Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 18
ILIPOISHIA
“Ngoja nimtumie ujumbe halafu ajibu, ndiyo mtaamini,” alisema mama Anna huku akiandika ujumbe wa simu…
“Baby, nimefurahi sana kwa mechi ya leo. Halafu mechi ya kuichezea nyumbani kwako kama vile ni nzuri kuliko gesti au hotelini. Nimeipenda sana.”
SONGA NAYO MBELE…
Baada ya kuandika ujumbe huo, mama Anna aliwaonesha wenzake kisha akautuma kwenda kwenye namba ya Roi ambayo aliisevu kwenye simu yake kwa jina la ‘Wa Martha.’
Ni ndani ya dakika tatu tu, meseji ikajibiwa…
“Mimi pia nimeinjoi sana baby. Da! Yaani wewe ni kiboko, umeniteka kabisa Martha. Kesho twende tena nyumbani kwangu kama leo.”
Mama Anna alipoisoma meseji hiyo akawaonesha wenzake, wakacheka mpaka kupiga mikono ‘pa…pa’…
“Mimi nawaambieni, lazima wajina wangu aachike hivihivi anaona. Nimempa biti yule kaka ambazo mwenyewe hajawahi kupewa tangu azaliwe.”
Baada ya mazungumzo yao, Martha aliingia ndani kwake na kuwaacha wenzake wakiendelea na mazungumzo.
***
Roi alikaribishwa chumbani kwa Martha kwa mabusu mfululizo huku akipewa pole kwa kazi za mchana kutwa halafu akaambiwa…
“Baby, nilikumbuka kwamba kule nyumbani kwako baada ya kufunga, funguo uliiweka kulekule au ulikuja nayo?” aliuliza Martha…
“Iko kwenye gari.”
“Nilipenda kwenda kufanya usafi baby, labda kesho sasa.”
“Kesho sawa, utakwenda. Saa ngapi?”
“Jioni, kwenye saa kumi hivi.”
***
Usiku wa siku hiyo, Martha alihisi kitu tofauti kwa Roi. Licha ya kumshikashika ili achaji lakini alionekana hana habari na kwanza alikuwa mbali…
“Sweet, mbona kama upo mbali kimawazo?” aliuliza Martha…
“Hapana, kuchoka tu na shughuli.”
“Mmh! Baby jamani! Sasa ukichoka hivyo mimi nitapataje haki yangu?”
“Kesho bwana,” alisema Roi akilala baada ya kutoka kuoga.
***
Saa kumi na mbili, Martha alimka na kuamza kumshikashika Roi sehemu mbalimbali za mwili, hasa zile zenye kuamsha joto la mahaba. Roi alimgeukia, wakapashana joto zaidi na kuingia uwanjani kusakata mechi.
Kulikucha kabisa, Martha alitoka kwa lengo la kumtengea maji ya kuoga jamaa yake ambapo alikutana na mama Anna…
“Mambo mama Anna?” alisalimia Martha…
“Poa, umeamkaje?”
“Ah! Mi mzima bwana. vipi shemeji yangu?”
“Ameamka salama, anataka kuondoka kwenda kazini kwake muda si mrefu, namwekea maji ya kuoga.”
“Sawasawa, lazima upalilie bwana. Waoaji siku hizi hakuna,” alisema mama Anna akiingia ndani kwake. Lengo lake lilikuwa ni kumtumia meseji Roi kwani alijua Martha hatarudi muda ule chumbani…
“Baby umeamkaje?” alituma meseji Mama Anna.
“Poa, vipi wewe sweet, umeamkaje?”
“Mimi mzima tu. Ni kukumisi tu.”
“Mh! Je, mimi? Yaani natamani tungelala wote.”
“Usijali baby, kuna siku. Unakwenda kazini?”
“Yeah! Ndiyo nataka kujiandaa.”
“Leo vipi, tutaonana baby wangu?”
“Muhimu, si nilikwambia muda ule mpenzi wangu!”
“Saa ngapi na wapi?”
“Nitakujibu maana…” Roi aliikata meseji hiyo na kumpa wakati mgumu mama Anna kutafuta kwa nini meseji iliishia kwenye maana…
“Maana nini tena baby?”
“Nitakwambia Martha.”
Roi alisema maana kwa sababu, jana yake, Martha wake alitaka funguo ili akafanye usafi nyumbani kwake siku hiyo jioni.
***
Roi alitoka kitandani kwenda kuoga ambapo uani alikutana na wale wapangaji wenzake na Martha akiwemo mama Anna…
“Jamani mmeamkaje?” alisalimia Roi akiwa ndani ya taulo tu, kifua wazi. Alishangaa kuwaona wanawake wote wakimtumbulia macho yeye tena waziwazi na si kwa kuibia…
“Tumeamka salama, sijui wewe?” walimjibu, lakini mama Anna akaenda mbele zaidi kwa kusema…
“Sijui wewe baby wangu.”
Wakati anamalizia kusema baby wangu, Martha alitokea, akasikia.
Ili kuonesha kwamba alisikia kitu kisicho cha kawaida, Martha alimtumbulia macho mama Anna kama anayemuuliza unasemaje wewe?
“Vipi wajina?” mama Anna alijibalaguza kiaina kwani hata yeye alihisi maneno yake yalisikika na Martha…
“Poa tu,” Martha alijibu kwa mkato sana tena akiwa ameuelekeza uso wake chini.
Wakati huo, Roi alishazama bafuni kuoga lakini naye akijua maneno ya mwanamke huyo yamesikika na Martha…
“Hawa wanawake wa uswahilini hawa. Yaani kuvumilia hawawezi kabisa,” alisema moyoni Roi akiwa ameshaanza kuoga.
***
“Baby,” Martha alimwita Roi chumbani akiwa amekaa kwenye kitanda…
“Yes baby…”
“Yule mwanamke pale uani alikuitaje?”
“Yupi?”
“Yule mama Anna.”
“Mama ni yupi kati ya wale?” Roi alijizungusha huku akijua anazungumziwa nani.
ILIPOISHIA
“Ngoja nimtumie ujumbe halafu ajibu, ndiyo mtaamini,” alisema mama Anna huku akiandika ujumbe wa simu…
“Baby, nimefurahi sana kwa mechi ya leo. Halafu mechi ya kuichezea nyumbani kwako kama vile ni nzuri kuliko gesti au hotelini. Nimeipenda sana.”
SONGA NAYO MBELE…
Baada ya kuandika ujumbe huo, mama Anna aliwaonesha wenzake kisha akautuma kwenda kwenye namba ya Roi ambayo aliisevu kwenye simu yake kwa jina la ‘Wa Martha.’
Ni ndani ya dakika tatu tu, meseji ikajibiwa…
“Mimi pia nimeinjoi sana baby. Da! Yaani wewe ni kiboko, umeniteka kabisa Martha. Kesho twende tena nyumbani kwangu kama leo.”
Mama Anna alipoisoma meseji hiyo akawaonesha wenzake, wakacheka mpaka kupiga mikono ‘pa…pa’…
“Mimi nawaambieni, lazima wajina wangu aachike hivihivi anaona. Nimempa biti yule kaka ambazo mwenyewe hajawahi kupewa tangu azaliwe.”
Baada ya mazungumzo yao, Martha aliingia ndani kwake na kuwaacha wenzake wakiendelea na mazungumzo.
***
Roi alikaribishwa chumbani kwa Martha kwa mabusu mfululizo huku akipewa pole kwa kazi za mchana kutwa halafu akaambiwa…
“Baby, nilikumbuka kwamba kule nyumbani kwako baada ya kufunga, funguo uliiweka kulekule au ulikuja nayo?” aliuliza Martha…
“Iko kwenye gari.”
“Nilipenda kwenda kufanya usafi baby, labda kesho sasa.”
“Kesho sawa, utakwenda. Saa ngapi?”
“Jioni, kwenye saa kumi hivi.”
