sana mpaka movie nikaanza kuona kama siielewi elewi hivi. Channel zikaanza kupotea potea kimtindo.

Nikasema kimoyo moyo huyu anataka dawa tu, na dawa yake ninayo. Akazidisha manjonjo kwa kuparaza juu ya dodoki lililovimba nyuma ya boksa kama kifutu. Nikaona kama macho yanapoteza nuru sasa. Nikachukua remote na kuzima TV kisha nikabofya kitufe cha music system. Mziki lainii ukawa unarindima kwenye speaker zilizojipanga zikapangilika sebuleni hapo.

Ule mguu aliouweka juu ya kisturi ulionesha paja lililonona baada ya khanda kujivuta kwa pembeni. Nikameza mate ya uchu, nikageuka kumtazama machoni naye akanitazama kisha akatabasamu. Nadhani alishajua nimemuelewa vizuri sana. Nikakishika kidevu chake na kumuinua kidogo kisha nikazibusu lipsi zake nene za chini. Akayafumba macho yake wakati nikitumbukiza ulimi wangu kinywani mwake na kufanya kama nautoa kwa kuchanganya ulimi wangu na lips yake ya juu kama vile nanyonya pipi kijiti. Yaani naingiza ulimi ndani ya kinywa chake kisha naubetua kwa juu na kuuvuta kwa nyuma kama nautoa huku nimezing’anga’ania lips zake za juu. Nilikuwa nafanya hivi kwa upole kabisa kama vile sitaki aumie.

Nikamlaza taratibu kwenye kochi wakati huo naye mwenyewe akinisaidia kujiweka vizuri. Macho anayafumba na kuyafumbua kidogo kila ninapofanya unyonyaji wa lips zake za juu na chini nikichanganya na ulimi wake mwembamba. Mkono wangu wa kulia ulishauburuta khanga ya kifuani na kiunoni mbali kabisa na sisi. Alibaki na kibrausi chepesi cha pink na nguo ya ndani yenye kufunga vimikanda kwa pembeni.

Nikaegemeza mkono wangu wa kushoto pembeni ya shingo yake kama nimemkumbatia hv na sapoti nisimlalie jumla, mkono wa kulia ukifanya kazi ya kutalii kutoka kwenye sehemu laini ya nyuma ya goti na kuupandisha juu usawa wa kiuno kupita kwenye paja. Midomo yangu ilikuwa shingoni nikifanya kama namng’ata na kufyonza asali. Nilihisi akianza kupandisha kifua na kukishusha kama pumzi zinaenda mbio. Badi sijafika nafasi ninayoitaka, lazima heshima ya Wazaramo iwepo. Nikisharukwa na akili nikiwa dakika kama hizi sitaki kuruhusu chochote kiharibu mood yangu.

Naye hakubaki nyuma, mkono wake wa kushoto ulikuwa chini ya tumbo langu ukiwa umelikamata tango na kufanya kama unalikagua kwa kutoka chini kwenda juu na kurudi chini huku mkono wake wa kulia ukichezea shingo yangu pana. Nikaachana na shingo nikashuka mpaka kwenye embe bolibo na kuanza kuzifyonza taratibu mno pasi kutumia meno. Wengi tunakosea hapa maana tunakuwa kama tunafyonya Ukwaju ya Azam na meno. Nilikuwa nazifyonza embe bolibo kwenye ncha kisha kama nataka kulizamisha embe kinywani ile sehemu nyeusi yote kisha nalitoa tena na kuzunguusha ulimi kwenye kile ki nipple na kufyonza tena. Wakati huu bolibo zikishughulikiwa mkono wa kulia ukazivuta zile Kamba za washeli nazo zikaitika.

Yeye alishalegeza mkanda wangu kitambo na akahangaika kuishusha kaptula yangu kisha boksa. Nikanyanyua mikono na kukichoropoa kile kiblausi na kila kitu kikawa kweupe sasa. Nikashuka katikati ya embe bolibo na wakati huu nikajiweka sawa kwa mashambulizi ya kijeshi. Nikaingia katikati mikono nikiikamata pembeni ya kifua chake nikiishusha midomo yangu nikitambaa na ulimi mpaka kwenye tumbo. Pale kuna kijishimo cha mdako nikatumbukiza ulimi hapo na kuuzunguusha kidogo wakati mikono yote miwili ikichezea embe bolibo kwa kuzibinya kutoka chini kifuani na kama nazichua kupanda juu kwenye ncha. Pumzi za Rose zikawa zinapaa huku kifua kikipanda na kushuka. Tumbo lake likabonyea kwa ndani na nikaziona mbavu zake zikipanda na kushuka.

