Charles Taylor found Gulity at The Hague

Wakuu nimekuwa nafuatilia hii kesi ya Taylor japo mimi sio mwanasheria lakini nimekuwa navutiwa sana na jinsi kesi inavyoendeshwa hasa defensive lawyer Courtenay Griffiths ni makini sana japo hii kesi kushinda si rahisi . Leo hukumu inasomwa live on CNN na Judge Richard Lussick japo yeye Taylor amekana mashtaka yote na kusema yeye ni mwathirika wa njama za wabaya wake.

Binafsi kwajinsi ya uhalifu na mauaji yaliyofanyika Sierra lione wakati wa utawala wake huyu jamaa ana kesi ya kujibu.
 
Wakuu nimekuwa nafuatilia hii kesi ya Taylor japo mimi sio mwanasheria lakini nimekuwa navutiwa sana na jinsi kesi inavyoendeshwa hasa defensive lawyer Courtenay Griffiths ni makini sana japo hii kesi kushinda si rahisi . Leo hukumu inasomwa live on CNN na Judge Richard Lussick japo yeye Taylor amekana mashtaka yote na kusema yeye ni mwathirika wa njama za wabaya wake.

Binafsi kwajinsi ya uhalifu na mauaji yaliyofanyika Sierra lione wakati wa utawala wake huyu jamaa ana kesi ya kujibu.

Jahazi lake linazama, haponi kabisa.

Ushahidi hauko vizuri sana upande wake.

Viongozi wetu matumbo Yao ya moto, Aliyofanya Taylor na makosa yanayomkabili, ushahidi unavyochambuliwa ni Kama ambavyo viongozi wetu wanafanya.

ICC itapata wateja wengi sana.
 
huyu na george w bush wana tofauti gani? mbona bush hawajamkamata? give me a break!!! waonevu tu hao
 
  • Thanks
Reactions: tz1
Kwa jinsi ushahidi unavochambuliwa na kuhusishwa na Taylor namini kabisa hata yale mauji Zanzibar yakifanyiwa special court kama hii ya sierra Leone atrocities kweli hapatoki mtu.
 
huyu na george w bush wana tofauti gani? mbona bush hawajamkamata? give me a break!!! waonevu tu hao

Marekani wajanja, wao mpaka Leo hawajasaini statute inayotambua mahakama ie ICC, kwa Hali hiyo bush hawezi kushitakiwa. Viongozi wetu walirubuniwa na vihela wakasaini haraka haraka. Kumbe wao ni potential victims.
 
Kwa jinsi ushahidi unavochambuliwa na kuhusishwa na Taylor namini kabisa hata yale mauji Zanzibar yakifanyiwa special court kama hii ya sierra Leone atrocities kweli hapatoki mtu.

Hakuna Kiongozi atakayeaki Afrika, tuangalie tu jinsi ya kugonga mlango wa Fatou Bensouda
 
Taylor ana kesi ya kujibu,sentencing may 30.

Amepatikana na hatia. Kuwa na kesi ya kujibu ni pale upande wa mashitaka ukimaliza kutoa ushahidi basi mahakama inabidi ichambue ushahidi kuona Kama ushahidi huo umejenga kesi kumfanya mshtakiwa ajitetee

Mshtakiwa akijitetea nod mahakama unaweza sema amstakiwa ana hatia au la.
 
Jahazi lake linazama, haponi kabisa.

Ushahidi hauko vizuri sana upande wake.

Viongozi wetu matumbo Yao ya moto, Aliyofanya Taylor na makosa yanayomkabili, ushahidi unavyochambuliwa ni Kama ambavyo viongozi wetu wanafanya.

ICC itapata wateja wengi sana.




Usemayo ni kweli viongozi wa Afrika wakiwa naadabishwa namna hii vitendo vya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka vitapungua sana
 
Marekani wajanja, wao mpaka Leo hawajasaini statute inayotambua mahakama ie ICC, kwa Hali hiyo bush hawezi kushitakiwa. Viongozi wetu walirubuniwa na vihela wakasaini haraka haraka. Kumbe wao ni potential victims.



Wamarekani walijua haya wajiepusha nayo, ukweli ni kwamba serikali zote ni ovu sema zinatofautiana viwango tu vya uovu
 
Amepatikana na hatia. Kuwa na kesi ya kujibu ni pale upande wa mashitaka ukimaliza kutoa ushahidi basi mahakama inabidi ichambue ushahidi kuona Kama ushahidi huo umejenga kesi kumfanya mshtakiwa ajitetee

Mshtakiwa akijitetea nod mahakama unaweza sema amstakiwa ana hatia au la.

Thanks kwa sahihisho.
 
Wamarekani walijua haya wajiepusha nayo, ukweli ni kwamba serikali zote ni ovu sema zinatofautiana viwango tu vya uovu

Slobodan wa Yugoslavia wakati wa kesi yake kabla ya kufariki aliquestion hii kitu. Aliiomba mahakama ashitakiwe na rais wa marekani.
 
Sio uonevu hii inaitwa Justice, kusema kwamba Taylor asihukumiwe makosa yake kwasababu Bush nae ana makosa hiyo hoja haina uhai

so hiyo court ina mipaka ipi? ni kwamba lazima kiongozi awe kaua wananchi wake pekee, au akiwa kaiba hela anashtakiwa pia au niaje...mipaka iko mpaka wapi...maana tuna akina mugabe, museven. hapa kwetu zenj walishaua watu, pale magomeni kulishatokea vurugu wananchi wakafa, arusha juzi juzi tu so nataka nijue vikwazo wanavovitumia huko hague kwenye kukamata na kushtaki viongozi. Kumbuka hawa viongozi wanaopelekwa huko ni wale ambao walishapigwa chini na wananchi wao so wanakua sio powerful tena...But having said that sioni haja ya kumkamata kiongozi wa nchi yetu aliyeua watu50 wakati kuna kiongozi wa marekani aliyeua watu zaidi ya 100000 na hakamatwi ndio kwanza anapeta huko texas:A S angry:
 
Hivi Christopher Mtikila hawezi kufungua kesi huku, maana yeye ni mzee wa Kesi. Ila siku hizi ni kimya kabisa, amelishwa nini? Yamini au? Wenye taarifa zake watupatie wakuu.
 
Hivi Christopher Mtikila hawezi kufungua kesi huku, maana yeye ni mzee wa Kesi. Ila siku hizi ni kimya kabisa, amelishwa nini? Yamini au? Wenye taarifa zake watupatie wakuu.



Aisee sijui yuko wapi long time sijamsikia...labda ameshavalishwa gamba
 
Wondering why Taylor's trial was conducted by special court for sierra leone and not ICC (permanent tribunal) for crime against humanity? Msaada wanasheria.
 
Back
Top Bottom