China kujenga standard gauge reli ya TAZARA

China kujenga standard gauge reli ya TAZARA

satcom

Member
Joined
May 1, 2011
Posts
6
Reaction score
15
Alhuda 619, 16/05/2018- Ramadhan.

CHINA KUJENGA STANDARD GAUGE RELI YA TAZARA

Na Mwandishi Wetu

China inajiandaa kwa uwekezaji mkubwa nchini Tanzania.

Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao ametoa ahadi hiyo kwa Dkt. Salim Ahmed Salim Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania uliokuwa nchini China wiki moja iliyopita, huku akimuomba mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya CCM amfikishie Salamu maalum kwa rais wa Tanzania Dkt John Magufuli.

Katika mazungumzo hayo, yaliyohafanyika katika Hoteli ya Regent mjini Beijing nchini humo jumatatu iliyopita, Bwana Li Yuanchao aliyemuwakilisha Rais wa nchi hiyo Xi Jinping, amesema China ina nia kubwa ya kuiinua Tanzania kiuchumi ikikumbuka uhusiano wa kihistoria wa nchi hizi mbili na jitihada kubwa iliyofanywa na Tanzania kuirejesha China katika kiti chake umoja wa Mataifa.

Makamu wa Rais wa China alimwambia Dkt Salim na ujumbe wake kuwa nchi hiyo inaikumbuka na kuithamini zaidi Tanzania katika mataifa ya kiafrika.

“Makamu wa Rais wa China alieleza anavyokumbuka jinsi Dkt Salim wakati huo akiwa Umoja wa Mataifa alivyofurahi China kurejesha kiti chake”, mmoja wa wajumbe wa ujumbe huyo alimueleza Mwandishi nje ya mkutano huo wa faragha.

Amesema katika kuonesha China inavyothamini Tanzania, ujumbe wa Dkt Salim ulipewa mapokezi maalum katika Hoteli Homg Qiao State Guest ambayo ni maalum yenye ulinzi na utulivu mkubwa mjini Shanghai.

Akiwasilisha salamu za Mwenyekiti wa chama cha Kikomunisti cha China, rais Ximping kwa Comrade Salim, makamu huyo wa rais wa China aliuambia ujumbe wa Tanzania kuwa watu wa China wanaipenda Tanzania na kwamba serikali ya watu wa China ingependa kuwekeza kwenye miundombinu na kuonesha haja ya kuichukua tena reli ya TAZARA ili kuiboresha na kuiendesha kibiashara.

“Wanasema wakikubaliwa watang’oa reli iliyopo na watajenga reli mpya ya Standard Gauge kwa ajili hiyo walimuomba Dkt Salim wafikishie salamu hizo kwa Rais wa Tanzania Dkt Johm Magufuli ambaye walitoa mwaliko maalum kwake ahudhurie mkutano wa China na Afrika utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu”, ameeleza mjumbe mwingine.

Aidha amesema katika mazungumzo ya faragha kati ya Makamu wa Rais wa China na Dkt Salim, China imemuomba Rais Magufuli awape fursa maalum katika uwekezaji Tanzania ili China yenye uchumi mkubwa na nguvu duniani ioneshe jinsi inavyothamini udugu na urafiki baina ya mataifa haya mawili.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Dkt Salim uliondoka nchini kuelekea China jumamosi iliyopita na kuwasili siku ya pili kuitikia mwaliko wa chama cha urafiki katika ya Tanzania na China(Tanzania China Frirendship Promotion Association) ambacho Mwenyekiti wake ni Dkt Salim Ahmed Sali.

Jummane iliyopita ujumbe huyo ulihudhuria Kongamano la Serikali za mitaa ambalo pia lililohudhuriwa pia na Waziri Mkuu wa nchi ya Niger.

Katika Hotuba yake kwenye Kongamano hilo, Dkt Salim alielezea uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na China na uzoefu katika siasa za kimataifa ambapo alisifu msingi imara wa Tanzania ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere katika kupigania haki na usawa duniani ambao uliikutanisha Tanzania na mataifa kama China na mengine ya mfano wake.

Kabla ya hapo Dkt Salim alihojiwa na China Global Television Network ambapo siku ya jumanne mchana alitembelea Chuo Kikuu kikongwe cha Peking na kuzungumza na wanafunzi wa nchi za kiafrika wanaosoma Chuoni hapo kisha kukutana na Profesa Liu ambaye ni Mkongwe katika Chuo hicho.

Ukiwa mjini Shanghai ujumbe huo ambao pia ulimjumuisha Balozi wa Tanzania nchini humo Bwana Kairuki, ulitembelea mahali kilipoasisiwa Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China mwaka 1921 na kushuhudia picha za waasisi wake 12 wakiwa kwenye kikao wakiongozwa na Mao Ze Dong.
 
Wapewe kipaumbele katika uwekezaji ili waoneshe upendo wao, Hiiiiiiiiiiiiii bhagosha
 
Wachukue wachina wao wenye viduka vya ndala Kariakoo na wanaogonga panel beating wakawape ajira kwao kwanza.
 
Wao ndio wamemaliza Tembo na Faru wetu hivyo watulipe tu.
 
Aende china kwenye mkutano? Sidhani kama itawezekana
 
wasije wakachukua bandari zetu kama walivyofanya Sri Lanka oohooo
 
Siukubali mpango huo wa China... No way no way .!!
 
Alhuda 619, 16/05/2018- Ramadhan.