Nikashuka chini ya kitovu na kukutana na vimiche vya nyasi vidogo sana nadhani shamba lilisafishwa siku kama mbili zilizopita. Nikatembeza ulimi hapo kwenye shamba kama nazunguusha alama ya kuchora namba nane mikono ikiendelea na kazi ya bolibo. Rose akapiga ukunga na kuanza kuweweseka, “baby co… com... comeon…. Don’t do this to me please….” Yakamtoka maneno bi dada. “gimme dat thing, I cant hold honey…” Nikawaza, hawa vinyamkera wasije wakaua maana kichwa change kikawa kinakandamizwa maeneo yale ya bonde la ufa kana kwamba kipotelee huko. Nikasema kimoyo moyo, “huyu bhana kidogo tu anaita ambulance wakati sijamaliza miye kuandaa mtu. Ila kwa namna hali ilivyo ngoja niweke heshima.

Nikaanza kurudi juu kwa namna nilivyokuwa nashuka nikipanda kwenye kile kijishimo cha mdako tumboni, kisha kwenye mfereji wa maembe bolibo nikaendelea taratibu sana kama sitaki mpaka shingoni. Yeye wakati huu napanda juu taratibu alishaizunguusha miguu yake nyuma yangu kama tunacheza mieleka. Mikono yake yote imenikamatia shingoni utadhani tuna ugomvi. Nikamtazama usoni niakuta michirizi ya machozi imeshuka kwenda masikioni mwake. Kope zake zimeloa kwa machozi. Nikawa nambusu shingoni na kupanda kwenye lips zake nikibusu taratibu sana. Ile kabali ya miguu yake nyuma ya kiuno change akawa anaikandamiza zaidi. Shaft ilikuwa imara na imenyooka hasa, nikafanya kama napinda mgongo kwa juu hivi ili nijinasue na kabali yake ya miguu huku napanda juu.

Shafti ni kama ilitengenezwa kuelekea sehemu husika bila macho. Inajua sehemu yake vizuri sana. Nikapanda kwa juu zaidi nikipita masikio yake na shafti ikakutana na joto pamoja na grisi tayari kwa kuzunguusha diff. Nikaisukuma shafti taratibu sana nikisaidiwa na kabali ya miguu yake. Ukunga ukamtoka Rose baata ya kuhisi tumeweka shafti vizuri na mzunguuko wa propela umekaa vyema sasa. Zikasikia ngonjera za namna mbalimbali nikiisogeza shafti kulia, kushoto, juu na chini. Kuna wakati shafti ilipokuwa kushoto mlio wa sauti ya ingini uliongezeka sana na gari ikawa inadai gia zaidi na kushusha pumzi nzito. Kisha napeleka shafti kulia, juu na chini kisha naipeleka tena kushoto halafu nayonga pedali hapo. Nikawa namuona Rose akijinyonga na kujiachia mara kadhaa.

Nikahisi Wazaramo wanataka kuja kwa speed nikaweka shafti katikati, nikapeleka tena kushoto Rose akaitikia na kuniambia anakaribia kushuka kutoka Mlima Kilimanjaro kwa mara kadhaa sasa. Nikaongeza speed na ukunga ukaendelea kumtoka kwa sauti kuu zaidi. Akaning’ang’ania kwa nguvu nami nikaisukuma shafti kushoto zaidi huku nikiongeza mikito. Tukajikuta tunashuka mlima Kilimanjaro pamoja. Wazaramo wote niliwamimina kule Mwanarumango ndani kabisa. Nikabaki na Wazaramo wangu ndani huku nimemlalia bila kumuumiza kwa kujizuia wakati huo nikizunguusha nyonga taratibu amalizie kuzishusha pumzi zake baada ya safari ya kushuka Kilimanjaro.