***
Usiku wa siku hiyo, Martha alihisi kitu tofauti kwa Roi. Licha ya kumshikashika ili achaji lakini alionekana hana habari na kwanza alikuwa mbali…
“Sweet, mbona kama upo mbali kimawazo?” aliuliza Martha…
“Hapana, kuchoka tu na shughuli.”
“Mmh! Baby jamani! Sasa ukichoka hivyo mimi nitapataje haki yangu?”
“Kesho bwana,” alisema Roi akilala baada ya kutoka kuoga.
***
Saa kumi na mbili, Martha alimka na kuamza kumshikashika Roi sehemu mbalimbali za mwili, hasa zile zenye kuamsha joto la mahaba. Roi alimgeukia, wakapashana joto zaidi na kuingia uwanjani kusakata mechi.
Kulikucha kabisa, Martha alitoka kwa lengo la kumtengea maji ya kuoga jamaa yake ambapo alikutana na mama Anna…
“Mambo mama Anna?” alisalimia Martha…
“Poa, umeamkaje?”
“Ah! Mi mzima bwana. vipi shemeji yangu?”
“Ameamka salama, anataka kuondoka kwenda kazini kwake muda si mrefu, namwekea maji ya kuoga.”
“Sawasawa, lazima upalilie bwana. Waoaji siku hizi hakuna,” alisema mama Anna akiingia ndani kwake. Lengo lake lilikuwa ni kumtumia meseji Roi kwani alijua Martha hatarudi muda ule chumbani…
“Baby umeamkaje?” alituma meseji Mama Anna.
“Poa, vipi wewe sweet, umeamkaje?”
“Mimi mzima tu. Ni kukumisi tu.”
“Mh! Je, mimi? Yaani natamani tungelala wote.”
“Usijali baby, kuna siku. Unakwenda kazini?”
“Yeah! Ndiyo nataka kujiandaa.”
“Leo vipi, tutaonana baby wangu?”
“Muhimu, si nilikwambia muda ule mpenzi wangu!”
“Saa ngapi na wapi?”
“Nitakujibu maana…” Roi aliikata meseji hiyo na kumpa wakati mgumu mama Anna kutafuta kwa nini meseji iliishia kwenye maana…
“Maana nini tena baby?”
“Nitakwambia Martha.”
Roi alisema maana kwa sababu, jana yake, Martha wake alitaka funguo ili akafanye usafi nyumbani kwake siku hiyo jioni.
***
Roi alitoka kitandani kwenda kuoga ambapo uani alikutana na wale wapangaji wenzake na Martha akiwemo mama Anna…
“Jamani mmeamkaje?” alisalimia Roi akiwa ndani ya taulo tu, kifua wazi. Alishangaa kuwaona wanawake wote wakimtumbulia macho yeye tena waziwazi na si kwa kuibia…
“Tumeamka salama, sijui wewe?” walimjibu, lakini mama Anna akaenda mbele zaidi kwa kusema…
“Sijui wewe baby wangu.”
Wakati anamalizia kusema baby wangu, Martha alitokea, akasikia.
Ili kuonesha kwamba alisikia kitu kisicho cha kawaida, Martha alimtumbulia macho mama Anna kama anayemuuliza unasemaje wewe?
“Vipi wajina?” mama Anna alijibalaguza kiaina kwani hata yeye alihisi maneno yake yalisikika na Martha…
“Poa tu,” Martha alijibu kwa mkato sana tena akiwa ameuelekeza uso wake chini.
Wakati huo, Roi alishazama bafuni kuoga lakini naye akijua maneno ya mwanamke huyo yamesikika na Martha…
“Hawa wanawake wa uswahilini hawa. Yaani kuvumilia hawawezi kabisa,” alisema moyoni Roi akiwa ameshaanza kuoga.
***
“Baby,” Martha alimwita Roi chumbani akiwa amekaa kwenye kitanda…
“Yes baby…”
“Yule mwanamke pale uani alikuitaje?”
“Yupi?”
“Yule mama Anna.”
“Mama ni yupi kati ya wale?” Roi alijizungusha huku akijua anazungumziwa nani.