CHINA KUJENGA STANDARD GAUGE RELI YA TAZARA

Na Mwandishi Wetu

China inajiandaa kwa uwekezaji mkubwa nchini Tanzania.

Makamu wa Rais wa China Li Yuanchao ametoa ahadi hiyo kwa Dkt. Salim Ahmed Salim Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania uliokuwa nchini China wiki moja iliyopita, huku akimuomba mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya CCM amfikishie Salamu maalum kwa rais wa Tanzania Dkt John Magufuli.

Katika mazungumzo hayo, yaliyohafanyika katika Hoteli ya Regent mjini Beijing nchini humo jumatatu iliyopita, Bwana Li Yuanchao aliyemuwakilisha Rais wa nchi hiyo Xi Jinping, amesema China ina nia kubwa ya kuiinua Tanzania kiuchumi ikikumbuka uhusiano wa kihistoria wa nchi hizi mbili na jitihada kubwa iliyofanywa na Tanzania kuirejesha China katika kiti chake umoja wa Mataifa.

Makamu wa Rais wa China alimwambia Dkt Salim na ujumbe wake kuwa nchi hiyo inaikumbuka na kuithamini zaidi Tanzania katika mataifa ya kiafrika.

“Makamu wa Rais wa China alieleza anavyokumbuka jinsi Dkt Salim wakati huo akiwa Umoja wa Mataifa alivyofurahi China kurejesha kiti chake”, mmoja wa wajumbe wa ujumbe huyo alimueleza Mwandishi nje ya mkutano huo wa faragha.

Amesema katika kuonesha China inavyothamini Tanzania, ujumbe wa Dkt Salim ulipewa mapokezi maalum katika Hoteli Homg Qiao State Guest ambayo ni maalum yenye ulinzi na utulivu mkubwa mjini Shanghai.

Akiwasilisha salamu za Mwenyekiti wa chama cha Kikomunisti cha China, rais Ximping kwa Comrade Salim, makamu huyo wa rais wa China aliuambia ujumbe wa Tanzania kuwa watu wa China wanaipenda Tanzania na kwamba serikali ya watu wa China ingependa kuwekeza kwenye miundombinu na kuonesha haja ya kuichukua tena reli ya TAZARA ili kuiboresha na kuiendesha kibiashara.

“Wanasema wakikubaliwa watang’oa reli iliyopo na watajenga reli mpya ya Standard Gauge kwa ajili hiyo walimuomba Dkt Salim wafikishie salamu hizo kwa Rais wa Tanzania Dkt Johm Magufuli ambaye walitoa mwaliko maalum kwake ahudhurie mkutano wa China na Afrika utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu”, ameeleza mjumbe mwingine.

Aidha amesema katika mazungumzo ya faragha kati ya Makamu wa Rais wa China na Dkt Salim, China imemuomba Rais Magufuli awape fursa maalum katika uwekezaji Tanzania ili China yenye uchumi mkubwa na nguvu duniani ioneshe jinsi inavyothamini udugu na urafiki baina ya mataifa haya mawili.

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Dkt Salim uliondoka nchini kuelekea China jumamosi iliyopita na kuwasili siku ya pili kuitikia mwaliko wa chama cha urafiki katika ya Tanzania na China(Tanzania China Frirendship Promotion Association) ambacho Mwenyekiti wake ni Dkt Salim Ahmed Sali.

Jummane iliyopita ujumbe huyo ulihudhuria Kongamano la Serikali za mitaa ambalo pia lililohudhuriwa pia na Waziri Mkuu wa nchi ya Niger.

Katika Hotuba yake kwenye Kongamano hilo, Dkt Salim alielezea uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na China na uzoefu katika siasa za kimataifa ambapo alisifu msingi imara wa Tanzania ulioasisiwa na Mwalimu Nyerere katika kupigania haki na usawa duniani ambao uliikutanisha Tanzania na mataifa kama China na mengine ya mfano wake.

Kabla ya hapo Dkt Salim alihojiwa na China Global Television Network ambapo siku ya jumanne mchana alitembelea Chuo Kikuu kikongwe cha Peking na kuzungumza na wanafunzi wa nchi za kiafrika wanaosoma Chuoni hapo kisha kukutana na Profesa Liu ambaye ni Mkongwe katika Chuo hicho.

Ukiwa mjini Shanghai ujumbe huo ambao pia ulimjumuisha Balozi wa Tanzania nchini humo Bwana Kairuki, ulitembelea mahali kilipoasisiwa Chama cha Kikomunisti cha Watu wa China mwaka 1921 na kushuhudia picha za waasisi wake 12 wakiwa kwenye kikao wakiongozwa na Mao Ze Dong.
Tazara tangu mwanzo ni SGR, labda useme kinachohitajika ni kuweka miundo mbinu ya umeme ili kuwa na treni zinazotumia umeme na kwa hiyo kuwa na mwendo kasi.
 
Reli ya Tazara ilijengwa kwa kipimo cha standard gauge,au wanataka watuwekee umeme ili kuiboresha?
 
Tazara tangu mwanzo ni SGR, labda useme kinachohitajika ni kuweka miundo mbinu ya umeme ili kuwa na treni zinazotumia umeme na kwa hiyo kuwa na mwendo kasi.


Tazara siyo Standard gauge. Ina upana wa 1.067mm.

Standard gauge ina upana wa 1.435mm.

Kitu ambacho hakieleweki hapa ni kama watajenga reli mpya au wataongeza upana wa hii ya sasa.
 
Back
Top Bottom