Chenge,Werema: Tume imedanganya kiasi kilichopo kwenye mchanga, wajivua lawama

Kapewa kiti cha mbele cha bunge kwa kura na kelele za ndiooooo...ooo, pamoja na madudu yote aliyokuwa nayo. Wa kuwahukumu zaidi ni nyie wa ndiooooo.
Mkuu Ostrichegg,haya maCCM ni majuha majuha ya kiwango cha SGR. Kesho kutwa utasikia wabunge wa maCCM ambao walimpigia kura za ndiooooo Chenge kuwa mwenyekiti wakimshushia matusi na kumpa majina yote mabaya ya kuhusika kwake kwenye deals zinazolitafuna hili Taifa,as if wao sio waliompa kura za ndioo na kumpa uenyekiti. Ni msukule tu ndio anaweza fanya hivyo.
 
Wakati cabinet inapitisha mikataba hii inayotutafuna yeye magufuli alikuwa member kwenye cabinet, yeye pia hatasalimika kwenye hili, alishiriki kikamilifu mno kutuibia
Maamuzi ya baraza la mawaziri ni siri,ulijuaje kama alikubali?
 
Eti "tume idanganye kwa lipi"

Kamuulize ana kilango malechela.
(magufail alitaka kutajiwa idadi ya watumishi hewa hata kama hawapo!!!! na ukweli umesimama vile vile kwamba hawajatutajia watushi hewa bali wenye vyeti feki)
Mtu anaambiwa kile kitu anachopenda kusikia.
 
Hii ngoma sio nyepesi kama akina Polepole na Shaka Hamidu Shaka wanavyotaka umma uamini. Hii huenda ikawa ni kashfa mbaya kuliko zote katika nchi hii itakayoharibu kabisa image ya nchi, Serikali, academia, etc. Italigharimu taifa kwelikweli.

Tume iliyofanya uchunguzi wa jambo zito kama lile in less than 3 months hawawezi kuja na reliable findings. Mkulu naye alifanya haraka mno; angetulia akaweka jicho la tatu kujadili findings za Tume kwa kina na umakini wa hali ya juu kabla ya kufikia maamuzi. Tumeingia cha kike watanzania; tutalipa na tutalipa gharama kwelikweli. Mwenye ufahamu na atafakari.
Umesema kweli mkuu, Rais mwenye busara na hekima ya kiuongozi hupokea taarifa akatulia, akazisoma kwa utulivu, akajiuliza maswali na kufanya cross-checking of facts kabla hajafikia kuhukumu...sasa we have a joke of a president mkurupukaji na mlipukaji...tena nashangaa alifanyaje maamuzi makubwa vile wakati alitangaza kuwa hajazisoma hizo report na aliomba dk.5 eti akazipitie!

Hivi hajiulizi ni kwanini Mkapa alipokea ripoti za Jaji Warioba juu ya Rushwa na ile ya Jaji Kissanga juu ya haki za binadamu akazisoma na kuzifukia? Hajiulizi kwanini JK hakuwahi kuyatangaza majina ya wauza Unga hadharani?
 
Mkuu barafu;
Picha uloiweka imenikumbusha mbali sana. Huyo jamaa wa katikati kweli ana siri nyingi sana za taifa hili. Akifa nazo, tutalia siku zote tutakazo ishi sisi tuliobaki.
Kabla hatujaanza kuandamana kumpongeza JPM nadhani hakutakuwa na ubaya wowote kuomba ushauri kutoka kwa Chenge kuwa; Je, tumpongeze au tusubiri kidogo??
Chenge:
Anajua alipopindishia mkato
Anajua watakapo tumalizia.
Sasa; Tumuombe tu kuwa hatutamgusa lia, atuoneshe mtego ulipo yeye asepe atuachie hilo valangati. Tunao kina Tundu Lisu na TLS.
Werema naye; Anajua alichofunika kwa maneno mengi. Naye atuoneshe asepe. Sisi tupambane nao wala hatutamgusa. Kama walipewa msamaha wezi wa Epa itakuwa hawa wa kalamu za kisheria??
Mkuu mangatara,moja ya ushauri bora sana sana huu. Sisi hatutakuwa wa kwanza kutoa immunity kwa hawa washenzi kama tukikubaliana na wakatupa way out. Kama ulivyosema wale wa EPA walisamehewa japokuwa hata hatuna hakika kama yale mabilioni waliyarudisha kweli. But kama tunaweza kuona way out toka kwa kina TL & co.,hakuna haja ya kuwaachia hawa majambazi. Na hii isiishie kwa "vidagaa" tu kama hawa,maana hawa yawezekana walitumikishwa na wenye mamlaka makubwa zaidi yao,so nao pia wavuliwe immunity zao wasulubiwe. Muhusika yeyote yule kwa level yoyote ile achukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa waliopo au wajao. Tatizo ni je,mshika mpini ana dhamira ya dhati ya kuwapigania Watz?
 
