Chimbuko la matatizo yote haya ni Freeman Mbowe

Chimbuko la matatizo yote haya ni Freeman Mbowe

Kweli kabisa, Mbowe ndio alisababisha hata Daudi AlberBashire (mungu wa DSM) akapata masomo yote saba F na kutumia cheti cha mtu mwingine.

Mbowe mbaya sana kwa kweli, amemsababishia hata mtakatifu Yohane kuwaita wahudumu wa ndege "air hostage" badala ya "air hostess"
Baba hii hii ya kuitana hostage ilinipitaje ..ckuipata kabisaa
 
Tumechoka na haya manung'uniko dhidi ya Mbowe. Hamna hoja nyingine ya kuleta humu? Watu wangapi wameandika kuhusu Mbowe? Sasa leteni mada zingine. Kama huna kaa kimya waache Chadema na chama chao.
hadi atoke
 
Acha kumvunjia heshma Freeman Aikael Mbowe
Kabla ya kumlaumu Mbowe Jiulize aliposhika Madaraka ya Uenyekiti Chadema ilikuaje?

Mie huwa Kama simkubali Mtu haimaanishi sikubali mazuri yake

Freeman Mbowe Ni Moja ya Wanasiasa wa Upinzani wenye mikakati Sana Tena Sana Tatizo Ni Moja tu 'kazungukwa Na Akina Yericko'

Alimkaribisha Lowassa Kwa Kuwa aliamini Lowassa anaweza akapasua CCM Na wengi wa Nje ya CCM waliamini hivyo

Ntakupa mfano mmoja?

Unajua Kwanini Dr Slaa alichelewa kujitokeza hadharan kupinga ujio wa Lowassa?

Aliskilizia kwanza Kama Kweli CCM ingepasuka Na Wabunge 50 Na Wenyeviti wa Mikoa 30 wangehamia Chadema Na Kama ingetokea hivyo asingepinga ujio wa Lowassa huko, ila alipoona Hakuna Mafuriko ndio akajitokeza kupinga wakati huo tayari Hata dirisha la Tume kuchukua form lilishafungwa

Freeman Ni political strategists japo anakosa kitu kimoja tu 'Wanachama watiifu ' Na laiti angekuwa Na Wanachama watiifu wa Muda wote Kama Seif Sharif Hamad Basi mambo yangekuwa tofauti Sana
Imagine unakaa vikao vizito vya Siri Na wenzio kupanga Mikakati ya Kisiasa Halafu kesho unawaona wako upande wa pili Hii inakutia wasiwasi wa kuwaamini Hata uliobaki nao kwa Kuwa hujui yupi Nyoka yupi sio Matokeo yake unapunguza kasi
Watanzania wanapenda kuona sura mpya zinazokuja na mwamko Mpya.

Sio kwa sababu ya Mbowe.
Mbowe angemaliza tu muda wake akapumzika zake na ubunge wake.
Pia angepunguza maadui ambao sasa hawajulikani kuwa ni ndani ya Chama au nje.

Matokeo ya kung'ang'ania madaraka ni kuwa na maadui kila upande wengine wa kutengeneza tu. Ndio maana mpaka ndani ya Chama haamini MTU. Nje ya Chama haamini vyama vingine vya upinzani, kule CCM pia haamini mtu. Serikalini haamini mtu, kwenye vyombo vya dola haamini mtu. Angejua kuwa hakuna mtanzania anayemuunga mkono kwa kuhodhi Chama kama mali yake bali ni watu wenyewe wanaotafuta mabadiliko.

Nitakupa mfano.
Mrema alipofukuzwa Uwaziri na Mzee Ruksa alipotoka alipojiunga na NCCR mageuzi ,jina lake lilivuma sana na kupokelewa na mafuriko ya watu.
NCCR ikapanda Chati kwa kasi ya ajabu. Hapakua na mkakati wowote alioufanya nchi nzima ilivuma kwa kishindo cha mrema kujiunga na NCCR Mageuzi.

