Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,692
- 272,558
kuna mahali imetajwa adhabu atakayoipata yeyote atakayejifanya ofisa wa tume au kuingilia kazi za tume ! Hebu Makene tuwekee hiyo bhana ! Sipati picha Mwigulu kunyea ndoo aisee !
Someni vizuri hapa, hakuna mahali ambapo Lissu (au CHADEMA in that context) wamesema Bw. Kipeya ameondolewa. Waziri Chikawe ndiye kajibu vitu visivyokuwepo, tunachelea kusema kadanganya. Someni hapa chini;
Mheshimiwa Spika,
Hata mahali ambapo wananchi wasiokuwa wanaCCM walifanikiwa kupenyeza katika chekecheke la mchujo wa WDC wamefanyiwa mizengwe na wanaCCM ili waondolewe katika orodha ya wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya. Mfano mzuri ni yaliyomkuta Bw. Beatus Kipeya aliyechaguliwa mjumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya ya Arusha Mjini kwa kupitia Kata ya Sombetini. Mara baada ya Bw. Kipeya kuchaguliwa kwenye kikao cha Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Sombetini cha tarehe 8 Aprili, 2013, siku hiyo hiyo Katibu wa CCM Wilaya ya Arusha Allan G. Kingazi alimwandikia Mkuu wa Wilaya ya Arusha barua ya malalamiko juu ya kuchaguliwa kwa Bw. Kipeya.
Pamoja na kumpa Mkuu wa Wilaya salaam za Chama chao, Katibu wa CCM Kingazi alilalamika kwamba Afisa Mtendaji wa Kata ya Sombetini amemruhusu ... raia wa Burundi Bwana Beatus Ndanyahubwi Kipea (ambaye katika kugombea ametumia jina la Beatusi Kipea ili asijulikane kama ni Mrundi ila mtu wa Kigoma yaani Muha) kugombea nafasi ya Ujumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya na akashinda, kinyume na maagizo ya Tume ya Katiba, kwamba Mjumbe ni lazima awe Raia wa Tanzania.
Baada ya maelezo mengi kuhusu Urundi wa Bw. Kipeya, Katibu wa CCM Kingazi anamwambia Mkuu wa Wilaya yafuatayo: ... (N)ashauri matokeo ya Uchaguzi wa Wajumbe wa Baraza la Katiba ufutwe na utangazwe upya. Aidha, Afisa Mtendaji huyo achukuliwe hatua za kinidhamu kwa kuvuruga kwa makusudi Uchaguzi wa Muundo wa Baraza la Katiba la Wilaya.
Mheshimiwa Spika,
Kitu cha kwanza cha kushangaza kuhusu barua ya Katibu wa CCM Kingazi ni kwamba aliyetumiwa malalamiko ni Mkuu wa Wilaya ambaye, kwa mujibu wa ibara ya 42(3), 44(3) na 46(3) ya Katiba ya CCM Toleo la 1982, Mkuu wa Wilaya ni mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Wilaya, Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya na Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya. Kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Mwongozo wa Tume, Mkuu wa Wilaya hana mamlaka yoyote kushughulikia jambo lolote linalohusu uchaguzi wa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya. Kwa maana hiyo, sababu pekee ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha kuandikiwa malalamiko haya ni kwa sababu ni kada wa CCM!
Mheshimiwa Spika,
Ukiacha Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Arusha, watu wengine wote walionakiliwa barua ya malalamiko ya Katibu wa CCM Kingazi ni makada wa CCM. Hivyo basi, nakala za malalamiko hayo zinaonyeshwa kupelekwa kwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Katibu wa CCM Mkoa, Mkuu wa Mkoa (ambaye pia ni mjumbe wa vikao vyote vya kikatiba vya CCM katika ngazi ya mkoa), Afisa usalama wa Taifa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Jiji la Arusha. Wote hawa hawahusiki kisheria kwa namna yoyote ile katika mchakato wa uundaji wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya. Chombo pekee ambacho kinahusika kisheria na mchakato wa kuunda Mabaraza hayo na ambacho kilitoa Mwongozo wa namna ya kuyaunda, yaani Tume, haikuandikiwa wala kunakiliwa barua ya malalamiko ya Katibu wa CCM Kingazi!
