Chatanda ataka 20% ya Wagombea nchini wawe Wanawake

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,897
941

Chatanda Ataka 20% ya Wagombea Nchini Wawe Wanawake

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, amesema kutokana na hali ilivyo wanataka asilimia 20 ya wagombea wa majimbo, udiwani na serikali za mitaa wawe wanawake hasa katika uchaguzi ujao.

Chatanda amebainisha hayo wakati akizungumza kwenye mkutano maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa uliowashirikisha wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Mkutano huo ambao lengo lake ni kufanyia kazi msimamo wa Rais Samia katika kuleta umoja wa kitaifa kwa kudumisha maridhiano, ustahimilivu, mabadiliko na kujenga upya umoja wa kitaifa kwa vitendo.

GC_HliwWMAEU7II.jpg
 
..Ndio.

..kila nafasi iwe na mgombea mwanamke, na mgombea mwanaume.

..hata Raisi awepo mwanamke, na Raisi mwanamme.

..kuwe na usawa kwa nafasi zote.
 

Chatanda Ataka 20% ya Wagombea Nchini Wawe Wanawake

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Chatanda, amesema kutokana na hali ilivyo wanataka asilimia 20 ya wagombea wa majimbo, udiwani na serikali za mitaa wawe wanawake hasa katika uchaguzi ujao.

Chatanda amebainisha hayo wakati akizungumza kwenye mkutano maalumu wa Baraza la Vyama vya Siasa uliowashirikisha wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Mkutano huo ambao lengo lake ni kufanyia kazi msimamo wa Rais Samia katika kuleta umoja wa kitaifa kwa kudumisha maridhiano, ustahimilivu, mabadiliko na kujenga upya umoja wa kitaifa kwa vitendo.

View attachment 2861647

Muulize hivi , Ilikuwaje alishiriki huu unyama ?

2183704_IMG_1183.jpg
 
Sidhani kama tunahitaji upendeleo kwa Wanawake
Tumekuwa na viti maalumu kwa miaka 50, hivi vimesaidiaje akina Mama wanaojifungulia sakafuni!

Viti Maalumu au upendeleo maaalum kwa Wanawake hauna msaada wowote kwa asilini 99.9 ya Wanawake

Kwani si tunao pale Dodoma kwa sasa? Nini kipya au cha maana wanafanya

Waingie katika ushindani kama Wanaume. Hatuhitaji idadi ya jinsia tunahitaji watu wa kulisaidia Taifa

Futa viti maalumu, futa upendeleo wa aina yoyote , weka mizani ya ushindani sawa
 
Back
Top Bottom