Eng Kimox Kimokole
JF-Expert Member
- Jun 9, 2010
- 1,032
- 759
CHOMBEZO:
PAULA MFARANSA MWENYE VISA
SEHEMU YA KWANZA
Mtunzi: Eng. Kimox Kimokole - 0786507507
Ni asubuhi njema sana yenye kajimvua ka kiaina kanakosababisha kuwepo na hali ya vuguvugu lenye kukera kiasi. Naamka kivivu kitandani kama nimelazimishwa. Nasikilizia viungo vya mwili vinavyokataa kunipa ushirikiano. Mwili kama nimepigwa na virungu usiku kucha.
Najivuta kukaa kitandani mikono nimeitambaliza kulia na kushoto kichwa nakitupa kifuani kuegemea na kidevu kukipa sapoti nikivuta kumbukumbu namna usiku wa jana tulivyoitumia na ‘mchizi’ wangu Baraka Lusewa pale SamakiSamaki Posta tukigonga vitu. Baraka akipiga KVANT kama kawaida yake na Sprite mimi nikisukuma vitu vya Whisky. Natokwa na tabasamu namna mara ya mwisho alivyokuwa anaamka huku miguu imepoteza uwezo wa kubeba mwili.
Nikamkamata mkono kumkalisha chini nikamwambia, “Kaka mambo si mambo, twende nikusindikize hapo hotelini ukapumzike maana kesho una issue zako mahakamani unakumbuka?” Hatunaga shida mimi na Baraka kwenye swala la maelewano. Akanyanyuka kachangamka sana. Tukaanza kukatoka huku tumeshikana mabega.
Akakipoka kichupa cha KVant kilichobaki mezani kama mwivi vile. Tukatoka nje na kumuelekeza akae kiti cha abiria nimpeleke Kilimanjaro Hyatt alikofikia.
Fikra zangu zikatibuliwa na maumivu fulani ya kimsumali shingoni, nikajikata kofi la hasira Phaaa!! Mbu gani wa asubuhi hawa aagh!!! Naamka kinyonye kuingia bafuni kujiswafi kisha natengeneza kifungua kinywa. Mayai mawili, chai ya maziwa na soseji tatu. Kidogo najihisi nguvu za mwili zikitamalaki ninapoitupia chai kwenye koo langu. Hu undo uzuri wa whisky ninazokunywa, sinaga mning’inio asubuhi wa kukera.
Najikuta navutiwa na kaudadisi ka kutaka kujua rafiki niliyekutana naye jana usiku pale Kilimanjaro Hotel Hyatt usiku wakati nikimuacha Baraka. Ooooh Paula. Najiegemeza kwenye kochi taratibu na kikombe changu cha chai, nashusha pumzi nikivuta kumbukumbu za mara ya kwanza tulipokutana na Paula binti wa Kifaransa nilipozulu Dortmund Ujerumani kwenye mishe za maisha.
Mimi na Paula kwa mara ya kwanza tulipanda wote treni kutoka Bochum Nord kwenda Dortmund. Mimi nikifika pale Dorstfeld na yeye akiwa Westfalenhalle. Tulikutana kwenye mishe mishe za kusaka noti maisha yaende tukajikuta marafiki. Unajua hawa wenzetu wenye ngozi nyeupe urafiki kwao ni jambo jema.
Kumbukumbu zinanijia namna ilivyokuwa rahisi kuwa na urafiki na Paula kutokana na ubaguzi mkubwa kutoka kwa Wajerumani. Ukienda hata dukani ukauliza kitu ili ununue kwa kiingereza muuzaji anakutumbulia macho tu mpaka utamke hiko unachokitaka kwa kijerumani ndo anakuuzia. Hali hii mara nyingi ilinikera. Lakini baada ya kuwa na kampani ya Paula angalau nikapata wa kuchonga chonga nae na kupiga hadithi mbili tatu.
Sasa hamadi!!! Jana usiku nagongana kibega na Paula Hyatt The Kilimanjaro Hotel baada ya kupita pale kwenye kipimo cha kukagua vitu vya chuma. Nilikuwa napaki vitu vyangu mfukoni huku nafunga mkanda wa kiuno vyema na wakati huo nimesogelea mlango wa kioo wa pili. Kama hujafika Hyatt baada ya checkup ya vitu vya chuma na kuji sanitizer kujiepusha na corona kuna milango ya vioo miwili inayofunguka yenyewe ukiikaribia.
Sasa Baraka akiwa nyuma yangu mimi mbele nafunga mkanda mlango wa kioo ulipofunguka nikapigana kikumbo kiasi na mtoto wa kizungu. Nikanyanyua sura kumpa samahani, mara paaaap!!! Hamad ni Paula!!!!