Wangetokea mashabiki maandazi kama wa Mbowe wangemsifu na kusema kuwa Mrema ni Mpambanaji mwenye mikakati ya kujenga Chama na blah blah nyingi wakati hakuna mkakati wowote zaidi ya watu kusaka mabadiliko popote wanapoona kuna mtu mpya.

2004 Bob Makani akamwachia Kijana Mdogo Freeman Aikael Mbowe aongoze Chadema kwa nafasi ya Uenyekiti.
Watanzania hasa vijana ambao walikua wamechoka na CCM na wengine hawakua na vyama wakakimbilia Chadema kwa sababu ya kuona ni Chama Pekee Chenye Mwenyekiti Kijana mdogo . Chama kukakimbiliwa na Vijana wengi wasaka mabadiliko ndani na nje ya Tanzania .

Mbowe akaendelea kuimarisha Chama Kwa wakati wake wa miaka Kumi kama walivyofanya waasisi wa Chama Bob Makani na Edwin Mtei ambao waliongoza kabla ya Mbowe.
Chadema kikafanikiwa kuungwa mkono na vijana na wasomi wengi.
Kijana msomi Zito Zuberi Kabwe naye kama Mbowe alikua na ndoto za kupokea Kijiti cha kuongoza Chama na kukipeleka Mbele zaidi.

Kama ilivyo kawaida muda wa Uenyekiti wa Mbowe ulipokaribia kuisha Zito alianza kujipanga kimkakati kutafuta uungwaji mkono.

Mbowe alijua wazi kabisa kuwa Zito alikua na uungwaji mkono mkubwa sana ndani na nje ya Chama kutokana na uwezo wake mkubwa katika kujenga hoja na kuungwa mkono na vijana wengi na wasomi.
Mbowe aliingiwa na hofu kubwa ya kuachia Uenyekiti kwenda kwa mtu mwingine. Kundi lake pia likawa na hofu ya kupoteza nafasi zao ndani ya Chama. Wakati huo pia Chama kilikua kimerudisha Ladha ya Ukabila na kaudini kwa mbali.
Zito akafuatiliwa kila anapokwenda kwa lengo la kumtafutia kisa cha kumwita msaliti ili aondolewe . Na kama sio uimara wa Zito kiroho na kimila nadhani wangekua wamemfanya kitu kibaya kabisa kama Chacha.

Mwaka 2015 Mbowe alicheza na akili za Zito na Lowasa na Kundi la ulipo tupo .
Watu wengi hawalielewi hili wanabaki tu kusema Mbowe amejenga Chama bila kujua kuwa Mbowe ndiye amevuruga Chama kwa kuua Demokrasia ya ndani na kujenga mfumo wa kibabe,kiburu ,matusi,kutishana ,dharau kwa wengine n.k.
Ndio maana vijana wengi wa Chadema ni viburi sana na kuhisi kila mtu ni mjinga hajui chochote isipokuwa wao tu.

Mbowe alipoona Lowasa amekatwa alianza kuingiwa na hofu kubwa juu ya Lowasa kwenda ACT kwa Zito Kabwe.Aligundua wazi kuwa Lowassa angeenda kwa Zito ungekua ndio mwisho wa Chadema kuwa na Mbunge Tanzania.
Mbowe alifanya juu chini kumtafuta Lowasa ajiunge Chadema.
Kwa hiyo 2015 mafriko yale yaliendelea kuwa ni ya Watanzania wenyewe kusaka Mabadiliko.

Namkumbusha Mbowe :-
.....Kila tunapokaribia uchaguzi kunatokea jambo Moja kubwa la kuwavuta watanzania wapenda mabadiliko kumfuata mtu maarufu. ACT wamelamba Dume . Kwa sasa ACT ndiyo habari ya mjini. Tujiulize ni kwa nini Maalim Seif pamoja na kuwa alikua ndani ya ukawa lakini hakujiunga na Chadema?! Bila shaka kila mtu atajua kuwa Uongozi wa Chadema haukubaliki na wapenda Mabadiliko.