Baada ya dakika kama 5 hv nikajiondoa kifuani kwake na kukaa mwisho wa kochi nikimtazama namna machozi yanavyomtoka huku akiwa bado amefumba macho yake na hasemo chochote. Sijui huwa wakati kama huu anawaza nini. Natamani kumuuliza ni nini huwa anakiwaza kiasi hawezi kutamka chochote. Nikajiegemeza ubavuni mwa kochi hivyo hivyo kisha nikawasha TV na kuweka sauti ndogo sana. Yeye punde tu akapitiwa na usingizi mzito sana. Sikutaka kumsumbua, nikamuacha alale tu. Baada ya dakika 47 akazinduka na nikamsaidia kumnyanyua kumpeleka chumbani ili tukaoge. Akanikumbatia akitabasamu tukikokotana mpaka bafuni kuoga.

Tukiwa bafuni akaanza tena uchokozi kwa kuniogesha huku akiisafisha shaft. Nayo bila hiyana ikafura kwa hasira. Nikamuinamisha nikampelekea moto mwingine. Ukelele aliopiga ni kama mtu anayechinjwa. Kichapo juu ya kichapo. Nikamgeuza na kumsimamisha wima kisha nikanyanyua mguu wake mmoja usawa na kiuno changu nikapeleka moto tena. Akanikumbatia tena kwa nguvu wakati Wazungu wakishuka kwa kasi sana ndani ya kisima chenye chemchem ya maji ya uvuguvugu. Akajichomoa mikononi mwangu huku akitetemeka na kuniambia “utaniua wewe muone kwanza” na kukimbilia kitandani akajibwaga kama mzigo. Nikabaki namuangalia tu na kucheka. Hakunisemesha chochote tena. Nikaoga na kwenda kujilaza pembeni yake…

Itaendelea
 
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA

SEHEMU 6

Mtunzi:
Eng. Kimox Kimokole - 0786507507

Tukapitiwa na usingizi na Rose, mimi nikiwa nimelala chali naye amejilaza kifuani kwangu kwa muda mrefu kidogo. Tukaja kushtuka saa 1 jioni jua likiwa limetuama. Rose akarudi tena bafuni na kuoga kisha akaanza kujiandaa kwa safari ya kurudi Mbezi Beach maeneo ya Jogoo. Baada ya kujiandaa tukasogea sebuleni nikiwa nimemshikilia kiuno naye kazunguusha mkono wake begani mwangu. Tukasimama katikati ya sebule, akaweka mikono yake yote shingoni mwangu nami nimeshika kiuno chake kwa mikono miwili, akanitazama kisha akasema, “Kimox, nakupenda mpenzi, asante kwa dozi nzuri mpenzi wangu....wewe ni kiboko yangu unajua?” Aliyasema hayo macho kayaelekeza kwangu.

Nikambusu kwenye paji la uso kisha nikambusu mdomoni na kumwambia, “Najua mpenzi wangu, nakupenda pia baby” Tukakaa kwenye kochi la mtu mmoja nikiwa nimempakata mapajani mwangu. Rose akatoa simu na kubofya program ya UBER ili kuiita gari ije imchukue kumrudisha Mbezi Beach. Akabofya kuchagua gari kisha akasubiri. Simu ikaonesha gari iliyo jirani ikisogea maeneo tulipo.

Uber ikafika getini na mara simu yake ikaita, akanitazama na kunibusu kisha akaniambia, “Uber anapiga” Nikamuuliza bei akaniambia ni 23,000/- tu nikawa naelekea kwenye kochi kubwa kuchukua wallet, akanikamata mkono kama alijua nini nataka kufanya, akanambia, “acha bhanaaaa, sasa pesa gani hiyo mpenzi? Nitalipa we nisindikize nje my love...” alisema wakati anapokea simu na kumwambia dereva anatoka.

Tukatoka mpaka getini akaingia kwenye Uber siti ya mbele akafunga mkanda. Nikamsogelea dirishani nikamuinamia na kumpa kiss na kumwambia, “ufike salama mpenzi wangu, nakupenda.” Akatabasamu na kunirudishia kiss kisha akanijibu kimahaba, “nakupenda pia baby.” Uber ikageuza na kupotea machoni mwangu nikiwa bado nimesimama nje ya geti nikiitazama. Nikarudi sebuleni na kukaa kwenye kochi kuangalia TV.