Aliponyanyua sura naye akawa kama ameganda hivi ananifananisha. Neno likanitoka kibwege bwege hivi “...Paula?”. Naye akaendelea kunitazama na mara akasema “Kimox, is that you again?”. My gosh!!! Paula alikuwa ametupia vazi la kiafrika hasa utadhani mtoto wa Kitanga flani hivi.
Ana dera kama la Kihindi na mtandio aliouzunguusha shingoni wa rangi ya hudhurungi, masikioni kaning’iniza hereni ndefu za duara zinazogusa mabegani zile kubwa. Nywele kazimwaga kwa nyuma. Chini ana viatu vya kimasai vilivyomkaa vizuri kama alitengenezewa maalumu kwa ajili yake. Na vile ana shepu ya kibantu, utadhani siyo Mzungu wa Ufaransa kama una macho juu juu waweza jikwaa akikupita na bahati mbaya ukageuka uone kama yaliyomo yamo.
Mkono wa kulia alishika simu kali Vivo X50 Pro na bega la kulia kaning’iniza kijimkoba kinachoendana na rangi ya dera na mtandio. Tukabaki tunatazamana kama majogoo yanayogombea mtetea. Akanisogelea nami nikamsogelea akanipa kumbatio mwanana sana. Rafiki yangu wa Dortmund Ujerumani leo nakumbana naye tena Tanzania....
Nikapiga tena funda la chai ya maziwa na kuisokomeza soseji yote iliyokuwa mkononi mwangu huku nikitabasamu. Nikamwemwesa midomo huku fikra zikipita kichwani mwangu, “...hivi huyu Paula, Bongo hii kafata nini?”. Nikajijibu mwenyewe tena macho nimeyakodoa kulitazama feni la pangaboi linalozunguuka kimya kimya kama vile ndiyo mara yangu ya kwanza kuliona “...ila haina mbaya, amenambia namba ya chumba alichopo na kesho atakuwa na mapumziko, basi nitakwenda kumuona Rafiki yangu huyu dah!!!”
Mara unaingia ujumbe kwenye simu yangu, namba ni ngeni ila ni ya tiGo 0679 547...., nakutana na ujumbe “Hello! Kimox!! Good morning. Its Paula...”. Nikakumbuka kumbe jana alichukua namba yangu. That’s great. Nikabofya kitufe cha reply nikamjibu...
Itaendelea
PAULA MFARANSA MWENYE VISA
SEHEMU YA KWANZA
Mtunzi: Eng. Kimox Kimokole - 0786507507
Ni asubuhi njema sana yenye kajimvua ka kiaina kanakosababisha kuwepo na hali ya vuguvugu lenye kukera kiasi. Naamka kivivu kitandani kama nimelazimishwa. Nasikilizia viungo vya mwili vinavyokataa kunipa ushirikiano. Mwili kama nimepigwa na virungu usiku kucha.
Najivuta kukaa kitandani mikono nimeitambaliza kulia na kushoto kichwa nakitupa kifuani kuegemea na kidevu kukipa sapoti nikivuta kumbukumbu namna usiku wa jana tulivyoitumia na ‘mchizi’ wangu Baraka Lusewa pale SamakiSamaki Posta tukigonga vitu. Baraka akipiga KVANT kama kawaida yake na Sprite mimi nikisukuma vitu vya Whisky. Natokwa na tabasamu namna mara ya mwisho alivyokuwa anaamka huku miguu imepoteza uwezo wa kubeba mwili.
Nikamkamata mkono kumkalisha chini nikamwambia, “Kaka mambo si mambo, twende nikusindikize hapo hotelini ukapumzike maana kesho una issue zako mahakamani unakumbuka?” Hatunaga shida mimi na Baraka kwenye swala la maelewano. Akanyanyuka kachangamka sana. Tukaanza kukatoka huku tumeshikana mabega.
Akakipoka kichupa cha KVant kilichobaki mezani kama mwivi vile. Tukatoka nje na kumuelekeza akae kiti cha abiria nimpeleke Kilimanjaro Hyatt alikofikia.
Fikra zangu zikatibuliwa na maumivu fulani ya kimsumali shingoni, nikajikata kofi la hasira Phaaa!! Mbu gani wa asubuhi hawa aagh!!! Naamka kinyonye kuingia bafuni kujiswafi kisha natengeneza kifungua kinywa. Mayai mawili, chai ya maziwa na soseji tatu. Kidogo najihisi nguvu za mwili zikitamalaki ninapoitupia chai kwenye koo langu. Hu undo uzuri wa whisky ninazokunywa, sinaga mning’inio asubuhi wa kukera.
Najikuta navutiwa na kaudadisi ka kutaka kujua rafiki niliyekutana naye jana usiku pale Kilimanjaro Hotel Hyatt usiku wakati nikimuacha Baraka. Ooooh Paula. Najiegemeza kwenye kochi taratibu na kikombe changu cha chai, nashusha pumzi nikivuta kumbukumbu za mara ya kwanza tulipokutana na Paula binti wa Kifaransa nilipozulu Dortmund Ujerumani kwenye mishe za maisha.
Mimi na Paula kwa mara ya kwanza tulipanda wote treni kutoka Bochum Nord kwenda Dortmund. Mimi nikifika pale Dorstfeld na yeye akiwa Westfalenhalle. Tulikutana kwenye mishe mishe za kusaka noti maisha yaende tukajikuta marafiki. Unajua hawa wenzetu wenye ngozi nyeupe urafiki kwao ni jambo jema.
Kumbukumbu zinanijia namna ilivyokuwa rahisi kuwa na urafiki na Paula kutokana na ubaguzi mkubwa kutoka kwa Wajerumani. Ukienda hata dukani ukauliza kitu ili ununue kwa kiingereza muuzaji anakutumbulia macho tu mpaka utamke hiko unachokitaka kwa kijerumani ndo anakuuzia. Hali hii mara nyingi ilinikera. Lakini baada ya kuwa na kampani ya Paula angalau nikapata wa kuchonga chonga nae na kupiga hadithi mbili tatu.
Sasa hamadi!!! Jana usiku nagongana kibega na Paula Hyatt The Kilimanjaro Hotel baada ya kupita pale kwenye kipimo cha kukagua vitu vya chuma. Nilikuwa napaki vitu vyangu mfukoni huku nafunga mkanda wa kiuno vyema na wakati huo nimesogelea mlango wa kioo wa pili. Kama hujafika Hyatt baada ya checkup ya vitu vya chuma na kuji sanitizer kujiepusha na corona kuna milango ya vioo miwili inayofunguka yenyewe ukiikaribia.
Sasa Baraka akiwa nyuma yangu mimi mbele nafunga mkanda mlango wa kioo ulipofunguka nikapigana kikumbo kiasi na mtoto wa kizungu. Nikanyanyua sura kumpa samahani, mara paaaap!!! Hamad ni Paula!!!!
Aliponyanyua sura naye akawa kama ameganda hivi ananifananisha. Neno likanitoka kibwege bwege hivi “...Paula?”. Naye akaendelea kunitazama na mara akasema “Kimox, is that you again?”. My gosh!!! Paula alikuwa ametupia vazi la kiafrika hasa utadhani mtoto wa Kitanga flani hivi.
Ana dera kama la Kihindi na mtandio aliouzunguusha shingoni wa rangi ya hudhurungi, masikioni kaning’iniza hereni ndefu za duara zinazogusa mabegani zile kubwa. Nywele kazimwaga kwa nyuma. Chini ana viatu vya kimasai vilivyomkaa vizuri kama alitengenezewa maalumu kwa ajili yake. Na vile ana shepu ya kibantu, utadhani siyo Mzungu wa Ufaransa kama una macho juu juu waweza jikwaa akikupita na bahati mbaya ukageuka uone kama yaliyomo yamo.
Mkono wa kulia alishika simu kali Vivo X50 Pro na bega la kulia kaning’iniza kijimkoba kinachoendana na rangi ya dera na mtandio. Tukabaki tunatazamana kama majogoo yanayogombea mtetea. Akanisogelea nami nikamsogelea akanipa kumbatio mwanana sana. Rafiki yangu wa Dortmund Ujerumani leo nakumbana naye tena Tanzania....
Nikapiga tena funda la chai ya maziwa na kuisokomeza soseji yote iliyokuwa mkononi mwangu huku nikitabasamu. Nikamwemwesa midomo huku fikra zikipita kichwani mwangu, “...hivi huyu Paula, Bongo hii kafata nini?”. Nikajijibu mwenyewe tena macho nimeyakodoa kulitazama feni la pangaboi linalozunguuka kimya kimya kama vile ndiyo mara yangu ya kwanza kuliona “...ila haina mbaya, amenambia namba ya chumba alichopo na kesho atakuwa na mapumziko, basi nitakwenda kumuona Rafiki yangu huyu dah!!!”
Mara unaingia ujumbe kwenye simu yangu, namba ni ngeni ila ni ya tiGo 0679 547...., nakutana na ujumbe “Hello! Kimox!! Good morning. Its Paula...”. Nikakumbuka kumbe jana alichukua namba yangu. That’s great. Nikabofya kitufe cha reply nikamjibu...
Itaendelea