Hata 2020 wengi watatoka CCM na CUF lakini hawatajiunga na Chadema chini ya Mbowe.
Labda akubali kuwapa watanzania kile wanachokitaka kwa muda mrefu yaani Sura mpya itakayowavuta wasaka Mabadiliko.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mtazamo wako , ila ungesema mtu flani hivyo nadhani saa hii tungekuletea ugali sehemu, maneno yako yote niyaki nafiki tupu
 
Watanzania wanapenda kuona sura mpya zinazokuja na mwamko Mpya.

Sio kwa sababu ya Mbowe.
Mbowe angemaliza tu muda wake akapumzika zake na ubunge wake.
Pia angepunguza maadui ambao sasa hawajulikani kuwa ni ndani ya Chama au nje.

Matokeo ya kung'ang'ania madaraka ni kuwa na maadui kila upande wengine wa kutengeneza tu. Ndio maana mpaka ndani ya Chama haamini MTU. Nje ya Chama haamini vyama vingine vya upinzani, kule CCM pia haamini mtu. Serikalini haamini mtu, kwenye vyombo vya dola haamini mtu. Angejua kuwa hakuna mtanzania anayemuunga mkono kwa kuhodhi Chama kama mali yake bali ni watu wenyewe wanaotafuta mabadiliko.

Nitakupa mfano.
Mrema alipofukuzwa Uwaziri na Mzee Ruksa alipotoka alipojiunga na NCCR mageuzi ,jina lake lilivuma sana na kupokelewa na mafuriko ya watu.
NCCR ikapanda Chati kwa kasi ya ajabu. Hapakua na mkakati wowote alioufanya nchi nzima ilivuma kwa kishindo cha mrema kujiunga na NCCR Mageuzi.

Wangetokea mashabiki maandazi kama wa Mbowe wangemsifu na kusema kuwa Mrema ni Mpambanaji mwenye mikakati ya kujenga Chama na blah blah nyingi wakati hakuna mkakati wowote zaidi ya watu kusaka mabadiliko popote wanapoona kuna mtu mpya.

2004 Bob Makani akamwachia Kijana Mdogo Freeman Aikael Mbowe aongoze Chadema kwa nafasi ya Uenyekiti.
Watanzania hasa vijana ambao walikua wamechoka na CCM na wengine hawakua na vyama wakakimbilia Chadema kwa sababu ya kuona ni Chama Pekee Chenye Mwenyekiti Kijana mdogo . Chama kukakimbiliwa na Vijana wengi wasaka mabadiliko ndani na nje ya Tanzania .

Mbowe akaendelea kuimarisha Chama Kwa wakati wake wa miaka Kumi kama walivyofanya waasisi wa Chama Bob Makani na Edwin Mtei ambao waliongoza kabla ya Mbowe.
Chadema kikafanikiwa kuungwa mkono na vijana na wasomi wengi.
Kijana msomi Zito Zuberi Kabwe naye kama Mbowe alikua na ndoto za kupokea Kijiti cha kuongoza Chama na kukipeleka Mbele zaidi.

Kama ilivyo kawaida muda wa Uenyekiti wa Mbowe ulipokaribia kuisha Zito alianza kujipanga kimkakati kutafuta uungwaji mkono.

Mbowe alijua wazi kabisa kuwa Zito alikua na uungwaji mkono mkubwa sana ndani na nje ya Chama kutokana na uwezo wake mkubwa katika kujenga hoja na kuungwa mkono na vijana wengi na wasomi.
Mbowe aliingiwa na hofu kubwa ya kuachia Uenyekiti kwenda kwa mtu mwingine. Kundi lake pia likawa na hofu ya kupoteza nafasi zao ndani ya Chama. Wakati huo pia Chama kilikua kimerudisha Ladha ya Ukabila na kaudini kwa mbali.
Zito akafuatiliwa kila anapokwenda kwa lengo la kumtafutia kisa cha kumwita msaliti ili aondolewe . Na kama sio uimara wa Zito kiroho na kimila nadhani wangekua wamemfanya kitu kibaya kabisa kama Chacha.