Nikachukua simu na kuanza kupitia magroup mbalimbali ya whatsapp maana ni kitambo sikushika simu nikiwa na Rose. Nikakutana na ujumbe wa picha wa Paula. Nilipoifungua nikakuta picha ya paka mdogo na caption ikisema, “I gotta new friend...” Na ujumbe wake mwingine akiniambia tukutane Jumanne maana kuna vikao vimembana sana na shughuli nyingine za kiofisi. Aliniomba samahani kwa kutokaa pamoja kuzungumza na ana hamu kubwa ya kusikia stori kutoka kwangu. Nikamjibu msg zake kwamba asijali, kila kitu kitaenda sawa.

Kimoyo moyo nilishukuru ahadi kuwa Jumanne maana nilihitaji muda wa kupumzika na kufanya usafi Jumapili. Mara nyingi usafi huwa nafanya Jumapili kwa kuziweka nguo kwenye mashine ya kufulia na kuzipanga vyema na usafi mdogomdogo wa home nikisaidiana na Kalunga. Kwenye saa mbili hivi Kalunga akarudi akaandaa chakula kilichohifadhiwa na Rose tukala tukabaki sebuleni kucheki TV na stori za hapa na pale.

Kalunga ni kijana mkarimu, mpole na mwenye kuwiwa kujifunza vitu vingi sana. Mara zote amekuwa mdadisi wakutaka kufahamu baadhi ya ambavyo anadhani mimi nafahamu. Kwa hiyo muda mwingi ni kama tuko darasani kufundishana vitu mbalimbali. Nafurahia sana uwepo wake mdogo wangu huyu. Si mtu wa hasira hata kidogo. Kila mmoja aliondoka kwa wakati wake kwenda kulala kimya kimya.

Jumapili tuliamka yeye akiwa amenitangulia kwa mbali sana. Bila shaka nimelala sana kwa sababu ya mtanange na Rose. Tukaingia shughuli za usafi wa weekend na mishe nyingine. Baada ya mikiki mikiki ya usafi nakadhalika tukakaa kwenye bustani kama kawaida yetu tukipiga stori. Hatuishiwi stori sisi kwa kweli. Akanyanyuka kwenda kuleta juice, ghafla nikamkumbuka Nino. Nikawaza, “Hivi huyu mwanamke hata salamu kweli? Au kakereka kwa ile show ya kwenye Mazda?” Nikachukua simu ili nimpigie kumjulia hali lakini nikaghairi. Nikairudisha simu mfukoni nikapotezea. Kalunga akaja na jagi la juice tukaendelea kunywa na kupiga soga.

Asubuhi ya Jumatatu pilika za kuianza siku zinataradadi. Naingia kujiswafi bafuni kisha kupata kifungua kinywa na kurudi kujiandaa kwa kazi za kiofisi. Nachagua suti moja matata sana ya kijivu na shati nyeupe navaa, natupia na tai nyekundu. Najitazama kwenye kioo kikubwa na kuridhika na unadhifu wangu.

Naelekea parking na kuchukua funguo ya Subaru Legacy nyeusi yenye rim za kibabe sana. Kama kawaida naiwasha na kuiacha silence ili kukagua kama iko sawa kwa safari. Nikarudi ndani kuchukua wallet yangu niliyoisahau, nikakutana na Kalunga ndo anatoka kuamka. Tukasalimiana wakati akielekea jikoni, nikamuaga kuwa mi natoka sasa tutaonana baadae. Sikusubiri jawabu lake nikachomoka hadi kwenye gari nikaisogeza kulijongea geti nikapotelea barabarani.

Saa mbili kasoro dakika 12 nikawa naziruka ngazi za ofisi mpaka kwenye sehemu ya kujisajili mahudhurio ya siku kwa alama za vidole (Biometric attendance) nikaelekea kwenye meza yangu kuanza majukumu ya siku. Nilikuta wafanyakazi wachache kwa kuwa ni kawaida yangu kuwahi sana. Nikaanza kazi zangu nikipangua tray in kwenda tray out. Mida ya saa nne hivi nikashuka chini nitoke nje kwenda kununua karanga, huwa napenda kutafuna karanga mbichi mara nyingi nikiwa kazini. Nikazishuka ngazi taratibu kama sitaki kwa mapozi ya suti.

