Chimbuko la Uislam na Karen Armstrong

Mwanzoni zilikuwa mbili. Baadae katika kuwaridhisha/kuwashawishi/kutafuta kukubalika kwa wayahudi waliompokea Madina, Muhamad aliamrisha ziwe tatu kuendana nao. Sasa zilifikaje tano. Tuendelee na usomaji hapa.
Kwa ufaham wangu hiki kipart kinashida kidogo au upotoshaji kwa kuwa kweli waislamu mwanzo walisali Mara mbili kwa siku ila mwaka wa kumi na mbili tangu mission ya Muhammad(Pbuh) iliamriwa kusaliwa Mara tano hapo kabla hawajaamia yathrib (medina) ambapo waliishi karibu na wayahudi hivyo sio sahihi kuwa waliiga kusali Mara tatu kama Armstrong alivyoeleza kutoka kwa wayahudi kwani waislamu walihamia Medina mwaka wa 13 tangu mission ya Muhammad (pbuh) kuanza
 
Unasoma story za Wikipedia unatuleta hapa
 
Kiarabu kinaweza kuwa ngumu kwako kueleweka, labda nikueleweshe kupitia kifaransa, neno "Vous" linapotumika huwa na maana ya wewe (umoja) au ninyi, lkn kwenye umoja si kwamba linatumika kwa kila mtu, la hasha. Ikiwa mtu unamheshimu, utatumia " Vous " yaani wewe ninayekuheshimu yaani mtu mwenye cheo, lkn akiwa mtu wa kawaida unasema 'tu '

Kwenye English language, "You " pia humaanisha wewe au nyinyi, je ni wakati gani na mazingira wasomi wa English wapo wengi wataeleza.



Kwa hiyo kwenye kiarabu litumikapo neno نحن "sisi " kwenye nafsi ya umoja humaanisha utukufu au cheo,

Wasio jua huwa wanaingia mzima mzima eti wakiona ni hoja yenye kusupport imani ya Mungu zaid ya mmoja.La hasha sivyo.

Magwiji huwa wanawacheka wakiwaona kama ni wenye upungufu wa elimu.
Sasa mkuu kutaka kujua tu hivyo paka nikajifunze hiko kiarabu tena,duh
 
Mission ya Muhamad ilianza lini?
 
Unasoma story za Wikipedia unatuleta hapa
Onyesha kipi nimekitoa "Wikipedia". Ukiweza naacha kujadiliana katika hii mada.

Bado nakudai juu ya suala la imani. Usitake kuvaa viatu navyo vaa mimi,ona sasa vinavyo kupwaya.

Nipo ...
 
Hii ni Quran imesema tukampa injili ila haijaiita injili ya Issa.

je, na mimi nitakuwa sahihi kuiita Quran 'Quran ya mtume' na sio 'Quran takatifu'?
Unapo ambiwa Injili ya Issa si kwa maana yake bali alipewa na Mola wake kama muongozo,na ukisema Qur'aan ya Muhammad kwa maana ya kupewa kitabu haina shida.
 
Wew na mwamedi wezi tu!credible source ni Bible pekeyake nimeisoma yote mara 7
 
Uandishi wa namna hii,kama uko hivi katika hicho kitabu una makosq mengi sana. Kuna mengi ya kuzua.

Yaani huyu mama alitakiwa arejee vitabu vya asili vilivyo elezea habari ya Mtume,sababu kila kitu kipo wazi.
kutoka kabila la Kureshi alikuwa akiipeleka familia yake kwenye milima ya Hijra iliyopo nje ya mji wa Maka kwa ajili ya kufanya maombi kipindi cha mwezi wa Ramadhani.
Mfano hiki kipande,muandishi alitakiwa aweke ushahidi,sababu kina ukakasi. Maana familia ya Mtume ipi ? Na hayo maombi walikuwa wanayaelekezea wapi na kwa nani ?

Milima ya Hijra ndiyo milima gani ?
 
Nikijua kwamba square root ya mbili ni kazima iwe ndogo kuliko 2, halafu mtu akaniambia square root ya 2 ni 10, na mimi najua 10 ni kubwa kuliko 2, nikasema 10 haiwezi kuwa square root ya 2, kwa sababu square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2, hapo sijawemeza kujua kwamba 10 si square root ya 2, bila hata kujua squar3 root ya 2 ni nini?

Unabishia hesabu?

Unasema square root ya 2 ni 10?
 
Hivi huwa unaelewa ninacho kiandika ?

Ungekuwa umeelewa usingerudia huu utoto.
 
Ni typo, Mount Hira and not Hijra.
 
Hivi huwa unaelewa ninacho kiandika ?

Ungekuwa umeelewa usingerudia huu utoto.
Nitaelewaje mtu unabishia hesabu?

Nimeona njia rahisi kabisa ya kuelezea mantiki ni hesabu, hesabu simple haina ubishi.

10 haiwezi kuwa square root ya 2.

Kwa sababu square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 10.

Hivyo naweza kujua 10 si square root ya 2, bila hata kujua square root ya 2 ni ipi.

Jibu la 10 kuwa square root ya 2 lina contradict basic principle ya kwamba square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2, na hivyo jibu hili si sahihi, naweza kujua jibu hili si sahihi hata kabla ya kujua jibu sahihi ni lipi. Naliondoa jibu hili kwa "elimination method".

Hapo tumeona mtu anaweza kujua jibu fulani si sahihi, bila hata kujua jibu sahihi. Sihitaji kujua mji mkuu wa Tanzania ni mji gani ili kujua kwamba Washington DC, mji ulio Marekani, hauwezi kuwa mji mkuu wa Tanzania, ikiwa najua mji mkuu wa Tanzania ni lazima uwe Tanzania.

Unabisha nini sasa hapo?
 
Soma nilicho kiandika,nimeeleza kwa Kiswahili chepesi sana.

Nashangaa unapo hamisha hoja kwa kusema nabshia hesabu wakati jambo hilo hulikuti katika nilicho kiandika,na nimeweka wazi msingi wa hoja yako na yangu ni katika dhana yako juu ya aisyejua na ukadhania kwa kukata kabisa atasema ya kuwa square root ya 2 ni 10, na hoja yako nyingine ni kujaalia "contradiction" sehemu ambayo hakuna "contradiction", lakini kwa kutokuwa makini unaleta hoja mpya ya kusema nabishia hesabu ?

Nani amekwambia kwamba 10 inaweza kuwa square root ya 2 ? Kuwa makini mzee.

Huwezi kujua square root ya 2 kuwa ni ndogo kuliko 2 kama hujui nini maana ya Square root,hili weka akilini.

Kaka unasinzia nini ? Au kama umeshughulishwa tulia kwanza ndiyo ujenge hoja. Usipoteze muda kwa jambo ambalo sijaliandika.
 
Tuanze polepole.

Hoja yangu ya msingi ni kwamba, mtu anaweza kujua jibu fulani si sahihi, kwa sababu lina contradict basic principle, bila hata ya kujua jibu sahihi ni lipi.

Unakubaliana na hoja hii au unaipinga?
 
Kunyenyekea kwake na kutii.
Ni vipi kwenye kunyenyekea na kutii pekee kumfanye mtu aitwe muislam? Ni wazi lazima kuwe na utofauti wa kimatendo ambayo itamtanabaisha mtu kuwa muislam. Wapo waliotii na kunyenyekea kwa Mungu wao tofauti na anayetambulika kwa jina la Allah je yafaa kuitwa waislam?

Uislam una misingi (nguzo) je unao ushahidi wa kimatendo aliyoyafanya Adam kutimiza nguzo zote tano za uislam?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…