Mwaka 2015 Mbowe alicheza na akili za Zito na Lowasa na Kundi la ulipo tupo .
Watu wengi hawalielewi hili wanabaki tu kusema Mbowe amejenga Chama bila kujua kuwa Mbowe ndiye amevuruga Chama kwa kuua Demokrasia ya ndani na kujenga mfumo wa kibabe,kiburu ,matusi,kutishana ,dharau kwa wengine n.k.
Ndio maana vijana wengi wa Chadema ni viburi sana na kuhisi kila mtu ni mjinga hajui chochote isipokuwa wao tu.

Mbowe alipoona Lowasa amekatwa alianza kuingiwa na hofu kubwa juu ya Lowasa kwenda ACT kwa Zito Kabwe.Aligundua wazi kuwa Lowassa angeenda kwa Zito ungekua ndio mwisho wa Chadema kuwa na Mbunge Tanzania.
Mbowe alifanya juu chini kumtafuta Lowasa ajiunge Chadema.
Kwa hiyo 2015 mafriko yale yaliendelea kuwa ni ya Watanzania wenyewe kusaka Mabadiliko.

Namkumbusha Mbowe :-
.....Kila tunapokaribia uchaguzi kunatokea jambo Moja kubwa la kuwavuta watanzania wapenda mabadiliko kumfuata mtu maarufu. ACT wamelamba Dume . Kwa sasa ACT ndiyo habari ya mjini. Tujiulize ni kwa nini Maalim Seif pamoja na kuwa alikua ndani ya ukawa lakini hakujiunga na Chadema?! Bila shaka kila mtu atajua kuwa Uongozi wa Chadema haukubaliki na wapenda Mabadiliko.

Hata 2020 wengi watatoka CCM na CUF lakini hawatajiunga na Chadema chini ya Mbowe.
Labda akubali kuwapa watanzania kile wanachokitaka kwa muda mrefu yaani Sura mpya itakayowavuta wasaka Mabadiliko.


Sent using Jamii Forums mobile app
asante kwa maelezo ya kina
 
Kuliko Mbowe na Chama chake waingie madarakani ni bora tuongozwe na JPM hata miaka 20.
Mbowe ni Dikteta mbaya kuliko Hitler.
Mbowe hajawahi kukubali kukosolewa au hata tu mtu kuzungumzia Uenyekiti wake.

CCM ni chma cha kijamaa.
Chama cha Kilibearali kispokua na Demokrasia kama ilivyo Chadema ni hatari kuliko Genge la majambazi wale waliokua wanateka mabasi Biharamulo Kule Kagera.

Mbowe siwezi kumlinganisha na thamani ya Nchi hii na thamani ya ulimwengu wa Demokrasia.

Siku mtakapojua Demokrasia inajengwa kwa gharama kubwa ya kuweka mbali umaarufu,ubinafsi na kupoteza kwa ajili ya Taifa ndio siku mtakapojua kuwa Demokrasia ni kubwa kuliko Mbowe na Chadema.

Nchi za Afrika nyingi kwa kuendekeza watu zimejukuta zinaingiza vyama na watu wa hovyo madarakani kwa kisingizio cha kupigania Demokrasia ya kupata Urais ili waibie nchi.
Mwizi na dikteta kama Mbowe hawezi kamwe kuongoza mageuzi na harakati za kidemokrasia Tanzania.

Mtu yeyote atakayekuja na Hoja za kuipamba Chadema bila kueleza matatizo ya ndani ya Chadema ni lazima nitampinga na kuishambulia hiyo mana na Mbowe mana ndiye Dikteta aliyebaki kuhujumu Demokrasia akishirikiana na kundi Kubwa la Mafisadi ndani ya CCM. Kundi la wafanyabiashara wezi na wauza Unga.
Mbowe nyie mmemjua juzi.

