Chenge: Mimi ni nyoka mwenye makengeza msaka pesa

Chenge: Mimi ni nyoka mwenye makengeza msaka pesa

Kwa hiyo miaka yote ya uwaziri wake alifanya kwa maslahi ya jimbo lake na si ya taifa? [emoji16]
 
Sasa kama yeye NI MJANJA WA KUTAFUTA PESA ATAFUTE KWA JASHO LAKE

NA SIO KUVIZIA FEDHA ZA WALALAHOI KISHA ANAENDA KUIBA,,HUO SIYO UJANJA HUO NI WIZI NA UFALA
 
kauli za chenge zinaudhi mnoo jamani, ivi kama ingekua nchi za watu wanaojielewa huyu mzee angekuwa wapi now?
 
Naona kaamua kweli kufunguka ili wale ambao bado walikuwa hawamjui vizuri, sasa wamjue. Ni vizuri tu maana huwezi kuwa shetani na ukajifanya wewe malaika. Yeye kaamua kuonesha ushetani wake ili kila mtz ajue.
 
....upuuzi anaongea sb analindwa na mifumo ya kipuuzi na wapuuzi wenzake.
 
Baada ya kuona hii kauli,nikaanza kutafakari wadhifu Wa Mh.Change. Alishawahi kuwa Mwanasheria Mkuu Wa serikali,ametuandikia katiba pendekezwa akiwa Mwenyekiti Wa uandishi. Sasa hii imekaaje Watanzania kuongozwa na Nyoka katika jambo muhimu la Taifa kujizaa upya?sote tunajua sifa za Nyoka.Inamaana hii katiba tuiite ni zao la Nyoka? Ni maoni yangu tu. Source:Gazeti la Nipashe Leo.
 
  • Thanks
Reactions: Gor
Baada ya kuona hii kauli,nikaanza kutafakari wadhifu Wa Mh.Change. Alishawahi kuwa Mwanasheria Mkuu Wa serikali,ametuandikia katiba pendekezwa akiwa Mwenyekiti Wa uandishi. Sasa hii imekaaje Watanzania kuongozwa na Nyoka katika jambo muhimu la Taifa kujizaa upya?sote tunajua sifa za Nyoka.Inamaana hii katiba tuiite ni zao la Nyoka? Ni maoni yangu tu. Source:Gazeti la Nipashe Leo.
.....anaongea hayo ndani ya taifa ambalo kuna kikundi chenye mamlaka ambayo ni walarushwa na wanalindani,katika nchi yenye mifumo makini na isiyolindana asingeongea upuuzu huo na wala hasingeaminika tena......Chenge ameshiriki ufisadi mwingi sana kama ya rada,ndege,TTCL,epa etc
 
Baada ya kuona hii kauli,nikaanza kutafakari wadhifu Wa Mh.Change. Alishawahi kuwa Mwanasheria Mkuu Wa serikali,ametuandikia katiba pendekezwa akiwa Mwenyekiti Wa uandishi. Sasa hii imekaaje Watanzania kuongozwa na Nyoka katika jambo muhimu la Taifa kujizaa upya?sote tunajua sifa za Nyoka.Inamaana hii katiba tuiite ni zao la Nyoka? Ni maoni yangu tu. Source:Gazeti la Nipashe Leo.
kaka kama hujui ...nikwambie kile nikionacho..kuna nyakati zinakuja naam nyakati ni sasa ambazo waovu hawataulizwa na mtu ila watajiumbua wenyewe huyo...ni nyoka kweli na tena ni nyoka wa zamani....kwa kuwa ametuambia mwenyewe yy ni nyoka basi tuanze kumuita mheshimiwa nyoka..au Mr. nyoka.........hata mm nimesshangaa sn kujiiita nyoka?
daaaaaaaaa......................
 
Msaka pesa ategemei hela ya walipa kodi au deal za serikari ndio ajite mjanja. Angekuwa na miradi walau atakama anajipendelea na kuiuzia serikari tungeona hana moral authority, but at least what he is doing is legal na ujanja pia umetumika. Lakini mtu anatumia nafasi yake na kalamu tu kuiweka nchi at disadvantage halafu anajiita mjanja ,huku ndiyo kuwafanya wananchi maboya.

Andrew Chenge is nothing more than the scum of the earth, yaani Chenge akipata ubunge tena hao wapinzani wajue safari yao ya mabadiliko bado sana kwenye taifa hili and something is wrong with their message; Chenge pia watamshindwa kama CCM itampitisha kusimama tena on what he represent as a politician, aiwezekani.
 
Binafsi nina mtazamo tofauti kidogo juu ya Mh Chenge huyu bw. ni miongoni kati ya wasomi wachache sana wa sheria ambao mimi binafsi nawaheshimu sana. Na ninaamini kabisa kwamba endapo elimu yake hii angeitumia vizuri kwa ajili ya manufaa ya Watanzania tuliowengi basi nchi hii tungekuwa mbali sana kwenye mambo mengi sana ya kisheria ambayo tungenufaika nayo kupitia kwake (mfano Mikataba ya madini n.k)

Chenge anaweza akawa si mpigaji sana wa hela kama ambavyo watu wengi wanavyomuona kwa sura ya nje. Labda tu ni kwa sababu ameonekana yumo karibu kila kashfa inayohusu ukwapuaji wa fedha ndio maana imefikia pahala sasa watu wanamwona kama ni bonge la mpigaji.

Wito wangu kwa Mh huyu ni kujitafakari upya na kuona umuhimu wake yeye kwa taifa hili. Nasema hivi kwa sababu kama kweli Chenge ana roho ya umimi basi elimu yake ya Sheria haina faida yoyote kwa Watanzania.

Mh. Chenge hebu sema na nafsi yako hivi kweli Mwenyezi Mungu alikuumba ili uwe kama hivi ulivyo? Kama jibu ni hapana basi hebu badilika baba ili utimize yale makusudi ya wewe kuwepo hapa duniani kama Mwenyezi Mungu alivyokusudia uwe.

Mwisho niseme tu kwamba bado nafasi unayo ya kulitumikia taifa hili kwa moyo wenye kutii na kusamehe onesha utumishi wako ili uache kumbukumbu njema katika mioyo ya Watanzania.

Mimi naamini kabisa kwamba Uongozi ujao bado utapata nafasi nzuri tu ya kuwa miongoni mwa wenye maamuzi ktk madaraka ya nchi hii Basi kama ni hivyo basi mwombe Mungu akupe hekima na busara katika kutenda kazi zako.

NI HAYO TU
 
jamaa ameniongezea hasira mbaya basi tu ngoja ninyamaze


10427351_866344436740128_157479849132446865_n.jpg




10888648_1399356027038746_1356101145180531121_n.jpg
 
Kweli huyu jamaaa anahitaji apigwe gun ya kichwa na ni mwizi kweliiiii😱:thumbdown:
 
Tumeruhusu uongozi kuwa ufadhili, wawakilishi wa wananchi kuwa wafadhili na hivyo kuhalalisha kuibiwa fedha zinazotokana na jasho letu, kodi zetu wenyewe kutumiwa kutudanganya kuwa tumepewa misaada!

Tunawapa maadui wa uma, wanyonyaji na watesi wa wananchi mamlaka ya kuendeleza uovu wao.

Shime wananchi, tuungane tupigane vita vya ukombozi dhidi ya udhalimu na dharau kwa uhuru wetu. Mapambano kwa ajili ya kulinda uhuru na kuondoa aina za unyonyaji zinazojitokeza baada ya nchi kupata uhuru kutoka kwa wakoloni ni endelevu muda wote wa uwepo wa wanadamu duniani. Vita hii haina chama, dini, kabila au jinsia!
 
Katika biblia kitabu cha mwanzo sura ya tatu,Mungu aliweka uadui kati ya binadamu na nyoka.

akasema mwanadamu atamponda nyoka kichwa na nyoka atamponda binadamu kisigino.

Nampongeza Mh.cSenge kwa kujitambua matendo yake na kujieleza kwamba ni adui mkubwa wa watanzania.

maana watanzania ni binadamu,ni zamu yenu wana bariadi kuendelea kumchagua nyoka awaongoze au kumponda kichwa mkaweka binadamu mwenzenu awaongoze.

Ninampongeza kwa kujitambulisha mwenyewe maana wenye mamlaka wanamuogopa na yeye analijua hilo akaona ni vema ajitaje mwenyewe.
 
Huyu jamaa anaogopeka sana serikalin,kwanza ni mchawi wa kutupwa sjui kama mnakumbka, alishawah kupigwa picha na mitambo ya bungen mwaka 2008 akiwa anaweka madawa ya kienyej,pili anaringa sana na taaluma yake ya sheria na anadiriki kusema Tanzania hakna anayemtoa knockout kwa sheria hata Mtikila hamuwezi.

Kuna Mnyantuzu Asiyekuwa Mchawi? Gambush Inahusika Sana Mkuu Na Yawezekana Yeye Ndiyo Akawa Mlezi Na Mfadhili Wa Hao Wachawi.
 
MIIKO YA UONGOZI WA UMMA
Utii wa miiko ya
uongozi wa umma
29.-(1) Bila kuathiri masharti ya Katiba hii, kiongozi wa umma
ataheshimu na kutii maadili ya uongozi wa umma na miiko ya uongozi.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoainisha:
(a) miiko inayopaswa kuzingatiwa na viongozi wa umma;
(b) utaratibu wa kumuondoa kazini kiongozi wa umma kutokana na
kuvunja miiko na kukiuka maadili ya uongozi wa umma;
(c) vitendo ambavyo Kiongozi wa umma hapaswi kuvitenda; na
(d) ngazi au orodha ya viongozi wa umma wanaofungwa na Ibara hii.

sijaona kosa la mheshimiwa chenge, as long as analete maendeleo kwa wananchi waliompa kura basi anafaa. pia nimerejea hiyo ibara tajwa, ninyi mmeielewaje?
 
Back
Top Bottom