Huyo Che. ndio walewale tunawafananisha na machifu waliodangwanywa kwa wisk ili wauze binadam wenzao utumwan,kwanza yeye alikuwa mwanasheria wakati kalamage anakimbilia nje ya nchi kusaini mikataba mibovu iliyosainiwa hotelini,kalamage alisema yeye ni kama yesu asiye na kosa alipotakiwa kujiuzuru hapo alimaanisha wahusika akina Che,Usimsikilize MTU ambaye siyo mzalendo alithubutu kusema yeye ana Akaunti Uswis yenye Mabilion lakin yeye anaziona kama vijisenti, kwa hiyo anatamani hata kuiuza hii nchi yote!!!!!!!!!!!!Sijui ni binadam wa aina gan?
 
Chenge sio mzee, ni mwizi. Mwizi hamushiki mwizi mwenzie. Chenge ana historian ya kuwaibia Watanzania. Chenge ni tajiri mkubwa, tajiri bila ya kufanya kazi. Chenge yuko kwenye kila janga kwa wizi Tanzania. Kwenye rada, Escrow, na wizi wa kila aina. Chenge ni mufano wa Mabutu Seseko wa Tanzania. Chenge anajuwa wizi wote unaotokea hapa kwetu, cha ajabu bado anapiga suit, na bado yuko bungeni. Nashangaa katiba yetu ina inaruhusu watu wenye mikono michafu wenye sifa za wizi wanakuwa Viongozi wetu. Chenge kwenye nchi zenye kupenda haki leo hii Chenge angekuwa anafundisha sheria gerezani.
Eti Chenge ni tajiri bila kufanya kazi...jiulize msomi wa Havard University, Naibu mwanasheria mkuu wa serikali kwa miaka mingi, Mwanasheria Mkuu wa serikali kwa miaka mingi, Consultant wa makampuni mengi ya kimataifa, mwanahisa katika makampuni mengi, Waziri na Mbunge...anakosaje kuwa tajiri(if at all)? Au unafikiri kazi ni hadi mtu akate na kuuza mkaa kule Kibiti?
 
Kha nimesikitika sana,watanzania tuna safari ndefu,Leo majority humu wanamwamini Chenge,tena huyu mwizi numero uno,maana ndo kanegotiate mikataba ya kusaidia kuibia Taifa,to be honest I thank God that my kids are not Tanzanians.
Hayo ni matokeo ya siasa za kinafiki, watu ambao kwa miaka zaidi ya kumi wanamshutumu chenge kwa kutumia taaluma yake na ofisi ya uma vibaya leo wanamwagia sifa kemkem!!
 
Chenge sio mzee, ni mwizi. Mwizi hamushiki mwizi mwenzie. Chenge ana historian ya kuwaibia Watanzania. Chenge ni tajiri mkubwa, tajiri bila ya kufanya kazi. Chenge yuko kwenye kila janga kwa wizi Tanzania. Kwenye rada, Escrow, na wizi wa kila aina. Chenge ni mufano wa Mabutu Seseko wa Tanzania. Chenge anajuwa wizi wote unaotokea hapa kwetu, cha ajabu bado anapiga suit, na bado yuko bungeni. Nashangaa katiba yetu ina inaruhusu watu wenye mikono michafu wenye sifa za wizi wanakuwa Viongozi wetu. Chenge kwenye nchi zenye kupenda haki leo hii Chenge angekuwa anafundisha sheria gerezani.
Kiongozi Mkuu wa nchi hayajui hayo unayoyajua wewe? Mbona miaka yote hiyo hatuoni lolote likitendeka? Tumempa uongozi kwenye bunge letu ambalo sisi ndo chama tawala. Acha wivu, Chenge chapa kazi na suala lolote litakalokuwa linahusu review ya mikataba au mjadala kuhusu mchanga, bonyeza kitufe. Yapo mambo serious ya nchi siyo hayo ya mchanga. Mchanga, mchanga, mchanga.....muwape watoto wakachezee huko.
 
Hayo ni matokeo ya siasa za kinafiki, watu ambao kwa miaka zaidi ya kumi wanamshutumu chenge kwa kutumia taaluma yake na ofisi ya uma vibaya leo wanamwagia sifa kemkem!!
Na nyie mliokuwa mnasema ndioooooo mbona Leo mnapinga?acha unafiki
 
Chenge alikuwa mwanasheria mku sawa lakini ktk makubaliano ya kibiashara sijui ni nani kati ya wanasheria anayekubaliana na mwekezaji husika ktk biashara
 
Tatizo huko kwenu hamtumii akili zenu, mnaburuzwa na ubongo wa mwenyekiti!
Madam, hebu jitafakari. Lowassa na Tundu Lissu ndio ubongo wa wanachadema. Waliojaribu kutumia bongo zao ni kama kina Zitto, Chacha Wangwe, Slaa, Shonza, Mtela, nk. Unajua nini kiliwapata.
 
Nina uhakika Tume ya JPM ya Makinikia imemdanganya sana Rais na Watanzania. Nina ushahidi ufuatao:

1. Wamewaaminisha watanzania kuwa kwenye kila kontena moja tunapoteza 1 Trillion shilings badala ya 300m walizosema Acacia. Hapa wanacheza na akili zetu na za JPM kwa kutaja figure hiyo kubwa wakati wanajua wazi kuwa hayo makinikia hayakushuka kutoka mbinguni. Kuna mtaji wa awali ulitumika yaani capex, kuna gharama za uzalishaji yaani opex na za usafirishaji. Chetu ni 4% ya hiyo 1Trillion ambayo ni 4Billion tu. Ili kuleta mtikisiko wa bongo zetu wakaona waseme tunapoteza 1Trillion kwa kila kontena badala ya kusema 4Billion. Lengo lao ilikuwa nini?

2. Mfumo waliotumia kukokotoa thamani ya madini ni wa uongo, maana wame assume kuwa recovery ni 100% kitu ambacho hakiwezekani. Hata kiwanda cha sukari hakina recovery ya 100% kwenye miwa iweje madini! Kwa teknolojia ipi utapata hiyo kitu?

3. Sampling method waliyoitumia inatia mashaka, ndio maana taarifa yao haiwekwi wazi ili sisi wajuzi wa sampling tuwakosoe. Aidha Lab ya GST waliyoitumia haina ISO hivyo haikubaliki kimataifa. Utamuitaje mtu mwizi kwa lab results za GST? Watuambie lab ipi zaidi ya GST waliyotumia yenye ISO. Vinginevyo ni kudanganya umma na kuiweka nchi kwenye hatari ya kushitakiwa kimataifa.

4. Hawakujipa muda kuhoji unalali wa resuts zao. Walipaswa kujiuliza maswali yafuatayo na kujijibu, je kwa results hizi ni kweli kuwa Acacia ni mzalishaji namba moja wa dhahabu duniani? Kama ndio, kwa nini wanaficha ukweli huo kwani si ingewasaidia kuongeza hata bei ya share zao kwenye soko? Je haya madini ya ziada tuliyoyaona zaidi ya dhahabu, shaba na fedha wanayoripoti serikalini je yanaweza kuchambuliwa kwa gharama gani na faida ikawepo au haiwezekani? Je wao Acacia wanalipwa hayo madini kama sio kwa nini wanakubali kupoteza fedha hiyo? Je kama wanalipwa, hiyo fedha ya ziada inaingia kwenye akaunti gani ambayo sisi hatuijui na je inawezekana hata USA na Canada hawaijui? Je serikali kupitia TRA na TMAA wanavyokagua financiàl records za Acacia huwa hawayaoni hayo mafedha ya ziada? Je hizi findings zetu ziko in line na taarifa za explorations na Feasibility study za migodi hiyo au tumegundua kitu kipya? Nina uhakika wangejiuliza maswali hayo wangedrop hizo findings za uongo na kuokoa nchi kwenye aibu hii.