Mimi Mbowe namjua mpaka Kijijini kwake Tangu 1994 . Ni kati ya Watu wasio na huruma na mtu yeyote linapokuja suala la Pesa na Umaarufu na Uhuni wa kila aina. Alipewa chama kwa wema akisogeze na kukabidhi wengine lakini alipogundua Fursa ya kufanya biashara za kuchapisha matisherti ,Kununua vifaa vya Chama kwa Tenda zake,kukikopesha chama na kujilipa mamilioni ya Ruzuku kama madeni hataki tena kuachia chama mpaka Kifie mikononi Mwaka na wajinga wachache wanaendelea kumuunga mkono kwa ubinafsi wao.
Taasisi yoyote isipokua na mabadiliko ya kiuongozi inageuka kuwa na matatizo ya Ukabila au udini!!

Mkumbatieni Mbowe tu mtabaki naye peke yake na Hakuna mtu atakayekubali kutumikishwa na Ziro mwingine. Bora yule ziro wa Kule kwenye mkoa mkubwa mana ameteuliwa tu. Lakini anayoyawaza na kuyafanya hana tofauti na Mbowe.
Mbowe kila siku ni mikakati na mipango na matamko yasiyotekelezeka kama Ziro mwenzake.

CCM chini ya Bashiru na JPM ni bora sana ukilinganisha na Chadema ya Mbowe isiyo na Itikadi zaidi ya kurukaruka na matukio.
Akili za vurugu na ubishi ubishi tu ndizo anazoziendekeza na kuziongoza ndani ya Chadema.

Sent using Jamii Forums mobile app
Poleni sana. Mnathubutu vipi kutamka kuwa "ccm ni chama cha kijamaa" na kwa tafsiri ipi? Ujamaa gani usiothamini wala kujaji utu wa watu? Pengine mnafanya ukasuku au ni upotoshaji wa makusudi na wa kimkakati. Hata huo utetezi uwe basi na mashiko na chembe ya kimantiki.

Wengi wenu Hitler mmemsikia tu kwenye mitandao ya kijamii kama huu wa jf; hakusoma historia yake. Kifupi alianza umaarufu wake kwa kushabikiwa na vijana wasiojitambua kupitia chama cha wafanyakazi cha Ujerumani. Akaishia kutawala nchi kwa udikteta na ukatili wa kutisha.

Bara la Afrika ni la kutolea mfano duniani kwa kuwa na watu ambao hawajui walikotoka wala wanakolenga kufika. Haijalishi mtu ameelimika au la; ni vigumu kuwatofautisha wasomi na wale ambao hawakubahatika kupata elimu rasmi (formal education) kwa ngazi zote za elimu. Wote wanachojali ni mlo mmoja wa siku. Watu wa aina hii ni wa kuogopewa kama ukoma. Wasomi wetu hawajachangia vyakutosha kubadili fikra za waafrika kwa ajili ya kuwaletea mageuzi na maendeleo.

". . . ccm chini ya Bashiru na JPM ni bora sana . . ." Mwandishi ameshindwa kujizuia kuficha mtazamo na mrengo wake wa kisiasa.
 
Poleni sana. Mnathubutu vipi kutamka kuwa "ccm ni chama cha kijamaa" na kwa tafsiri ipi? Ujamaa gani usiothamini wala kujaji utu wa watu? Pengine mnafanya ukasuku au ni upotoshaji wa makusudi na wa kimkakati. Hata huo utetezi uwe basi na mashiko na chembe ya kimantiki.

Wengi wenu Hitler mmemsikia tu kwenye mitandao ya kijamii kama huu wa jf; hakusoma historia yake. Kifupi alianza umaarufu wake kwa kushabikiwa na vijana wasiojitambua kupitia chama cha wafanyakazi cha Ujerumani. Akaishia kutawala nchi kwa udikteta na ukatili wa kutisha.

Bara la Afrika ni la kutolea mfano duniani kwa kuwa na watu ambao hawajui walikotoka wala wanakolenga kufika. Haijalishi mtu ameelimika au la; ni vigumu kuwatofautisha wasomi na wale ambao hawakubahatika kupata elimu rasmi (formal education) kwa ngazi zote za elimu. Wote wanachojali ni mlo mmoja wa siku. Watu wa aina hii ni wa kuogopewa kama ukoma. Wasomi wetu hawajachangia vyakutosha kubadili fikra za waafrika kwa ajili ya kuwaletea mageuzi na maendeleo.