Mheshimiwa Spika,
Mara tu baada ya Afisa Uhamiaji Mkoa wa Arusha Bw. R. Gowelle kupata nakala yake, alimwandikia Bw. Kipeya barua ya wito wa kufika ofisi ya uhamiaji Mkoa wa Arusha, ambapo alimtaka kufika ofisini kwake bila kukosa wala kutuma mwakilishi. Cha kushangaza ni barua hiyo imenakiliwa kwa Afisa Mtendaji Kata ya Sombetini, Mwenyekiti wa Mtaa wa Kirika A, Sombetini na Balozi wa Mtaa wa Zurich, Sombetini.
Mbali na Afisa Mtendaji Kata ambaye alikuwa mlalamikiwa, wengine wote walionakiliwa barua ya Afisa Uhamiaji Mkoa ni makada wa CCM na, kwa taarifa za Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, ndio walikuwa chanzo cha malalamiko ya Katibu wa CCM Kingazi. Kwa taarifa za Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Bw. Kipeya ni raia halali wa Tanzania anayetoka katika Jimbo la Muhambwe katika Wilaya ya Kasulu ya Mkoa wa Kigoma. Dhambi pekee na kubwa aliyoifanya na kustahili kusumbuliwa na Idara ya Uhamiaji ni kugombea na kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya ya Arusha wakati yeye sio mwanachama wa CCM.
Mzalendo??? Au mnafiki??? We umejivua nguzo mwenyewe fikiria kati ya anejivua na kuvuluiwa nguo!!!
hapa una malipo tu!! Insatiable kinyaaa mno!!!!
Nataka kujua zile mil 18 za masuala ya ukimwi
Hiyo imenitoa jasho, kumbe tayari walijua wanenda kufanya ufusika,da! Hili ajab jingine la dunia
Nyie misukule wa mwigulu mna shida sanaChikawe amemuumbua Tundu Lisu bungeni jioni hii kwa kutoa ushahidi kuwa Bw. Beatus Kipeya ambaye Lisu na Chadema wanadai kuwa alienguliwa na WDC ya Sombetini asiwe mjumbe wa baraza la katiba la kata kuwa ni mjumbe halali na hivyo kuthibitisha kuwa Tundu Lisu na Chadema anajaribu kulidanganya bunge na wananchi.
hivi Lisu ule ukichaa alishapona?
Chikawe amemuumbua Tundu Lisu bungeni jioni hii kwa kutoa ushahidi kuwa Bw. Beatus Kipeya ambaye Lisu na Chadema wanadai kuwa alienguliwa na WDC ya Sombetini asiwe mjumbe wa baraza la katiba la kata kuwa ni mjumbe halali na hivyo kuthibitisha kuwa Tundu Lisu na Chadema anajaribu kulidanganya bunge na wananchi.
hivi Lisu ule ukichaa alishapona?
mbona yupo uchi tangu zamani kanjanja wa sheria
kuna mahali imetajwa adhabu atakayoipata yeyote atakayejifanya ofisa wa tume au kuingilia kazi za tume ! Hebu Makene tuwekee hiyo bhana ! Sipati picha Mwigulu kunyea ndoo aisee !
Huyo Lissu sio yule ambaye mke wake anazalia watoto USA ,ili wawe raia wa USA,KWELI kama ni mzalendo mbona wife wake asijifungulie Tanzania kama Watanzania wengine? Pia kuna Waziri mwingine kijana ana mtindo huu...Hawa wanachezea watanzania hawana mapenzi na nchi yetu!
Chikawe amemuumbua Tundu Lisu bungeni jioni hii kwa kutoa ushahidi kuwa Bw. Beatus Kipeya ambaye Lisu na Chadema wanadai kuwa alienguliwa na WDC ya Sombetini asiwe mjumbe wa baraza la katiba la kata kuwa ni mjumbe halali na hivyo kuthibitisha kuwa Tundu Lisu na Chadema anajaribu kulidanganya bunge na wananchi.
hivi Lisu ule ukichaa alishapona?
Chikawe ni moja ya watu wajinga sana duniani waliowahi kuingia katika baraza la mawaziri, hawezi kujibu hoja yeyote ya Lissu sana sana atatoa matusi ya nguoni.