5. Tume hawakuchukua tahadhali kutoa conclusion hizo ambazo zinaituhumu Acacia kuwa ni wezi na watendaji ni wazembe. Hatari iliyopo ni impact yake kwenye jamii na kwa watuhumiwa. Ona sasa share za Acacia zimeporomoka na watendaji wamesimamishwa kazi na wanachunguzwa bila hata kusubiri ukweli halisi kujulikana. Hii ni pigo kubwa kwa watu hao. Ndio maana naunga mkono hoja ya serikali kuyanunua makontena hayo na kuyapeleka kwa marafiki zetu china kuyachakata ili tuone kama hayo madini aloyoyasema Prof Mruma yatapatikana. Yaani Tume itaumbuka mchana kweupe na serikali itapata hasara kwa kuaminishwa na hawa maprofesa waliopika data ili kupata vyeo.

Nashauri JPM awaite hao wajumbe wa tume wathibitishe mapema ukweli wa hizo data zao ili ikija kutokea tofauti wanyongwe. Ni maoni yangu, Msema Kweli Mpenzi wa Mungu.
Umesema kweli yote. Hakika wewe ni kichwa. Historia itakukumhuka. Watch out JPM unadanganywa
 
Mkuu mangatara,moja ya ushauri bora sana sana huu. Sisi hatutakuwa wa kwanza kutoa immunity kwa hawa washenzi kama tukikubaliana na wakatupa way out. Kama ulivyosema wale wa EPA walisamehewa japokuwa hata hatuna hakika kama yale mabilioni waliyarudisha kweli. But kama tunaweza kuona way out toka kwa kina TL & co.,hakuna haja ya kuwaachia hawa majambazi. Na hii isiishie kwa "vidagaa" tu kama hawa,maana hawa yawezekana walitumikishwa na wenye mamlaka makubwa zaidi yao,so nao pia wavuliwe immunity zao wasulubiwe. Muhusika yeyote yule kwa level yoyote ile achukuliwe hatua kali ili iwe fundisho kwa waliopo au wajao. Tatizo ni je,mshika mpini ana dhamira ya dhati ya kuwapigania Watz?

Mkuu;
Natamani nikujibu ila sijui nianzie wapi. Nikianzia mwisho naomba nikuambie kuwa, mshika mpini huenda kweli ana dhamira ya dhati. Ila, ameanzia mguu mbaya. Angejiandaa vizuri tu ahakikishe kuwa, ikijibu vibaya, tusiumie zaidi. Aache haraka kwani hatujaanza kuibiwa leo. Mshika mpini kuna sehemu kadhaa huko nyuma, alituaminisha kuwa yuko vizuri na kuwa hatua alochukua sisi tutashinda. Mwisho tukajalia.
Mfano; Samaki wa Mvietnam, tulishindwa na tukalipa samaki na meli. Mkataba wa barabara (Ujenzi) kama kule Rombo Kilimanjaro. Wanaotokea kule wanalijua lililo tokea. Aliusitisha mkataba lakini alijalipa zaidi ya makubaliano. Sasa, leo unatuaminishaje kuwa, huu mchanga utatuacha salama?? Simpingi mkulu, ila naogopa kumsindikiza kizimbani.
Kuhusu kuwasulubu wazee, hapo nakuhakikishia halitakaa litokee hilo la kuwavua immunity yao. Unajua kwa nini Tz hatupinduani bali tunaachiana viti?? Ni hiyo immunity. Ukiivunja weye itakuja kula kwako pia. Waache wapumzike tu kwa amani zao, walicho tudhulumu, ajuaye ni Mola. Ila, vidagaa hivi tuving'oe meno mchana peupe. Tuwafilisi, tuwaachie wawe huru kabisaa lakini wakikamatwa na noti ya 500 tu tuwakate mikono maana hawa wamelaaniwa. Wawe mfano kwa wengine
 
Katika hili nimeamini Tanzania ni wanafiki wa kwanza duniani,,, hivi na chenge nae kweli ni wa kumsapoti?? ,,,,
Unashangaa nini. Ccm si ndiyo wamempa Uenyekiti wa Bunge? Kuna kum support zaidi ya hapo? Kuna kumuamini zaidi ya kumpa uongozi wa juu katika chombo cha kutunga sheria, kuishauri na kuisimamia serikali?
Tutarajie nini.
 
Back
Top Bottom