Nikapita ofisini kwa kina Nino nikamuona akiwa busy na kazi. Nikatoa salamu kwa wote, nikamuona kama mwenye mshtuko mkubwa sana pindi macho yetu yalipogongana. Alikuwa kama mtu mwenye hofu hivi, macho yake akiyakwepesha kugongana na yangu kabisa. Nikamuita kipekee, “Nino wa Kimox uko poaaa?” akajibu kwa tabasamu, “Niko poa sijui wewe?” Nikapitiliza zangu nje kununua karanga kisha nikarudi kuendelea na kazi.

Rose akanicheki kwa kunipigia na kuniambia maneno kadhaa ya mahaba kisha tukaagana. Nikachapa kazi mpaka kwenye saa saba hivi muda wa chakula cha mchana Paula akanipigia video call, tukaongea kama dakika 20 hivi akinionesha na rafiki yake mpya (Paka) na kuniambia atanipa stori maana sasa tumekuwa marafiki watatu ahahahaha. Muda wa chakula Nino alikuwa na wenzake wakila leo wakiwa wamewahi sana kuliko kawaida. Hakuwa na habari kabisa na mimi kana kwamba hakuna kitu kilichofanyika kati yetu. Kidogo nikaona kama kitu cha ajabu hivi. Nilitegemea labda sasa kazini ingekuwa balaa na mishe za kurandana kama kumbikumbi zingetaradadi lakini wapiiii, ni kama hakuna kilichofanyika. Nikasema, “this is very interesting kwa kweli.”

Nikiwa mgahawani akaja kukaa mezani kwangu dada mmoja matata sana. Wakati akija mwendo wake kama anaiogopa sakafu namna hii... Nadhani aliichagua meza yangu sababu nilikuwa pekee na niko nadhifu ndani ya suti matata sana. Harufu ya uturi ikahanikiza pua zangu wakati akiketi. Nikapata salamu nzuri kutoka kwa mlimbwende huyu. Nikaitikia na kuendelea na hamsini zangu kana kwamba bado niko peke yangu. Muda mwingi nilikuwa nachezea simu tu sina time. Chakula changu kikaja nikawa busy na msosi. Nikanyanyua macho kuitazama meza ya kina Nino na wenzake nikawaona kama wanazungumza jambo hivi kwa namna walivyokuwa wanaangalia meza yangu.

Nikageuza shingo kutoka kushoto na nikatupa macho kwa huyu binti mbele yangu, tukagongana macho, nikatabasamu kibabe kwa tabasamu la mdomo kwenda pembeni kidogo na jicho kulibinya kidogo sana upande ule nilikobetulia mdomo. Binti akatabasamu pia kisha akadondosha macho yake kwenye sahani akiendelea kula. Mtoto mashaallah kwa kweli, mzuri hasaaaa na anafaa kwa kazi maalumu ila nikajisemea kimoyomoyo, “Nguruwe pita leo sina mkuki...” Nikaendelea na hamsini zangu.

Nikamaliza kula na huyu binti pia akawa amemaliza kula. Niliponyanyuka naye pia akanyanyuka. Ni kama vile tuliambiana tufanye kwa pamoja. Tukajikuta tunatazamani kisha tukatabasamu. Nikaanza kuelekea sehemu ya kulipa na yeye akielekea hapo pia. Ni kama tunaongozana hivi na kwa namna tunavyoonekana ni kama labda tulikuwa wote na tulivyodamshi. Bila shaka macho ya watu mgahawani yalikuwa kwetu. Niliyawaza hayo wakati nimefika kulipia na binti analipia pia. Nikatoka mgahawani bado ni kama tumeongozana na binti yule, tukiwa nje yeye akaenda kulia nami kushoto kuelekea ofisini kwangu.

Nikaingia kazini na kuendelea na majukumu ya siku kama kawaida. Baadae akaja Habiba mezani kwangu na kusimama mbele yangu mikono ameiegemeza kwenye meza na kuniambia, “Kimox hongera bhana...” Nikamtazama nikiwa simuelewi, “hongera? Ya nini Habiba?” Hakunijibu akaondoka zake huyooo. Nikabaki namtazama tu...

itaendelea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom