Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kuna jaribio la hatari limefanyika ambalo hatuna budi kulikataa, jaribio la aidha kulibebesha Jeshi letu lawama isiyostahili au la kulitumia kufanya lisiyostahili. Yote mawili ni ya hatari kwa taifa. Majibu ya Waziri Mkuu Bungeni mwaka jana kuhusu Meremeta ambayo yamerudiwa tena hivi juzi na Naibu Waziri wa Fedha. Bw. Jeremiah Sumari kuwa suala la Meremeta linahusu "ulinzi" na "Usalama wa taifa" yanatulazimisha kujihoji kama Jeshi hili bado liko mikononi mwa wananchi.
Swali hilo ni muhimu kwani wabunge wote wa CCM wamekubali wakiwa na akili timamu kutotaka kujua juu ya Meremeta na wamekubali hoja kuwa wao kama wawakilishi wa serikali hawawezi kujua kinachofanywa na serikali. Uamuzi wao huo ni kinyume na katiba na unawafanywa wasistahili kuwepo Bungeni kwani wanavunja Katiba ambayo waliapa kuilinda.
Inabidi sasa kuanza kuandaa orodha ya wabunge wote ambao wanakasirishwa na neno "ovyo ovyo" na kukaa kimya wakati mambo ovyo ovyo yanafanywa; wabunge ambao ni wakali Bunge linaposhambuliwa lakini wako bubu wakati Bunge linafanywa kituko cha uongozi.
Katika sehemu ya kwanza ya kulifunua suala la Meremeta tunaangalia kwanza hoja ya kisiasa na kisheria ya kwanini ni LAZIMA jeshi letu siyo tu liwe la "wananchi" kwenye vitabu na nembo, bali lazima liwe chini ya uangalizi wa wananchi (kupitia wawakilishi wao). Nje ya hapo tunalitakia taifa mabaya.
Attachments
Last edited: