Chasha Message: All the Best kwa Ujasirimali Members

Chasha Message: All the Best kwa Ujasirimali Members

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,942
Reaction score
9,464
wote wa jukwaa la Ujasiriamali, nichukue fursa hii kuwatakia kila la heri katika sikukuu ya Mwaka mpya na sikuu ya Krismasi.

Katika safari ya Ujasirimali kuna Changamoto nyingi sana tena mno, na si safari ya kitoto hata siku moja, inahitaji uvumilivu wa kipekee kabisa, Ujasiriamali una changamoto nyingi sana ambazo usipokuwa na uvumilivu inakuwa ni taabu sana, mara nyingi theory tunazo soma ni tofauti kabisa na uhalisia wa mambo yalivyo.

Ninacho weza kusema ni kwamba, tunatakiwa kupambana kufa na kupona na si kupambana kwa kitoto, ujasiriamali ni vita ambayo bila kugangamara ni lazima ushindwe, Sisi tuna fursa ya kufanikiwa lakini ni lazima tupambane, ni lazima tuende na wakati, ni lazima tujaribu kuiota kesho itakuwa vipi.

Changamoto kubwa inayo tukabili ni Sapoti, ila basi kama hatuna sapoti ya Gavament sio sababu ya sisi kukata tamaa, ni lazima kwa mfumo huu huu mbaya na mazingira haya haya tupambane kutoka, kwa sababu hata wakati wa vita kuu ya kwanza na ya pili ya Dunia kuna wajasiriamali walianzia hapo, pamoja na mazingira ya vita still watu waliweza kusavive katika ujasirimali, so why sisi?

Katika mazingira magumu kama haya tupambane na siku mazingira yatapokuwa mazuri yatukute tayari tuko kwenye game, na kamwe tusisubiri mazingira yawe rafiki ndo tuingie kwenye game. Wavumbuzi wengi walivumbua vitu vyao katika mazingira magumu sana, na hata ulaya na America si kwamba ilianza na mazingira mazur, no mazingira yaliwakuta so hata sisi ni lazima mazingira yatukute kwenye game na sio sisi tuyakute.

Katika biashara kuna challenge nyingi sana, kwa sasa kubwa kuliko yote ikiwa ni ushindani mkubwa hasa kutoka nje na gharama kubwa sana, ila ni lazima tuwekeze kwenye utafiti wa kupunguza gharama, kila mtu na biashara yake anatakiwa aumize kichwa kufikiria ni vipi anaweza punguza gharama ili aweze kusavaivu kwenye biashara? Kwa trend ilivyo, tusitarajie kwamba kuna siku kutakuwa na mteremko, no.

Ushindani uko kila mahali duniani, na ukipewa story za Wachina kwa wachina unaweza ona kwamba sisi huku tuna raha, hivyo ushindani ndo sehemu ya wewe kupambana na kutoka. Tunaweza fanikiwa kushawishi Serikali kuzuia baadhi ya bidhaa zisiingie Tanzania ili kulinda bidhaa za ndani , Je Hao wawekezaji wakija Tanzania na kuanzia biashara hapa hapa unazani watazuia wasiuze? Jibu ni hapana, so hatuna ujanja isipo kuwa kufight.

Wajasiriamali kwenye maeneo tulipo ni bora tukaunda club za kukutana angalau hata siku za weekend na kucheki trend ilivyo na nini cha kufanyika, kwa sasa biashara zinaenda kwa network, wenzetu unakuta siku za weekend ndo siku za wao kukutana na kupanga mikakati, ila sisi mara nyingi ndo siku za kwenda kushangilia watu wakiingiza pesa huko Uingereza, we need to change.

Success usually comes to those who are too busy to be looking for it." Henry David Thoreau
 
Pamoja sana Kamanda, Heri ya Mwaka Mpya na Krismasi kwako pia tukiomba uzima kuziona, Mungu ni Mwema. Kwa namna ya pekee wewe ni mmoja wa member humu unaehamasisha shughuli za Ujasiriamali na watu wanaokuelewa wanaitikia, mimi ni mmoja wao, mwaka huu, nilinunua Kuku vifaranga aina ya KENBRO kwako na sasa wanataga mayai ambayo nayauza.

Kuhusu kuanzisha Network, Linajadilika
 
Pamoja sana Kamanda, Heri ya Mwaka Mpya na Krismasi kwako pia tukiomba uzima kuziona, Mungu ni Mwema. Kwa namna ya pekee wewe ni mmoja wa member humu unaehamasisha shughuli za Ujasiriamali na watu wanaokuelewa wanaitikia, mimi ni mmoja wao, mwaka huu, nilinunua Kuku vifaranga aina ya KENBRO kwako na sasa wanataga mayai ambayo nayauza. Kuhusu kuanzisha Network, Linajadilika


Mkuu asante sana, tunatakiwa kupambana simchezo, kila la heri Mungu akipende tutaonana.
 
Asanteni Heri ya Xmas na mwaka mpya tunashukuru Chasha na wengine kwa kutuhamasisha kutuelimisha na kututia moyo, binafsi nimejifunza mengi na kufanikiwa kuanzisha vitu kupitia nyie. Labda mngeweka ajenda ya kukutana na wapi kwa kanda husika maana umbali nao ni kikwazo.

Likizo hizi wengi tumerudi miji yetu sasa, Mungu akipenda tutahudhuria maana kuna wadau wameanza lalamika watu hawana mwamko. Tuzidi kujulishana lini, wapi na nini kiwe ajenda kuuu. Blessings
 
Chasha Poultry Farm na Mama Joe

Napenda kuwasalimuni wote katika Jina lake Bwana wa mabwana.......hakika tumepotezana sana ila hakika nina imani ya kwamba tu wazima wote wa afya njema.....

Awali kabisa ni kwamba pale juu Mkuu Chasha amemaliza kusema niliyokuwa nayo nafsini, hili la kukutana na kuweka mambo shwafi ninapendelea sana nategemea tutalifanikisha zoezi hili murua kabisa kwa wakati muafaka.... Chasha Poultry Farm ningependa hata twendeni PM tupeane nambari kwa mawasiliano zaidi!

Mama Joe wapi Kubota??????
 
Last edited by a moderator:
Chasha Poultry Farm na Mama Joe

Napenda kuwasalimuni wote katika Jina lake Bwana wa mabwana.......hakika tumepotezana sana ila hakika nina imani ya kwamba tu wazima wote wa afya njema.....
Awali kabisa ni kwamba pale juu Mkuu Chasha amemaliza kusema niliyokuwa nayo nafsini,.....hili la kukutana na kuweka mambo shwafi ninapendelea sana nategemea tutalifanikisha zoezi hili murua kabisa kwa wakati muafaka.... Chasha Poultry Farm ningependa hata twendeni PM tupeane nambari kwa mawasiliano zaidi!

Mama Joe wapi Kubota??????

Mammbo ni vipi mkuu LiverpoolFC? mkuu nicheki kwenye 0767-691071 au 0783-69-10-72
 
Last edited by a moderator:
Asanteni Heri ya Xmas na mwaka mpya tunashukuru Chasha na wengine kwa kutuhamasisha kutuelimisha na kututia moyo, binafsi nimejifunza mengi na kufanikiwa kuanzisha vitu kupitia nyie. Labda mngeweka ajenda ya kukutana na wapi kwa kanda husika maana umbali nao ni kikwazo. Likizo hizi wengi tumerudi miji yetu sasa, Mungu akipenda tutahudhuria maana kuna wadau wameanza lalamika watu hawana mwamko. Tuzidi kujulishana lini, wapi na nini kiwe ajenda kuuu. Blessings

Mimi nazani mnaweza arange hata Morogoro inakawa siku ya weekend ambayo sisi wa mikoani tunaweza fika, ni ishu inayo wezekana, na hata kwa levo ya mikoa bado watu wanaweza kutana kuliko tuitane kwenda kushangilia sijui Manchester why wadau wasukutana kujadili very Paramount issues?
 
Chasha Poultry Farm Mama Joe pale juu amenena na hata wewe umemjibu barabara kabisa
Ni vema tukafanya hii issue iwe na uzito na tuafikieane tutakutana Mkoa upi na ingekuwa maridadi sana!

Sisi wa kanda ya kaskazini nafikiri tuko wazi na hatufungamani upande wowote........ Chasha Poultry Farm & Mama Joe hakika tuko pamoja!
 
Last edited by a moderator:
Good Moro ni pazuri nafikiri wengi wataweza kwa hili, lakini inavutia zaidi mtu ukijua lengo yaani ajenda nafikiri wenzetu wa chai day huwa wanajua ni misitu tu wa kuku usitie pua, sasa pamoja na kuwa umetaja wajasiriamali ila wengi wetu vile tumekuwa motivated na vitu ufanyavyo tunajua issue za vitu vya mifugo lazima viwepo, naweka tu mfano (msinichukie mwamba ngoma....)
1. Kutambuana wafugaji wa kuku aina moja mf broiler, layers, chotara na kienyeji

2. Kujuzana jinsi gani kuweza kushika soko jwa pamoja mf kuchukua tenda wewe wk hii mie ijayo nk

3. vyakula, chanjo na madawa na mbinu za kupunguza cost ktk ufugaji

4. ufugaji ndege wengine na soko vibali vyake mf kware, kanga na bata bukini
5.......................... ni mifano tu maana ni siku moja so vitu viwe vichache lakini tukija before hand tukijua nini tunatarajia nafikiri inatosha kabisa
Merry Xmas and Happy New Year to all
cc neggirl, goodmother, hossam, pachanya, pleo....ongezeeni



Mimi nazani mnaweza arange hata Morogoro inakawa siku ya weekend ambayo sisi wa mikoani tunaweza fika, ni ishu inayo wezekana, na hata kwa levo ya mikoa bado watu wanaweza kutana kuliko tuitane kwenda kushangilia sijui Manchester why wadau wasukutana kujadili very Paramount issues?
 