". . . ccm chini ya Bashiru na JPM ni bora sana . . ." Mwandishi ameshindwa kujizuia kuficha mtazamo na mrengo wake wa kisiasa.
Ndugu yangu tambua wazi kabisa kuwa Ujamaa unajengwa kwa Damu na Jasho.
Ujamaa unaweza ukafuta hata Kundi Fulani la itikadi inayotishia harakati zake, Dini,kabila au rangi.
Ujamaa na ugaidi vinatofautiana kidogo sana.

Hata hivyo ujamaa wa Tanzania ni tofauti mana upo katikati ya watu wenye Dini na hofu ya Mungu.

Hivyo kwenye ujenzi wa ujamaa usitegemee huruma toka kwa watawala wanaojipambanua kama wajamaa.

Fuatilia historia ya China.
Enzi za Mao watu zaidi ya Mil. 12 walifyekelewa mbali.
Ikiwa na maana ingekua ni Tanganyika wakati huo nchi ingebaki na paka mwitu na ngedere mana watu wangeisha.
Huo ndio ujamaa ambao sijawahi kuupenda. Lakini najaribu kuulinganisha juu ujamaa na kujitegemea wa Tanzania na Uliberali wa Madikteta kama Freeman Mbowe na kugundua kuwa Uliberali bila Demokrasia na kudhibiti Wezi mafisadi ndani ya vyama utakua ni mbaya kuliko Ujambazi.

Unajua ugaidi ni afadhali kuliko ujambazi.
Ugaidi ni falsafa ya kimaono ya kuisaidia jamii kwa itikadi Fulani lakini ujambazi ni wizi wa kutumia nguvu na silaha.

Uliberali wa Chadema Ukikosa Demokrasia tutakua na taifa baya haijawahi kutokea.
Mbowe atakua anatuwekea watawala wezi na majambazi.
Ujamaa uliojengwa na Mwalimu ulikua na una imani ya mwanaChama.
Sisi wote ni ndugu
Afrika ni moja
Nirasema kweli Daima
Fitina kwangu mwiko.
Sitatoa wala kupokea rushwa.
Nijielimsha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa manufaa ya wote.
N.k.

Ukiambiwa uchague kati ya mashetani wawili unachagua lenye kutenda wema japo kidogo.

Narudia tena Chadema kama Chama cha Kiliberali kinachopigania Demokrasia nchini ni Lazima kiwe na misingi ya Demokrasia na kiwajenge makada wake hivyo kuanzia ndani ya Chama. Atakayeona kuwa hawezi kukaa ndani ya Chadema kwa sababu Mbowe amestaafu Uenyekiti basi amfuate Machame akanywe naye Chain lakini sio kujenga Udikteta ndani ya Chama kwa kisingizio cha Eti Mbowe ni kiboko ya CCM.
Kiboko ni yule aliyewakosesha usinguzi watu wasiojulikana mpaka akiwa kitandani Hospitalini bado hawalali lakini Sio Dikteta,muuza unga,mkwepa kodi,ziro brain,mkabila,mdini,mhuni,mzinzi, mbaguzi, mtu asiyejulikana ndani ya Chadema Mwenyekiti wa kudumu ,Mbw anajijua mwenyewe.

Wanachadema wanataka Mabadiliko wasipoyapata ndani ya Chadema watayapata nje ya Chadema.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba nikurudishe nyuma, ni hivi chanzo cha haya yote ni Jakaya kukata jina la Lowassa pale dodoma, kama lowassa asingekatwa tusingekuwa na hali hiyo unayoizungumza.
 
Tumechoka na haya manung'uniko dhidi ya Mbowe. Hamna hoja nyingine ya kuleta humu? Watu wangapi wameandika kuhusu Mbowe? Sasa leteni mada zingine. Kama huna kaa kimya waache Chadema na chama chao.
Kumbe inawauma mnavyomuongelea JPM Mara kwa Mara nani anapenda

hardworking pays
 
Niseme tu ukweli na kwa dhati kabisa kuwa!!
Chimbuko la CCM kuendelea kubaki madarakani,Ugumu Wa maisha pamoja na wakati huu mgumu Tunaopitia kutafta suruhisho la kisiasa pamoja na hamahama inayoendelea!

Chanzo ni mwenyekiti Wa chadema Freeman mbowe; Kosa la mbowe kubwa ni kumpa nafasi lowassa agombee Urais: hapo ndipo alitibua kila kitu, Lowassa ambaye alikuwa na maneno matatu tu unampaje nafas ya kugombea? ( asalam aleikum, tumsifu yesu kristo, naombeni kura), Hakika mbowe hata nikilala njaa sitaacha kukulaumu!
  • Wakati tukitafta manukato na pafyumu nzuri kubadili hali ya hewa ndani ya chadema tutambue huyu mbowe ndiye aliyeruhusu harufu mbaya iingie kwenye chumba cha chadema!
  • Mbowe ndiye aliyepakua kinyesi kutoka nje na kukiingiza ndani,
  • mbowe ndiye aliyeingiza kirusi kwenye ulimwengu Wa siasa ya hamahama,
  • Laiti kama Dr.slaa angeachwa agombee nguvu na imani ya chadema ingedumu.
  • laiti kama Dr. slaa angeachwa agombee Libumba asingejiweka mbembeni na UKAWA
  • Laiti kama Dr. slaa angegombea imani na mshikamano ndani ya ukawa ungedumu
  • Mbowe ndiye aliyesababisha hata CUF kusambaratika.
  • Mbowe ndiye aliyesababisha LIPUMBA awe mamluki hadi kupelekea Maalim sefu kuhamia ACT
  • Mbowe ndiye aliyesababisha CCM ikashinda kwa kishindo
  • Mbowe ndiye aliyesababisha wabunge wengi Wa chadema kusaliti chama.
  • Mbowe ndiye chanzo Machungu na maumivu ndani ya mioyo ya watu wengi!
KUSEMA UKWELI SIKU HIZI NAMCHUKIA SANA MBOWE HAFAI

Sina shaka hata ile audio crip iliyosambaa kipindi kile "Baby can u fly to AR" ilikuwa yake! NAMCHUKIA sana mbowe! KIUFUPI nabaki chadema Kwa heshima ya TUNDU LISSU TU SAHIVI lakini vinginevyo nisingebaki!
Humchukii alisyeema lissu akifa asizikwe na bunge??
 
Kweli kabisa, Mbowe ndio alisababisha hata Daudi AlberBashire (mungu wa DSM) akapata masomo yote saba F na kutumia cheti cha mtu mwingine.

Mbowe mbaya sana kwa kweli, amemsababishia hata mtakatifu Yohane kuwaita wahudumu wa ndege "air hostage" badala ya "air hostess"
Vyovyote alivyowaita lkn alieleweka, wewe mwenyewe hapo unasemaga crass loom lkn bado watu wanakuelewa acha hoja dhaifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiongoz Usipotoshe hakuna Safar ndefu kwa upinzani kuitoa ccm kwa sasa ccm iko hoi kuliko hata mgonjwa wa icu kama huamini tume ifanye kazi kwa mujibu wa sheria na polisi wasiingilie siasa uone kama huyo magufuli na ccm yake kama hawajaenda lubambangwe kulima mahindi.
Acha ndoto za alinacha ndugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vyovyote alivyowaita lkn alieleweka, wewe mwenyewe hapo unasemaga crass loom lkn bado watu wanakuelewa acha hoja dhaifu

Sent using Jamii Forums mobile app
"I wish I kudu be IGP", ningerara mbere na wewe! Karibu CCM tuunge mkono juhudi za mtukufu dhidi ya mabeberu waliosababisha ongezeko la joto Dar!
 
Back
Top Bottom