Naaam! Mama Joe pale juu umeendelea kuweka mbolea katika shamba hili jamani!

Kuna jamaa mmoja kanipigia simu leo majira ya saa saba yapata kasoro akihitaji mwongozo katika ufugaji wa hawa kuku wa kienyeji.....niliongea naye dakika yapata nne na nikamwahidi ya kwamba nitampa mwongoza baada ya......na mpaka sasa bila shaka ananisubiria!

Na yeye anaishi Tabata jijini Dar es salaam ila hakika ni watu wenye kuhitaji mwanga katika ujasiriamali huu wa ufugaji!

Nambari zangu hii hapa Ndugu zangu
0717 71 44 99/0754 89 55 39

Mama Joe huyu Ndugu yetu Kubota yuko wapi?
 
Last edited by a moderator:
Good Moro ni pazuri nafikiri wengi wataweza kwa hili, lakini inavutia zaidi mtu ukijua lengo yaani ajenda nafikiri wenzetu wa chai day huwa wanajua ni misitu tu wa kuku usitie pua, sasa pamoja na kuwa umetaja wajasiriamali ila wengi wetu vile tumekuwa motivated na vitu ufanyavyo tunajua issue za vitu vya mifugo lazima viwepo, naweka tu mfano (msinichukie mwamba ngoma....)
1. Kutambuana wafugaji wa kuku aina moja mf broiler, layers, chotara na kienyeji
2. Kujuzana jinsi gani kuweza kushika soko jwa pamoja mf kuchukua tenda wewe wk hii mie ijayo nk
3. vyakula, chanjo na madawa na mbinu za kupunguza cost ktk ufugaji
4. ufugaji ndege wengine na soko vibali vyake mf kware, kanga na bata bukini
5.......................... ni mifano tu maana ni siku moja so vitu viwe vichache lakini tukija before hand tukijua nini tunatarajia nafikiri inatosha kabisa
Merry Xmas and Happy New Year to all
cc neggirl, goodmother, hossam, pachanya, pleo....ongezeeni

Mama Joe nazani si wafugaji wa kuku pekee, bali kwa watu wote ilimuradi unafanya biashara, Ujue hizi biashara zinategemeana sana mimi nafuga kuku lakini nahitaji network na wanao fanya kazi zingine, Inaweza husisha members wote ilimurad wanafanya business.

Network ni muhimu kwa sababu, hapo utawakuta walaamu wa IT na tunaweza fanya biashara na vile vile utawakuta wafuga Nguruwe, Ng'ombe, mbuzi, samaki, kilimo, na kazalika na kikubwa tunafahamiana na leo na kesho labda ninahitaji printing basi najua kuna members yuko Dar na anafanya kazi hiyo hivyo kwa nini nisimpe kazi?

Hayo yua wafuga Kuku, au wafuga ,mbuzi au wafuga samaki wanaweza fanya meeting sideline na meeting kubwa na inawezekana, hata Mapresident wakiwa na mikutano ya kimataifa huwa huko huko wana arange meeting na president mwenzake
 
Last edited by a moderator:
Chasha Poultry Farm......umenena Mkubwa ila ubovu moja wa member wa Jf ni hawana ahadi ya kiukweli kwani kuna kipindi nilishawahi kufunga safari mpk Dar kuonana na baadhi ya member ila hawakujitokeza kama nilivyotarajia na hao walikuwa wa kilimo,hiyo imenivunjaga moyo sana siwadanganyi.

Mi ningependa kama tutakutana tukiwa tano hata kumi maana nina imani watakuwepo member humu na tuangalie iyakavyokuwa!!
 
Last edited by a moderator:
Chasha Poultry Farm......umenena Mkubwa ila ubovu moja wa member wa Jf ni hawana ahadi ya kiukweli kwani kuna kipindi nilishawahi kufunga safari mpk Dar kuonana na baadhi ya member ila hawakujitokeza kama nilivyotarajia na hao walikuwa wa kilimo,hiyo imenivunjaga moyo sana siwadanganyi.

Mi ningependa kama tutakutana tukiwa tano hata kumi maana nina imani watakuwepo member humu na tuangalie iyakavyokuwa!!

Hilo ndo tatizo letu mkuu, na ndo kitnacho tugharimu,
 
Back
Top Bottom